Makapuku Forum

Makapuku Forum

Leo katika Historia

1844 - Mfalme Manelik II azaliwa.
Alikuwa ni mfalme wa Ethiopia.
04c1fa4851beca547075da384bf5bec6.jpg
8d73cefef170a35a5a709c0b8677963b.jpg
5eb16a19fd72e8f2e7db5c24a97ebc60.jpg

Alifariki 1913 akiwa nna imri wa miaka 69
Kama uliona kusoma Historia A sekondari ni somo la vibonde basi sikusimulii stori za vibonde !!
.......
 
Matatizo yalianza baada ya Mwinchande kurudi tena nchini ambapo kutokana na kufuzu kwake kwa alama za juu jeshi la polisi lilimtunuku vyeo zaidi na heshima yake kuongezeka mpaka kuwa kamanda mkuu msaidizi wa polisi nchini.
Lakini muda mfupi baada ya uteuzi na kupata heshima kubwa katika jeshi la polisi Mwinchande shauku yake ilihamia kwenda Arusha kumchukua mkewe Zainabu na mwanawe Shaaban.
Na hapo ndipo kisanga kilipoanza kubumbuluka mara baada ya kutofanikiwa kumkuta mkewe kijijini na bibi kukosa maneno yenye kueleweka hali iliyomfanya Mwinchande machale kumcheza na kuanza kufanya utafiti kwa watu wa kijijini waliomjua Zai.

Waswahili wanasema kuwa 'mtu atakunyima chakula si neno' na ndivyo ilivyokuwa mara baada ya Mwinchande kufanya utafiti wa siku mbili tu na kupata tetesi kuhusu Hussein japo hakujua kama alimuoa ila wambea walimwambia kuwa walimuona huyo mwanaume pale kwa bibi na wakatoa tetesi kuhusu jijini walipokuwa wanaishi hali iliyozidi kumpa mwanga na kumrahisishia Mwinchande jinsi ya kumnasa huyo mwanaume ambae aliona kuwa ni m baya wake kupita maeleazo, haiwezekani amtoroshe mkewe na mtoto.
Na ndipo baada ya kurudi Dar aliongea na vijana wake wa polisi waliobobea kwenye upelelezi na kuwakabidhi picha za mkewe Zai wamtafute kimya kimya maeneo yale ya jiji aliyopata maelekezo kule kijijini na ndipo zoezi la kumsaka Zai na kumpeleleza kwa siri lilifanikiwa na kuanza kumpeleleza mwanaume aliekuwa anaishi nae na kupata habari zake zote muhimu na hapo ndipo Mwinchande aliamua kumuandikia barua la onyo Hussein tena aliamua atumie mbinu ya jina litalomuweka kwenye mabano ili kama atakiuka aweze kumfanyia unyambisi bila shida.
Na katika kulifikiria jina ambalo litakuwa maalum kwake siku hiyo akiwa chumbani kwake usiku akijiangalia kwenye kioo ndipo lilipomjia wazo mara baada ya kuiona ile alama ya X chini kidogo ya shavu lake na kuona jina kivuli litalofaa kwake ni MR X.
Ila kabla hajafanya hayo yote alimtafuta Zai ambae alikuwa na line ya siri aliyoitumia kuwasiliana na Mwinchande kwa njia ya sams lakini Hussein hakuwahi kugundua uwepo wa hiyo line.
("Haiwezekani kabisaaa..! Dah! Yaani Zai asinisariti muda wote huo aje anisariti leo hii? tena akiwa na mtoto mdogo? hapa kuna mchezo tu na huenda huyo jamaa akawa mchawi na kama hii ripoti a vijana kudai kuwa ana udugu na Mnyungunyungu basi hii itakuwa dawa tu si bure")
Aliwaza sana Mwinchande na kuanza kuandika mwseji nzito kwenda kwa Zainab.
Baada ya Zai kupata ujumbe toka kwa Mwinchande wa kumuonya kuhusu usariti wake, aliamua kujitetea na kudai hata yeye hajui ilivyokuwa kuwa na hapo alizidi kumtia hasira Mwinchande aliyeamini kuwa hiyo njia iliyotumiwa si kosa la Zai bali ni uchawi wa Hussein na madawa.
Na hapo ndipo barua ya onyo ilipotumwa kwa Hussein na kupewa siku saba ahakikishe amemrudisha yule mwanamke kijijini kwao Arusha.

Ni ujanja na akili nyingi uliotumiwa na askali mpelelezi mmoja kumkabidhi Hussein ile barua ambayo ilipofika kwa Zai tu, alikanusha mdomoni na kujifanya hajui kitu lakini moyoni alijua kila kitu kuwa ile barua ilimuhusu yeye na mtu aliyejitambulisha kuwa Mr X ni mumewe wa kimila anayeitwa Mwinchande.
Kwa upeo wake Zai alijitahidi kujiiba na kuwasiliana na Mwinchande akimsihi asilipe ubaya wowote kwa yule mwanaume aliyemlaghai kichawi na kumtorosha wala wasifikie habari ya kumpiga na kumuua.
Suala lile la Zai awali Mwinchande aliligomea kwani alichohitaji yeye Hussein auawe kabisa.. Lakini kutokana na ombi la hisia kali tena za kiuungu na dini alilokuwa analiwasilisha Zai mara kwa mara ndipo lilimkubalisha Mwinchande na kumwambia Zai kuwa hatomuua tena Hussein kwa mikono yake.

* * * *

"Inspector wewe utaongoza hawa macoplo kwenda kuchukua zile maiti za ajali ambazo bado hawajatokea ndugu wa kuzichukua, kuna ya mama na mtoto aliyekatika kichwa mfanye haraka sasa."
ilikuwa ni mipango nyeti ya Mwinchande katika mtego alioudhamiria mara baada ya kupokea sms kutoka kwa Zai kuwa wanaelekea kule kwa baba yao mkubwa Manyungunyungu na wakati huo Mwinchande alikuwa katika hospitali ya Tumbi kulipoletwa maiti nyingi zilizotokana na ajali mbaya ya basi maeneo yale ya kibaha.
Alichokifanya Mwinchande harakaharaka na kutokana kuwa na makazi pia pale Kibaha aliondoka yeye na rafiki ake mmoja aliyempata kwa kumpa msaada wa matibabu ya mwanae na katika kuishi alipenda kumfundisha uninja na ndie aliyempa siri kidogo kuhusu yeye japo zilikuwa za uongo lakini rafikiake yule alimuamini mno hasa kwa msaada aliouonesha kwake kwa kumsaidia mwanae ambae alijua angekufa hivyo hata na yeye kumsaidia kwenye ile kazi aliona ni haki kabisa.
Hakuwa mwengine bali ni Ally ambae Mwinchande alipenda kumwita seven seven kutokana na kujuana nae siku ya tarehe 7 mwezi wa 7 hivyo akwa anamwita jina la Ally77. Na hapo ndipo walipochukua mavazi yao ya kazi (Kininja) ambayo waliyaweka kwa pembeni ya gari muda wanatoka na kuwahi Kibamba walipoiacha gari na kutembea kwa miguu karibu na ile jia panda walipochepuka na kuyavaa sasa mavazi ya Kininja na kupita njia za msitu mpaka sehemu moja waliyoona panafaa kutimiza lengo.
"tega upande ule mi natega upande huu, vijana wangu wanakuja taratibu na maiti. Nishampanga mke wangu akifika eneo hili atachutama kukojoa na hapo mimi nitatoka kumnyang'anya mtoto huyu mpuuzi kwani lazima amshike yeye na wewe utatoka nyuma yake na hilo gongo hakikisha unampiga maeneo yale niliyokuelekeza."
alitoa agizo Mwinchande na kueka mipango sawa.

Na ndivyo ilivyokuja kuwa mpaka Hussein anakuja kukamatwa na kusingiziwa kesi ya mauaji baada ya kuzimia pale chini punde alipopigwa na Ally77 ndipo muda zile maiti zilifikishwa na nguo alizovaa Shaaban alivalishwa yule maiti mtoto na kusogezwa pale kichakani huku mpelelezi mmoja akiwa maeneo karibu ya kijiji akingoja amri ya kwenda kuwaibua wananchi wenye hasira kali.
Zai alilia sana kwani alijua Hussein angeachwa tu pale na kuamka kujikuta pekeake lakini hakujua kama kuna mpango mwengine wa Mwinchande juu ya kumuua Hussein japo si kwa mkono wake lakini aliamini kisheria lazima atanyongwa.

Na hatimae Hussein alianza maisha ya jela na Mwinchande pamoja na Zai walianza maisha yao mapya katika jumba kubwa la kifahari ambalo ndani yake kulikuwa na chumba maalum kilichotengenezwa kwaajili ya mawasiliano maalum aliyokuwa nayasuka Mwinchande ili siku moja nchi isije kugundua kile alichokifanya na aliapa kuilinda siri yake mpaka mwisho wa maisha yake na kutokana na mbinu nyingi alizozipata Israel na India aliiendeleaza mission zake na kukichimba kizazi cha Hussein hasa mara baada ya kumuona bint mmoja aliyekuwa na mtoto wa kike akilia kule mahakamani na kudai kuwa yule mtoto ni wa Hussein na alikuwa na barua yake ambayo askali aliyeipokea aliitwa na Mwinchande mwenyewe ambapo aliifungua na kuisoma ile barua ndipo aliporuhusu ipelekwe huko gerezani kwa muhusika nae akaanza kufanya mipango ya kumueka katika anga zake mtoto wa Hussein aliyeitwa Asha.

Na hiko ndio kilikuwa CHANZO cha Mwinchande kugeuka kuwa mtu m baya na muuaji kwa kila anayeona anahatarisha

"Mwananguuuuuuuu Shaaaabaani mimi ndie mkosaaaajiii iiiiiih Najuutaa leeeeooooo aaaaaaaaaaaaaagh iiiiiiiiiiiiiih
Ona sasaa watuu niliowapeendaaa, watuu waliojitahidi kunionesha kila aina ya upendoooo, waliniaminiiii lakini leo nimewauaaaaa.... aaaaaah!! Mwanangu Shebby wewee si muuuajii wala babaako Hussein si muuajii hata Mr X piaaaaa. kwaani yoooote hayaa chanzo ni mimiii japo sijamuuaa mtuu kwa mkono wanguuuuuu... Lakini mimi ndie muuajii...Ooooooooooh eeeeeeeeeeeeh"
aliendelea kulia kwa uchungu sana Zainab mara alipokuwa anawasimulia chanzo cha matatizo Kamishna Shaaban na Cj4 aliyekuwa ameipakata maiti ya Hussein bubu huku wote machozi yakiwatoka baada ya kujua chanzo kizima.
"Maamaa, maamaa, mama ina maana Asha ni dadaangu? Mama!!! umeacha nimuoe dadaangu?!! aaaaagh."
aliumia zaidi Shaaban na alijua kuwa Asha hajui chochote kinachoendelea pale lakini kumbe Asha alishatumiwa ujumbe mfupi na Cj4 kumtaka kufika pale kwa kina Shebby haraka kutoa msaada kwani uvamizi umetokea.
Cj4 alifanya vile makusudi tu ili awaoneshe uwezo wa Asha ulivyo na kweli mara ghaaaaaaaaafraaaaa wakiwa wametahayuri wote ndipo walipomshuhudia mtu akiingia kwa style ya salakasi za ajabu kupitia dirisha lile alilovunja Shebby pindi akiingia na mara baada ya kuingia yule mtu na kutua mbele yao wote walishangaa kumuona ni mwanamke aliyezuia uso kwa nikabu nyeusi huku akiwa kavaa track suit juu na chini mikononi akiwa na visu vidogo zaidi ya vinane alivyovishika kimaajabu kwenye pachu pachu ya vidole vya mkono na kumfanya Shebby atake kuiwahi bastora yake lakini Cj4 alimkata ngwala punde tu alipotaka kuinuka na kumwambia.
"Huwezi ua tena kwa wasio na hatia mbele ya Cj4. Yule ni dadaako mke wako adui wa adui yako na yeye ndie Lady Ninja Asha."
maneno yale yalimfanya Shebby ataharuki zaidi hasa pale Asha alipodondosha vile visu chini na kupiga magoti akilia kwa uchungu kwa kubainika na kuona kile kilichokuwa mbele yake huku akifungua nikabu yake na kwa mara ya kwanza akawa dhahiri shahiri mbele yao kwa kuwahakikishia asemacho Cj4 na hapo hata Shebby alijikuta anapoteza fahamu kwa taharuki.


<<<< MIAKA 15 BAADAE >>>>
^^^^^^^^^^^^
* * *
^^

Ni katika makaburi ya Makanya Dar es Salaam wanaonekana watu wawili wakiwa wote wamevaa nguo nyeusi mmoja akiwa ni mtu mzima na mwengine mtoto wa miaka isiyozidi 14 wakiwa wamepiga magoti mbele ya makaburi yaliyojengewa kwa mtindo wa kufanana baada ya kuyasafishia na walionekana walifika pale kwa muda mrefu sana na kulikuwa na hadithi ndefu aliyokuwa anaisimulia yule Mkubwa kwa yule mtoto huku akimuonesha onesha makaburi yale.

"Hadithi hii imeniuma sana baba Cj4 aaah!! Mungu wasamehe ndugu zangu wote, kwa hiyo nini kilitokea sasa baada ya baba kujua kumbe mama alikuwa Ninja mara aliporudiwa fahamu?"
aliuliza yule mtoto.
"Baada ya babaako Kamishna Shebby kuzinduka ilikuwa tayari kashachelewa mara baada ya bibi ako kuzidiwa ghafra kwa presha iliyomshuka pindi alipogundua kumbe mumewe babu yako Mr X alikuwa amemtumia mamaako zaidi ya alivyojua yeye, kwani bibiako alijua kama mumewe anamtumia Asha lakini si kwa mauaji bali ni kumueka tu karibu ili amfiche kama yeye ni mtu m baya dhidi ya babaake ambae ndie babu yako mzazi Hussein.
Ilibidi sasa mamaako amuwahi kakaake ambae pia ni babaako pale chini pindi alipozinduka lakini nae alichelewa hata mimi pia nilichelewa kumuwahi kutokana na kumuweka chini babu yako Hussein aliyekuwa kashakufa na kumuwahi bibi yako Zai kwa kumpa msaada bila kujua nyuma yangu Shebby amezinduka na kwa kuchanganyikiwa kwa kile akionacho alishindwa kujizuia na kuiokota tena bastora yake na hapo nilisikia tu mlio wa risasi sambamba na kelele za mamaako Asha na nilipogeuka hakuwa Asha aliyepigwa risasi bali ni Shebby mwenyewe alijipasua kichwa na kusambaratika ubongo palepale.."
alipofika hapa kidogo alisita na kwa mara ya kwanza Cj4 chozi lilimdondoka hadhalani toka afuzu mafunzo ya Ukomando Cuba zaidi ya miaka 20 iliyopita.
"Mwanangu Hussein, sikumbuki lini ilikuwa mara ya mwisho kutoa chozi kwani hata kipindi yale yote yanatokea sikudondosha chozi. Zaidi nilisimama kiume kukabiliana nayo kwani ilibidi nimuache bibiako Zainab niliyeona wazi kuwa yupo katika hatua za kumalizikia baada ya presha kushuka sana na kushuhudia mwanae akijimaliza na hapo ilibidi niluke kishujaa kumuwahi mamaako Asha ambae nae alikuwa anataka ajimalize kwa bastora ile ile aliyojimalizia babaako.
Jinsi nilivyoruka sikuwahi kufundishwa wala kudhani kama nina uwezo wa kuluka vile, lakini ndivyo ilivyokuwa niliweza kumuwahi mamaako na kumuokoa mbele ya kifo alichokuwa anajitengenezea mwenyewe na nilichokifanya niliubetua mshipa wake mdogo wa fahamu uliokuwa nyuma ya sikio na kumzimisha.
Hapo ndipo nilipoweza kuwasiliana na mkuu wangu wa majeshi na kumpa taarifa zote kabla sijaondoka eneo lile huku nikiwa nimem beba mamaako ambae sikujua kumbe tayari tumboni ulikuwapo wewe."
Story ya Cj4 ilimuuma sana yule mtoto lakini alionesha alikuwa jasiri sana na mwenye moyo wa uvumilivu kwani alikuwa anatokwa machozi lakini aliweza kusikiliza kwa umakini na kuuliza maswali muhimu.
"Kwa hiyo baba Cj ilikuwaje sasa ulipoondoka na mama hasa pale fahamu zilipomrudia?"
"Mwanangu Hussein, mamaako kwanza alichelewa sana kupata fahamu hadi nilianza kuhofu lakini alipopata fahamu nilikuwa nae kwenye kambi maalum ya kijeshi ambapo ndipo nilipoelekea mara baada ya kutoka pale kwenye ile nyumba.
Niliongea nae na kumpanga kwa maneno ya kishujaa na mbinu maalum ambazo utakutana nazo pindi utapokuwa kama mimi hapo baadae, nikikutazama naona wazi utakuwa zaidi ya mimi.
Basi mamaako japo ilikuwa ngumu kuelewa lakini tuliweza kumdhibiti ndani ya kambi ile iliyokuwa haijulikani kabisa na watu wengi hadi kwa wanajeshi wengi wenye vyeo vya chini.
Japo alikuwa ni wa kuzimia mara kwa mara lakini hatimae aliweza kutulia taratibu kadri siku zilivyozidi kwenda hadi tulipomgundua kuwa alikuwa na mima baada ya kumfanyia vipimo vya utrasound pindi tulipoona tumbo linazidi kuwa kubwa na kugundua uwepo wako.
Sikuweza kuhudhulia mazishi ya babaako, bibiako, babu ako na babu ako mlezi wa babaako Mr X ambao wote walizikwa kwa pamoja hapa kama unavyoona makaburi yao yalivyofatana kwa sababu ya kuwa karibu na mamaako na kumliwaza japo niliweza kuyashuhudia baadae kupitia rekodi kamili ya ule mkanda tulioutazama tena sote jana usiku.
Serikali ndio waliolizima suala lile baada ya taarifa za ripoti yangu kamili kufika kwa muheshiwa Rais."
"sawa baba, sasa mama nae alikufa kufa vipi?"
"Mamaako kilichomuua ni sumu iliyokuwa mwilini mwake iliyokuwa ikimtafuna muda mrefu.
Sumu hiyo ilitokana na kile kisu cha kininja alichochomwa na Tyga siku ile usiku... Kwa hiyo siku aliyokuwa anajifungua ndio siku aliyofariki pindi alipokuwa anakupush kwa nguvu kumbe alikuwa anajimalizia baada ya sumu kushambulia sana maeneo ya uti wa mgongo na mbavu.
Mamaako alikufa kishujaa kwa kuwa aliweza kuvumilia hadi akafanikisha kumzaa Shujaa mpya ambae ni wewe mwanangu Hussein niliyeamua kukupa jina hili la babu yako ambae pia alikufa mikononi mwangu lakini kupitia wewe nikaona kama amezaliwa tena mikononi mwangu.
Na hivyo ndivyo ilivyokuwa Hussein wewe ulikuwa chini ya usimamizi wangu wala hukuwa na ndugu yeyote zaidi yangu.... Simama sasa nataka nikuulize nami maswali yangu."
aliongea Cj4 na kusimama sambamba na mtoto Hussein ambae ndie alikuwa mtoto halali wa Marehemu Dokta Asha au Lady Ninja na Marehemu Kamishna Shebby.

"Ulivyoelewa historia yako asili yake na matatizo yote chanzo ni nini?"
"MWANAMKE"
alijibu Hussein bila hata kusita.
"Vizuri na je, ulivyosoma historia ya ushujaa wa Samson dhidi ya Wafiristi hadi siri zake zikabainika na kukamatwa kupata mateso makali hadi alipoomba nguvu kumrudia na kufa pamoja na mamia ya watu je nae kilichomponza hasa chanzo ni nini?"
"MWANAMKE"
alijibu tena Hussein.
"Vizuri sana, na vipi kuhusu asili ya dhambi ya baba etu Adam kusariti ahadi aliyopewa na mungu na kushawishika kula lile tunda, kihistoria ulivyosoma shetani alimtumia nani kumshawishi kiurahisi Adam."
"MWANAMKE"
"Ni kweli mwanangu Hussein na hivi unajua kwanini Wanawake ni wengi kuliko Wanaume?"
"hapana baba Cj4, sijui."
"Basi ni kwasababu mtu wa kwanza kufa alikuwa ni mwanaume na alikuwa mtoto wa Adam aliyepigana na ndugu yake sababu ikiwa ni mwanamke. na hapo ndipo uwiano wa namba ulipozidi.
Kwa hiyo kwa uelewa wa kawaida kabisa umeona kumbe hata mtu wa kwanza kufa chanzo ilikuwa nini?"
"MWANAMKE baba Mh!!"
"Huo ndio ukweli ambao alikuwa anamaanisha babu yako wala si uchizi.. hivi unajua chanzo cha mimi kukuhadithia hadithi ya maisha ya asili ulipotokea chanzo ni nini?"
"Ndio baba chanzo ni Halima mtoto wa baba Kanali Suma mara baada ya kusababisha nimepigana na kumuumiza Amos mtoto wa Luten Frenk."
alijibu kwa upole Hussein.
"sawa kwa hiyo Halima ni nani?"
"ni mwanamke baba"
"kwa hiyo chanzo cha kukuhadithia ukweli huu na kukuonesha video ya mazishi mpaka sasa tupo hapa chanzo ni.....?"
"MWANAMKE"
"Ndio, sasa umejifunza nini hapa."
"Naapa baba Cj4 mbele za Mungu, mbele ya makabuli haya ya ndugu zangu kuwa nitakuwa makini makini sana na Wanawake kamwe sintokuwa mzembe wa kuwaaamini kwa asilimia zote kwa kuwa Wanamke wana ulemavu wa upeo na udhaifu wa asili."
aliapa kwa nguvu na sauti ya kumaanisha Hussein.
"sawa unadhani kwanini umeapa hivyo? hivi kiapo chako uko sahihi kweli?"
"Naamini baba Cj4 nipo sahihi, na ili nikuaminishe nipo sahihi kusema kuwa 'wanawake wana ulemavu wa upeo na udhaifu wa asili' nataka nikuulize swali."
"Uliza tu mwanangu."
"Je ni dini gani kati ya ukristo na uislam pamoja na matawi yake inasema Mungu alituma manabii na mitume wanawake kwaajili ya kuwaogoza na kuwaokoa watu?"
"Mh!! HAKUNA mwanangu wala sijawahi kusikia."
"unadhani Mungu ana upendeleo kwa wanaume?"
"Hapana, ila ninachojua Mungu alimuumba mwanamke kwa sababu ya kumtuliza na kumliwaza mwanaume."
"kwa hiyo hapo baba ndipo kwenye 'ulemavu na dhaifu wa asili ya mwanamke' japo wenyewe hawataki na naamini mwanamke asiyekubali kuwa dhaifu mbele ya mwanaume naamini ni muuaji na mwanamke asiyekubali kuwa ana ulemavu wa upeo basi atajiamulia vitu kama bibi Zai na faida yake ataiona mwishoni na atakuwa muuaji tu."
aliongea kwa uchungu Hussein na Cj4 alishangaa kuona maneno ya Hussein mtoto yanashabiana na nukuu za marehemu Hussein mkubwa na kuamua amkumbatie kwa nguvu pindi alipoona anazidi kuongea huku akilia na kumsihi sasa inatosha waondoke.
"Basi mwanangu basi mwanangu tuondoke sasa ila zingatia haya na ufanye utafiti na uwaokoe wanaume wengi wasiojua hili pamoja na kuwaelimisha wanawake wakubali udhaifu wao ili matatizo zaidi yasiendelee kutokea na kabla hujaongea nao wala kuwasimulia waulize kwanza je, WANAWAKE NI WAUAJI..!? sikiliza na uhesabu majibu yao kisha uwasimulie story hii na ikiwezekana uiandike kabisa na uitolee Kitabu ili wengi wakipate na mara utapomaliza kuwasimulia/kuandika waulize tena kwa mshangao swali lilelile la mwanzo kuwa WANAWAKE NI WAUAJI..!? uone tena majibu yao."


_________________________
____________
* MWISHO *
 
Leo katika Historia

1977 - Thierry Henry anazaliwa. (Imagine pipo walikuwa wanamuita chogo )
Ni mchezaji wa wa zamani wa Arsenal, Barcelona na Ufaransa.
Ni mchezaji bora zaidi wa Kigeni kuwahi kucheza EPL.
9e643bc00a65f07eccd138886ffc0a83.jpg
a710bacf7b1ac903efb1e9a052a5a9d1.jpg
6ca8aa4d22e1eabdfeb463643608342b.jpg
Babu Wenger enzi hizo kichwani zikiwa zinachaji alimchukua Henry akiwa hajulikani kabisa pale Juventus na kuja kumfanya mwanasoka tishio duniani
00e08939288474dd6ba70dd5bbb07f4a.jpg
f304ef2f72957dbd3cd03ed85120f978.jpg
Picha iliyotumika kumjengea sanamu pale Emirates pamoja na sanamu yenyewe
Katika mechi 254 alipasia kamba X 174 huku mengi yakiwa magoli ya kideoni
......
 
Leo katika Historia

1977 - William Gallas anazaliwa.
Ni beki wa zamani wa Chelsea, Arsenal na timu ya taifa ya Ufaransa.

2f4b00a5351b2fbc6672f663e9647602.jpg
f78b448f68d022515a26a3e8c5b7a507.jpg
3a5e26424905069b1d2b8603a2f9f5ba.jpg

Kitendo cha kunyanganywa jezi yake # 13 na kupewa Michael Ballack aliposajiliwa Chelsea kilimtibua na kuamua kususa timu na kutimkia Arsenal
Ni kama yaliyomkuta Anthony Martial last seasonaliponyanganywa jezi # 9 na Zlatan au Roberto Firmino kuporwa # 11 na Mohamed Salah
Yeye hakutaka ujinga
.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom