Makapuku Forum

Makapuku Forum

THE DOM

Sehemu Ya 6

Mtunzi..... MoonBoy

Simu No. +255714419487 WhatsApp

Instagram....

Ilipoishia Jana →↓↓↓↓←

SON OF PRESIDENT GU

Sasa sahi alpofika eneo la tukio, pale walipokuwa wanachepuliwa wale wanafunzi wengine,... Sahi alitamani sana kupita kwenye hako kamchepuko, mana yeye kama mpelelezi ana haki ya kujua kinachoendelea huku kwenye njia hii tofauti na wengine,...
"unataka ufanye nini"
Aliongea mwaju, huku sahi akijiandaa kuruka,..
Wakati huo mqaju anauliza yeye yupo mbali nae, mana wapo mwisho kabisa,..
"nataka nikajue wameenda kufanya nini wale, usikute wenzetu wanapewa mafunzo mazuri zaidi"
Sahi alisema hivyo, ili kumzuga mwaju asijue kama yeye ni mpelelezi,
"wewe mkaka, umekuja jana tu... Na hicho Kiherehere chako kitakuponza... Mazoezi ni haya haya hakuna mazoezi mengine"
Lakink wakati huo salehe wala hakutaka kumsikiliza mwaju, yaani kama kazi yake inavyomruhusu kufanya.... Sasa ile sahi anajiandaa kuruka ili kutua pembeni alishtukia kukamatwa mguu wake, na kujikuta anarudishwa katika line...
"lazima tukuchunguze kwa undani zaidi... Na utasema wewe ni nani hapa TMA"
Ilikuwa ni sauti ya mtu mwingine kabisa ambae hata hamjui, tena alivalia mavazi ya kiuwalimu, kana kwamba huyo ndio yule mwalimu aliowachepusha wanafunzi saba... Sasa sahi kaja na moto ambao hakutakiwa kuwa nao,.. Yaani kaanza kubainika akiwa na siku ya pili jeshini

ENDELEA..........

Sahi alikuwa hatamani hata kidogo kuona jambo linampita hivi hivi, yaani haitakiwi limpite,.. Sasa swala la wanafunzi wenzake kuchepuliwa katika mazoezi, hili lilimshangaza sana salehe, tena akiwa mwanajeshi aliofuzu mafunzo kule korea, na elimu yake ya upelelezi alioisomea kule korea, hawezi ona kitu kinakwenda tofauti akakinyamazia tu, sasa katika harakati za kutaka kujua kwanini wanafunzi kadhaa wamepitishwa huku, aligundulika na mwalimu wake,...
"lazima tukuchunguze kwa undani zaidi.... Na utasema Wewe ni nani hapa TMA"
aliongea kamanda huyo huku sahi akiwa hana hata wasiwasi juu ya swala hilo,....
"afande, mimi nilijua wanafunzi wageni wanapita huku, hivyo nikaona ngoja niende bila kuambiwa"
"afu wewe mbona unajifanya unajua kuongea sana, kwanini"
"hapana afande, najitetea tu ili usije nihisi vibaya"
"ujinga ujinga hautaki, nitakupa adhabu sasa hivi, mhuni wewe... Endelea na mazoezi, na ole wako tukio lijirudie tena"
Aliongea kamanda huku sahi akiendelea na mazoezi kama kawaida

Baada ya masaa kadhaa, wakiwa kambini wakati huo kila mmoja keshaoga na kutulia,... Unajua kuna JWTZ NA KUNA JKT... Kwahio hapa ni JWTZ.... Ukitoka JKT ndio uje JWTZ, ila kama kwenu kunasoma vizuri Basi unakuja moja kwa moja JWTZ, ila ni zamani lakini sio kwa serikali hii ya majipu...

Sasa wakiwa kambini muda wa kupata chakula cha mchana, upande wa wanaume vyao na upande wa wanawake vyao,... Mwaju akiwa yupo ofisini kwa kamanda aliokuwa zamu ya mafunzo ya leo, aliulizwa kuhusu kijana huyo, na wakati huo mr Nyange alikuwepo akisikiliza swala hilo, kumbe jambo lile halikuishia pale mazoezini, bali kamanda kalileta kwa mkuu wa majeshi ili ajue kuna kijana anaruka ruka sana,...
"we mwaju, unamjua yule kijana"
Mwaju aliulizwa na kamanda tita, huku mr Nyange mkuu wa majeshi, akiwa anasikiliza tu,...
"hapana afande, sifahamu na pale nilikuwa namuuliza tu jina lake, mana sauti yake inafanana sana na mtoto General"
Aliongea mwaju na kumfanya General Nyange anyanyue mdomo
"Enheeee, kumbe hata wewe umejua eee,... Kiukweli tita yule kijana tofauti yake ni sura pekee, yaani kila kitu ni mtoto wangu... Mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi"
Aliongea general Nyange kwa masikitiko makubwa sana,...
"sasa, sisi tunakupa kazi,.. Mfuatilie yule kijana.. Fanya kila liwezekanalo ukiwa kama mwanamke, zijue taarifa zake, yeye ni nani, na kaja kufanya nini"
Aliongea kamanda tita huku general akimuuliza tita kuwa
"kwani wewe umejuaje kama sio wa kawaida"
"General, unajua hata wewe unaweza kumjua mwanajeshi kwa kumuangalia jinsi alivyosimama... Na mimi nimejua pale alipotaka kiruka, nikajua tu huyu sio mtu wa kawaida,.. Alikuwa anaruka kiprofesheno sana, yaani sikutegemea.. Na sikutaka ajue kama swala hilo nimelijua"
"ohoooo, basi binti, fanya kazi yako, na, mimi kama mkuu wa majeshi nitakupata nafasi muda wowote wa kuwa nae, lakini hakikisha unaleta taarifa zake hapa ndani"
"sawa afande, nitaifanya kazi vizuri"
Mwaju ana mwaka wa pili sasa toka aje hapa jeshini hivyo, ana kiwango kikubwa cha uelewa katika mafunzo, mana kabakiza miaka kadhaa tu kumaliza mafunzo na kurudi majumbani kwa ajili ya kupangiwa maeneo ya kazi... Sasa Mwaju anajikuta anaaza kazi nyingine ya upelelezi ambayo hajawahi hata kuiota katika ndoto zake,.

Wakati huo sahi alikuwa anacheza gemu kwenye saa yake,.. Kumbe sio saa ni simu tosha, kwani kuna mahari ukibofya, inafunguka na kuwa kama simu ndogo ya tachi... Na ukibofya tena inarudi kujikunja kama saa, yaani ni hatari sana pale saa hii itakapogundulika hapa jeshini,.. Ila uzuri ni kwamba saa hio inaporudi katika hali ya saa, hua inakuwa na muonekano wa kawaida sana, yaani hata uichunguze vipi huezi jua.. Ila sasa saa hio inapofika sehemu yenye kamera inapiga alarm na kuwasha miale inayo muelekeza kamera ilipo, sasa ni hatari kwa mtu mwingine kuwa nayo...

Basi sahi alikuwa akicheka na gemu, unajua uzuri ni kwamba jeshini hakuletwa kwa ajili ya upelelezi, bali jeshini kaja tu kama mwanafunzi wa kawaida ili kujiwekea nguzo katika kazi yake, usiku ulipofika sahi akiwa kalala zake, kama kawaida mwaju alipewa nafasi kubwa sana ya kutoka wakati wowote ule na hata wanajeshi waliopo lindo siku hio wanajua kuwa mwaju kapewa ruksa kutoka upande wa wanawake kwenda kwa wanaume, mana anakijua chumba cha sahi,.. Sasa ikiwa ni mida ya saa nane hivi za usiku, Sahi aliamka ili kwenda kupata haja ndogo, milango ni mingi sasa Sahi alitokea mlango wa nyuma na mwaju anakuja kwa mlango wa mbele, mana hana wasiwasi na hilo.. Lakini sasa sahi akiwa chooni, alishangaa kuona vitochi tochi vikimulika kwa mbaali sana kule nje ya uzio wa jeshi,...
"wanafunzi gani wanajifunza usiku, tena nje ya jeshi?"
Sahi alijiuliza na wakati huo mwaju ndio anafanikiwa kuingia katika chumba cha sahi,... Sasa sahi kuangalia vizuri, alishangaa geti la pembeni kuwa wazi, yaani kuna geti kuu, alafu kuna vile vigeti vya pembeni ambavyo vimezungushiwa waya ila hata karandinga la jeshi linapita bila wasiwasi,... Sasa mbaya zaidi vitochi hivyo vilikuwa vikielekea huku jeshini,.. Salehe hakuweza kulinyamazia jambo hilo, alitoka chooni kisha akaangalia walinzi wa kijeshi jinsi walivyo kaa... Alianza kukroo na ukuta, na uzuri wa sehemu za jeshi sio rahisi kuwekwa kamera,.. Huaga hakuna.. Sasa mwaju huku ndani alishangaa kukuta hakuna mtu wala nini, akatoka nje lakini pia hakumwona, alirudi katika kile chumba na kuanza kusachi,... Nia yake haikuwa kusachi, alikuwa aje kuanza kumteka hata kimapenzi usiku huu ili ajue kinachoendelea kwake, lakini kwa bahati mbaya hajamkuta mhusika, na hilo nalo ni tatizo la kutoka nje ya kambi usiku,.. Sasa uzio wa jeshi umezungushiwa waya tu, yaani zile wayameshi, sasa salehe alipoona walinzi wamekaa hovyo, aliruka juu, na kutua nje ya uzio wa jeshi,.. Hii ni hatari sana kwake, kwasababu mwanafunzi yeyote haruhusiwi kutoka nje ya jeshi bila ruhusa,....

Sasa alitembea kwa utaratibu mkubwa sana, mpaka akafika eneo la tukio,.. Sasa kumbe zile tochi sio kuwa zilikuwa zikitembea, bali ni watu walikuwa wanapikia silaha, kutoka kwenye gari ya jeshi kwenda kwenye gari la kawaida aina ya fuso,.. Sahi alitega mahali na kuangalia mwanzo mwisho mpaka wakamaliza kupakia silaha,... Sasa cha ajabu na cha kushangaza, alionekana mkuu wa majeshi mr Nyange akiwa katika eneo hilo, sahi alishangaa mno,... Mara katokea mwarabu mmoja aliokuwa kashika briefcase ya pesa na kumkabidhi mr Nyange,... Baada ya kukabiziwa pesa hizo,.. Gari la jeshi lilisukumwa mpaka kambini, yaani sio kuwashwa, bali linasukumwa kimya kimya ili watu wasishtuke
"usiondoke sasa hivi, mpaka tufike kambini ndipo nikuruhu uondoke"
Aliongea mr nyange huku makamanda wengine wakianza kulisukuma gari hilo,.. Sasa kwakuwa ni mstuni na kiza kimetanda haswa hata vile vitochi vimeshazimwa hivyo wote wakajaa kwenye gari kusubiri ruksa ya mkuu wa majeshi aseme waondoke...

Sasa kijana hajataka gari hio iondoke, alikroo mpaka chini ya gari,.. Kisha alitoa kisu kidogo sana, kisha akaanza kuchokonoa kufuli la Tools Box (box la supana).. Kweli alifanikiwa na kuingia chini ya gari, kitu cha kwanza kufungua ni propela, wakati huo majangili wapo kwenye ganasikiliza Music kwa njia ya hedifoni, hivyo hata kukuru kukuru hawawezi kuisikia....

Ghafla simu ya muarabu inaita...
"hello mr nyange"
"yes mnaweza kuondoka sasa"
Aliongea mr nyange, huku mwarabu akikubali na kusema
"ok, see you next month"
"ok, wish you a good luck"
"ok... "
Mwarabu aliwasha gari ikawaka, na hapo wapo tayari kwa kuondoka...

Sasa huku chumbani, kumbe sahi aliacha simu, na huezi amini simu yake ilionewa na mwaju, na kama unavyojua simu ya sahi ilivyo beba siri nzito ambazo anawasiliana na Mheshimiwa rais, sasa mwaju keshaipata simu hio,....
"yes, nimefanikiwa kupata simu,.. Sasa wacha nimpelekee General Nyange aichunguze"
Lakini sasa cha ajabu na cha kushangaza, mwaju aliitupa simu kitandani baada ya kuona picha juu ya screen sever, mwaju alishangaa huku akiishika tena hio simu na kuangalia hio picha kwa makini...
"huyu kijana, ana uhusiano gani na huyu mtu, mbona picha yake ipo hapa"
Mwaju Alijiuliza swali hilo huku akisema tena kuwa
"lazima General nyage mjue huyu kijana"

Je? Nini kitaendelea???..... Mwaju kaona picha ya nani kwenye simu??? Na je atafanikiwa kuifikisha simu hio???? USIKOSE

ITAENDELEA.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom