Lee
JF-Expert Member
- Jul 31, 2013
- 44,006
- 150,541
Manchester City wamedhamiria kufunga dirisha la usajili kwa kumwaga fedha kwa kumsajili Alexis Sanchez, 28, au Kylian Mbappe, 18. Pep Guardiola hatoridhika mpaka ampate Sanchez anayedhaniwa kuwa na thamani ya pauni milioni 50 au Mbappe ambaye ada yake inaweza kufika pauni milioni 100. (Daily Mail)