Makapuku Forum

Makapuku Forum

Chelsea huenda wakatumia fedha zaidi wakati Antonio Conte akitaka kumsajili Antonio Candreva, 30, kutoka Inter Milan na pia mshambuliaji wa Swansea Fernando Llorente, 32 na pia kiungo wa Everton Tom Davies, 19. (Sun)
 
Chelsea huenda wakatumia fedha zaidi wakati Antonio Conte akitaka kumsajili Antonio Candreva, 30, kutoka Inter Milan na pia mshambuliaji wa Swansea Fernando Llorente, 32 na pia kiungo wa Everton Tom Davies, 19. (Sun)
 
Chelsea vilevile wanataka kuwasajili Cedric Soares na Ryan Bertrand kutoka Southampton baada ya kumkosa Danilo na Benjamin Mendy. (Daily Star)
 
Mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 28, yuko tayari kupunguziwa mshahara ili aweze kujiunga na Manchester City. Sanchez anapenda kwenda City kuliko Bayern Munich, PSG au Juventus. (Independent)
 
Arsenal na Liverpool huenda wakaamua kumsajili Karim Benzima, 29, iwapo Real Madrid wataamua kumuuza ili kumchukua Kylian Mbappe. Hata hivyo Real huenda wakamtumia Benzima pia kama chambo kwa Monaco ili kupunguza bei ya Mbappe. (Don Balon)
 
Liverpool wanamfuatilia kiungo wa kimataifa wa Poland, Sebastian Szymanski, 18, ambaye anachezea Legia Warsaw. (Polska Times)
 
Liverpool wamewaambia Crystal Palace watoe pauni milioni 30 kumchukua beki Mamadou Sakho, 27, na kuwa hawatokubali kumtoa kwa mkopo tena. (Daily Mirror)
 
Emre Can amefikia makubaliano ya maslahi binafsi na Juventus na anasubiri dau rasmi la pauni milioni 30.4 kutolewa ili kufanikisha uhamisho wake. (TMW)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom