HISTORIA YA CHE GUEAVARA:
SEHEMU YA 01:
Ktk hii dunia kuna vitu vingi vya kustajabisha na kushangaza, lkn Mara nyingi mashujaa au watu wengi waliowahi kufanya mambo makubwa walitoka na wanatoka familia za kimaskini sn.
Mara chache sn kukuta shujaa au mtu aliefanya maajabu au mambo makubwa atoke familia yavye mihela ya kufa MTU.
Huyu jamaa GUEAVARA alizaliwa mnamo tarehe 14/05/1928 Rosario nchini Argentina. Alikua alikua mtabibu alikua mfuasi wa itikadi za kisoshalist za kari Marx.
Che anajulikana hasa kw harakati zake za kimapinduzi dhidi ya utawala wa kibepari huko America ya kusini na Africa.
Wakati akisomea utabibu , che alizunguka ktk nchi mbalimbali za MAREKANI ya kusini na kujionea mwenyewe umaskini uliopitiliza .
Alisikitishwa sana na maisha ya ufukara waliokua wanaishi wananchi wengi huku wachache wakimiliki Mali za inchi hizo. Alifikiria sn jinsi ya kubadili hali hii na kuamua Kua njia pekee ya kuleta usawa ni mapinduzi, kuondoa ufukara na umaskini ili kira binadamu angalau apate kinachomstahili ni kufanya mapinduzi hakuna namna nyingine.
.ilipofika miaka ya 50 akiwa anasomea udaktari huko Mexico huyu bwana che GUEAVARA alikutana na Fidel Castro na Raul Castro ambapo watatu hao walipanga mapinduzi ya kumng'oa Raisi wa Cuba wakati huo Fulgencio Batista amabe alikua na mahusiano ya kimaslahi na MAREKANI .
Che alipata nguvu na uaminifu mkubwa kutoka kw Fidel Castro na kupandishwa Kua kiongozi wa wanamgambo (Guerilla insurgents)
Punde tu baada ya fulgencio Batista kukimbia Cuba, che alihusika km mtu muhimu ktk serikali ya Cuba iliyoongozwa na Fidel Castro.
Akiwa km gavana wa benk kuu ya Cuba ambapo saini yake ilianza kutumika ktk noti za Cuba. Baadae km waziri wa kilimo wa Cuba .
Mwaka 1964 akiwa km mmoja ya msafara wa watu wa serikali ya Cuba ktk umoja wa mataifa aliweza kupata sifa ya mwanamapinduzi halisi wa kukumbukwa pale alipotoa hotuba ndefu ktk ukumbi wa UN akilaumu wazi ukimya wa umoja huo juu ya kilichokua kinaendelea Africa ya kusini. (Ubaguzi wa rangi) alinukukiwa akisema ...WALE WANAOUA WATOTO WAO NA KUWABAGUA KILA SIKU KW SABABU YA RANGI YA NGOZI ZAO. NI WAZUNGU WANAWAUA WATU WEUSI NA HAWAKAMATWI.
Aliendelea kusema serikali ya kikabulu inawalinda wauaji na mbaya zaidi inawaadhibu watu weusi kwakua tuu wanataka haki zao na utu wao. vipi watu hawa ( makaburu) wakaitwa watetezi na walinzi wa amani?.
Mwaka 1965 ikiwa ni miezi michache baada ya kutoa hutuba , Che alitoweka ktk maisha haya ya kawaida na hakuna aliejua Che kaenda wapi?...
Je alitowekaje?,
Je inaweza Kua hotuba aliyotoa ilimponza?, usikose...
. ITAENDELEA...........