Obe
Platinum Member
- Dec 31, 2007
- 10,282
- 35,645
Muziki: Ni Jumamosi Tulivu
Huwa hatuweki maneno Jumamosi, tunabaki kusoma ya kwenye kanga tu maana kila mmoja anakuwa ametulia nyumbani na kwa sisi tunaokaa kwenye nyumba za kupanga basi ni burudani tu, huku kunakaangwa nyama na biriani , hapa ndondo na tembele zote zikichagizwa na maneno mazuri ya kwenye kanga. Vitenge subiri mbio za mwenge ndo uvae.
Ni jumamosi wadau, nawasalimu sana na kiufupi wikend ndo inaisha hivyo. Umuhimu wako wewe kapuku hapa Jukwaani sina namna ya kuuelezea maneno yakatosheleza. Yaani ni nusu na robo jumlisha roba
Muziki sasa, leo turudi bakulutu kidogo. Nani hapendi muziki ambao ulikuwa ukipangiliwa sawia. Studio kubwa kama kiwanja cha mpira, sio studio za kileo ambazo kachumba kadogo tu kama tule tuvyumba twa pale Buguruni au Temeke basi studio inatosha kutoa muziki wa kina Diamond. Tuyaache haya usije uliza nimejuaje, hata Kigamboni si hutu tuvyumba pendwa tupo pale karibu na viwanja vya Shababi? Huwa naenda kupasha kama veteraani kwenye viwanja hivi, ondoa shaka. Ukitaka nitakupeleka, tunapasha Jumamosi asubuhi na Jpili.
Burudika na sauti-midundo mitamu ya wakongwe
Huwa hatuweki maneno Jumamosi, tunabaki kusoma ya kwenye kanga tu maana kila mmoja anakuwa ametulia nyumbani na kwa sisi tunaokaa kwenye nyumba za kupanga basi ni burudani tu, huku kunakaangwa nyama na biriani , hapa ndondo na tembele zote zikichagizwa na maneno mazuri ya kwenye kanga. Vitenge subiri mbio za mwenge ndo uvae.
Ni jumamosi wadau, nawasalimu sana na kiufupi wikend ndo inaisha hivyo. Umuhimu wako wewe kapuku hapa Jukwaani sina namna ya kuuelezea maneno yakatosheleza. Yaani ni nusu na robo jumlisha roba
Muziki sasa, leo turudi bakulutu kidogo. Nani hapendi muziki ambao ulikuwa ukipangiliwa sawia. Studio kubwa kama kiwanja cha mpira, sio studio za kileo ambazo kachumba kadogo tu kama tule tuvyumba twa pale Buguruni au Temeke basi studio inatosha kutoa muziki wa kina Diamond. Tuyaache haya usije uliza nimejuaje, hata Kigamboni si hutu tuvyumba pendwa tupo pale karibu na viwanja vya Shababi? Huwa naenda kupasha kama veteraani kwenye viwanja hivi, ondoa shaka. Ukitaka nitakupeleka, tunapasha Jumamosi asubuhi na Jpili.
Burudika na sauti-midundo mitamu ya wakongwe

