Makapuku Forum

Makapuku Forum

88a6279bf81ce31b0824214e8ae42e7c.jpg
 
YOELI 2

12.Lakini hata sasa asema BWANA ,Nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote,na kwa kufunga ,na kwa kulia ,na kwa kuomboleza

Asante Baba kutuamsha salama.tunaomba toba kwa yote tuliyokosa kwa mawazo,maneno na matendo uturehemu twakusihi.

Bariki MAKAPUKU wote mahali hapa ,tupe moyobwa kukutegemea na kukuamini na kila tunapoenda kinyume na mapenzi yako ,kwa matakwa yetu wenyewe hima tukurudievkwa kuomba,kutubu,kuomboleza ili utusamehe na tujute tusirudie yale runayozoea kutenda kwa kukusudia au bahati mbaya,tufundishe kusamehe wenzetu kama vile unavyotusamehe,asante kwa siku ya leo endelea kutuweka karibu tukufundushana kwa upendo na kuchukuliana.
fariji wafiwa,wajane,yatima ponya wagonjwa watie moyo waliovunjika moyo waendelee kukutegemea.

Asante BABA maana kila siku unasikia na kujibu maombi yetu.

Katika jina la YESU Amen

SIKU NJEMA WAPENDWA
Neno hilo hilo lipo:

Yeremia 4:1

"Kama ukitaka kurudi, Ee Israel asema BWANA , utanirudia mimi na kama ukitaka kuyaondoa machukizo yako, yasiwe mbele ya macho yangu, ndipo hutaondolewa."

Lakini pia Nabii Hosea

Hosea 12: 6

"Basi, mrudie Mungu wako ;shika fadhili na hukumu ; ukamngojee Mungu wako daima."

Kila siku neno la Mungu linatukumbusha kuwa tunapaswa kurudi kwake, tunapaswa kuwa karibu na uwepo wa Mungu.

Maisha ya mwanadamu yana changamoto nyingi sana ambazo zinamuweka mbali na Mungu..ila bado Mungu anatupenda na kutupa nafasi za kutubu..

Mbarikiwe makapuku wotee. Na mshike amri za Mungu.

Nawatakia Siku njema.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom