Muziki Maalum: Jumapili ya Baba
Wikend siandiki sana maana ni siku ya kukaa na familia, kutafakari na kumshukuru Mungu kwa yote ya wiki jana na kuomba zaidi wiki mpya. Ndicho nachofanya na leo ni siku maalum kabisa ya kumtafakari Baba, yes, father's day kwa kimombo.
Haina umaarufu sana kwetu maana sisi Baba ni baba na anakuwa nawe muda wote unapokuwa akihakikisha unalala sehemu sahihi, unapata nafasi ya kusoma unapotoka shule, na zaidi anakufundishi kuyakabili maisha kama mtoto unayehitajika na familia na taifa kwa ujumla.
Mtoto kutokujua kusoma sio kosa la baba, ila mtoto asipojua kusoma kwa sababu baba hajanunua mafuta ya taa au karabai au kulipia bili ya umeme basi hilo ni kosa la baba na tutamlaumu.
Najua kabisa humu Makapuku tupo ma-Baba tunaojitambua na kutimiza majukumu yetu, tunafanya kazi kuhakikisha wale tunaoishi nao wanakuwa na angalau furaha kila wakituona.
Ni kazi ngumu kumuelezea baba, maana yeye haitaji maneno mengi kumueleza na si mtu wa compliments kama mama😀, baba anaweza kukupa hela na usimwambie asante ila moyoni anajua umeshukuru kikamilifu. Mama atakusaidia kujua kusoma na Baba atakununulia madaftari na vitabu.
Na zaidi baba ni mtu makini kwa sababu kanichagulia mama bora kabisa.
Tumwangalie Luther Vandross gwiji la soul, mshindiwa tuzo nane za Grammy akiimba kuhusu Baba.
Happy Father's Day Makapuku wenzangu
kiongoziMuziki Maalum: Jumapili ya Baba
Wikend siandiki sana maana ni siku ya kukaa na familia, kutafakari na kumshukuru Mungu kwa yote ya wiki jana na kuomba zaidi wiki mpya. Ndicho nachofanya na leo ni siku maalum kabisa ya kumtafakari Baba, yes, father's day kwa kimombo.
Haina umaarufu sana kwetu maana sisi Baba ni baba na anakuwa nawe muda wote unapokuwa akihakikisha unalala sehemu sahihi, unapata nafasi ya kusoma unapotoka shule, na zaidi anakufundishi kuyakabili maisha kama mtoto unayehitajika na familia na taifa kwa ujumla.
Mtoto kutokujua kusoma sio kosa la baba, ila mtoto asipojua kusoma kwa sababu baba hajanunua mafuta ya taa au karabai au kulipia bili ya umeme basi hilo ni kosa la baba na tutamlaumu.
Najua kabisa humu Makapuku tupo ma-Baba tunaojitambua na kutimiza majukumu yetu, tunafanya kazi kuhakikisha wale tunaoishi nao wanakuwa na angalau furaha kila wakituona.
Ni kazi ngumu kumuelezea baba, maana yeye haitaji maneno mengi kumueleza na si mtu wa compliments kama mama😀, baba anaweza kukupa hela na usimwambie asante ila moyoni anajua umeshukuru kikamilifu. Mama atakusaidia kujua kusoma na Baba atakununulia madaftari na vitabu.
Na zaidi baba ni mtu makini kwa sababu kanichagulia mama bora kabisa.
Tumwangalie Luther Vandross gwiji la soul, mshindiwa tuzo nane za Grammy akiimba kuhusu Baba.
Happy Father's Day Makapuku wenzangu
Kesho tutakuwa nae humuKashatekwaa
AtakujaTumemsubiriaaa ajee
KwemaAisee duh
Ok Mkuu, ngoja tuupitie huo uziSalaam Team,
Natumai mu-wazima.
Naamini kuwa, humu watu ni wamoja, na kupitia huo umoja na ndio maana leo makapuku ipo hapa.
Natanguliza shukrani
Ahsante, naomba upitie halafu uniambie.Ok Mkuu, ngoja tuupitie huo uzi