Makapuku Forum

Makapuku Forum

b212fdc67efa4c2779c3a3e629f3affb.jpg
 
Katika dondoo za bbc ...


Shughuli za kibinadamu ikiwemo ukataji wa miti kiholela nchini Tanzania, wachangia uharibifu mkubwa wa mazingira.

Uchafu wakithiri nchini DRC, watu kumi na wanne wafa kwa ugonjwa wa kipindupindu

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron aibuka na ushindi wa viti vingi katika bunge la nchi hiyo

Vyombo vya Usalama nchini Mali vinasema vimeokoa zaidi ya wageni thelathini kutoka katika kituo kimoja cha Utalii, kilichokuwa kikishambuliwa na watu waliokuwa na silaha.

Maofisa nchini Nigeria wamearifu kwamba nusu ya chakula cha msaada kilichokuwa kimepelekwa kwa watu waliosambaratishwa kutoka katika makaazi yao na kundi la wana mgambo wa kiislam hakijawafikia walengwa

Nchini Uganda kuna asasi inayotoa ushauri wa masuala ya kisheria bure kwa wananchi na ili kufanikisha zoezi hilo imekuwa ikitekeleza shughuli zake kupitia mitandao ya kijamii.

Ulaji wa samaki unaonekana kupungua maeneo ya pwani ya Kenya kutokana na gharama ya juu ya kitoweo hicho
 
Salaam Team,

Natumai mu-wazima.

Kuna jambo ambalo limenishangaza kidogo, ambalo ningeomba ku-share nanyi.

Kuna hii thread Dada, uliza lolote la msingi kuhusu sisi wanaume, nitakujibu

Baada ya kuona kumekidhiri nyuzi za wadada/wanawake wengi wakiuliza maswali kuhusu sisi wanaume, maswali ambayo majibu waliyoyapata hayakujitosheleza

Hivyo, Mimi kama mwanaume, nikajitolea kuwapa fursa wanawake/wadada waniulize maswali nami ningewajibu nikiamini kwamba, majibu yangu yatawakilisha Wanaume.

Na kwenye majibu yangu nilijikita zaidi kufafanua tofaUti iliyopo kati ya sisi "Wanaume" na wavulana.

Kuna pahali nikakejeliwa, mmoja alikisema "hakufungua hata huo uzi, baada ya kuona kama una maudhui ya makapuku forums.

Nikajiuliza, kwani kuna shida gani lwenye nyuzi za makapuku forums?

Sijawahi ona tatizo nimeanza kufuatilia makapuku forum kwa muda mrefu sana.

Jambo la pili ambalo limenishangaza, ni kulaumiwa kuwa sijajibu maswali ya watu, kitu ambacho naamini kuwa sio kweli.

Kama patakua na mwenye muda, naomba ajaribu kupitia huo uzi na aniambie wapi ambapo sijajibu swali la msingi.

Ama kipi kibaya nilichoongea.

Naamini kuwa, humu watu ni wamoja, na kupitia huo umoja na ndio maana leo makapuku ipo hapa.

Natanguliza shukrani
Kamwe usiyumbishwe kwa maneno ya wafitini wewe songa mbele na kile unachokiamini
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom