Makamu wa Rais Dkt. Mpango: Kuna Mawaziri wana tuhuma za Uchawi

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,571
108,922
"Natambua kuwa Binadamu tuna Kasoro zetu na hakuna aliyekamilika 100% ila jitahidi sana Kuishi Kimaadili na kutunza Kutunza Siri za Serikali na Heshimuni Taasisi hii ya Rais hata kama hamumpendi aliyeko" Rais Samia Suluhu Hassan

Chanzo: Gazeti la Nipashe la Leo

"Nawaomba tu kuanzia sasa zile Shutuma za Rushwa Ngono tusizisikie pia. Epukeni Ulevi, Majungu na hasa hasa Uchawi bali jikiteni katika Kumuamini Mwenyezi Mungu pekee na siyo kupenda Ushirikina ambao hauna nafasi katika Serikali yetu hii" Makamu wa Rais Dk. Philip Isidory Mpango

Chanzo: Gazeti la Habari Leo la Leo

Ukiwa tu Critical Thinker kwa Kauli hizi Mbili za hawa Waandamizi Wakuu Kikatiba Rais na Makamu wake utagundua kuna Mapungufu makubwa yanayohitaji Mjadala na kwamba huenda Serikali yao inahitaji Msaada mkubwa wa Kimaombi kwa Mwenyezi Mungu (Allah) kuliko zote zilizopita.

Haya JF Great Thinkers 'tiririkeni' sasa.

 
Halafu MATAGA wala hawajali,they simply don't care.Wao kila kuitwapo leo wanapandisha nyuzi mpya kumsifia fisadi!🤡🤡🤡
She misses the suitability principle, All along not equally smothered with the necessary principle. Integrity is the bottom line to the President office bearing traits. Kula ila usile sana hakikisha isiwe rahisi mimi kujua wewe unakula sana, iba ila watu wasijue very interesting with our queen of Tooro.
 
Nimeshangaa Dr Moango kusema serikali hii haina uchawi.

Ndumba zinafanya kazi aiseee hadi wachawi hawaonekani.
Wala hajasema serikali haina uchawi. Amesema hawategemei kusikia mambo ya ndumba, meaning story za ndumba zimeshamiri kwenye ofisi za serikali mpaka imekuwa kama jambo la kawaida, ingawa serikali yenyewe haitambui mambo ya ndumba
 
Dah! Afu wakukamate umeiba kuku uje uone unavyosagwa sagwa utadhani unashambuliwa na yale ma raptors na ma stealth fighters yaani F22 na F35.

Lkn wao their stomachs are as dry as Saharan desert of which there is no rain that can quench out its thirsty.

The Mickey cattle of Africa who seem to have lost their heads.
 
Urais ni TAASISI....ni lazima awepo mmoja pale juu asimamie na kuangalia mambo....hata kama humpendi aliyeko pale juu basi IHESHIMU TAASISI NA MAELEKEZO YA SERIKALI-Mh.Rais SSH

Nini maana yake ?!!!!

Hayati mzee Karume aliwahi kusema ya kwamba MWAFRIKA ANAPOZIDI KUSOMA HUWA MPUMBAVU na ndio maana yeye huteua wasaidizi hata wasio na elimu kubwa....hapa alitufungua vyema bongo zetu kuwa ELIMU ina thamani inapotumiwa IPASWAVYO na hutegemei MSOMI akawa na haya yafuatayo:-

1)USALITI KWA KIONGOZI/VIONGOZI WAKE

2)UNAFIKI NA "NDIMI MBILI"

3)UROHO ULIOPITILIZA

4)KUINGILIA KAZI/MAJUKUMU YASIYOMHUSU

5)KUBAGAZA KIAPO KIAPO KIAPO KIAPO KIAPO


#Siempre JMT
 
Makamu wa Rais Dr. Mpango wakati akiwahutubia Mawaziri amedai kuwa kuna Mawaziri wanafanya Majungu na wengine wana tuhuma za Uchawi. This is serious. Kama Mawaziri wanafanyiana uchawi kweli tutegemee hawa hawa wataweza kutuletea maendeleo?

Imagine, kama Mawaziri wanafanyiana hivyo, vipi huko chini yao, Makatibu Wakuu, Wakurugenzi .... mpaka kwenye mashina yao. No wonder kule kwenye Maria Spaces kuna mtu amedai Maza lazima kila baada ya wiki tatu anakwenda ZNZ kuombewa dua... labda kumuepusha na hawa wa Mainland.
 
Back
Top Bottom