Makamu wa Rais Dkt. Mpango akutana na Rais Samia Ikulu ya Chamwino

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358
Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango amekutana na Rais Samia Ikulu ya Chamwino katika shughuli ya kupokea hundi ya msaada wa waathirika wa mafuriko ya Hanang ambayo mpaka sasa yamepelekea vifo vya watu 85.

Ukimya wa Dkt. Mpango takriban mwezi mmoja ulizua sintofahamu katika mitandao ya kijamii huku wengi wakidai ni mgonjwa anapatiwa matibabu nje ya nchi na wengine wakihitimisha kuwa hatuko naye duniani.

Kabla ya kukutana na Rais, Dkt Mpango alishiriki ibada ya misa Dodoma Kanisa Katoliki Parokia ya Mwenyeheri Maria Theresa Ledochowska, Jumapili leo Desemba 10, 2023. Ibada hiyo imeongozwa na Padre Dionis Paskal Safari.

Akitoa hotuba fupi kanisani, Dkt. Mpango amesema kuwa alikuwa nje ya nchi mwezi mzima kwa kazi maalum. Amesema kuwa yeye ni mzima kabisa wa afya na hajapungua hata kidogo.

Ameendelea kusema kuwa yamesemwa mengi, na wengine bado wanasema mimi ni mzuka. Amesema kuwa mitandao ni mizuri ila baadhi ya watu wanaitumia visivyo. Inaumiza watu wengi . Wapo wengi ambao wameumizwa na maneno ambayo hayana msingi, kwa hiyo tujitahidi kutumia mitandao ipasavyo kwa kumuogopa Mungu.

Kwa hiyo wale waliokuwa wanatuma picha yangu na mshumaa pembeni, wengine wanasema mzee amekata moto, bado kabisa, kazi ambayo Mungu alinituma kufanya bado sijaimaliza.




20231210_103220.jpg
 
Akiwa kanisani amesema haya


Mitandao ni mizuri ila wengine Wanaitumia Vibaya. Tuitumie kwa Kumuogopa MUNGU. Waliokuwa wanatuma picha yangu na Mshumaa pembeni, Wengine wanasema Mzee amekata moto, Kazi ambayo MUNGU amenituma kuifanya sijaimaliza. Wakati Utakapofika nitarejea kwa Muumba wangu” Philip Mpango.
 
Akiwa kanisani amesema haya


Mitandao ni mizuri ila wengine Wanaitumia Vibaya. Tuitumie kwa Kumuogopa MUNGU. Waliokuwa wanatuma picha yangu na Mshumaa pembeni, Wengine wanasema Mzee amekata moto, Kazi ambayo MUNGU amenituma kuifanya sijaimaliza. Wakati Utakapofika nitarejea kwa Muumba wangu” Philip Mpango.
Wazee wa vilinge wakina Mshana Jr na mapicha yao ya mishumaa,,, nguvu za giza zimeshindwa......... Mseminari mteule ajae
 
Nje kwa gazi gani maalum makamu wa rais? Sijawahi kusikia kiongozi mkubwa wa umma anaingia mtini kisirisiri eti kwa kazi maalum.....kukiwa na ombwe la taarifa kutoka serikalini ni lazima mitandao ilijaze ombwe hilo....kosa ni la serikali wala siyo mitandao ya kijamii
 
Waha wakizama ziwa Tanganyika wakaongea na viumbe wa huko ndani ya ziwa, hata kama umekufa unafufuka.

Halafu jamaa akipiga miksa na za Burundi
 
Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango amekutana na Rais Samia Ikulu ya Chamwino katika shughuli ya kupokea hundi ya msaada wa waathirika wa mafuriko ya Hanang ambayo mpaka sasa yamepelekea vifo vya watu 85.

Ukimya wa Dkt. Mpango takriban mwezi mmoja ulizua sintofahamu katika mitandao ya kijamii huku wengi wakidai ni mgonjwa anapatiwa matibabu nje ya nchi na wengine wakihitimisha kuwa hatuko naye duniani.

Kabla ya kukutana na Rais, Dkt Mpango alishiriki ibada ya misa Dodoma Kanisa Katoliki Parokia ya Mwenyeheri Maria Theresa Ledochowska, Jumapili leo Desemba 10, 2023. Ibada hiyo imeongozwa na Padre Dionis Paskal Safari.

Akitoa hotuba fupi kanisani, Dkt. Mpango amesema kuwa alikuwa nje ya nchi mwezi mzima kwa kazi maalum. Amesema kuwa yeye ni mzima kabisa wa afya na hajapungua hata kidogo.

Ameendelea kusema kuwa yamesemwa mengi, na wengine bado wanasema mimi ni mzuka. Amesema kuwa mitandao ni mizuri ila baadhi ya watu wanaitumia visivyo. Inaumiza watu wengi . Wapo wengi ambao wameumizwa na maneno ambayo hayana msingi, kwa hiyo tujitahidi kutumia mitandao ipasavyo kwa kumuogopa Mungu.

Kwa hiyo wale waliokuwa wanatuma picha yangu na mshumaa pembeni, wengine wanasema mzee amekata moto, bado kabisa, kazi ambayo Mungu alinituma kufanya bado sijaimaliza.

Kwahiyo wanataka kutuaminisha alikwenda kutafuta misaada ya maafa na amefanikiwa kuipata! Sidhani kama ana unabii huo wa kuota matukio.
 
Back
Top Bottom