Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,987
Makamu wa Rais, ametoa agizo hilo leo Februari 27, 2024 alipozindua Jukwaa la Kodi na Uwekezaji Jijini Dar es Salaam, ambapo amesema hatua hiyo itasaidia kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini.
Kabla ya kufungua Kongamano hilo, Dkt. Mpango alitembelea mabanda ya washiriki wa mkutano huo akafurahishwa na utekelezaji wa maboresho ya mazingira ya uwekezaji na biashara nchini na hivyo kuipongeza Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji inayoratibu na kuhamasisha uwekezaji nchini.
Katika salamu zake kwa washiriki wa Kongamano hilo, Prof. Kitila Mkumbo (Mb.), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, amesema Tanzania imekidhi vigezo vyote vya nchi inayovutia wawekezaji.
Vigezo vingine alivyovianisha ni; Uwepo wa soko kwa bidhaa watakazozalisha wawekezaji, utulivu wa kiuchumi na utulivu wa fedha kwa ujumla, uwepo wa vipaji na nguvu kazi, ubora wa miundombinu, viwango vya chini vya kodi, gharama ndogo za kuajiri wafanyakazi, Uwepo wa ardhi, na uwepo wa fedha za kugharamia miradi ya uwekezaji wa ndani.
Jukwaa la Kodi na Uwekezaji ni fursa ya wafanyabiarasha na wawekezaji kutoa maoni na kushiriki mjadala unaolenga kuibua changamoto mbalimbali za kisera, kisheria ili kusaidia maboresho ya uwekezaji na biashara nchini.