Maisha katika nyumba za kupanga

Maisha katika nyumba za kupanga

Nilipokuwa kijana nilipanga Chumba uswazi,kina Dada wakataka kunizoea mara tukusaidie kufua,nakataa,tukusaidie kupika nakataa,mara leo tumepika kisamvu hao wameshaleta ndani,nawaambia situmii.Mara naamka asubuhi nakuta wamemwaga maji yameingia mpaka ndani mwangu,kisha wanasema kaka tukusaidie kupiga deki nawakatalia.

Basi jioni moja narudi nyumbani nakuta wamefua vyupi vyao kisha wameanika kwenye mlango wa kuingia ndani mwangu.Khaaa! sikuongea na mtu,kipindi hicho nilikuwa mvutaji hasa,mara zote nilikuwa natembea na lighter,nikaiwasha nikavichoma vyupi vyao mpaka vikayeyuka,kesho yake mwenye nyumba akanipa Notice.🙂
 
Habari za leo wandugu,

Dunia hii kuna wengine hawajawahi kabisa kuishi katika nyumba za kupanga, wengine maisha ya uswazi hawayajui kabisa, basi leo nimeona tuangalie maisha katika nyumba za kupanga. Ukweli ni kuwa maisha katika nyumba za kupanga si mabaya, ni wewe mwenyewe utakavyoiweka akili yako.

Unaweza kujifunza mapishi katika nyumba za kupanga, kwani kupika wote mnapika pamoja, kama ulitoka kwenu hujui kipika chapatti, utakutana na wapangaji wenzako ambao tena wanapika chapatti za biashara, na utajifunza kukanda unga hapo. Si chapatti tu, ni mapishi mengi.

Ukitaka kuishi vizuri kwenye nyumba za kupanga usiwe mbea na mfuatiliaji wa mambo ya watu pia usipende kuanika ya kwako. Ukikuta unaongelewa wewe dharau tu, kama hujaanika sana yako watakayo kuwa wanaongea watakuwa wanahisi.

Rafiki zangu wa kiume kama watatu hivi waliniambia bikra zao zilitolewa na wapangaji wengine wakati wakiwa wadogo kwenye nyumba za kupanga, mimama isiyokuwa na haya anamsubiri mama wa kijana ametoka, ndipo kijana anapoitwa chumbani, huko anakuta ameandaliwa chai na vitafunwa na akapewa mchezo. Kama vile wale wa ushuani wanaposema bikra zimetolewa kwa ma housegirl huku kwetu kwa Mtogole kuna mengi pia yanaendelea.

Dhumuni la waraka huu ni kufahamishana dunia inavyoendelea katika nyumba hizi, kuna mengi yanayoendelea ambayo wazazi hawayafahamu. Fikiria kama hili li mama linalomuitia kijana wako chai lina magonjwa, mpaka uje uhfahamu mtoto ameathirika kabla hajafikisha miaka 20.

Siku njema.

Tena tulipokuwa wadogo ilikuwa ukitumwa soda kama ikiwa moja unaweka na chupa tupu ya ziada ili ukirudi ziwe zinagongana gongana ili kuwarusha roho, watoto wenzako, halafu zile Ice cream zetu chafu inaweza liwa na watoto wote wa mtaaa dhu ilikuwa hatari sana
 
Nyumba za kupanga ni majanga, nakumbuka nilipokuwa kwenye nyumba ya kupanga, baba mwenye nyumba alikuwa mbabu fulani hivi ni cha umbea balaa. Yeye akishaamka kazi yake ni kukaa tu barazani toka asubuhi mpaka jioni. Mgeni wangu yeyote tunayefika naye, lazima amwone na kumuuliza maswali mengi sana.

Sasa siku moja kuna mgeni wangu wa kike alikuja kunitembelea, kumsalimia tu na kabla hajaingia katika ndani mwangu, mara ooo umekuja kwa rafiki yako, ila angalieni maji hayatoki toka asubuhi, yamekatika sijui mtatumia nini?
 
Everyone wants happiness, no one wants pain, but you can't have rainbow without have a little rain.
 
Kuna m-Jaluo mmoja wa Kenya alipata kazi kwenye kampuni moja mjini, basi alipangisha huku kwetu uswaz, sasa asubuhi anamuona baba mwenye nyumba anakwenda msalani na birika bovu hivi, yule jamaa alikuwa anataka sana kujua shughuli ya lile birika kule maliwatoni.

Siku moja alipanda juu ya mnazi anamlia timing mzee, mzee aliingia na birika akatawaza, basi m-Jaluo alienda kuhadithia wenzake ofisini, nyinyi watu ya TZ mnapiga deki m***ko.
 
Ninapoishi mimi natarajia kuacha kodi... Nihame, kodi yangu inaisha mwezi wa 8 ila siku si yingi Mungu akipenda nasepa
 
Teh teh.. Mkuu kipindi hicho nimeamia uswazi nikiwa bado mgeni mgeni kuna dada alitaka kuniunguza aisee..Nikaja kupata ripoti zake kijiweni siku moja kabla ya tukio ...Kuanzia siku hiyo nikaona umuhimu wa kujichanganya na washkaji wa kitaa.. Hawa jamaa wanaripoti za matukio yote yanayoendelea kitaa..
Pole sana kupona
 
Kiujumla maisha ya kupanga si ya mchezo nimagumu na mabaya mno na waweza kuharibikiwa muda wowote ule
 
"Raha" ya nyumba za kupanga ni pale nyumba inapokuwa na familia zaidi ya sita lakini choo na bafu ni kimoja!
1486248620888.jpg
 
Dah Kuna siku ilinibid nipige show ya mchana mlango ukiwa wazi, nilibahatika kupata mgen wa kike ikabidi nimpeleke kweny geto la rafik yang, sas pale kwa jamaa nafahamika na baadh ya wapangaji Wengne, yaan Ile kuniona nafika na mgeni wangu Dah akina mama wawil bhana wa pale wakachukua nguo zao wakaja barazan kabisa na chumba na kuanza kufulia hapo. Dah nilipagawa; nikasema sio kesi sifung mlango na show napiga kam kawa, maana nikifunga tu mlango watajua tayar Mchezo ushaanza, walikuja kustuka mtt anatoka ndan anaenda kuoga, kwisha habar Yao
 
Anachamba wala haogopiii sasa angalia hiyo nyumba anayo ongelea wanapikia ukumbini,choo cha makuti,sasa nilipouliza why huyu mama yuko hivi eti anavyotaka wewe mpangaji ukipika chakula lazima umpe kibakuli chake usipompa ndio utaiona harusi ya Bibi...
Huyu mama kweli chiboko
 
nilishawahi kupanga nyumba msewe na mama mwenyenyumba anaishi hapo hapo akawa anakataza tusiingize mademu getho nikawa namshangaa sana.
Kwahiyo mkuu ulikuwa unamvizia kama hayupo na unaleta demu au mchanamchana.
 
Asubuhi mnawahi foleni ya kuoga maana bafu si ni moja..... Mwingine anaweka ndooo mwingine jiwee kila Mara anatoka kusogeza foleni take mbele
Mkuu mitaa gani hiyo maana so interesting....
 
Nyumba za kupanga zina vijambo...kuna kipindi nilikuwa nimepanga sehemu ...ni zamani kidogo sasa nikanunua gari tatu kutoka japan mbili zilikuwa za rafiki zangu walikuwa mikoani zote zilikuja kwa pamoja...sasa nilipozitoa bandarini nikazipaki hme hapo nilipopanga ......kodi wakati huo nilikuwa nalipa laki mbili nanusu...jioni yake niliporudi nikakutana na barua mama mwenye nyumba amepadisha kodi kutoka laki mbili na nusu mpaka laki tano na ya parking....balaa
 
Back
Top Bottom