Maisha bila watoto wala ndoa

Maisha bila watoto wala ndoa

Naomba kujua kwa walioamua kuishi bila bila kuoa/kuolewa maisha yao yote na bila kuwa na watoto kabisa(sio kwasababu hana uwezo wa kuzaa).

Ni mambo gani yaliwasaidia kuishi hiyo lifestyle? Umelala kwa muda gani na attention yako umehamishia wapi zaidi tofauti na ndoa/Watoto?
Attention Iko Kwa Mungu & nguvu nyingi kwenye pesa pia .
 
Kila mtu aishi maisha aliyo yachagua na anayo ona yanamfaa zaidi au yanampa furaha zaidi,

Love the life you live
Live the life you love.
Uko sahihi sana,
Lakini afrika ukishaanza kufika 25 na kuendelea maswali ya kuoa na kuwa na watoto yanakuwa mengi sana. Cha kushangaza unakuta wanaokuuliza sio ndugu wa karibu wala rafiki.
Mtu asiyekua na msaada na maisha yako kwa namna yeyote hana mamlaka ya kukushauri ndoa, anaona kama unachelewa na hata ukimwuliza ndoa yangu wewe inakufaidisha na nini ama nisipooa unapungukiwa na nini? Hawanaga majibu.

Kuna watu walikua na afya njema na mafanikio wakashauriwa kuingia kwenye ndoa, wakalost mazima.
Na kuna watu ndoa zimewafanikisha
 
Naomba kujua kwa walioamua kuishi bila bila kuoa/kuolewa maisha yao yote na bila kuwa na watoto kabisa(sio kwasababu hana uwezo wa kuzaa).

Ni mambo gani yaliwasaidia kuishi hiyo lifestyle? Umelala kwa muda gani na attention yako umehamishia wapi zaidi tofauti na ndoa/Watoto?
Bro Enendeni duniani mkazaliane, Tumia makende vizuri mzee.
 
Ukiwa kijana na afya njema uwezi kuona umuhim wa ndoa, lakini ninavyozidi kuwa mtu mzima naona kabisa maamuzi yangu ya ujanani hayakua sahihi, kuna baadhi ya wanawake hawakua smart ila walinipenda kweli ningetuliaga na mmoja kwa sababu nakiri hakuna mwanamke mkamilifu. Mwanamke wa kuwa nae uzeeni na ukiwa na mafanikio ni mashaka sana, hapo hakunaga mapenzi ya kweli ukifilisika ama ukiumwa vizuri wanakimbia.. so kama una nafasi ya kuoa ndoa ni muhimu, watoto sio muhimu saana. Cha msingi hakikisha kama huna watoto una akiba ya kutosha, jiwekeze sawasawa, mpunga ukiwepo huwezi kosa wa kukuuguza
Umenena vyema Sana mkuu
 
Nothing beyond love, ukiona unapoteza test yake kwa namna yoyote ile jibu haupo normal!

Inaweza kuwa hizo behind ndio time disturb hiyo mental yenyewe
Kutokuwa sawa hakumaanishi ni mental illness, kwa dunia ya sasa moja ya jambo gumu zaidi ni kupata mwenza wa kudumu naye, so kwa upande wangu navyoona teknolojia inavyoendelea kuharibu vijana (asilimia kubwa ya vijnana), naona ni jambo la kawaida mtu kuwa pekee. Sisemi ni sahihi ila ni kawaida. Mfano ukiangalia, dunia ya sasa, vijana wengi wa kiume wanaona ufahari kutembea na wanawake wengi kwenye maisha yao na wanawake wanaona fahari kuwa na wanaume wengi na wakubwa zaidi kwenye maisha yao, kwa mtu aliye serious kutafuta mtu wa kudumu naye ni sawa na kutafuta sindano kwenye haystack.
 
Ukiwa kijana na afya njema uwezi kuona umuhim wa ndoa, lakini ninavyozidi kuwa mtu mzima naona kabisa maamuzi yangu ya ujanani hayakua sahihi, kuna baadhi ya wanawake hawakua smart ila walinipenda kweli ningetuliaga na mmoja kwa sababu nakiri hakuna mwanamke mkamilifu. Mwanamke wa kuwa nae uzeeni na ukiwa na mafanikio ni mashaka sana, hapo hakunaga mapenzi ya kweli ukifilisika ama ukiumwa vizuri wanakimbia.. so kama una nafasi ya kuoa ndoa ni muhimu, watoto sio muhimu saana. Cha msingi hakikisha kama huna watoto una akiba ya kutosha, jiwekeze sawasawa, mpunga ukiwepo huwezi kosa wa kukuuguza
Umenena vyema mkuu
 
Hii mada nimeipenda sana... Kuna watu hapa wametumia Logic na wengine wametumia Emotions katika kuchangia hii mada. Anyway nimemuelewa sana Ambition plus kwenye comment yake no. 42
 
Back
Top Bottom