Mahojiano ya Dogo Patten na Mjini FM yazua mjadala Mitandaoni, ya muiuibua Haji Manara

Mahojiano ya Dogo Patten na Mjini FM yazua mjadala Mitandaoni, ya muiuibua Haji Manara

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,499
Wakuu!

Baada ya msanii chipukizi wa Singeli, Dogo Patten, kususia mahojiano kwenye kipindi cha Gen Talk cha Mjini FM, gumzo limeibuka mitandaoni likihusisha watangazaji na mashabiki. Tukio hilo limezua hisia kali baada ya vipande vya mahojiano kuonyesha watangazaji wakimshinikiza msanii huyo kuzungumzia masuala ya shule badala ya muziki wake, jambo lililowafanya mashabiki wengi kuhisi ni dharau na “kubully” kwa msanii mdogo mwenye umri chini ya miaka 18.

Haji Manara, mkongwe kwenye tasnia ya utangazaji, alilaani tukio hilo akisema:

"Mmeonyesha dharau kubwa kwa muziki wa Singeli na kumfanya kijana ajione ni nothing. Tokeni hadharani kumuomba radhi na muache kujipa uungu mtu hewani."




 
Tunadharailiana SANA ILA UPANDE MWINGNE wanaweza kua na nia NJEMA TU elimu ni muhimu ILA Kam DOGO kachagua mziki wamsapoti TU nasi kumpangia MTU cha kufanya HAPO DOGO atajionaa SI CHOCHOTE kitu
 
Mboni ni msikivu shida ni nini?
 
Tatizo wameshindwa kujiongeza. Dogo kaishia form 2 kaacha shule. Mwaka huu ndio ange kuwa form 4 . So dogo hakuwa tayari kuwaambia kwamba kaishia form two. Ila dogo na yeye ameanza kuvimba
 
Tatizo wameshindwa kujiongeza. Dogo kaishia form 2 kaacha shule. Mwaka huu ndio ange kuwa form 4 . So dogo hakuwa tayari kuwaambia kwamba kaishia form two. Ila dogo na yeye ameanza kuvimba
Kuvimba vipi? Eleza kidogo ueleweke mboni mimi nimeona hao maprezenta ndio wanamhutubia tena kwa kumpiga bijembe zamu kwa zamu yeye alichoongea kuvimba kipo wapi mboni hakuna hio clip?
 
Mtu kasema tu siko tayari kuzungumzia hilo na si vibaya.

Tuzungumzie mziki. Mnashuapaza shingo hao jamaa ndio wana shida, dogo anaweza kuwashinda akili.
 
Mtu kasema tu siko tayari kuzungumzia hilo na si vibaya.

Tuzungumzie mziki. Mnashuapaza shingo hao jamaa ndio wana shida, dogo anaweza kuwashinda akili.
Kwani kilichompeleka Studio zao ni kuzungumzia Muziki wake au kuzungumzia Shule anayosoma?
 
Watangazaji wale ni vilaza,sio kila swali lazima lijibiwe.
Ndo yale yale ya Diva vs Bushoke
 
Mbona me naona mashambulizi ya upande mmoja tu dogo hapewi nafasi ya kujitetea
 
Mbona sijaona video ya dogo kuongea mpaka watangazaji wakaanza kuongea hayo?
 
Interview imeonyesha, watangazaji ni wajinga halafu dogo ana akili kubwa.

Bodi ya ithibati ndio imekuja kuwaumbua hao watangazaji waliokuwa wanamshauri Dogo akasome, kumbe wao wenyewe hao watangazaji hawajasoma kufaa kufanya kazi ya kutangaza.
 
Tunadharailiana SANA ILA UPANDE MWINGNE wanaweza kua na nia NJEMA TU elimu ni muhimu ILA Kam DOGO kachagua mziki wamsapoti TU nasi kumpangia MTU cha kufanya HAPO DOGO atajionaa SI CHOCHOTE kitu
Watunzi wengi wa muziki hawana au elimu zao ni ndogo, elimu ni kipaji ndiyo sababu kila mwaka wapo wenye shahada za muziki toka vyuo vikuu lakini hawavumi.
 
Watangazaji ni hamnazo hao.

Jamaa linashauri limekunja sura kabisa
 
Watanzania wengi ni vichaa. Mirembe waanzishe tawi ktk kila mkoa.
 
Back
Top Bottom