Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Nasikia kuna uvumi kwamba, Sitta ndo anaonekana msafi kidogo. Ikitokea JK hakubaliki mwakani Sitta ndo wanataka awe mbadala. Nawakilisha.
 
Nasikia kuna uvumi kwamba, Sitta ndiye anaonekana msafi kidogo ndani ya chama. Ikitokea JK hakubaliki mwakani Sitta wanataka awe mbadala. Nawakilisha wakuu.
 
Nafikiri labda ungejifunza uzuri katiba ya CCM. NEC ndio kikao kikuu, kilichopo kidemokrasia, na ni sahihi kwa kufanya hivyo ilivyofanya.
Mkuu Pakacha, sijazungumzia ukuu wala uhalali wa kikao hicho kuzungumzia issue hiyo. Ninachokizungumzia ni matumizi busara kwenye approach waliyoichukua ili kufikia lengo bila kutumia nguvu nyingi.
Ni kweli kuwa NEC ndicho kikao sahihi kabisa kufanya walichofanya. Lakini kwa ajili ya matokeo mazuri zaidi, wangeweza kuongea nae offline (if you know what I mean). Badala yake, ni kufuata taratibu kama walivyofanya na kupata political damage inayokuja.
 
Hakika chama kinaenda kubaya nadhani ss wanasoma maandishi ya ukutani lakini wanayapuuza. Licha ya Spika kujaribu kuikwamua Serikali pale inapolemewa lakini bado inaonekana anakiua chama. Ama kweli tafsiri rahisi la neno "chama" ni genge la wahuni lenye nia moja na lengo moja la kuzichonya raslimali za nchi fulani kwa malengo ya kunufaisha matumbo yao, familia zao, ndugu zao, wakwe zao kwa namna yeyote ile kama, fitna, kuua kwa ajali za kupanga hata sumu.
Cha muhimu km waraka wa katoliki unavyotuhimiza mabadiliko ya katiba ni muhimu. Spika asiwe na chama. Tangu lini refarii anatoka timu pinzani. Hii itasaidia kushindwa kubanwa na genge la wanachama wa chama.
 
ila ukumbuke kura zao nyingi zinatoka kule kijijini kwenu ambako usafiri ni wa kutumia trecta na sukari mpaka ww ukienda likizo ndo uwapelekee.

Mkuu hili ndio tatizo kubwa na udhaifu ambao unatumiwa na mafisadi kuendelea kutunyonya kila wanavyopenda. Nashindwa hata kuamini jinsi CCM ilivyopata hata kura Biharamulo. Sielewi ni kwanini watu wanaipigia kura CCM wakati hakuna hata matumaini ya siku moja wao kubadilika na kuwa na maisha bora.
Mrema alisema siku moja watu miguu peku, suriali chakavu na makalio nje lakini wanasema idumu CCM.
Kuna haja ya kudelegate haki yetu ya kufanya maamuzi. Tuwape madraka watu wachache ambao wanaweza. Kutuchagulia watu wanaofaa kuongoza, kuliko wale wanohongwa pilau, sukari, T-shirt au mafuta ya kupikia.
 
Mabadiliko katika jamii ni hatua (process) ambayo lazima kuwepo watu wa kujitoa mhanga ili vizazi vijavyo viishi katika hali nzuri. Kama Sitta atazimwa na CCM na akapotea kwenye uringo wa siasa zetu, ameshapanda mbegu. Tuombe mbegu ikuwe wengine wajitoe, hasa hasa ili katiba yetu ibadirishwe wawepo wagombea binafsi, CCM itageuka kichuguu.
 
Wakuu njia mbadala kuwang'oa hawa mafisadi katika chama ni kutumia haki yetu ya msingi na ya kikatiba kutoa elimu kwa raia wakiwemo ndugu zetu,marafiki zetu na jamii nzima inayo tuzunguka sisi wenyewe tuwe mfano wananchi wakiwakataa hawa basi na hakika tutashinda hawa jamaa wapo wachache sana na wanatumia pesa kwa kununua haki yetu ya kikatiba tuwakatae sasa hivi tuseme sasa basi mwisho hizo flana na kofia mnazo gawa bure tuzikatae jamani yaani unauza uhuru na haki yako kwa kofia ya 2000/= kweli? Akina mama mnanunuliwa kwa Khanga za 4000/= kweli?? Jamani najisikia uchungu sana najua na ninaelewa nyote mna ndugu vijijini anzeni leo kuwaelimisha ndugu zetu wasikubali hawa wakoloni weusi watupande kichwani sasa mwisho na wakomee hapo hapo tuwakatae tusicheke nao tunavyo zidi kuwapigia makofi ndo wanazidi kutuumiza kwa miaka 5 tena jamani tunahitaji mabadiliko elimisheni ndugu zetu huko vijijini ndiko wanadanganyika sana kwa kununuliwa Pombe mikutanoni na baadae anauza haki yake kwa Pombe jamani inatia uchungu sana hawa jamaa sasa basi maana wakiwalaghai wao wanakuja kuishi Dar es salaam.
 
Nasikia kuna uvumi kwamba, Sitta ndiye anaonekana msafi kidogo ndani ya chama. Ikitokea JK hakubaliki mwakani Sitta wanataka awe mbadala. Nawakilisha wakuu.

Na hii inaonekana ndiyo inayompa shida muungwana kwani hana uhakika wa kupata support ya asilimia 80 ndani ya chama kama kuna mtu strong na msafi kiasi kama Sita.Kwa kweli inasikitisha sana mahali CCM imefika na kama hawatajirekebisha hakika wanachungulia kaburi kama chama cha KANU - Kenya.

Wakati huu ni muda muafaka kwa wapenda mageuzi wote kupanga mikakati ya namna ya kiukiondoa CCM madarakani 2010 kwa kuwa kama chama kimeonyesha wazi hakiko kwa niaba ya wananchi wala kutetea maslahi ya watanzania walio wengi bali kiko kwa niaba na maslahi ya mafisadi.

Kwa mtanzania yoyote mwenye akili timamu hatachagua kiongozi yeyote yule toka CCM kwenye uchaguzi ujao kwani kwa kufanya hivyo atakuwa analiangamiza Taifa.

Huu ndio wakati muafaka wa kufanya mageuzi na kwa kuanzia tuanze na kuwaelimisha wananchi kabla hawajashiriki kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.Kuanguka kwa CCM kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa itachangia sana mwamko mpya wa kuleta mageuzi kwenye uchaguzi mkuu wa 2010.
 
=Recta;555458]Mkuu Pakacha, sijazungumzia ukuu wala uhalali wa kikao hicho kuzungumzia issue hiyo. Ninachokizungumzia ni matumizi busara kwenye approach waliyoichukua ili kufikia lengo bila kutumia nguvu nyingi.


Binafsi sioni tatizo lolote kwa hiki walichokifanya. Kazi kubwa ya NEC ni kuhakikicha uhai wa chama unalindwa. Sasa kama Sitta kwa kutumia mamlaka ambayo pia ameyapata kupitia kwenye chama chenyewe anaanza kukidhoofisha, ni halali ashughulikiwe. Naona wamepotoka sana kutomwajibisha. Ama akae kwenye chama na kushirikiana na wenzake au arudishe kadi. Hawezi kuwa popo; awe CCM na wakati huo apambane na wanaCCM wenzake kwa kivuli cha ufisadi. Huko ni kukidhoofisha chama na hawezi kuruhusiwa kufanya hivyo kama kweli chama kina watu makini (kwa mtazamo na malengo yao)!


Ni kweli kuwa NEC ndicho kikao sahihi kabisa kufanya walichofanya. Lakini kwa ajili ya matokeo mazuri zaidi, wangeweza kuongea nae offline (if you know what I mean). Badala yake, ni kufuata taratibu kama walivyofanya na kupata political damage inayokuja.

Hili linaweza kujadilika kwa sababu wajumbe wameshindwa kutimiza wajibu wao. Huyu alitakiwa kupewa adhabu kali ili liwe fundisho kwa wengine. Mifano ya akina Jumbe, Maalimu Seif and Mrema ilifaa kutumiwa. Jambo la msingi ni kuwa lazima chama kiwe na watu wenye lengo moja. Kama kuna wenye lengo (au malengo) tofauti na wegine (tena walio wengi) basi wakatafute jukwaa jingine!
 
Mkuu Pakacha, sijazungumzia ukuu wala uhalali wa kikao hicho kuzungumzia issue hiyo. Ninachokizungumzia ni matumizi busara kwenye approach waliyoichukua ili kufikia lengo bila kutumia nguvu nyingi.
Ni kweli kuwa NEC ndicho kikao sahihi kabisa kufanya walichofanya. Lakini kwa ajili ya matokeo mazuri zaidi, wangeweza kuongea nae offline (if you know what I mean). Badala yake, ni kufuata taratibu kama walivyofanya na kupata political damage inayokuja.
Angalia upande wa pili wa shilingi. Kwa nini Bw. Sitta anatumia Bunge kutoa mambo mazito mazito yenye kukifadhaisha Chama chake, badala ya kutumia busara kwanza kuziibua hizo issue katika lujna yao CC- ambapo yeye ni mwanachama tena mwenye nguvu -kwa nini ameidharau CC halafu wewe unataka afanyiwe busara na CC hiyo hiyo.?
 
Asubuhi leo nimewasikia wale vijana wa Clouds FM wakimkejeli mtu (bila kumtaja jina) radioni, wanasema ''....kama unaona vipi rudisha kadi, sio kusemasema tu watu oooh mafisadi...., sasa unaomba huruma,...oooh nisameheni mzee mwenzenu....!'' Sijui huwa wanatumwa na nani wale vijana!

Na TBC radio kipindi cha asubuhi wakamtoa Chiligati akisema ''.....kama mtu hawezi kuwa na nidhamu ya chama, anataka kuzungumza bila utaratibu kama mlevi, arudishe kadi yetu akajiunge na chama kingine cha walevi wenzie...!"

Baada ya kupitia hii thread na kusoma magazeti ndio nimepata picha halisi kuhusu anayesemwa, lakini hakika nashangaa sana nchi hii inakopelekwa. Inahitajika sadaka ya ajabu kuepusha mustakabali huo wa hatari, na ninatamani hawa akina Sitta na wenzake wangekuwa na ujasiri huo.
 
Wajameni?

Me napenda kuwarudisha nyuma kidogo tu, mjue kuwa nda ya CCM yetu kuna watu wakufikia,kuna watu wakuletwa, kuna watu waoo ndio wananiita washika dau,kuna watu wao ndio ati waasisi na kuna watu wanao taka mapinduzi kweli ya dhati tokana na nyakati, na kuna watu wao hawajui kitu wao ni kufuata upepo na kuna watu wao hawataki kukubali kuwa ni muda wa mageuzi umefika na alama za nyakati ndizo zinataka kuchukua nafasi yake na ndio wanafiki. pili kuna hawa wenzangu UV-CCM sijaona kabisa msimamo wao wa jumui yao kama vijana na wanakauri mbiu gani ya 2010 wao ukiwachunguza san kuanzia ngazi za mashina,twawi kata,wilaya, mkoa hadi halimashauri kuu taifa ukweli ni kwamba twapigana majungu fitina chuki na ndipo hapo mtaona wazeee mpaka leo wanaendelea kutawara nchi kwa wanavyo taka kama mwabisha niambieni kuanzia umri miaka 25 hadi 40 ni asilimia ngapi yao wameshika nyadhifa zile za hali ya juu kabisa na wamezitendea haki na kuwa weka sawa vijana wenzao ktk mageuzi ya kisiasa, kiuchumi na kidemicrasi ya haki???

Sasa leo CCM wamesahau lile tamko lililotolewa miaka ya nyuma na Hayati Horce Kloimba "CCM IMEKOSA DIRA" lile jinamizi ndilo sas linawarudi hawakutaka kukubaria na na ule usemi kweli hawa hawa viongozi walikuwepo madarakani kipindi icho na hao hao sasa wanarumbana kwasababu hawakukubali kutambua kuwa hawakuona mwelekeo wa dira ya chama chao i mean alama za nyakati hawakuziona na ndizo hiz sasa zawatokea mbele yao na itawa tia aibu kweli kweli,

Leo Sitta kuonyesha makali ndani ya bunge kuanza kuweka msimamo wa bunge kumbe ndani huko bungeni kuna wana CCM wanayao mambo hawataki kabisa kukubali alama za nyakati ndizo zimefika.

Sitta me nakuunga mkono kanyaga buti kwani watanzania wanaona kipi ni bora na kipi ni kibaya.mapinduzi yaja na ndio hayo yameanza wanafiki hawataki.

Sitta kanyaga buti twende huo ndio mwanzo
 
Inasikitisha kuona uongozi katika nchi yetu ukiwa kwenye hali mbaya kiasi hiki. Kinachosikitisha zaidi ni kiburi cha hao watawala kutoona kuwa wamekosa mwelekeo na wameishiwa kabisa busara za kuwa viongozi, na wananchi kwa upande mwingine kutojua nini wafanye. Kuna watu wana mawazo kuwa wao ni kwa ajili ya kuwa watawala na wana haki na kitu chochote katika nchi hii, wanaweza hata kuja nyumbani kwako na kuamua nini wachukue hata kama ni mke, binti, mume na chochote watakachokitaka, simply kwa sababu wao wapo kwenye tabaka la CCM. Wanaona UCCM unakuja kwanza kabla ya UTANZANIA, na yeyote anayetaka kuingia kwenye nyendo zao watatumia gharama yoyote kumwangamiza. Hii ni hatua mbaya sana. Sasa nadhani wanatumia ule msemo wa Dan Corleone "Give them an offer they can't refuse....". Hii ni mafiatic style ya uongozi.

Uhuru wazee wetu walioudai wa kuweza kujiamria mambo yetu, kumiliki rasilimali zetu ulidaiwa kwa ajili ya kundi fulani tu katika nchi hii, inasikitisha tulimuondoa mkoloni wa kutoka mbali tukapandikiza wa kwetu ambao ni wabaya zaidi. How far can these people go? wewe na mimi hatuwezi kujua, lakini tuelewe kuwa tunakoelekea ni kubaya zaidi.

Ubovu katika utawala wa nchi, umeelekea kwenye sekta nyingi tu katika nchi hii. Kwa mfano ni vigumu kuiamini habari yoyote inayotoka katika chombo cha habari kwa sasa bila kujua chombo hicho cha habari kina maslahi gani kuhusu au kinyume na habari hiyo. Nina mashaka hilo lipo kwenye sekta nyingi nyingine.

Kwa nini tuache mambo haya yaendelee? Tusipofanya kitu haya mambo yataendelea kutusumbua siku zote, wakifa wao watawaachia vilaza watoto wao na wajukuu wao. Kama hatufanyi lolote tunaonekana pia sehemu ya tatizo hili. Ukielimisha jamii yako ya karibu kuhusu wajibu wao kwa kupandikiza uongozi wenye kuwajibika kwa watu wao na sio kwa CCM au chama tutakuwa tumechukua hatua moja kwenda njia sahihi.

Hivi kuwa CCM ni kitu cha maana sana? kwa sasa naweza kusema kuwa waoga ndio wanaoshabikia na kulilia kubaki katika chama hicho, kwa sababu hawana ujasiri wa kupambana kwa hoja, bila kulindwa na fedha za mafisadi. Historia inatuonyesha kuwa majasiri wamepenya wakiwa na limited resources, wengine wamepiga kampeni kwa kutumia baiskeli bila support ya bendi na vitu kama hivyo mwishoni wakaprevail. nadhani tuondokane na dhana kuwa haiwezekani, mbona Karatu, Kigoma (hizi zote haziko mjini wananchi waliweza kupokea ujumbe wa mabadiliko?)
Ni muda kama Sita na wenzake wanaotaka kutusadikisha kuwa wana nia ya dhati ya kupambana na hawa wahuni, wajitoe ili wasiendelee kuchafuka. Wananchi watawapa support na watarejea kwa ujasiri mkubwa kupambana na hilo genge.
 
Haiwezekani, Ingawa simfagilii sita na kundi lake la mashujaa lakini hii itakuwa imevuka mipaka. Kwa sababu hawa jamaa ingalau wanfanya ifikapo 2010 nchi iwe na mtaji bila wao kwa sasa jamaa wangemaliza nchi kabisa na Rais mpya atakapo kuja atakuta hamnakitu

jamani ni lazima tufanye kitu na tusisubiri tufanyiwe kitu
 
Asubuhi leo nimewasikia wale vijana wa Clouds FM wakimkejeli mtu (bila kumtaja jina) radioni, wanasema ''....kama unaona vipi rudisha kadi, sio kusemasema tu watu oooh mafisadi...., sasa unaomba huruma,...oooh nisameheni mzee mwenzenu....!'' Sijui huwa wanatumwa na nani wale vijana!

Na TBC radio kipindi cha asubuhi wakamtoa Chiligati akisema ''.....kama mtu hawezi kuwa na nidhamu ya chama, anataka kuzungumza bila utaratibu kama mlevi, arudishe kadi yetu akajiunge na chama kingine cha walevi wenzie...!"

Baada ya kupitia hii thread na kusoma magazeti ndio nimepata picha halisi kuhusu anayesemwa, lakini hakika nashangaa sana nchi hii inakopelekwa. Inahitajika sadaka ya ajabu kuepusha mustakabali huo wa hatari, na ninatamani hawa akina Sitta na wenzake wangekuwa na ujasiri huo.

Hawa Clouds ni mashabiki wasiojua chochote. Ni rahisi sana kuwatumia kama unapenyeza hoja yako kinamna (kwa mpangilio na fedha kidogo). Laiti wangefahamu wanachokishabikia wangenyamaza kimya
 
Ngoma ikilia sana hupasuka, hata huyu mnyama CCM sasa anapwaya, anaonekana kuwa kenge tu kwenye msafara wa mamba. Watanzania wamekata tamaa na sasa hivi wanatafuata 'mwokozi'. kadi yetu ya mpiga kura ni ya muhimu sana 2010!! Lets all say 'NEVER AGAIN' CCM!

acha walindane nasi tunajilinda wenyewe
 
Pakacha,
Mkuu hakuna serikali yoyote inayoweza kumhukumu Msika wake kwa sababu analitumia bunge kuwaadhibu viongozi wa chama chake ambao wanakiuka ilani za chama...Spika hayupo bungeni kuwakilisha chama isipokuwa kusimamia vikao vya Bunge kwa uwazi..ni kama hakimu ambaye pamoja na kuwa ni mwanasheria basi mnataka lazima awe upande wa district Attoney ktk mashtaka yote...
Nina hakika kabisa kuwa Demoktratic hawana uwezo wala nguvu ya kumnyang'anya kadi ya chama Nancy Pelosi kwa sababu tu anapingana na baadhi ya senata wa chama chake.
Binafsi sijaona kifungu wala sehemu ambayo inamweka Sitta hatiani kwa kushambulia viongozi wabaya ndani ya chama. Hajawahi kusema wala kuhoji katiba, ilani na mwongozo wa chama chake akiwa bungeni..
Mkuu wangu kumkataa Sheikh au Padre fulani haikuondoi ktk Uislaam au Ukristu...Ila nachoweza kusema JK anawachezea CCM sasa hivi. Kwa kuleta mada hii ktk kikao cha CC, JK anataka kuwajua wote waliosimama upande wa pili na walivyokuwa wajinga samaki wengi wameivaa ndoana yake. Leo hii JK anawafahamu wote waliosimama upande wake au wa Lowassa. Kazi imekwisha kilichobakia ni kuifanyia kazi report nzima na ndio maana Mzee wetu Mh. mwinyi anaifanyia kazi..
 
Pakacha,
Mkuu hakuna serikali yoyote inayoweza kumhukumu Msika wake kwa sababu analitumia bunge kuwaadhibu viongozi wa chama chake ambao wanakiuka ilani za chama...Spika hayupo bungeni kuwakilisha chama isipokuwa kusimamia vikao vya Bunge kwa uwazi..ni kama hakimu ambaye pamoja na kuwa ni mwanasheria basi mnataka lazima awe upande wa district Attoney ktk mashtaka yote...
Nina hakika kabisa kuwa Demoktratic hawana uwezo wala nguvu ya kumnyang'anya kadi ya chama Nancy Pelosi kwa sababu tu anapingana na baadhi ya senata wa chama chake.
Binafsi sijaona kifungu wala sehemu ambayo inamweka Sitta hatiani kwa kushambulia viongozi wabaya ndani ya chama. Hajawahi kusema wala kuhoji katiba, ilani na mwongozo wa chama chake akiwa bungeni..
Mkuu wangu kumkataa Sheikh au Padre fulani haikuondoi ktk Uislaam au Ukristu...Ila nachoweza kusema JK anawachezea CCM sasa hivi. Kwa kuleta mada hii ktk kikao cha CC, JK anataka kuwajua wote waliosimama upande wa pili na walivyokuwa wajinga samaki wengi wameivaa ndoana yake. Leo hii JK anawafahamu wote waliosimama upande wake au wa Lowassa. Kazi imekwisha kilichobakia ni kuifanyia kazi report nzima na ndio maana Mzee wetu Mh. mwinyi anaifanyia kazi..

Mkandara umenifurahisha sana (red colour). JK atakuwa kichaa endapo anaweza kufanya mchezo hatari kama huo. Ana mfumo wa kumtosha kujua yupi yuko upande gani na kwa hiyo hana sababu ya kuleta mtafaruku kwenye kikao ili kupata hiyo taarifa.

Hata hivyo sikubaliani na wewe kwenye hoja kuwa Sitta hajachemka kukidhoofisha chama. Kushambulia wenzio wakati mko kwenye mapambano ni kuleta dhahama! Sitta anajua Chama chake kinasimamia nini na kwa hiyo hawezi kuanza kutafuta ustaa kwenye mchezo kwa kuwaangamiza wachezaji wa timu yake mwenyewe. It doesn't make sense and for that matter he is a looser!
 
Nami naunga mkono Six angegoma kuomba msahama.....wamfukuze awe shujaa wa ufisadi,....kuliko kuomba msamaha....awe kibogoyooo maana yake nini??hakuna kitu aisee nchi hiii imekwisha na haifai tena

Mbona Mrema alingatuka then Mbona hamkumpa USHUJAA?? Kumbuka sisi watanzania ni watu wa ajabu sana. Tutaongea tuuuu hapa ng,atuka sijui nini akitoka akafulia mtaanza kumponda. Well amejitahidi sana lakini kwa jinsi hali ya kisiasa ilivyo nafikiri what he did was right.
 
Back
Top Bottom