The Khoisan
Platinum Member
- Jun 5, 2007
- 18,639
- 18,272
Angalia upande wa pili wa shilingi. Kwa nini Bw. Sitta anatumia Bunge kutoa mambo mazito mazito yenye kukifadhaisha Chama chake, badala ya kutumia busara kwanza kuziibua hizo issue katika lujna yao CC- ambapo yeye ni mwanachama tena mwenye nguvu -kwa nini ameidharau CC halafu wewe unataka afanyiwe busara na CC hiyo hiyo.?
Mzee sikubaliani nawe hata kidogo. Sitta anatumia busara zake kuliendesha bunge la kidemokrasia bila upendeleo. After all, Sitta siyo muibua scandles ndani ya bunge ila ni wabunge wenyewe na yeye anachofanya ni kusimia ili wasije vunja sheria au vuka mipaka ya kazi zao. Ingawa spika amewekwa kulinda maslahi ya CCM lakini huwa naye ana mipaka yake. Kama maji yanazidi unga wanategemea yeye afanye nini????
CCM na CC yao ndiyo ambao hawatumii busara na wanawasukuma NEC kwa vile kuna midabwda mingi kule ambayo kazi zao ni kufuata posho na mlo Dodoma.