Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Мкuu unamaanisha nini hapa?

Lowassa anataka kusafishwa ili awe tayari kutwaa madaraka makubwa ya nchi hii. Bunge la juzi lilizidi kumuangamiza baada ya kuikataa report ya serikali ya utekelezaji wa mapendekezo ya Bunge yaliyotokana na Kamati Teule ya Mwakyembe. Kitendo cha Bunge kung'ang'ania kwamba serikali haijatekeleza lolote ilikuwa inaonyesha kwamba waliowajibika kwa kujiuzulu walikuwa na makosa. Lakini kama ile report ya utekelezaji ingekubalika, basi Lowassa angepata nguvu ya kujenga hoja kwamba alionewa na hivyo yuko clean.
 
Mimi mshangao wangu siku zote ni pale watu wanapoendelea kuwaamini kwamba unaweza ukakata mti ulioukalia na bado ukabaki salama. Kama wewe unafikiri ni shujaa na unapambana na ufisadi ni sharti utoke CCM. Huwezi kupambana na ufisadi halafu ukabaki CCM. The logic is simple. Ufisadi na dhuluma ndio unaoendelea kuiweka CCM madarakani. Ndio kusema unapopambana na ufisadi unapambana na CCM, unataka kuiangusha CCM, hapa lazima utakwama. CCM haiwezi ku-survive bila ufisadi, dhuluma, uongo, ubabaishaji, umantimanyongo, n.k.

Hawa ndugu zangu wana options mbili: to walk out of CCM or to shut up! Lazima wachague sasa, vinginevyo waache kutuzuga.

Na watanzania wenzangu narudia wito wangu wa kila siku. Kama kweli tunachukizwa na ufisadi na mwenendo katika nchi, hatuna njia ya kumaliza hayo zaidi ya kuachana na CCM. Kuendelea kuikumbatia CCM ni kuendelea kukumbatia hayo yote. Unless tumezoea kulalamika na tunaogopa tukiitoa CCM kwamba tutakosa cha kuongea vijiweni na pengine itabidi JF ifungwe maana tutakuwa tumefilisika kihoja, lazima tudhamirie kuachana na CCM katika uchaguzi ujao.
 
Mimi mshangao wangu siku zote ni pale watu wanapoendelea kuwaamini kwamba unaweza ukakata mti ulioukalia na bado ukabaki salama. Kama wewe unafikiri ni shujaa na unapambana na ufisadi ni sharti utoke CCM. Huwezi kupambana na ufisadi halafu ukabaki CCM. The logic is simple. Ufisadi na dhuluma ndio unaoendelea kuiweka CCM madarakani. Ndio kusema unapopambana na ufisadi unapambana na CCM, unataka kuiangusha CCM, hapa lazima utakwama. CCM haiwezi ku-survive bila ufisadi, dhuluma, uongo, ubabaishaji, umantimanyongo, n.k.

Hawa ndugu zangu wana options mbili: to walk out of CCM or to shut up! Lazima wachague sasa, vinginevyo waache kutuzuga.

Na watanzania wenzangu narudia wito wangu wa kila siku. Kama kweli tunachukizwa na ufisadi na mwenendo katika nchi, hatuna njia ya kumaliza hayo zaidi ya kuachana na CCM. Kuendelea kuikumbatia CCM ni kuendelea kukumbatia hayo yote. Unless tumezoea kulalamika na tunaogopa tukiitoa CCM kwamba tutakosa cha kuongea vijiweni na pengine itabidi JF ifungwe maana tutakuwa tumefilisika kihoja, lazima tudhamirie kuachana na CCM katika uchaguzi ujao.

Tatizo hapa Mkuu ni kwamba tulioko JF hatutoshi kuifanya CCM ishindwe kwenye kura. Sasa huwa najiuliza ni nini tukifanye ili hata yule mkulima wa pale katahoka-Biharamulo awe na mawazo ya ki-JF?
 
Mimi mshangao wangu siku zote ni pale watu wanapoendelea kuwaamini kwamba unaweza ukakata mti ulioukalia na bado ukabaki salama. Kama wewe unafikiri ni shujaa na unapambana na ufisadi ni sharti utoke CCM. Huwezi kupambana na ufisadi halafu ukabaki CCM. The logic is simple. Ufisadi na dhuluma ndio unaoendelea kuiweka CCM madarakani. Ndio kusema unapopambana na ufisadi unapambana na CCM, unataka kuiangusha CCM, hapa lazima utakwama. CCM haiwezi ku-survive bila ufisadi, dhuluma, uongo, ubabaishaji, umantimanyongo, n.k.

Hawa ndugu zangu wana options mbili: to walk out of CCM or to shut up! Lazima wachague sasa, vinginevyo waache kutuzuga.

Na watanzania wenzangu narudia wito wangu wa kila siku. Kama kweli tunachukizwa na ufisadi na mwenendo katika nchi, hatuna njia ya kumaliza hayo zaidi ya kuachana na CCM. Kuendelea kuikumbatia CCM ni kuendelea kukumbatia hayo yote. Unless tumezoea kulalamika na tunaogopa tukiitoa CCM kwamba tutakosa cha kuongea vijiweni na pengine itabidi JF ifungwe maana tutakuwa tumefilisika kihoja, lazima tudhamirie kuachana na CCM katika uchaguzi ujao.

Nakusupport kwa hili lakini changamoto kubwa tutaiondoje CCM na tume ya uchaguzi inafuata matakwa ya mafisadi walioshika nchi hii
 
Kwa kweli Muungwana anaiangusha chama. Anashindwa kukemea maovu, inawezekana ana sababu maalum labda atarekebisha haya yote baada ya kuwa na uhakika na kurudi 2010.

Uchanguzi 2010 unamtia hofu ndio maana kwa mara nyingine ana SIDE na waliomweka madarakani.

Mimi ndo maana nampenda EL, Edward ni kiongozi shupavu anakisimamia anachokiamini.

Zuma (EL) atarudi tu!!!!!!!!!!!!!!

Bora Zuma kuliko Muungwana hasa kwenye MSIMAMO.
 
Haya,

Tunaomba sasa kujadili hoja zingine (agenda zingine)... maana kwa wabongo hoja zinazohusu watu na mipasho ndio hoja!
 
Gazeti la Mtanzania leo leo linaripoti kuwa Sita ameomba msamha ili kujinusuru asifukuzwe uanachama. Kama kweli Sita ameomba msamaha maana yake ni kwamba yeye si msafi. Ni miongoni mwa mafisadi waliopo ndani ya CCM. Nimewahi kudokezwa na mfanyakazi wa Baraza la mitihani kuwa mtoto wa Sita aliwahi kupewa tenda ya kutoa matokeo ya kidato cha nne au sita? kwa njia ya message za simu za viganjani bila kufuata sheria ya manunuzi. Tenda hiyo ilitolewa wakati mke wa Sita akiwa Waziri wa Elimu!! Yawezekana anahusika na ufisadi mahali pengi. Sasa asipoomba msamaha si ataumbuliwa na yeye?
 
- Worry who? Six? hapana he is just fine, the last thing Mtandao wanaweza kufanya ni kumchokonoa Six, kwenye one on one level hawawezi ku-afford hilo Spika ambaye amewapa wabunge wa sasa malipo ya ajabu sana, hawana ubavu wa kumgusa,

- Labda wakamkabe koo kwenye kugombea ubunge ambako the dataz ni kwamba wako naye huko sambamba sana, CCM haiwezi kummyamg'anya kadi a sitting Spika, ambaye amemsaidia sana Muungwana kumuondoa adui yake namba moja EL na besides,

- Kumnyanga'anya kadi Six, no! Muungwana does not operate that way kwa sababu itakwenda against the rules za ku-maintain popularity yake, ndio maana Msekwa alirudishiwa mlo.

Respect.

FMEs!

Thanks FMES, what you say is really encouraging and i hope it turns out to be!!

Pamoja sana
 
Kwa kweli Muungwana anaiangusha chama. Anashindwa kukemea maovu, inawezekana ana sababu maalum labda atarekebisha haya yote baada ya kuwa na uhakika na kurudi 2010.

Uchanguzi 2010 unamtia hofu ndio maana kwa mara nyingine ana SIDE na waliomweka madarakani.

Mimi ndo maana nampenda EL, Edward ni kiongozi shupavu anakisimamia anachokiamini.

Zuma (EL) atarudi tu!!!!!!!!!!!!!!

Bora Zuma kuliko Muungwana hasa kwenye MSIMAMO.

Sawa Mangi!!! umesomeka....
 
Jamani hiyo kazi anayoifanya Sitta ni ya chama cha mapinduzi,kama tunavyosema ufisadi tunaupinga wote bila kujali chama.
Mzee Sitta kaza buti tuko pamoja katika kujenga chama kipya kisichokuwa na mafisadi.
 
sina hakika kama hiki ndiyo chama cha mzee wa kizanaki alichokihasisi? Taarifa zilizopo wazee ambao wangekemea maovu ya chama wanarambishwa peremende na mafisadi! wasomi wa bongo nao wamebaki kulalamika tu no action! katika mabadiliko yoyote lazima wachache wajitoe mwanga.sita alitakiwa kusimamia anachokiamini kwa maslahi ya nchi.kama kweli ameomba radhi huo ndiyo mwisho wa ushujaa wake. hayati baba wa taifa aliwahi kuwambia ccm siyo mama yangu,kwa vile aliwahi kuwasema vibaya mambo yalivyokuwa yanakwenda vibaya.wasomi wa tanzania wametanguliza maslahi binafsi na hawako tayari ku risk kwa ajili ya nchi kama walivyofanya wazee wetu akina mwalimu nyerere,kwame,kenyatta na wengineo. wakina mgeja siwatu wa kuibadili nchi hii. waliomuweka katika nafasi hiyo ya uenyekiti wa chama mkoa wa shinyanga kwa fedha zao ni mafisadi wanaotikisa nchi. hivyo hizo kelele ni za kulinda maslahi ya wafadhili wake! wakati wa kuthubutu ndiyo huu!
 
Tatizo ni jinsi hao wooote walivyogeuza siasa kuwa mwajili wao pekee. Wengi wakiachishwa siasa, hawana la kufanya.
Six na wengine wataendelea kupata taabu mpaka pale CCM itakapopata Mwenyekiti. Haina mwenyekiti.

Mwenyekiti lazima awe ni 'thinker' na mwenye kulinda msimamo na heshima ya chama anachokiongoza. Siamini kama ni hivyo kwa huyu waliyenaye maana kikao kama hicho ni cha kuonyesha msimamo wa chama. Badala yake imekuwa ni kuonyesha misimamo binafsi na matakwa binafsi kama huyo mwenyeviti wa shinyanga anavyofanya.

Kama chama kinachotawala kinaruhusu mawazo kama hayo basi ni ishara kwamba hatuna muelekeo wa nchi. Labda kama kuna atakayejitolea kufanya mapinduzi ya kijeshi kama ilivyokuwa Gambia.
 
Mtiririko wa mawazo ya wachangiaji juu ya mada hii, unaonyesha kuna kundi linawatetea mafisadi ambao Sitta anapambana nao Bungeni. Najua mtampinga Spika Sitta kwani wengine wetu huu JF munafaidika/mlifaidika na fedha chafu za kifisadi. Hala hala mti naq macho
 
Kitendo cha Spika Sitta kukaangwa kwenye kikao cha NEC kinadhihirisha kwamba mafisadi wana ngivu isiyo na kifani na hata wamekiteka chama cha CCM, pia wameiteka dola. Wabunge wa CCM wanaopinga ufisadi inabidi wajipange upya. This war must not be lost.
 
Spika Sitta, umetusaliti kabisa sisi ambao tulidhani tumempata mpiganaji. Kwanini usirudishe hiyo Kadi kama wewe umedhamilia kuupiga vita ufisadi. Unaomba msamaha wa nini???????? umekosa nini?????????????Tunakosa imani na wewe. Toka huko hapakufai Mhe. Spika
 
Tatizo hapa tuliopo humu sio wapiga kura na wapiga kura hawajui haki zao za kuchagua viongozi bora inabidi kama una ndugu anza sasa kuwapa Elimu mimi nimesha elimisha ndugu zangu 50 na wao nimewapa kazi ya kuelimisha jamaa zao na marafiki zao.
 
ila mzee sita nasikia amomba radhi mambo yameisha ila hawakumtendea haki huyu mzee
 
Nimeamini kuwa chama na serikali inaongozwa na kundi dogo lenye nguvu ya noti, yaani MAFISADI design ya PAPA. Inakuwaje badala ya kumpongeza Mr. Six kwa juhudi kubwa aliyoweza hadi kuruhusu uhuru wa mawazo bungeni na kukomesha ile tabia sugu ya wabunge kusinzia bungeni mithili ya mlaji wa samaki aitwaye pono!!! Unakumbuka jinsi ambavyo idaidi kubwa ya wabunge walikuwa wanauchapa usingizi maana walikuwa wanasubiri agenda ipite na kushtushwa ma makofi. Leo hii bunge nani athubutu kulala wakati muda wowote ule mwiba unaweza kumchoma through nondo zinazoporomoshwa pale. Mr. Six you made our house live and active na leo hii wanakumabia basi utoe tiketi ya kuchapa usingizi?? Kama umekubali hayo basi you are coward!!! Unafahamu vema sheria na kanuni za bunge, sasa iweje ukubali kuomba msamaha kwa kitu ambacho ni sahihi??? Simamia uwezo na ujuzi wako na vifungu vya sheria na kanuni!!!Yaani ukitishiwa nyau unaogopa??? Kwa nini usikubali wakutose halafu uje mbele ya hadhara na kuongea na wazalendo, watakuelewa na watakupa kura. Huu ulikuwa ni wakati muafaka kwa ssm kupasuka vipande viwili vya keki, i.e queen cake!!!!

Sasa bunge lijalo siji litakuwaje!!! Naamini umeomba msamaha kijanja huku ukijipanga vizuri kupambana na mafisadi na ikifika wakati basi simama na kusema siko tayari kuyumbishwa katika kazi niifahamuyo na kubwaga manyanga. Tutakuwa tayari kukupokea kwa mabango ya ushujaa. Please, dare!!!!
 
Spika Sitta, umetusaliti kabisa sisi ambao tulidhani tumempata mpiganaji. Kwanini usirudishe hiyo Kadi kama wewe umedhamilia kuupiga vita ufisadi. Unaomba msamaha wa nini???????? umekosa nini?????????????Tunakosa imani na wewe. Toka huko hapakufai Mhe. Spika

Sitta hajaonewa hata kidogo. Yeye anaijua vizuri CCM na ndiyo maana akapewa nafasi kubwa kiasi hicho ya kuwa spika. Kama anataka kupambana na ufisadi anaweza lakini siyo ndani ya CCM. Kama ningekuwa mjumbe wa NEC nisingekubali msamaha wa Sitta. Ile adhabu ya kumfukuza ilikuwa halali kabisa ili CCM iwe na watu wanaofuata utaratibu waliojiwekea. Hapo hakuna cha maslahi ya nchi! Ni maslahi ya chama kwanza.

Sitta asitake kuleta mambo ya ajabu ajabu. Kamwe askari hawezi kwenda mstari wa mbele huku kakaa upande usio wake. Atasababisha madhara makubwa sana na hilo ndilo analolifanya Sitta. NEC inayo haki ya kuhakikisha CCM iko salama na kwa hiyo maadui wote wasiokitakia mema chama inabidi watoswe. Kwa hiyo Sitta na kundi lake wanatakiwa kurudisha kadi mara moja, ili wakatafute jukwaa jingine la kuendeshea mapambano yao. Wanaanzia wapi kuwapiga vita wafadhili wakuu wa chama?
 
Back
Top Bottom