Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Nami naunga mkono Six angegoma kuomba msahama.....wamfukuze awe shujaa wa ufisadi,....kuliko kuomba msamaha....awe kibogoyooo maana yake nini??hakuna kitu aisee nchi hiii imekwisha na haifai tena
 
Sitta atikiswa ndani ya NEC Majirahttps://www.jamiiforums.com/index.p...a-nec&format=pdf&option=com_content&Itemid=57 https://www.jamiiforums.com/index.p...nt&print=1&page=&option=com_content&Itemid=57 https://www.jamiiforums.com/index.p...uZWMmb3B0aW9uPWNvbV9jb250ZW50Jkl0ZW1pZD01Nw==
Monday, 18 August 2009 16:43 *Aundiwa fitna za kung'olewa

Na John Danieli, Dodoma

HALI ya kisiasa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imezidi kuwa tata, baada ya kundi linalodaiwa kuwa na mlengo wa 'kubeba' mafisadi, kutaka Spika wa Bunge, Bw. Samuel Sitta awajibishwe kwa madai ya kukisumbua chama hicho kutokana na msimamo wake mkali dhidi ya wazembe serikalini.

Habari za uhakika kutoka ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama hicho (NEC) kinachoendelea hapa, Mjini Dodoma, zilieleza kwamba mara baada ya kuanza jana majira ya saa 12 jioni wajumbe waliopangwa walisimama mmoja mmoja na kueleza kwamba bila CCM kumwondoa kiongozi huyo wa Bunge, mambo ya kisiasa hususani hatima ya CCM katika uchaguzi mkuu ujao itakuwa mashakani.

Hivyo dawa pekee ni kumwondoa katika nafasi yake ya uspika na kumfukuza uanachama wa CCM hoja ambayo hata hivyo ilipingwa vikali na kundi la wajumbe linalopinga ufisadi, huku wakitaka kabla ya kiongozi huyo kuchukuliwa hatua, watuhumiwa wote wa ufisadi wakamatwe na wafukuzwe uanachama wa CCM kwanza.

"Hawa watu walijipanga wiki mbili zilizopita kabla ya NEC, walifanya vikao vyao, wakatenga mabilioni ya pesa........ (anamtaja mmoja wa wajumbe wa NEC, jina tunalihifadhi kwa sasa), akatumwa kwenda Zanzibar akagawa pesa kwa baadhi ya wajumbe wa NEC kutoka Zanzibar, sasa wamekuja kwenye kikao na ajenda moja tu, nayo ni kutaka kumg'oa Spika Sitta," kilisema chanzo chetu ndani ya NEC na kuongeza.

"Baada ya hapo watawashughulikia wafuasi wake wote wanaopinga ufisadi, lakini tunajua tatizo ni nini, tunatambua uongozi wa huyu spika Sitta umewabana na kuwakosesha amani, lakini tunasubiri uamuzi wa kikao, na mwenyekiti, lakini wakishindwa kuwadhibiti mafisadi hawa tumekwisha," kilisema chanzo hicho.

Habari zaidi zilieleza kwamba kundi hilo linaloaminika kudhaminiwa na watuhumiwa ufisadi ndani ya CCM, linaongozwa na mmoja wa Manaibu Waziri, Mwenyekiti wa CCM Mkoa na Katibu wake pamoja na wajumbe kadhaa kutoka Kanda ya Ziwa pamoja na Zanzibar.

Kutokana na ajenda hiyo kuzua mjadala mkali, jana siku nzima wajumbe wa NEC walishinda wakijadili ajenda moja tu ya hali ya kisiasa nchini huku mafisadi wakionekana kuzidi kujiimarisha zaidi ndani ya CCM

Baada ya mashambulizi kuongezeka zaidi kwa siku nzima dhidi ya Spika Sitta na wafuasi wake wanaopinga ufisadi, ilielezwa kuwa juhudi za baadhi ya wajumbe wanaofurahishwa na kasi ya Spika Sitta zilionekana kutokuzaa matunda hadi jana jioni kutokana na kundi hilo la mafisadi kuonesha dalili toka awali kutaka kuteka kikao cha NEC, kwa hoja zao ambazo kwa nje zilionekana kutaka kudai maslahi ya CCM, lakini kwa ndani zinaonekana kuipeleka CCM kaburini kama ilivyofanyika kwa Chama cha KANU nchini Kenya.

Ilielezwa kuwa licha ya Spika Sitta, kutakiwa kung'olewa kwenye wadhifa wake, pia Spika wa Baraza la Wawakilishi, Bw. Pandu Kificho, naye hakuweza kuepuka dhahama hiyo, baada ya wajumbe kadhaa kutaka naye awajibishwe kwa kung'olewa kwenye wadhifa wake kutokana na Baraza lake kutuhumiwa kumtukana Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali kwa ujumla pamoja na Bunge la Muungano.

"HIvyo ndivyo hali ilivyokuwa ndani ya NEC, hata sisi hatukutegemea. Wajumbe walimtaka Kificho naye ang'olewe kwa kuwa Baraza lilimtukana Waziri Mkuu, Serikali ya Jamhuri ya Muungano na hata Bunge. Kama hali itaendelea hivi, ni wazi kwamba CCM inachungulia ilipo KANU kwa sasa, lakini yote hayo bado ni mchango wa wajumbe, tusubiri mamuzi ya kikao leo usiku (jana)," kilisema chanzo chetu ndani ya NEC.

Ilielezwa kwamba chanzo cha Spika Sitta kutaka kutolewa inatokana na itikadi yake kutokuyumba katika masuala mazito yanayohusu ufisadi kama vile Richmond, TRL, TICTS,na kukataliwa kwa mswada wa marekebisho ya sheria mbalimbali.

Hali hiyo imeelezwa kufanya baadhi ya mawaziri kumchukia kwa kuwa kasi yake inawapa wakati mgumu bungeni. Jumla ya mawaziri 7, wametajwa kuwa wanahusika na kuungana na kundi la mafisadi kutaka kiongozi huyo ang'olewe.

"Bunge chini ya Spika Sitta linajadili maslahi ya watanzania wanaokadiriwa kuwa milioni 40 kwa sasa, anayezungumza kuwa Sitta anawasaliti CCM anajali maslahi ya kundi lake, watoto wake, marafiki zake na ndugu zake. Tunaelkea kufikia ndoto ya Mwalimu Nyerere, kuwa CCM ikiyumba nchi itayumba. NI wazi sasa ufisadsi unayumbisha CCM, kama hatutawang'oa nchi itayumba," alisema mmoja wa wajumbe wa NEC bila kufafanua.

Hadi tunakwenda mitamboni, kikao cha NEC kilikuwa bado kinaendelea japo wajumbe kadhaa walionesha kutoridhika na mwenendo wa kikao hicho.

-----------
Lowasa ni mtu wa kulipiza visasi anakamia aondoke na sitta siku zote, Nchi haitatulia kama Lowasa ataachiwa hivi hivi
 
Tatizo hapa Mkuu ni kwamba tulioko JF hatutoshi kuifanya CCM ishindwe kwenye kura. Sasa huwa najiuliza ni nini tukifanye ili hata yule mkulima wa pale katahoka-Biharamulo awe na mawazo ya ki-JF?

Heshima mbele mkuu!

Kama uko Tanzania basi anza na kuprint kijarada cha mkuu "Mwanakijiji" CHECHE ukiweza kuprint na kusambaza 10 kila tolea utakuwa umefanya cha maana. Wengi kweli hawaijui jamiiforums lakini ukifanya hilo taratibu tutawafikia wengi. Sad I am in Tanzania.

Anza na hili toleo:
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/36225-2010-ni-mwaka-wa-uhuru-wetu.html

Play your part!


Njimba
 
Mkuu habari zote kuhusu Spika kwenye magezeti ya leo zinafanana, na hii ni pamoja na habari ya Spika kuomba radhi ambayo unasema si kweli (hata mimi nashangaa iweje aombe radhi). Nafikiri source wa habari hizi ni mmoja na ni wa kambi moja na amezitoa habari hizo kwa sababu maalumu.
 
Narekebisha kidogo. Baada ya kusoma habari ya Majira naona kuna tofauti kidogo na ile ya magazeti ya Tanzania Daima, Mwananchi na Citizen. Naona habari hii ya Majira inavutia zaidi na ina habari zaidi.
 
Uwanja pekee waliobaki nao ambao ni tambarare akina RA, EL ni NEC ambayo imejaa watu wa ajabuajabu rahisi kutumika, uwezo mdogo kifedha, wengi ni brain-washed.
Kumuondoa Sitta kwa sasa hawawezi. Wanakumbuka walivyopata taabu Mrema alivyoondoka na uchaguzi mkuu wa 1995 ulivyowahangaisha hadi Mwalimu kunyanyuka kuokoa jahazi. Hawana mtu kama Mwalimu kwa sasa.
Mabalozi nao wako macho na fedha zao ndio kila kitu kwa mambo yetu hapa.
 
Kama "jina tunalo" na hutaki kulisema, mimi msomaji unanambia jina unalo ili iweje, niifanyie nini siri yako wewe?

Hivi umepita mafunzo ya uandishi au mliokotwa okotwa Uwanja wa Fisi mkawe cheap labor kwenye newsroom?

Unaogopa kutaja jina la mjumbe wa Halmashauri ya CCM?

Tanzania Daima ni miongoni mwa viji gazeti ambavyo Sitta alisema vinatumiwa na mafisadi. Usishangae kuona takataka kama hizi.

Nyie bwana,mnafikiri kila kitu unaweza kuandika.Sometimes jinsi mtu alivyoiptata habari inakuwa vigumu kuanza tu kuandika jina lake kwa kuwa it can be taken against you in the court of law. Kumbuka lile ni gazeti na linakuwa na motive mbalimbali pamoja na kuendelea ku-exist. So pale si kama JF where you can write and express anything. So please spare them bwana. Cha msingi wewe umeipata habari that is engough ufanye mwenyewe research kujua ni nani.
 
Mafisadi wamwandama Spika Sitta hadi NEC




Na Mary Edward Nipashe



18th August 2009












Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Samuel Sitta.



Mvutano mkali uliibuka jana ndani ya mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi Taifa (NEC) baada ya kundi linalotuhumiwa kwa ufisadi kushawishi wajumbe wa mkutano huo kumpigia kura ya kutokuwa na imani na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Samuel Sitta.
Kundi hilo linadai Spika amekuwa kikwazo kwao na ndiye anayeshawishi baadhi ya wabunge ndani ya Bunge kuendeleza kuliumiza kundi hilo.

Kundi hilo linalalamikia taarifa ya hivi karibuni iliyotolewa bungeni na Sitta kuwa kundi hilo linalotuhumiwa kwa ufisadi linataka kumuua hali ambayo ilimlazimu kuomba ulinzi wa ziada kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Kundi hilo linatuhumiwa kuwashawishi wa wajumbe kwa nguvu zote na kutumia fedha nyingi ili kuungwa mkono kufanikisha kumng’oa Spika.
“Unajua tangu jana mvutano uliopo ni suala la kundi hili la watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi kushinikiza Spika aondelewe kwenye nafasi yake... limekuwa likifanya kampeni kubwa na kushawishi wajumbe kwa fedha nyingi...lakini hali inavyoonekana limeshindwa kwa sababu wajumbe wanaoliunga mkono ni wachache hata kama zingepigwa kura kwa vyovyote vile lisingeshinda,” kilisema chanzo chetu cha habari.

Chanzo hicho kiliongeza kuwa mvutano huo uliibuka kwenye kikao cha Kamati Kuu kilichoketi kwa muda wa siku mbili kuanzia Jumamosi na Jumapili ambapo kundi hilo lilitaka hoja hiyo ya kumng’oa Spika iwe sehemu ya ajenda katika mkutano wa NEC.

Hata hivyo, baada ya mvutano mrefu bila kupatiwa majibu, suala hilo liliibuliwa tena kwenye mkutano huo ambapo kundi hilo limekuwa likishikilia msimamo wake wa kung’olewa kwa Sitta.

Taarifa hizo zinaeleza kuwa ushawishi wa kundi hilo umekuwa hauna nguvu kwa vile wajumbe wengi walikuwa upande wa Spika na kusababisha nia yake kutotekelezwa.

Rais Kikwete alitarajiwa kulitolea uamuzi suala hilo baadaye katika kikao kilichokuwa kinaendelea jana usiku.

Kuhusu kung’olewa kwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, chanzo hicho kimedai kuwa halikuwa kwenye ajenda lakini tetesi zilidai kuwa huenda likaibuka kwenye ajenda ya mengineyo.

“Huyo mzee sijui ana nini, maana wajumbe wengi walishapeleka mapendekezo kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete la kumwondoa, lakini hadi sasa hakuna kinachoendelea,” kilisema.

Wakati huo huo, Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Said Bwanamdogo, amechaguliwa kuwa Mjumbe wa NEC kupitia Jumuiya ya Wazazi.




CHANZO: NIPASHE

Nimefatilia magazeti mengi nadhani "Tanzania Daima" kama Spika alivyoelezea kuwa wanamwandama, bado hawamtendei haki.
 
Jamani mjadala usiende kwenye personalities, tulenge kukikosoa chama. Hayo ya kuanza kutuhumiana usafi na uchafu wa mtu, tuwaachie wenye chama wanaosuguana huko kwenye vikao vyao.

Ndugu yangu Mtanzani ukianza kujibu vitu vidogo vidogo kama hivi kesho utajikuta kwenye magazeti ya Majira na title kubwa kweli kamba unatetea mafisadi. Ukiona post inakugusa na haijakufurahisha ipite tu kama vile hujaiona, ukianza kujibu tu ndiyo utakuwa unafungulia chokochoko na chimba chimba maana kambi ya upinzani ndani ya chama chako iko makini kuangalia mabandiko yako na ukiteleza tu wanayachukua kama yalivyo na kwenda kuyaweka gazetini kama jinsi ulivyojibu.

Hizo ndiyo siasa ndugu yangu, hata uwe msafi kama malaika lakini bado jamaa watatafuta hata kidoa kidogo sana ili kukutoa kasoro.

Let us face and focus on the state issues not individual personalities. Tujue how we can move TZ from the point it is.
 
Waliyomnyanyua na kufika kuwa mkiti wa CCM mkoa wa shinyanga ni pamoja na mtu mmoja anaitwa Phantom ama Hilal Soud ambaye aliiba fedha uarabuni ambako alikuwa mhasibu Jeshini na kukimbilia Shinyanga, huyu jamaa ni MNEC wa Shinyanga, amenyanyang'anya ardhi ya wananchi wa Maganzo kwa ajili ya mgodi wa almasi hadi leo hii hajawalipa fidia, na alipewa - eneo la diamond protected area ambalo lilikuwa likilindwa na sheria ambayo waziri wa Madini Yona aliifuta ili kumruhusu Phantom kuchukua eneo la mgodi.

Je ni kweli Hilal Soud aliiba fedha uarabuni? je una uhakika na hilo?
 
Hawa watu wana matatizo...si kidogo. Nazungumzia watu waliochukizwa na kukerwa na procedures za Bunge na technicalities na kusifiwa kuwa walizungumza kwa hasira na kuonesha kukerwa. Yaani, zawadi kubwa wanayogombania ni nani abakie CCM nani asibakie. Watu walioshiwa uongozi huonekana kwa kufuata mkumbo.

Yaani humo kwenye kikao chao chote watu na akili zao na wengine "wasomi" wamekaa kujadili Mtu? Kwamba kati ya mambo yote yanayolihusu taifa letu saa na wakati huu wao wanagombania chama?

Kwa kweli imebidi niwatolee uvivu kuanzia Mwenyekiti wao hadi x,y!!
Wakuu, Katiba ya nchi hairuhusu Mbunge kushitakiwa popote kutokana na kauli aliyoitoa ndani ya Bunge. Sijui viongozi wetu hawa wanatumia mamlaka na sheria gani kukiuka katiba na kutaka kutoa hukumu kwa Spika kutokana na kauli au matamshi yaliyotolewa ndani ya Bunge. Ni uvunjaji wa sheria mama kufanya hivyo.
Mimi kwa muda mrefu (hadi jana) nimekuwa nikiamini kuwa CCM inazingaia imani yake. Imani kuwa "Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa". CCM hii inayoona viongozi wanaotetea imani za chama kuwa ni waasi ni CCM ipi? Je, ni vikao gani vya chama ambavyo vimebadili imani hiyo ya CCM? Je, ni kiburi gani kinachoweza kuwafanya viongozi hao kutumia muda mrefu wa kikao kikubwa kama hicho cha chama kuzungumzia uongozi wa muhimili huru wa Bunge na utendaji kazi wake hata kufikia kumtishia Spika kumnyang'anya uanachama?
Ni kosa gani alilofanya Spika? Ingekuwa Spika ameita vyombo vya habari au kuhutubia nje ya Bunge na kuanza kuzungumzia ufisadi wa viongozi wa CCM kwa kashfa, walau ingeleta maana kwa wajumbe hao wa NEC kumkanya. Na njia nzuri ya kumkanya mwanachama ambae ana mamlaka makubwa kama ya u-Spika, ni kumuita kwenye kikao cha viongozi wachache (kama CC) na kuzungumza nae kwa heshima inayostahili. Si kumbwatukia kwenye kikao cha viongozi wengi kiasi hicho.


Inatisha, inasikitisha na inaua matumaini yote ya kuwa tuna uongozi makini wenye nia njema kwa Taifa letu.
 
Hivi Spika ni wa chama au wa bunge? Kama spika amechaguliwa na bunge chama kitawezaje kunyanganya uspika? Nadhani watakosoana tu na hawezi hata kumnyang'anya hako kakadi kao kwa maana watakuwa wamejimaliza moja kwa moja. Lakini huyo bwana alivyo mbishi hata akiambiwa arudishe kadi unadhani atakubali. Atapiga chenga kwa super super speed. Waacheni waajikaange tu sisi tutafukia. Zidumu fikra sahihi za wazalendo wa JF.
 
ukweli ni kwamba katika utendaji wowote ukisimamia ukweli wa mambo hutapendwa na jamii ambayo uwongo kwao ni ukweli.mwacheni mheshimiwa sitta aendelee kusimamia ukweli wa mambo
 
dah!wakuu nimeyakubali mawazo yenu hasa huyu mtoa mada.

issue hapa yatupasa tujue na kujihoji sisi wananchi pamoja na serikali nini hasa kinachosababisha samwel sitta awekwe kitimoto?sababu hata wale wanoijua vizuri historia ya bwana sitta kuanzia pale kwenye mgomo wa chuo kikuu mwaka wao, mpaka sasa kapitia ngazi mbalimbali za uongozi; na mambo yake yote ni mazuri hasa pale alipokuwa BET.Ukiangalia vizuri suala hilo unaona kwamba viongoz wetu wanadhan watanzania wa sasa ndo wale wa kipindi kile ambacho tv ilikuwa inapatikana ikulu tu.
sasa kama wanataka kumnyang'anya kadi,iyo ndo inaonyesha jinsi gani serikali inavyokumbatia ufisadi na haina uhuru wa watu kutoa mawazo yao.
yawapasa wakili kwamba serikali imeshindwa na wanaojiuzulu wajiuzulu mapema kuliko aibu inakuja kuwakuta kwenye uchaguzi ujao.
HIYO NI AIBU KWA CCM.INAWAPASA WAMUHESHIMU SAMWEL SITA NA SIO KUMUWEKA KITIMOTO NA KUMTISHIA KUNYANG'ANYA KADI.

poppin them thanx!
 
Na njia nzuri ya kumkanya mwanachama ambae ana mamlaka makubwa kama ya u-Spika, ni kumuita kwenye kikao cha viongozi wachache (kama CC) na kuzungumza nae kwa heshima inayostahili. Si kumbwatukia kwenye kikao cha viongozi wengi kiasi hicho.

Inatisha, inasikitisha na inaua matumaini yote ya kuwa tuna uongozi makini wenye nia njema kwa Taifa letu.
Nafikiri labda ungejifunza uzuri katiba ya CCM. NEC ndio kikao kikuu, kilichopo kidemokrasia, na ni sahihi kwa kufanya hivyo ilivyofanya.
 
Mzee Mwanakijiji,
Nguvu hii wangeiweka kuwajadili kina Lowassa, Rostam na viongozi wengine mafisadi waliojiuzuru hakika wananchi tungewapa mkono mzito mkutano huu wa CC..hata kama wangefikia maamuzi wakasema tumetoa ONYO KALI kwa mafisadi..basi wananchi wangeivaa kamba hii shingoni..
Hizi ndio political game zinazotakiwa kuchezwa na CC lakini hili la Sitta, bila shaka ndio kwanza wanamwongezea sifa, Umaarufu na nguvu kubwa ya ushindani.

Kweli sasa hivi Sitta ni sawa na Nyati aliyejeruhiwa, lakini wanachoshindwa kujiuliza ni kwamba kwa nini walitaka kumwinda Nyati ngangari kati ya kundi zima! Siku zote Simba humchagua Nyati dhaifu ktk kundi..

Wametumia mifano ya kina Jumbe, Seif Sharrif Hamad na Mrema lakini wanasahau kwamba watu hawa kwa wakati tofauti wamewapa shida kubwa sana ktk chaguzi zilizofuata na wananchi hawakuwa makini na macho kama leo hii kiasi kwamba tutarudia makosa yaleyale..

Mkuu Mkandara, ni kweli kabisa kuwa wametumia vibaya sana kikao hicho ambacho kingeweza kurudisha imani ya wananchi kwa chama hicho. Wangeweza (hata kwa unafiki tu) kuonyesha kuwa wanaijua misingi ya chama na wako tayari kuilinda. Wangeonyesha pia kuwa wamesikia kelele za wananchi kuhusu mmomonyoko wa maadili ya baadhi ya viongozi wa chama na wako tayari kurekebisha. Hii yote ni ili kuweza kujihakikishia ushindi mwakani. Kuanza kupambana na wale wanaojibu mahitaji ya wananchi kwa vitisho, kunakiweka chama hicho katika hali mbaya zaidi kisiasa. Nilidhani wangekuwa wa kwanza kujua hivyo. Wameshafanya makosa mengi na wasiotakiwa kuwa maarufu kisiasa wakawa maarufu sana. Naona hakuna walichojifunza. Labda sanduku la kura litasaidia kidogo.
Mkuu, inasemekana kutokana na taarifa hapa kuwa imeundwa kamati ya kuchunguza ilikuwaje hali ikawa kama ilivyokuwa. Ninavyohisi mimi ni kwamba, imeundwa kamati ya kuchunguza kama Spika atarudia tena mambo ambayo amekuwa akiyafanya Bungeni na hivyo kudhoofisha chama. Kwa maana nyingine ni kwamba wameunda regulatory committee ya kuhakikisha hali hii hairudiwi tena (na Spika wala wanaomuunga mkono Bungeni). Sababu ya kudhani hivyo ni kuwa, hakukuwa na haja ya kuunda kamati kwani tuhuma zimeshatolewa, wajumbe wakataka anyang'anywe kadi, inasemekana akaomba msamaha. Kwanini sasa kuwe na uchunguzi? Unachunguza nini? Hansard za Bunge zipo wazi hazina haja ya kuchunguza. Nadhani wamepania kumnyamazisha Sita na wenzake kabisa na kwa nguvu nyingi.
Mkuu mfano walioutoa kuhusu Seif, Jumbe na Mrema hauna maana kabisa. Hauna maana kwakuwa Spika ni far more intelligent, learned na focused kuliko hao wote. Ni mwanasheria, mwanasiasa mkongwe, ni kiongozi wa Bunge (taasisi yenye nguvu sana nchini). Hawawezi kudharau kadi yake hasa wakati huu. Endapo Spika Sitta akiamua kuirudisha kadi yao au wakiamua kunyang'anya kadi hiyo, ni dhahiri kuwa ataondoka na Wabunge wengi sana wa CCM na wenye nguvu, wanaokubalika na wenye uwezo wa kurudi Bungeni kupitia vyama vingine. Wasijidai kutojua siasa ndogo kiasi hicho.
 
Back
Top Bottom