Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Nyepesi nyepesi zinazojiri kutoka NEC ya CCM Dodoma jana Spika Samwel Sitta kawekwa mtu kati kwa namna anavyolipeleka Bunge mpera mpera.

Miongoni mwa wachangiaji waliomshambulia wazi wazi ni Mwenyekiti wa CCM Shinyanga ambae bila kumung'unya maneno alimwambia Sitta alirudishe kadi ya CCM. Kwa ujumla wachangiaji wengi wameonyeshwa kutoridhiswa na utendaji wa Sitta isipokuwa wawili tu Eng Stellah Manyanya na Mh John Shibuda.

Chungu kimefunikwa na kikao kinaendelea leo ambapo tusishangae kusikia Sitta kasitishwa U-Spika.

Stay tuned...

Nadhani sasa kila anae litakia mema Taifa hili anaamini kuwa tunaelekea tulipo kuwa tunapataka.maana watchujana kama maji na mafuta mwisho wa siku chama kitagawanyika kisha sasa hata yale waliokuwa wanayakalia wakidai ni kwa ajili ya usalama wa taifa yatawekwa adharani.
 
Sita ni number ya uharibifu na mapinduzi na kupitia Samwel Sitta haya yanawezekana Tanzania. We have waited for so long this time to come!
 
Sita ni number ya uharibifu na mapinduzi na kupitia Samwel Sitta haya yanawezekana Tanzania. We have waited for so long this time to come!

Natamani mpasuko mkubwa utokee lakini si rahisi kwasasa,hakuna dalili ya kusambaratika kwa chama cha mapinduzi kwa siku za karibuni.Wataparurana sana mwisho wa siku wataelewana na wataendelea kutafuna keki ya taifa taratibu.Mheshimiwa Sitta bado atatakiwa kupata uungwaji mkono mkubwa ndani ya CC na NEC kitu ambacho sina hakika kama kipo kweli.Ndani ya bunge JMT hakuna shaka Six ana kundi kubwa linalomuunga mkono.

Mheshimiwa Sitta anaweza kuendelea kushikilia msimamo wa kutaka mafisadi waadhibiwe/watoswe lakini tusisahau uchaguzi uko karibu sana sirahisi kwa muungwana kukubali kuwatema mafisadi ambao wengi wamesaidia kumfikisha hapo alipo.Muungwana atapenda zaidi kuonekana neutral ili apate uungwaji mkono kutoka pande zote mbili.

Wajumbe wa NEC na CC ni wanasisa wanaochanga karata zao kwa kuangalia zaidi maslahi ya kisiasa kuliko kuangalia msatakali wa nchi,kwa mtaji huo basi tutegemee zaidi maamuzi ya kisiasa.
 
Ukombozi utakaopatikana kutokana na VITA YA MAFISADI kamwe hauwezi kuwa ukombozi wa Mtanzania. Ukombozi utakuja kutokana na uthubutu wa wasio na udau katika tabaka fisadi kujenga demokrasia makini, upinzani makini na uongozi makini nje ya madhabahu ya mfumo fisadi....

omarilyas
 
  • Eti wapinga ufisadi na watetea mafisadi wamo kwenye kikao cha siri na mwenyekiti wa kikao ni Raisi na kiongozi wa nchi.
  • Eti Spika kiongozi wa Bunge linalowawakilisha wananchi kwa ujumla wao anawekwa kikaangoni kwenye kikao hiki cha siri.
  • Eti Mwenyekiti wa mkoa wa chama cha CCM hamung'unyi maneno na amtaka Spika arudishe kadi ya chama.
  • Eti Spika kakimbiwa na wajumbe isipokuwa wawili tu Eng Stellah Manyanya na Mh John Shibuda.
  • Halafu eti tusishangae kusikia Spika wa bunge Jamhuri ya Muungano, Sitta, kasitishwa U-spika.
Trust people like Masatu to come up with this kind of spin, I wouldnt have expected otherwise. Big up Masatu, you are doing just fine - ukiona vyaelea, vimeundwa !!
Yangu macho kwani huu usiri wa kikao cha manyang'au umetanda hila na giza - unatisha !
 
Mh sitta pamoja na wewe una matatizo lakini wakitaka kadi yao wape ukaungane na Slaa upande wa pili. Tunahitaji nguvu upande wa pili

Awape kina nani?. Hiyo kadi ni ya nani?, kadi ni ya Sitta hao wanaopiga kelele ni vibaraka wa mafisadi wametumwa waongee kwa niaba ya kina RA na EL et al. Humo hafukuzwi mtu, Sitta anakuza Demokrasia bungeni, hawa wanaoongea hivyo ni wahafidhina wasiojua kuwa muda unawatupa mkono.
 
mafisadi wananguvu sana katika chama tawala kwa maana hata hao viongozi walisaidiwa kufikia hapo na mafisadi hivyo mtu yeyote anayepingana na hao siye mwana ccm mfano mzuri issue ya kagoda imefia wapi?
 
CCM haiokoleki, haiponyeki, na haibebeki! Ni ukosefu wa maono kufikiria kuwa matatizo ya CCM ni Spika Sitta!

Hata hivyo, wafanye hima kutimiza unabii; imesemwa na itatimia.
 
Vipi kimejiri nini huko NEC kwa kirefu? Mkulu FMES we trust you when it comes to this NEC and CC thing.

Masatu ni kweli alituspin na hadithi yake ya Spika kutoswa? kama ni kweli kwanini analeta habari za kishabiki zisizo kweli katika jamvi?

Nawasilisha
 
Duu
mimi binafsi nawashangaa watanzania wezangu ktk uangaliaji wa mambo na ufuatiziaji wa nyenendo,labda mimi ndiye naangalia ktk kingo za box.

Hawa mananyang'au wanao pukuchuwa nchi yetu wamekaa ktk makundi mawili ama ktk majeshi mawili ,moja la angani na lingeni la ardhini.

Lilo angani kazi yake ni kushambulia ,ni kundi ambalo liko upande wapukutuaji nchi kwa uwazi,na kundi la pili ni lile la ardhini ambalo linajinadi linapinga mafisadi ,ni kundi lilo hatari maana limejiunga na wananchi wapigania haki wa kweli ,tatizo linaanza kwamba wenye miono miepesi watapotezwa nalo,lakini hata hivyo haliitaji ugumu kulitambuwa kwani matendo yao ni tosha.

Huwezi sema una uchungu na nchi yako na unapigania ubadhirifu unaofanyika nchini kwako wakati huo huo wewe ukaishi kwenye nyumba ya mabilion ya fedha wakati ukitoka nje kilometa 1 ndani ya hekalu lako unakutana na masikini wa kutupwa ,eti tu kwa vile Bunge/ama sheria imefuata.

Hii ni sawa kabisa japo ni ngumu kuielewa yani ya kwamba je ni sahihi? kwa mjibu wa sheria/Bunge ikipitisha sheria kwamba Sitta yani spika kila siku asubuhi awe anakamata watanzania 100 na kuwalamba viboko vya nguvu itakuwa sahihi kwa vile sheria imefuatwa.?

Wapigania haki ktk nchi yao hawako tu kuangalia nini bunge/sheria inasema bali ni watu wenye kuvuta hisia za kizalendo na haki (right) ya natural ,mazingira na pia kuwa na huruma kwa ndugu zao.

Hawa akina Sitta,Mwakyembe,Kilango ,RA,Lowasa nk wote kwangu wapo ktk chungu kimoja ,tusdanganyike!! hata majambazi wanapoenda kuvamia basi na ktk mgawo ,mmoja wao akawa mjanja hugeukana na hata kupelekea kufyatuliana risasi ,anayemfyatulia jambazi mwenzie risasi si kwamba ni mwema ,ama jambazi mwingine anaenda kumchomea mwenzio polisi na huyu jambazi aliyechoma si mjambazi mwema eti kwa vile kaenda kutoa siri za jambazi mwenzie.

Mimi nafikiri tuwe huru (labda mie ndiye siye) ktk kutafari mambo tuiipe akili homework na tuichoshe zaidi ,pia tujaribu kuangalia na kuoanisha historia ya mhusika huko nyuma na anachokihubiri ktk mda muafaka.
 
kweli huyo mwenyekiti ana nguvu ya kumshambulia sita
hii habari kama inawalakini...
 
Duu
mimi binafsi nawashangaa watanzania wezangu ktk uangaliaji wa mambo na ufuatiziaji wa nyenendo,labda mimi ndiye naangalia ktk kingo za box.

Hawa mananyang'au wanao pukuchuwa nchi yetu wamekaa ktk makundi mawili ama ktk majeshi mawili ,moja la angani na lingeni la ardhini.

Lilo angani kazi yake ni kushambulia ,ni kundi ambalo liko upande wapukutuaji nchi kwa uwazi,na kundi la pili ni lile la ardhini ambalo linajinadi linapinga mafisadi ,ni kundi lilo hatari maana limejiunga na wananchi wapigania haki wa kweli ,tatizo linaanza kwamba wenye miono miepesi watapotezwa nalo,lakini hata hivyo haliitaji ugumu kulitambuwa kwani matendo yao ni tosha.

Huwezi sema una uchungu na nchi yako na unapigania ubadhirifu unaofanyika nchini kwako wakati huo huo wewe ukaishi kwenye nyumba ya mabilion ya fedha wakati ukitoka nje kilometa 1 ndani ya hekalu lako unakutana na masikini wa kutupwa ,eti tu kwa vile Bunge/ama sheria imefuata.

Hii ni sawa kabisa japo ni ngumu kuielewa yani ya kwamba je ni sahihi? kwa mjibu wa sheria/Bunge ikipitisha sheria kwamba Sitta yani spika kila siku asubuhi awe anakamata watanzania 100 na kuwalamba viboko vya nguvu itakuwa sahihi kwa vile sheria imefuatwa.?

Wapigania haki ktk nchi yao hawako tu kuangalia nini bunge/sheria inasema bali ni watu wenye kuvuta hisia za kizalendo na haki (right) ya natural ,mazingira na pia kuwa na huruma kwa ndugu zao.

Hawa akina Sitta,Mwakyembe,Kilango ,RA,Lowasa nk wote kwangu wapo ktk chungu kimoja ,tusdanganyike!! hata majambazi wanapoenda kuvamia basi na ktk mgawo ,mmoja wao akawa mjanja hugeukana na hata kupelekea kufyatuliana risasi ,anayemfyatulia jambazi mwenzie risasi si kwamba ni mwema ,ama jambazi mwingine anaenda kumchomea mwenzio polisi na huyu jambazi aliyechoma si mjambazi mwema eti kwa vile kaenda kutoa siri za jambazi mwenzie.

Mimi nafikiri tuwe huru (labda mie ndiye siye) ktk kutafari mambo tuiipe akili homework na tuichoshe zaidi ,pia tujaribu kuangalia na kuoanisha historia ya mhusika huko nyuma na anachokihubiri ktk mda muafaka.


Maneno yako mazito sana mkuu .Nimekusoma nami naongezea kwamba Sitta , Mwakyembe nakundi lake akina makinda hawana nia njema na Nchi.Sitta ana mission yake kajificha nyuma ya kusema anapinga ufisadi .Hakika nasema hawana uchungu maana mwisho wa yeye huibeba serikali openly na Mwakyembe na wenzake hupika kelele na mwisho wanasema wanaunga mkono hoja asilimia 100.

Hii ya spika kubanwa nadhani ni wapambe wake wanaleta ili wa gauge upendo nje tunasemaje ila ukweli utajulikana tu CCM imesha kufa hakuna siri imebakia kutumia maguvu tu kwa kila jambo .
 
Kikwete hana ubavu wa kumweka kitimoto Sita hata siku moja.

Li-CCM halitagawanyika vipande. Litabakia limoja, lakini dhaifu kama leyland bovu la miaka ya sabini. Huko mbeleee litakuwa scrap.
 
- so far dataz zenye uhakika ni toka jana juhudi za kutaka ku-reconcile makundi yaliyoko ndani ya CCM kuelekea uchaguzi wa 2010 kutokana na kauli nzito ya JM, ambaye the dataz ni hakutaka kuhudhuria kikao hiki toka last week amejificha UK,


FMEs!

Mkuu heshima mbele, labda kuna sehemu namiss taarifa huyu JM ni nani?
 
Back
Top Bottom