GEOMO
Senior Member
- Jul 11, 2009
- 105
- 21
Nyepesi nyepesi zinazojiri kutoka NEC ya CCM Dodoma jana Spika Samwel Sitta kawekwa mtu kati kwa namna anavyolipeleka Bunge mpera mpera.
Miongoni mwa wachangiaji waliomshambulia wazi wazi ni Mwenyekiti wa CCM Shinyanga ambae bila kumung'unya maneno alimwambia Sitta alirudishe kadi ya CCM. Kwa ujumla wachangiaji wengi wameonyeshwa kutoridhiswa na utendaji wa Sitta isipokuwa wawili tu Eng Stellah Manyanya na Mh John Shibuda.
Chungu kimefunikwa na kikao kinaendelea leo ambapo tusishangae kusikia Sitta kasitishwa U-Spika.
Stay tuned...
Nadhani sasa kila anae litakia mema Taifa hili anaamini kuwa tunaelekea tulipo kuwa tunapataka.maana watchujana kama maji na mafuta mwisho wa siku chama kitagawanyika kisha sasa hata yale waliokuwa wanayakalia wakidai ni kwa ajili ya usalama wa taifa yatawekwa adharani.