Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Katika hali halisi hatuna Rais mwenye maamuzi na msimamo katika nchi yetu, bado tuna wakati mgumu sana kwa upande wa viongozi wenye kukubalika si kwa ufundi wa kuongea tu bali na vitendo, kiongozi mwenye mapungufu hawezi kuzungumzia mapungufu hayo kwa wengine, mambo haya hata wakati wa YESU yalikuwepo, huwezi kumwambia mwenzio atoe kibanzi katika jicho lake wakati wewe mwenyewe una boriti
 
Lunyungu,

Wewe ni msanii kweli kweli, inabidi ujiunge na The Comedy. Unatunga mambo kuja kuwafurahisha JF?
Na JF ilivyo na wajinga wengi, eti wanapiga makofi.

Huyo jamaa yako hakusema chochote kwenye NEC na alipotaka kusimama alizimwa na akanyong'onyea.

Kwa taarifa yako aliaga hapa Kyela kwamba yeye ni mtu muhimu mno kwenye vikao vya NEC na kwamba afadhali wakosekana akina Prof. Mwandosya na Prof. Mwakyusa kuliko kukosekana yeye.

Pia aliahidi kurudi Kyela Jumatano kuendelea na ziara yake ya kuzima moto wa Mwakalinga. Lakini baada ya kujeruhiwa Dodoma kaingia mitini.

Wapambe wanasema jemadari kajeruhiwa, yuko msituni kutafuta mbinu nyingine.

Kyela hapa ndio mazungumzo pekee; kwamba hawa jamaa kumbe hawajali maslahi yetu maana kama wangelikuwa wanajali maslahi ya wananchi si wangelisema chukueni kadi zenu?
mkuu naona unafanya PR Bonanza.

Nijuacho mimi ni kwamba CCM ni kwishney kilichobakia ni umaarufu binafsi wa wanachama wake na si utekelezwaji wa sera zake.

Wenyekujua kusali, huu ndio wakati wa kuliombea TAIFA. ndugu zetu wanaoingia ktk mfungo waweke mkazo kuliombea TAifa na viongozi wetu ili wageuke kutoka njia zao mbaya....
 
Moja ninalokubaliana na habari hii ni kuwa hili suala halijaisha na litaiweka pabaya CCM. Nionavyo mimi Spika Sitta na si mwengine yeyote katika CCM alie na ufunguo wa tatizo linaloikabili CCM. CCM hakijawa chama safi na hata hayo makundi yote si safi lakini walitumia udikteta kuitawala jamii likiwamo Bunge na walifanikiwa.
Spika Sitta anaweza kulirejesha Bunge katika enzi zake na makundi yakapotea kwani siamini kuwa kuna wengi ndani ya Bunge ambao hawaweki mbele nafasi ya kuchaguliwa kuliko haja ya kutetea masilahi ya Taifa.
Wanaoitwa mafisadi wanatumia kipato walichohodhi kurejea Bungeni na wale wanaoitwa wapiganaji wa Ufisadi wanatumia jina la ufisadi kurudi Bungeni. Mwisho wa siku wote wanalengo la kuiweka CCM madarakani. Hilo wanalitambuwa na tusubiri tuone watafika pahala wata Compromise na victims ni wananchi.
 
JK mwenyewe keshategwa na mafisadi. Maana walimsaidia hivyo hata issue iwe ya namna gani hawezi kutoa msimamo wowote kwani hataki kuudhi kundi lolote. Hivyo kuna mengi yanakuja tusubiri tuone mpaka 2010 yatatokea mangapi.
 
Sitta akisema liwalo na liwe watamfukuza chama kweli? Kama wanamfukuza basi CCM wamejipalia mawe ya moto for 2010 wazi wazi. Kwa sasa watanzania wameenda shule na wanajua lipi jema na bovu. kazi ipo CCM kubalini you are loosing it
 
Nimekwishasema awali na ninarudia tena......

"Kweli hawa mafisadi ni wajinga sana. Wanashindwa kuelewa kuwa siyo CC wala NEC ya CCM yenye mamlaka ya kisheria kuweza kumwondolea S.6 uspika!

Wanachoweza kufanya ni kumwondolea ubunge kwa kumnyang'anya uanachama wa CCM, lakini siyo uspika kwa maana kisheria, siyo lazima mtu kuwa mbunge ili kuchaguliwa spika. Spika wa Bunge la Jamhuri, kwa mujibu wa katiba ya JMT, anaweza kuwa au asiwe Mbunge. Raia yeyote anaweza kuchaguliwa na Bunge la JMT, kwa njia ya kura za siri, kuwa Spika wa Bunge la JMT.

Hawa jamma vilaza kweli kweli, spika S.6 akiondolewa uanachama wa CCM an hivyo kupoteza ubunge, hawezi kupoteza uspika kwa 'automation', isipokuwa hadi kura zipigwe bungeni; kwanza za kutokuwa na imani naye, na halafu za kumpata spika mpya iwapo S.6 atashindwa katika kura za kutokuwa na imani naye."

Poleni vilaza wa mtandao wa CCM-fisadi.
 
Saizi harudi tena bungeni atapita vipi beki za mwakalinga ? hata bao la kuotea hatapata na alivyo foward butu.teh teh teh
Taratiibu mnaanza kuhama kwenye mada,mnataka mturudishe kuleeee kwa Mwakyembe Vs Mwakalinga.....
 
Hakuna dogo katika siasa.

Kiongozi anaweza akawa yupo physical lakini uwepo wake katika execution ukawa haupo. Kimya kingi cha kiongozi hujaza watu mashaka mashaka. Tukumbuke kiongozi ndo anatoa mwelekeo. Imagine a scenario katika medani ya kivita ambayo kiongozi wa msafara anakaa kimya sehemu inayodai order kutoka kwake.

Itakuwa balaa kama tukiendelea kukaa kimya kama hatuyaoni yanayotuzunguka au kama vile hatujui kuongea wakati tuna uwezo wa kuzungumza masaa ishirini na manne bila kuchoka
 
Sophist,

Mkuu nakubaliana na wewe sana tu ila lazima utambue kwamba ikiwa Sitta atanyang'anywa uanachama wa CCM atakuwa amepoteza Ubunge wake na hatuia inayofuata ni kupigwa kura bungeni ambako wajumbe wa CCM ndio majority.. Hivyo dhahiri Wapambanaji tutashindwa kwani ikiwa chama kimefikia maamuzi hayo wabunge wengi kama sii wote itabidi waheshimu maamuzi ya chama kwa kuogopa kutopewa nafasi mwaka 2010. Nina hakika hakuna mbunge atakayekubali kuzikwa kaburi moja na Sitta.

Kitakacho fuatia ni aidha Sitta kujiuzuru yeye mwenyewe kama alivyofanya Spika wa UK au kupigiwa kura bungeni.. Matokeo yake ni ushindi kwa Mafisadi..

Kitu kimoja tu ambacho wengi wanashindwa kukielewa hapa ni kwamba Upinzani ndani ya CCM si kati ya Mafisadi na wasiokuwa Mafisadi, wema against mashetani ila ni kati ya Lowassa, RA na kundi la viongozi waliopiga chini against JK. Hawa watu wanataka kurudi ktk Uongozi kwa nguvu zote na wapo wajinga wanaofikiria kuna Uwezekano mkubwa wa Lowassa kurudi kutokana na nguvu ya fedha..

Kwa hiyo wajumbe wote ndani ya CCM wamejipanga kwa makundi haya, ila nasikia kundi la Asilia limejipanga na JK, na usitegemee Siita kuondolewa wala kunyang'anywa kadi kwani Mh. Mwinyi, Makamu mwenyekiti mzee wangu P. Msekwa na Mh. Kinana wote hawa wapo kundi la JK... Mchezo umekwisha yote yanayozungumzwa ni vioja vilivyotokea ktk mkutano mkuu lakini hakuna mjumbe hata mmoja anayefahamu kinachoendelea na baraza lile.
.
Ila hofu ayngu kubwa ni kwamba baraza hilo litoe Onyo mapema kwa makundi yanayotaka kuigawa CCM kwa sababu Sitta hakuwa mwanzilishi wa mgawanyiko ndani ya chama ila wajumbe wenyewe ndio walichagua kumfuata shetani au kubakia na imani ya chama. Maswala mazito kama Richmond, Sitta asingeweza kabisa kuyakwamisha ikiwa JK mwenyewe kisha chagua tume maalum (ya IKULU)kuyashughulikia. Kifupi wamekwisha mkuu wangu kilichobakia ni watu kujipanga tu...

Vyama vya Upinzani, huu ndio wakati wenu mzuri wa kushambulia kwani CCM wameshusha ngao zao na focus yao ni ugonvi wa ndani...Utumieni muda huu kujitangaza vizuri badala ya kuingilia yanayotokea ndani ya CCM..mtakuja pigwa kisu cha mbavu ktk ugonvi usokuwa wenu.. waachieni wananchi tulonge kwa niaba ya haki na katiba.. Mnapoteza muda kutetea na kujadili hoja za chama CCM. wakati mnatakiwa kujipanga na kutumia nafasi hii ambayo nyati wawili wanagombana.

Kwa mtazamo wangu CCM wana kila haki ya kumzungumzia Sitta kama mwanachama wa CCM na wanayo haki kikatiba kumweka kitimoto akiwa kama mwanachama wa CCM..
 
ama kweli mungu mkubwa..ubarikiwe sana ndugu yetu mwana wetu kijana wetu na mzee wetu FMES kwa kutuletea haya mambo ya ndani ya CCM..tunaamini kuwa ni ya ukweli mtupu unless mtu mwingine ajitokeze na kulipinga hilo na atupe data nyingine tofauti...kinyume ya hapo tunaa mini hayo ndio yanayozungumzwa kwenye vikao vya juu kabisa vya chama kilichoshika dhamana ya kuiongoza nchi yetu..........watanzania wenzangu tuna shida kubwa sana inayotukabili katika safari yetu ya nchi tunayotamani..kwa namna hii na upuuzi huu unaoendelea kwenye vikao vikubwa vya aina hii..safari bado ni ndefu,wale askari wetu tuliowatuma wakapigane naona sasa wanaenda kuzidiwa nguvu...sasa wakuwasaidia ni sisi wenyewe tulio watuma kazi hii nzito..embu tuanzie na zile kura za 2010, sababu hamna silaha nzito na ya hatari katika haya mapambano kama kura....na wenye mamlaka ya kutoa kura hiyo ni sisi wananchi..emb tuungane tuwasaidie wenzetu kwenye hii vita kwa staili hiyo na hakika ushindi utakua ni wetu...ANGAMIZA wote wanaojaribu kuwaangusha makamanda wetu...tunatakiwa TUWAPOTEZE kabisa!!!
 
..wananchi mzingatie sana manung'uniko ya Dr.Mwakyembe.

..kwanza, anashangaa msimamo na muelekeo ambao Mwenyekiti wake ameamua kuchukua.

..pili, alitarajia malipo fulani lakini sasa anasikitika kwamba alichokipata sicho alichotarajia.

NB:

..ufisadi CCM ni sawa na cancer ambayo imesambaa na kushambulia viungo vyote muhimu ktk mwili.
 
..wananchi mzingatie sana manung'uniko ya Dr.Mwakyembe.

..kwanza, anashangaa msimamo na muelekeo ambao Mwenyekiti wake ameamua kuchukua.

..pili, alitarajia malipo fulani lakini sasa anasikitika kwamba alichokipata sicho alichotarajia.

NB:

..ufisadi CCM ni sawa na cancer ambayo imesambaa na kushambulia viungo vyote muhimu ktk mwili.
Jokakuu,
Mkuu hata wewe ungetegemea kupata kinga ya rais ikiwa umeifanya kazi ulopewa ipaswavyo..
Tunachokosea sisi Watanzania tunafikiria kwamba kiongozi bora ni yule Mbunifu wa idea na kisha mtendaji mkuu yaani Mwakyembe ndiye angeanzisha vagi la Ufisadi na kulifikisha hapo lilipo.. Hapana mkuu wangu kapewa kazi na kaifanya kwa uadilifu kama ilivyotakiwa, sasa inapofikia kushutumiwa na wabunge wakati JK mwenyewe alimpongeza wakati mapazia ya Ikulu yamefunikwa, ulitemegea Mwakyembe aseme kitu gani!.
Kwanza hakuna mtu mwenye guts za kusimama pale akamwambia JK kama alivyosema Mwakyembe... Sii Spika wala Malecela wote walikuwa wakitazama sinema na popcorn zao pembeni..
Now, alichotaka kuzawadiwa Mwakyembe ni JK kuonyesha kuridhika na kazi aloifanya Mwakyembe hadharan, na hakuna sehemu ya muhimu kama pale ..yeye ndiye alowatuma kusafisha vagi la Richmond na kazi ilikamilika..ila asichokifahamu Mwakyembe ni kwamba yeye ni Chale wa rais, kama wale machale wa sinema za Kichina.

JK hajawahi kusema in Public kusifia tume zake au mtu yeyote katika maswala yote ya Ufisadi, lakini kisha defend baadhi ya watu in public pamoja na kwamba anajua kuwa Ufisadi upo na majina yao yote yako mezani kwake Ikulu.
 
Last edited:
ni kweli kabisa, mtu kama kusila hategemewi kuwa na jipya zaidi ya kutegemea fadhila za ccm na kuishia kupiga makofi tu.
 
Ni dhahiri kuwa JK ameshazidiwa nguvu. kama anashindwa kutoa msimamo katika chama, basi hatuna kiongozi wa nchi


Kwani ulikuwa hujui? Hili lilikwisha dhihilika toka zamani!! Udanganyika wetu ndio unatufanywa tunyanyasike.
 
Mkandara said:
Jokakuu,
Mkuu hata wewe ungetegemea kupata kinga ya rais ikiwa umeifanya kazi ulopewa ipaswavyo..
Tunachokosea sisi Watanzania tunafikiria kwamba kiongozi bora ni yule Mbunifu wa idea na kisha mtendaji mkuu yaani Mwakyembe ndiye angeanzisha vagi la Ufisadi na kulifikisha hapo lilipo.. Hapana mkuu wangu kapewa kazi na kaifanya kwa uadilifu kama ilivyotakiwa, sasa inapofikia kushutumiwa na wabunge wakati JK mwenyewe alimpongeza wakati mapazia ya Ikulu yamefunikwa, ulitemegea Mwakyembe aseme kitu gani!.
Kwanza hakuna mtu mwenye guts za kusimama pale akamwambia JK kama alivyosema Mwakyembe... Sii Spika wala Malecela wote walikuwa wakitazama sinema na popcorn zao pembeni..
Now, alichotaka kuzawadiwa Mwakyembe ni JK kuonyesha kuridhika na kazi aloifanya Mwakyembe hadharan, na hakuna sehemu ya muhimu kama pale ..yeye ndiye alowatuma kusafisha vagi la Richmond na kazi ilikamilika..ila asichokifahamu Mwakyembe ni kwamba yeye ni Chale wa rais, kama wale machale wa sinema za Kichina.

JK hajawahi kusema in Public kusifia tume zake au mtu yeyote katika maswala yote ya Ufisadi, lakini kisha defend baadhi ya watu in public pamoja na kwamba anajua kuwa Ufisadi upo na majina yao yote yako mezani kwake Ikulu.

Mkandara,

..kwa jinsi nilivyoiangalia hii picha nadhani JK yuko upande tofauti na Mwakyembe.

..tatizo letu wengi tunatafuta kila njia ya kujiaminisha kwamba JK yuko upande wa kina Mwakyembe, Mengi, na Kilango.

..kama JK angekuwa anapinga ufisadi, basi angewasafisha mara moja, kwasababu Raisi wa Tanzania ana madaraka makubwa sana.

..kama JK alimpongeza Mwakyembe kwa kazi nzuri wakati wa faragha ni nini kinachomshinda na kumpongeza na kumlinda ktk vikao rasmi kama NEC.

..serikali ya JK imeshindwa hata kutekeleza mapendekezo ya Tume ya Mwakyembe. kwangu mimi hicho ni kithibitisho kwamba JK hakubaliani na kazi iliyofanywa na Mwakyembe na wenzake.

..tatizo langu na Mwakyembe ni kuendelea kwake kumbembeleza na kujikomba kwa JK wakati anaona kabisa kwamba JK alimtapeli kama ni kweli kama unavyodai kwamba alimpongeza kwa kazi nzuri.

..alichopaswa kufanya Mwakyembe kama kweli yeye ni mpiganaji ni kuita a spade a spade. he needs to come out and tackle JK head on kwamba yeye[JK] sasa ndiyo kikwazo cha kuwashughulikia mafisadi.

..sasa hapo ndipo unapoona kwamba hata hawa tunaoita Mashujaa ni wabangaizaji tu. walitaka malipo fulani, ambayo mimi nadhani ilikuwa ni kukaribishwa ktk mlo wa mafisadi.

..as long as hakuna anayemtishia JK kuchukua hatua, basi hii inayoitwa vita ya mafisadi ni makelele matupu.

..JK hawezi kuchukua hatua wakati Mengi,Kilango,Malecela,Mwakyembe siku zote wakifungua midomo yao wanaimba sifa za jinsi JK alivyo Jemedari Mkuu wa vita dhidi ya mafisadi. hatua gani anazochukua wakati amekataa kutekeleza mapendekezo ya tume ya Mwakyembe? hivi hamuoni kwamba ni USANII tu unaendelea hapa?
 
Field Marshall Es!

NB: Wajumbe wengi wa kikao hicho wanajiuliza swali moja muhimu, kwamba kwa nini Rais aliruhusu kutokea kwa yote yaliyojiri kwenye hiki kikao?


Novmba ndio mwezi wa kuweka bayana uamuzi wa Richmond, na kwakua muungwana amekwishaguswa na ikulu ikajikanyaga kumtetea lililobaki ni moja tu mabavu lazima yatumike kuzima ishu....karamagi alishasema wakati fulani yuko tayari kuweka bayana kama atakabla, na mwakyembe alishasema watasema yote hata yaliyofichwa...na ndo kuchekela na kila kitu vikatokea huko....Novemba ndio wtajua nchi hii ni yetu soteeeeee
 
Jokakuu,

Interest za rais comes first.. kuwasafisha kina Spika hana haja maadam wanabakia ktk nafasi zao. Sitta akiendelea kuvaa joho lake joto la jiwe watalipata huko bungeni na nina hakika wengi wa watu hawa hawatarudi..Ndio imetoka hiyo!

Mkuu wangu ktk Utawala maneno matupu hayajengi wala hayafanyi kazi isipokuwa position uloshika ktk mashambulizi..Rais angetakiwa kumtetea Sitta tu kama ingefikia hatua ya kumwondoa Sitta uanachama kama vile JK alivyosimama ilipofikia hatua ya kumsimamisha Mkapa mahakamani.

Mwakyembe ni ushabiki wake tu unajua tena Machale hawakosi kuichangia mada. Lakini hakuna haja ya JK kumsafisha Mkapa wala mjomba wake kwani what is at stake ni utawala wake yeye, Mwakyembe na Sitta ni mabehewa tu..Behewa bila kichwa halina faida.
 
Sitta akisema liwalo na liwe watamfukuza chama kweli? Kama wanamfukuza basi CCM wamejipalia mawe ya moto for 2010 wazi wazi. Kwa sasa watanzania wameenda shule na wanajua lipi jema na bovu. kazi ipo CCM kubalini you are loosing it

...wangekuwa wanajua jema na bovu CCM wasingekuwa madarakani!
 
Back
Top Bottom