Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

tingatinga maana yake linachimba barabara halafu ikiwa nzuri linazuiwa kupita..kwi kwi kwi
btw mwambieni Mwakalinga atafute jimbo lingine mapema Mwakyembe injini kubwa!

Injini kubwa wapi mafisadi wamemtowa jasho,kama yeye ngangari asingelia kwa mwenyekiti angmtolea mimacho ,harafu katupa kadi la kijani chini na kanyata kidume kutoka nje.Lakini wapi bwana?

Kwanza hajui kujenga hoja ,hoja za kitoto alijenga yani mfano ulinipa embe mwaka jana na leo unakuja kuniomba yai nikakunyima eti unaniambia unajuwa mwaka jana mimi nilikupa embe, west of kaloliz ,ninajuwa ulipa embe lakini mimi nimaamuwa kukunyima yai then what?

ukubwa dawa tinga tinga ndo linaelewa siasa kulinganisha na ngoma zilizokuwa humo ndani
 
Injini kubwa wapi mafisadi wamemtowa jasho,kama yeye ngangari asingelia kwa mwenyekiti angmtolea mimacho ,harafu katupa kadi la kijani chini na kanyata kidume kutoka nje.Lakini wapi bwana?

Kwanza hajui kujenga hoja ,hoja za kitoto alijenga yani mfano ulinipa embe mwaka jana na leo unakuja kuniomba yai nikakunyima eti unaniambia unajuwa mwaka jana mimi nilikupa embe, west of kaloliz ,ninajuwa ulipa embe lakini mimi nimaamuwa kukunyima yai then what?

ukubwa dawa tinga tinga ndo linaelewa siasa kulinganisha na ngoma zilizokuwa humo ndani


Mkuu lakini umesoma alivyomtolea mimacho mwenyekiti wake...kwi kwi kwi
Hoja gani ya kugawiana mayai unayozungumza hapa?Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni jamani.Mwakyembe ni arrogant lakini namkubali manake arrogance yake anaitumia vizuri!
 
Injini kubwa wapi mafisadi wamemtowa jasho,kama yeye ngangari asingelia kwa mwenyekiti angmtolea mimacho ,harafu katupa kadi la kijani chini na kanyata kidume kutoka nje.Lakini wapi bwana?

Kwanza hajui kujenga hoja ,hoja za kitoto alijenga yani mfano ulinipa embe mwaka jana na leo unakuja kuniomba yai nikakunyima eti unaniambia unajuwa mwaka jana mimi nilikupa embe, west of kaloliz ,ninajuwa ulipa embe lakini mimi nimaamuwa kukunyima yai then what?

ukubwa dawa tinga tinga ndo linaelewa siasa kulinganisha na ngoma zilizokuwa humo ndani

MkamaP,

Wala usihangaike na hao Ze Comedy, wala huyo shujaa wao hakuwa na hata courage ya kuongea kwenye NEC. Mengi yanayoandikwa hapa ni kufurahishe kijiwe sawa na yale ya CHADEMA kushinda kule Biharamulo.

Jamaa nasikia wamejificha kwa aibu maana watu wanawaambia kama wanajali maslahi ya wananchi si wangesema chukueni kadi zenu?
 
- Mwalimu bwana hapa ndipo ninapomkumbuka sana, maana yeye alikuwa na tabia moja ya ajabu sana lakini nimegundua kua ilikuwa ni saafi sana, yeye mijitu mizima yenye wake na watoto kama hawa kina Kusila na Guninita, alikuwa akiisubiri yakimaliza kutema sumu zao, anayaita Ikulu kwa chakula,

- Yalivyo majinga yanakambilia nyumbani kujivalisha vizuri kuwahi pilau la Ikulu, yakifika kule yanamkuta Mwalimu anayasubiri, Guess what! Mwalimu anayakaribisha na kuchomoa fimbo chini ya desk lake, na kuyaambia yainame chini haraka sana na kuanza kuyalamba bakora kama matoto madogo garademiti!

I mean what else can you do na haya maguo guo, chapa bakora tu shwaini!

Respect.


Field Marshall Es!

Kaka hivi Kusila si ndiye mwenyekiti wako kule jimboni ama? Angalia yale macho ya simba jizee yasije chagua ajenda moja tu hapo 2010. Kumfundisha adabu a.k.a FMES...

omarilyas



omarilyas
 
Mkuu lakini umesoma alivyomtolea mimacho mwenyekiti wake...kwi kwi kwi
Hoja gani ya kugawiana mayai unayozungumza hapa?Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni jamani.Mwakyembe ni arrogant lakini namkubali manake arrogance yake anaitumia vizuri!

atupe kadi la kijani chini kama mrema kama kweli yeye ni kidume
 
Akiwakimbia atawapa kichwa halafu watammaliza kiurahisi.Acha apambane nao akiwa humohumo ndani!

sasa atapambana vipi? umesoma ule mwongozo waliotoa?? ni marufuku kusemasema nje ya vikao vya ccm ,sasa atapambania wapi?
 
Huyu binafsi nina muona kama ni mmoja ya wa Tanzania ambao wanajua ni nini na ni nani na wapo bungeni kwa ajili ya nani.Ni vema wadau mkapitia na kuona maoni yake dhidi ya NEC.

HALI ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) bado tete, mbali ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho kuonya baadhi ya wabunge wanaokiuka na kwenda kinyume na maadili ya chama.

Onyo hilo linalodaiwa kutaka kulinyamazisha kundi la wabunge wanaoonekana vinara wa vita dhidi ya ufisadi limeonekana kugonga mwamba na kupingwa na baadhi ya makada wa chama hicho.

Akizungumza na gazeti hili jana, Mbunge wa Maswa Bw. John Shibuda (CCM) alisema haina maana kuwanyamazisha wabunge na kwamba Watanzania wanahitaji ufafanuzi juu ya kauli ya NEC kwamba Bunge limekuwa likikidhalilisha chama na Serikali.

"Vitu gani vilivyosemwa bungeni vimekidhalilisha chama mbele ya umma na kupoteza kura kwa wanachama wake kama kuna mtu mmoja mchafu lazima tumsafishe ili chama kibaki safi," alisemma Bw. Shibuda.

Bw. Shibuda alisema kuwa Watanzania wanahitaji kuambiwa ni udhalilishaji gani ambao umefanywa na Bunge kwa CCM na Serikali kiasi cha baadhi ya makada katika mkutano huo kumtaka Spika Samuel Sitta kujiuzulu.

"Mimi nitakubaliana na uamuzi huo wa NEC kama tutaoneshwa ni Katiba gani ya nchi au chama ambayo wabunge tumekiuka kwa kuikosoa na kuisimamia Serikali bungeni?" Alihoji Bw. Shibuda na kuongeza kuwa;

"Napata shida kuyaamini hayo yaliyotolewa kwa vyombo vya habari na hata mengine yanayoandikwa, lakini kama ni kweli basi yanapingana na katiba zote, ya nchi na ile ya chama, ambao zinaeleza wazi kazi ya mbunge na mwanachama."

Bw. Shibuda alisema chama cha siasa ni imani hivyo kumnyang'anya kadi mwanachama haina maana ya kuwa amemuondolea imani ya chama chake kwani kumfukuza Padre kanisani si kumnyang'anya Ukristu wake.

"Wabunge wanatakiwa kuwa kama manabii na mitume ambao hawakumwasi Mungu kutokana na mapambano ya Wafalme. Wabunge pia hawapaswi kuogopa vita hii kwani wamekula kiapo kuwatetea wanyonge!" alisema.

Akinukuu Ibara ya 63 kifungu cha 2 cha Katiba ya nchi, alisema imeelezwa wazi kazi za wabunge kuwa ni kuikosoa na kuisimamia Serikali ambapo CCM pia inawahimiza wanachama wake kusema kweli daima na kujibidisha kutafuta elimu na maarifa kwa ajili ya kuwatumikia Watanzania.

"Sasa wabunge kuikosoa serikali tatizo liko wapi?" alihoji Bw. Shibuda na kuongeza kuwa wabunge walioamua kujitosa katika mapambano dhidi ya ufisadi na watendaji wazembe wa Serikali hawapaswi kukata tamaa.

Aliwataka kutorudi nyuma kwani kufanya hivyo ni kusaliti katiba waliyoapa kuilinda, kitu ambacho ni sawa na uhaini mbele ya umma wa Watanzania.

Bw. Shibuda alisema kuwa Bunge la sasa chini ya mfumo wa vyama vingi kazi yake ni kujenga fikra endelevu na watu wenye uwezo wa kuchambua mambo tofauti na zamani ambapo lilikuwa chombo cha kupitishia habari kutoka kwa Baraza la Mawaziri.

"Bunge la leo lina wanaharakati wa fikra, maarifa, elimu mchanganyiko na uzoefu hivyo walioko Serikalini wanapaswa kuwa na sifa hizo pia ili kuweza kuhimili hoja zinazotolewa na siyo kulalamika kuwa wanadhalilishwa kwani majadiliano ni nguvu za hoja!" Alisema Bw. Shibuda

Alihoji kuwa "Kwanini watu wachache wenye pesa waachiwe wayumbishe chama ?"Alishauri kuwa watu hao pamoja na waganga njaa wanapaswa kufukuzwa mara moja ili wabaki maskini jeuri wasikubali kununuliwa kwa maslahi ya watu binafsi."

Alisema Rais Kikwete anakielewa chama vizuri na pindi inapotokea misukosuko kama hiyo ni faida kwa mwalimu kupata ubunifu wa kuleta somo mbadala.

"Mimi simsemei Rais lakini namfahamu ameruhusu yatokee hayo ili akija kuchukua hatua watu wasilalamike ndiyo maana hakuruhusu Spika ang'olewe kwani alijua kuna upungufu," alisema na kuongeza kuwa;

"Bunge legelege huzaa Serikali legelege ndiyo maana Bunge la leo siyo kama la zamani lililokuwa likifuata itikadi na fikra ya chama kimoja.

kauli ya Bw. Shubuda imekuja baada ya NEC iliyokutana mjini Dodoma hivi karibuni kuunda kamati ambayo imepewa jukumu kuhakikisha wabunge wa CCM na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wanarudi katika nidhamu ya chama na kuacha malumbano yanayotoka na hoja nzito za kuikosoa na kuisimamia serikali.

Akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni mwishoni mwa kikao hicho Katibu wa NE, Itikadi na Uenezi Bw. John Chiligati alisema kuwa kamati hiyo itachunguza kiini cha wabunge wake kuwashambulia mawaziri bungeni na kutoa kashfa mbalimbali bila kuzingatia maadili ya chama.
 
Huyu Shibuda simfahamu vizuri lakini kauli zake za hivi karibuni hasa kuhusiana na mafisadi zinanifurahisha sana. Kama ataweza kupambana na kundi la mafisadi ndani ya chama na Serikali basi atahitaji msaada mkubwa sana toka kwa Watanzania. Pia kwa hali ilivyo nchini hivi sasa nahofia hawa wapiganaji dhidi ya mafisadi ndani ya CCM maisha yao yako hatarini, mafioso waliomo ndani ya CCM na Serikali wanaweza kabisa kutishia uhai wa hawa wapiganaji.
 
Date: 8/20/2009

Wabunge CCM kuendelea kupambana na ufisadi

Leon Bahati na Exuper Kachenje
Mwananchi


SIKU chache baada ya Halmashauri Kuu ya CCM (Nec) kuwaonya wanachama wanaopambana na mafisadi hadharani, wabunge kadhaa wa chama hicho wamesema hawatasalimu amri na badala yake wataendelea kupinga ufisadi popote bila kujali onyo hilo.

Wakati wabunge hao wakiitunishia misuli Nec, Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk Milton Makongoro Mahanga amefurahia uamuzi wa Nec akisema umetolewa kwa kadri alivyotarajia.

Wakizungumza na Mwananchi wabunge ambao wamekuwa wakitoa tuhuma mbalimbali za ufisadi ndani na nje ya Bunge walisema wataendelea 'kufa' na mafisadi na kwamba tamko hilo kamwe haliwezi kuwatisha.

Nec ilitoa tamko Agosti 17 mwaka huu baada ya kumaliza kikao chake mjini Dodoma, ikipiga marufuku viongozi na wanachama wake kuishambulia serikali bungeni, ikidai kuwa vita ya ufisadi ni ya chama na si ya kikundi cha watu wachache ndani ya chama hicho. Nec iliunda timu ya watu watatu kuwafuatilia wabunge wenye tabia hiyo.

Mkutano huo pia ulimweka kitimoto Spika wa Bunge, Samuel Sitta huku wajumbe wakitaka anyang'anywe kadi yake ya uanachama kwa madai kuwa ana ruhusu na kushabikia mijadala inayoiweka serikali kwenye hali ngumu.

Mbunge wa Vunjo (CCM), Aloyce Kimaro, mmoja wa wabunge wanaotaka suala la tuhuma dhidi ya rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa kuhusu mgodi wa Kiwira lishughulikiwe, alisema: ”Sidhani kama kuna mtu amefungwa mdomo na Nec.

Mdomo upo palepale na watu wataendelea kuongea. Nec haiwezi kumfunga mdomo spika wala wabunge. Haya ni mabadiliko muhimu ambayo CCM lazima ipitie, ili kuondoa rushwa.”.

Mbunge huyo kutoka mkoa ambao CCM imekuwa ikipata shida kwenye uchaguzi, alisema kwa mujibu wa sheria na kanuni zake hakuna mtu nje ya Bunge la Jamhuri ya Muungano mwenye uwezo wa kumfunga mdomo spika wala wabunge kuzungumzia ufisadi, isipokuwa bunge lenyewe.

Alisisitiza kuwa, ili CCM iondoe rushwa nchini na ambayo hata Rais Jakaya Kikwete anakiri kuwa ipo, lazima ikubali kupitia kipindi hiki ambacho kitaendelea kuwepo mpaka mambo yatakapokaa sawa hapo baadaye.

“Tumeisikia Nec, lakini wavumilie tu kwani lazima mabadiliko yatokee. Wananchi ndio wenye chama na ndio wanaotaka wabunge wao wapambane na uovu na ufisadi,” alisema Kimaro.

Alisema ni lazima watuhumiwa wa rushwa wafikishwe mahakamani.

Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, ambaye pia ni mmoja wa vinara wa vita dhidi ya ufisadi, aliwataka wananchi kuondoa shaka kuhusu uamuzi huo wa Nec akisema kuwa wao kama wabunge wako imara na wataendelea kutetea maslahi ya wananchi bila kuogopa.

"Katiba ya CCM inaeleza vizuri kuhusu ufisadi na inaeleza wazi kwamba, rushwa ni adui wa haki. Pia inakataza mtu kutumia cheo chake ili kujinufaisha," alisema Ole-Sendeka na kuongeza kuwa tayari kifungu hicho kimempa rungu dhidi ya mafisadi.


Ole-Sendeka alisema alikuwa hajasoma magazeti ili kuona maazimio hayo ya Nec, lakini anaamini kuwa CCM imeweka misingi ya kupambana na rushwa hivyo hakuna kitakachomzuia kusema ukweli kwa manufaa ya wananchi.

Kauli yake iliungwa mkono na mbunge wa Bumbuli, William Shelukindo ambaye alisema kama wabunge wakikaa kimya katika maslahi ya nchi, watakuwa hawawatendei haki wananchi ambao wanawawakilisha na kuwatetea mbele ya serikali.

Alitoa mfano wa suala ambalo wabunge hawatarudi nyuma katika kuibana serikali kuwa, utekelezaji wa maazimio ya Bunge kuhusu kashfa ya utoaji wa zabuni ya umeme wa dharura kwa kampuni tata ya Richmond Development LLC.

Katika sakata hilo, kamati teule ya Bunge iliyokuwa chini ya mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe ilitoa ripoti iliyomtaja waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa na kusababisha ajiuzulu na baadaye kufuatiwa na mawaziri wawili, Nazir Karamagi na Ibrahim Msabaha.


Bunge pia lilipitisha maazimio ambayo baadhi hayajatekelezwa, kiasi cha kuufanya mkutano uliopita uiagize serikali kuwasilisha taarifa ya utekelezwaji wa maazimio hayo kwenye mkutano ujao wa Novemba.


Kwa upande mwingine, Shelukindo aliiunga mkono Nec kwamba, kuna haja ya wabunge kudhibitiwa kwa sababu wengine wamefikia hatua hata ya kuwakejeli viongozi wa serikali badala ya kutumia hoja katika kujenga hoja.

Uamuzi huo wa Nec umetolewa baada ya mkutano uliopita wa Bunge kuwa moto kutokana na wabunge wengi, hasa wa chama tawala kuikalia kooni serikali, na hasa Baraza la Mawaziri wakilituhumu kwa kubariki mikataba ya ufisadi na kuweka kipaumbele kwenye miradi inayohusu maeneo yao.

Naye Dk Mahanga alielezea kufurahishwa na uamuzi wa Nec wa kuzuia “wasema ovyo” katika vita dhidi ya ufisadi, akisema busara zake zilishaona hilo, anaripoti Leon Bahati.

Mahanga alijikuta kwenye kiti moto baada ya kuingilia mjadala wa hali ya CCM kwenye uchaguzi ujao, ambao ulianzishwa na makamu mwenyekiti wa zamani wa CCM, John Malecela ambaye alisema tuhuma za ufisadi dhidi ya wanachama wa chama hicho utawaweka pabaya baadhi ya wabunge kwenye uchaguzi wa mwaka 2010.

Mahanga, bila ya kuwataja waliomuunga mkono Malecela, alisema wale wanaotoa tuhuma za ufisadi bila ya kuwataja majina watuhumiwa, au kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria au kuwashtaki ndani ya chama, wanafanya kazi ya upinzani ya kuichafua CCM na hivyo akawashauri wajitoe kwenye chama hicho tawala.

Jana Dk Mahanga, ambaye ni Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, alisema suala hilo lilikuwa linamkera na kwamba uamuzi wa Nec wa kudhibiti wanaopinga ufisadi hadharani, ikiwa ni pamoja na kwenye vikao vya Bunge, umeunga mkono yale aliyoyaeleza.

Dk Mahanga alizungumza hayo kwenye mahojiano na gazeti hili jana, alisema kauli yake haikuwa ni utabiri bali ni busara ambazo mtu yeyote makini angeweza kuzitoa baada ya kutafakari mwenendo wa chama pamoja na vita dhidi ya ufisadi.

“Mtu yeyote ambaye anatafakari kwa makini jinsi hali ilivyokuwa, atakuwa na jibu kuwa suala la kuropoka ropoka tu na kutuhumiana kwa ufisadi, siyo njia sahihi na kamwe hakusaidii chama bali kukiharibu,” alisema Dk Mahanga.

Njia sahihi, alisema, ni malalamiko kushughulikiwa kulingana na taratibu za chama na siyo kuyasema majukwaani ili kuufurahisha umma.

Baadhi ya wabunge ambao pia walizungumza na gazeti hili na kuomba majina yao yasitajwe gazetini kwa vile wao si wasemaji, walipinga vikali tamko la Nec.

Walisema suala la ufisadi siyo la kuficha na mbunge yeyote ana haki ya kufanya hivyo kwa maslahi ya wananchi.

Walisema suala la kufichaficha mambo na kuoneana huruma litaendelea kulea ufisadi na kwamba, atakayeumia ni mwananchi hasa wa kipato cha chini.

"Hivi mbona hatuwaonei huruma Watanzania hawa wanaovuja jasho kwa kodi, halafu lijitu, tena lenye uwezo wa kifedha linachukua mali zao na kujilimbikizia! Sisi viongozi ni lazima tufike mahali tuwaonee huruma walalahoi hawa," alisema mmoja wa wabunge hao.

Uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwa hata Spika Samuel Sitta ambaye alikuwa kwenye wakati mgumu wakati wajumbe wapatao 22, walipopendekeza atimuliwe kwenye chama, bado ana msimamo wa kuendeleza vita ya ufisadi.

Wakizungumza na gazeti hili jana, watu waliokaribu na Sitta walisema mbunge huyo wa Urambo Mashariki hawezi kudhibitiwa kwa kauli hiyo ya Nec, hasa ikizingatiwa analiongoza bunge kulingana na kanuni na taratibu ambazo zipo kwa mujibu wa katiba ya nchi.

"Mbunge hawezi kusimama kutoa hoja yenye maslahi kwa wananchi, halafu spika amuambie : "kaa chini!"

Alisema kitendo hicho kitakuwa ni udikteta na kuonya kuwa wabunge wana kanuni ambazo wanaweza kuzitumia, ili kumdhibiti spika.

"Kama kuna watu serikalini au wabunge wanaofurahia msimamo huo wa Nec, wajue wanajidanganya kwa sababu hauna nguvu yoyote ya kudhibiti uhuru wa bunge," alisema.

"Bunge lina nguvu ya kujadili mambo ambayo si spika wala Nec wanaoweza kuyazuia."

Kuhusu tamko lililotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chiligati kwamba "Bunge limeanza kuwa kama mchezo wa kikundi cha televisheni cha vichekesho kinachojulikana kama The Comedy, wabunge hao walisema kwamba hiyo ni dharau inayoonyesha kejeli, dhihaka na fedheha kubwa kwa bunge mbele ya wananchi.

"Kama suala ni uhuru ambao umefanya wabunge kuvuka mipaka na kila mmoja kuamua kufanya lolote bungeni, basi Nec isingesema na kuacha tu hewani. Ingeorodhesha kanuni zilizovunjwa na wananchi wakaelewa," alisema mmojawao.

Akitangaza maamuzi ya Nec, Chiligati alisema: “Bunge limeanza kuwa kama mchezo wa (kikundi cha televisheni cha vichekesho) The Comedy.

“Yaani kila mtu anafanya mambo yake mwenyewe, hali ambayo inaweza kusababisha watu kurushiana hata viatu ndani ya ukumbi wa bunge. Sasa hali hii maana yake nini? “Kwa hiyo tumesema inatosha, hapo tulipofikia tusiendelee mbele. Wanaoropoka hovyo ni walevi na tumeona kuna kundi dogo ambalo limejiona kama ni wateule wa kuzungumzia sakata hilo (la ufisadi) bila ya kujua wabunge wote wana haki ya kuzungumzia suala hilo, lakini kwa utaratibu tena kwa kupitia katika vikao vya kamati za wabunge.”
 
I love the man........though he need to make sure CCM is divided in three or four pieces, Shibuda you can! t

Naogopa karibu kila kauli ya mwana CCM naona wamejipanga kuwadanganya wadanganyika, this is team work

is they are serious and they real meant to lead this country rudisheni kadi at least kusema

'I AM NOT YOU'
 
I love the man........though he need to make sure CCM is divided in three or four pieces, Shibuda you can! t

Naogopa karibu kila kauli ya mwana CCM naona wamejipanga kuwadanganya wadanganyika, this is team work

is they are serious and they real meant to lead this country rudisheni kadi at least kusema

'I AM NOT YOU'

Mkuu hii trick ya kusema rudisheni kadi ni very cheap, undemocratic na misguided. Kwanini arudishe kadi wakati anayosema yanaendana kabisa na katiba ya CCM? Nakumbuka enzi zile tulipokuwa tunaimba ahadi 10 za mwanaTANU, ambazo zilirithiwa na CCM Rushwa ilikuwa adui wa haki, lakini sasa tunaona kuwa wanaopinga rushwa ndiuo wanakuwa maadui wa CCM. Kwani chama kimepiga u-turn na kubariki rushwa??
 
Mkuu hii trick ya kusema rudisheni kadi ni very cheap, undemocratic na misguided. Kwanini arudishe kadi wakati anayosema yanaendana kabisa na katiba ya CCM? Nakumbuka enzi zile tulipokuwa tunaimba ahadi 10 za mwanaTANU, ambazo zilirithiwa na CCM Rushwa ilikuwa adui wa haki, lakini sasa tunaona kuwa wanaopinga rushwa ndiuo wanakuwa maadui wa CCM. Kwani chama kimepiga u-turn na kubariki rushwa??

Kama CCM hii hii hajabariki rushwa basi akae humohumo, katiba zipo vitabuni, zinaimbwa, zinasomwa zinajulikana, tatizo katiba inakuwa hai pale inapokuwa inafanya kazi katika ulimwengu asilia. ukisema hivyo basi hakuna neno mapinduzi maana wote madikteta, viongozi wabaya, wanajua miiko, katiba na habari zote za uzuri unaotakiwa.

CCM ya sasa inahitaji action, na kwa mawazo yako then 'elite' ya wafuasi wataendelea hivyo hivyo vizazi na vizazi!

Ikiwa kuongea tu kutatufikisha kunako , haya na tuongee tu
 
Huyu mzee ameona mbali. Amesoma alama za nyakati. Amegundua huu siyo wakati wa kukumbatia mafisadi. Siku zao zinaelekea ukingoni, wanaanza kuogopa vivuli vyao.
 
Jamani hata mimi naona ni afadhali CCM ikufukuze, kuliko wewe kuondoka. Kwa sasa hali iliyomo ndani, ni mbaya sana, kwa hiyo hata tupingwe namna gani, hatuondoki.
"Rushwa ni adui wa haki, sitatoa wala kupokea rushwa".
 
Ni kweli wadau zile zama za kusema chama kimesema naona hazina nafasi tena kama kweli wanataka kuendelea kuwa watawala hainabudi wakasoma alama za nyakati zinasema nini kuliko kubaki na mitazamo ya enzi za mwalimu.
Kuna haja wa Tanzania siku moja hata tukachagua kula mleda kuliko kuishi kwa kunusa harufu ya nyama.
 
hii vita ni ngumu na inahitaji uvumilivu ili kuishinda, kama ni kweli mzee shibuda na wenzie wakawa na misimamo yao isiyo yumba itasaidia kukivunja chama chao na hapo ndipo tutakapopata uhuru wa kweli
 
Mheshimiwa Kayanza Peter Pinda kama kweli hakuna mafisadi sisiem naomba uweke wazi ripoti ya kituo cha mabasi Ubungo.
 
Back
Top Bottom