Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,565
- 7,993
Lunyungu,
Wewe ni msanii kweli kweli, inabidi ujiunge na The Comedy. Unatunga mambo kuja kuwafurahisha JF?
Na JF ilivyo na wajinga wengi, eti wanapiga makofi.
Huyo jamaa yako hakusema chochote kwenye NEC na alipotaka kusimama alizimwa na akanyong'onyea.
Kwa taarifa yako aliaga hapa Kyela kwamba yeye ni mtu muhimu mno kwenye vikao vya NEC na kwamba afadhali wakosekana akina Prof. Mwandosya na Prof. Mwakyusa kuliko kukosekana yeye.
Pia aliahidi kurudi Kyela Jumatano kuendelea na ziara yake ya kuzima moto wa Mwakalinga. Lakini baada ya kujeruhiwa Dodoma kaingia mitini.
Wapambe wanasema jemadari kajeruhiwa, yuko msituni kutafuta mbinu nyingine.
Kyela hapa ndio mazungumzo pekee; kwamba hawa jamaa kumbe hawajali maslahi yetu maana kama wangelikuwa wanajali maslahi ya wananchi si wangelisema chukueni kadi zenu?
We engineer wewe,
umesahau kale ka msemo ka kiswahili.... "UKISUSA WENZIO TWALA"??
Lakini pia kujali maslahi ya wananchi sio lazima kuwatupia kadi zao, kwani wao tu ndo wenye chama? Suala hapa ni kwamba kwa imani hiyohiyo waliyonayo na chama chao cha kifisadi pamoja na wapambe wao, inabidi waendelee kukabiliana nao humo humo ndani ya ku-CCM.
Huo ushauri wa kuwataka warudishe kadi za CCM, inabidi uanze na Mwakalinga, mshauri arudishe kadi ya kifisadi ajiunge na chama kilicho makini na kinachojali maslahi ya wananchi. Sio mnajifanya kuwashauri wenzenu warudishe kadi ili mpate unafuu na ushindi kiulaini. Jipangeni kisawasawa, mjengoni hamuingii kirahisi ati.
Last edited: