Maajabu ya Upinzani Tanzania: CHADEMA wanashangilia ACT kuibiwa kura na CCM

Wanashangilia au kueleza hali halisi? Bila kubadilisha mifumo haya mambo hayataisha

Watu wa ajabu sana yaani wanalaumu Chadema kwa CCM kuiba kura. Kwanini hauongelei kura kuibiwa wewe unaona hiyo ni sawa ! Badala yake unaongelea watu wanaocheka wakati demokrasia inadidimizwa halafu unajifanya eti mzalendo 😂
ACT kuibiwa kura ndio kitu ambacho kilitakiwa kujadiliwa kwa nguvu na CDM na kuiuliza CCM maswali kuwa walikuwa wanamsingizia Magufuli huku wao wanafanya hayo hayo, Cha ajabu Chadema wanaipongeza CCM na kuicheka ACT
 
Kuna chaguzi ndogo zilizofanyika katika maeneo mbalimbali nchini, na Chadema waliamua kutoshiriki, ACT wao wakafanya maamuzi yao kama chama huru cha siasa kushiriki, ACT wamelalamika na kusema kuna ukiukwaji mkubwa wa taratibu za uchaguzi zimefanyiwa kwenye chaguzi hizo.

Maajabu ni kuwa viongozi wa chama kingine cha upinzani, CHADEMA, akiwemo mwenyekiti wao wa kanda ya kaskazini Godbless Lema wamekuwa wakishangilia hayo madhila waliyofanyiwa ACT na dola, huku wao wakitarajia kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu ujao katika mazingira haya haya.

Maswali yangu ni;

CHADEMA wao wamekuwa wakishiriki uchaguzi mkuu kila mwaka katika mazingira haya haya lakini ACT wao wakishiriki inawaona ni wasaliti, tawi la CCM.

CHADEMA haiamini katika uhuru wa vyama vingine vya siasa? Kwamba vyama vingine vya siasa vikifanya maamuzi kama wanavyofanya wao (kama kushiriki uchaguzi mkuu uliopita na ujao) wanakuwa ni tawi la CCM?
Chadema ni genge la wasakatonge kupitia siasa!
Kwao siasa ni kama biashara na wanapoona chama kingine kikiibuka na kuelekea kupata ushawishi mkubwa kwa wananchi.
Chadema wanaona kama wanaporwa biashara yao.

Pale Chadema mtu pekee ninayemuona akiwa na kariba halisi ya uanasiasa ni huyo J.J.Mnyika.
Hawa wengine kina Lema & the Company ni walanguzi wa kisiasa.

Sema Tanzania hatujapata upinzani wa kweli wa kisiasa.

Fikiria Chadema ilichowafanyia kina Advocate Mwabukusi pale walipoona wanaenda kuwapiku ushawishi kwa watanzania!
 
Kuna chaguzi ndogo zilizofanyika katika maeneo mbalimbali nchini, na Chadema waliamua kutoshiriki, ACT wao wakafanya maamuzi yao kama chama huru cha siasa kushiriki, ACT wamelalamika na kusema kuna ukiukwaji mkubwa wa taratibu za uchaguzi zimefanyiwa kwenye chaguzi hizo.

Maajabu ni kuwa viongozi wa chama kingine cha upinzani, CHADEMA, akiwemo mwenyekiti wao wa kanda ya kaskazini Godbless Lema wamekuwa wakishangilia hayo madhila waliyofanyiwa ACT na dola, huku wao wakitarajia kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu ujao katika mazingira haya haya.

Maswali yangu ni;

CHADEMA wao wamekuwa wakishiriki uchaguzi mkuu kila mwaka katika mazingira haya haya lakini ACT wao wakishiriki inawaona ni wasaliti, tawi la CCM.

CHADEMA haiamini katika uhuru wa vyama vingine vya siasa? Kwamba vyama vingine vya siasa vikifanya maamuzi kama wanavyofanya wao (kama kushiriki uchaguzi mkuu uliopita na ujao) wanakuwa ni tawi la CCM?
Unajiuliza maswali ya kijinga mura! CHADEMA walichokuwa wanataka ni kuwa na nguvu ya pamoja kati ya vyama vya upinzani! Ka hawara ka CCM kakaona kawakomoe CHADEMA kakasema mazingira yako sawa! Sasa yako wapo? Lema yuko sahihi kukazomea ka ACT! In short Zitto ameleta siasa za kipumbavu! CCM nayo kama hayana akili, hayajui kula na vipofu, kwenye hizi uchaguzi ndogo yangekuwa yanasimamia haki ili kuwakata kilimilimi wapinzani. Hapo yangekuwa yanapata points za kuongelea.
 
Unajiuliza maswali ya kijinga mura! CHADEMA walichokuwa wanataka ni kuwa na nguvu ya pamoja kati ya vyama vya upinzani! Ka hawara ka CCM kakaona kawakomoe CHADEMA kakasema mazingira yako sawa! Sasa yako wapo? Lema yuko sahihi kukazomea ka ACT! In short Zitto ameleta siasa za kipumbavu! CCM nayo kama hayana akili, hayajui kula na vipofu, kwenye hizi uchaguzi ndogo yangekuwa yanasimamia haki ili kuwakata kilimilimi wapinzani. Hapo yangekuwa yanapata points za kuongelea.
Chadema mbona nao wanashiriki uchaguzi katika mazingira haya haya?
Kipindi cha Magufuli si walikuwa wakisusia uchaguzi ndogo lakini wakaja kushiriki uchaguzi mkuu na mazingira yakiwa hayajabadilika?

Mwaka huu si wamesema watashiriki uchaguzi wa serikali za mitaa?
Mwakani si wamesema pia watashiriki uchaguzi mkuu ?
So Chadema wakishiriki ni sawa ila ACT ikishiriki ni nongwa?
 
Ukiwasusia nyani shamba la mahindi wanatafuna yoote kwa vigelegele.

Tatizo ni kuwa vyama vichache makini vikisusia uchaguzi, vile vyama chawa vya ccm vitashiriki, halafu itaonekana vyama vingi vimeshiriki na ccm itapewa ushindi wa "kishindo" wa mchongo kama siku zote
Kwahio tuendelee kushiriki hali ya kua tunajua atushindi
Kisa ukimsusia nyani mahindi atakula yote
Na usipo msusia kinatokea nini
 
Kwahio tuendelee kushiriki hali ya kua tunajua atushindi
Kisa ukimsusia nyani mahindi atakula yote
Na usipo msusia kinatokea nini
Mafanikio yanakuja kwa jitihada na mapambano, siyo kususa.

Kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 walijaribu kufanya hivyo, kulikuwa na impact gani?!
 
Kuna chaguzi ndogo zilizofanyika katika maeneo mbalimbali nchini, na Chadema waliamua kutoshiriki, ACT wao wakafanya maamuzi yao kama chama huru cha siasa kushiriki, ACT wamelalamika na kusema kuna ukiukwaji mkubwa wa taratibu za uchaguzi zimefanyiwa kwenye chaguzi hizo.

Maajabu ni kuwa viongozi wa chama kingine cha upinzani, CHADEMA, akiwemo mwenyekiti wao wa kanda ya kaskazini Godbless Lema wamekuwa wakishangilia hayo madhila waliyofanyiwa ACT na dola, huku wao wakitarajia kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu ujao katika mazingira haya haya.

Maswali yangu ni;

CHADEMA wao wamekuwa wakishiriki uchaguzi mkuu kila mwaka katika mazingira haya haya lakini ACT wao wakishiriki inawaona ni wasaliti, tawi la CCM.

CHADEMA haiamini katika uhuru wa vyama vingine vya siasa? Kwamba vyama vingine vya siasa vikifanya maamuzi kama wanavyofanya wao (kama kushiriki uchaguzi mkuu uliopita na ujao) wanakuwa ni tawi la CCM?
Huoni kuwa wewe ndiye una matatizo,

Badala ya kuwashangaa CCM waiba kura, unashangaa mashuhuda wa WIZI wa kura.

Una tatizo kubwa,

Jitafakari.
 
ACT ni CCM hao hao. Ngedere na Nyani wameibiana mahindi hapo kesi anapewa tumbiri aamue.
 
Sawa na hata ukishiriki kutakuwa na impact gani
Hujui kwamba baadhi ya wagombea huwa wanashinda hadi waĺishaongoza Halmashauri kadhaa?

Ule wa jiwe haukuwa wizi tu, ulikuwa ni unyang'anyi wa mchana kweupe, kwa hiyo haufai kutumiwa kama kigezo
 
ACT kuibiwa kura ndio kitu ambacho kilitakiwa kujadiliwa kwa nguvu na CDM na kuiuliza CCM maswali kuwa walikuwa wanamsingizia Magufuli huku wao wanafanya hayo hayo, Cha ajabu Chadema wanaipongeza CCM na kuicheka ACT
Ni chuki tu za kisiasa tu zinawasumbua.
 
Back
Top Bottom