Hawa wazungu wangekuwa na nia ya kumaliza ufisadi na rushwa Afrika na nchi nyingine basi wasingekuwa wanaruhusu mabenki yako kuweka hela za wizi. Wanatupiga viini macho tu!!!
Nakubaliana na wewe. Kuna 'udaku' mwingine unafanya vichwa vijisugue kutoa mawazo. Kwa mfano nilikuwa na wazo lifuatalo;
Kwa nini tusipetition hizi balozi zilizopo TZ ili zote ziwanyime viza washukiwa wote wa Richmond, EPA, BOT n.k. mpaka hapo ukweli utakapojulikana? Maana serikali haijali kwa vile wengi waliomo ni wahusika otherwise wangeharakisha kuwanyang'anya pass zao kama walivyokuwa na haraka ya kuwatia ndani moderators wa JF. Waungwana mnasemaje??
Umalizwaji wa ufisadi Afrika si wajibu wa wazungu bwana....ufisadi Afrika utamalizwa na Waafrika wenyewe lakini kwa bahati mbaya hilo haliwezekani na sababu mnaijua!!!
Hapo ni kweli tunatakiwa tuumalize wenyewe tu,Lakini yale mabenki ya Zurich,Cayman Islands na kwingineko yasingekuwa yanakubali kuweka hizi hela za ajabu ajabu,Tukiamua tunaweza chukulia mfano wa Romania walivyomuondoa Nicolae Ceausescu.
Ufisadi wa afrika unaumiza watu wa chini.
Hawa wazungu wangekuwa na nia ya kumaliza ufisadi na rushwa Afrika na nchi nyingine basi wasingekuwa wanaruhusu mabenki yako kuweka hela za wizi. Wanatupiga viini macho tu!!!
Hiyo tunatatua wenyewe tu!
Cha kufanya ni kuwapokonya hati za kusafiria.
Hawa wadaku wengine kwa nini hawaziweki hizi habari kwenye udaku? mods, tafadhali pelekeni hii habari kwenye udaku, yaani inawekwa kwenye habari mpya au kwa kimombo "breaking news" na ma mods mnakubali.
Huyu mwenzetu maesikia tetesi (kumbukeni Richmond nayo ilianza kama tetesi) na ameiweka hapa akisema bayana kuwa kama kuna mtu mwenye data zaidi aongezee.Sasa kosa lake liko wapi?How many times watu wamekuja hapa na mawazo yao binafsi ambayo definitely source ni wao wenyewe (holders wa mawazo hayo).
Udaku ni kusema Lowassa kajiunga na chadema but kusema "kuna habari/etetsi kuwa lowassa ana mpango wa kujiunga na chadema" sio udaku.Ni muhimu kila habari iwe na chanzo lakini vp kuhusu tetesi kwa mfano hiyo ya dude liitwalo AGENDA 21?Au vipi kitu kitwacho "MTANDAO" ambacho licha ya kutajwa sana hakuna mahala popote panapozungumzia dude hilo lilivyoundwa,lilikuwa/lina members wa ngapi,etc.
Tukitaka source kwenye kila posts,then hii itageuka kuwa sehemu ya ku-copy na ku-paste tu ilhali kuna habari lukuki za mtaani (na tusisahau kuwa hatuna transparent media inayoweza kuandika kila kitu).Naamini kwamba iwapo tetesi hii ingepostiwa na "jina linaloaminika" wala isingeshutumiwa namna hii.Let's be fair for our own JF's benefits.
Narudia kwamba tena kusema kwamba sababu kamili ya kunyimwa hazijawa clear .Bado nina ninatafuta uhalali wa hii habari .Nikiwa na habari sahihi nitasema ila ukweli wa kinyimwa Visa si udaku Lowasa kanyimwa Visa ya UK .
He has our diplomatic passport, does he still needs a Visa to enter UK?
MUWAJIBIKAJI ANYANG'ANYWE PASSPORT? YOU MUST BE KIDDING ME, SAA HIVI ANAUGUZA MAJERAHA YAKE YA "AJALI YA KISIASA" THE LAST THING SERIKALI WANT TO DO IS KUMUONGEZEA MAUMIVU MUWAJIBIKAJI KWA KUMNYANG'ANYA PASSPORT YAKE, OH PULIIIIIZ LETS STOP THIS DAYDREAMING BUSINESS!HIVI BADO ANAYO PASPORT??? USALAMA HAWAJAICHUKUA WAKATI TARATIBU ZA KUWAPELEKA MAFISADI MAHAKAMANI ZIKIENDELEA??
Taratibu za kuomba Viza kwa Diplomatic passport-holders ni tofauti na za akina sie. Hawa wanaombewa na foreign na hawalipii viza fees na incase watanyimwa viza balozi husika hutoa maelezo kwa maandishi kwenda foreign office.
HIVI BADO ANAYO PASPORT??? USALAMA HAWAJAICHUKUA WAKATI TARATIBU ZA KUWAPELEKA MAFISADI MAHAKAMANI ZIKIENDELEA??
The man he still have his passport . Kwa serikali yeye hana kosa kajiondoa kwa manufaa ya Chama chake alisema Bungeni.Na kumpokonya PP ni nani kati ya hao wote ? Kama Mkapa kaiba hadi kipofu kaona na yuko andunda, kama Rais kashindwa kutaja nahata kuwahukulia hatua wauza madawa na wote wa EPA na BOT nani wa kumvaa Lowasa ?Kama Rostam kagomea kamati ya Bunge na hajafanywa lolote leo umvae Lowasa na passport ?
Lowasa sio waziri mkuu tena, Dowans wanaendelea kuvuta mshiko kama kawaida na wao ni kampuni hewa vilevile, sasa hata mafaili brela wamechomwa moto, watz tumekuwa pilato tunahukumu kufuata makelele ya watu.
Naimani Lowasa ni mtu hodari tena mchapa kazi, alimtimua Bagdad enterprise pale mnazi mmoja, kamtoa baru city water, kawafurumsha ng'ombe ihefu, kasimamia mradi wa maji shy kahama.
kaanzisha sekondari kata sasa hivi hausigeli na wakata nyasi za ngombe wamekuwa adimu watoto wote wanapiga kitabu, huku vijijini asubuhi utakutana na msururu mrefu wa watoto wakiendesha baiskeli kwenda sekondari kata. Tutakuja mkumbuka sio muda mrefu.
Lowasa sio waziri mkuu tena, Dowans wanaendelea kuvuta mshiko kama kawaida na wao ni kampuni hewa vilevile, sasa hata mafaili brela wamechomwa moto, watz tumekuwa pilato tunahukumu kufuata makelele ya watu.
Naimani Lowasa ni mtu hodari tena mchapa kazi, alimtimua Bagdad enterprise pale mnazi mmoja, kamtoa baru city water, kawafurumsha ng'ombe ihefu, kasimamia mradi wa maji shy kahama.
kaanzisha sekondari kata sasa hivi hausigeli na wakata nyasi za ngombe wamekuwa adimu watoto wote wanapiga kitabu, huku vijijini asubuhi utakutana na msururu mrefu wa watoto wakiendesha baiskeli kwenda sekondari kata. Tutakuja mkumbuka sio muda mrefu.
ILE YA WEAZIRI MKUU KASHANYANG'ANYWA kwa sasa anayo passport ya kidiplomasia ya kawaida tu kama wabunge wengene nadhani ya waziri mkuu ni no 4 so hawezi kuwanayo tena