Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Am old skol nafa na Chicago Bulls .... Unakumbuka era ya namba 23 ... Waaa bald baldest conquered.

YNWA
Duh mkuu wewe ni wa old school, Kipindi cha MJ GOAT wa Bulls mimi denver niliyoanza kushangilia ni ile ya Carmelo, kizingiti chetu alikua ni Kobe Alitusumbua sana

Sasa hivi yupo Jocker na wenzake akina Jamal na Gordon, Braun amerudi wameongezwa Hardaway na Valanciunas Oktoba ifike ligi ianze

mwaka huu NBA na EPL nasheherekea kote kote😄
 
Duh mkuu wewe ni wa old school, Kipindi cha MJ GOAT wa Bulls mimi denver niliyoanza kushangilia ni ile ya Carmelo, kizingiti chetu alikua ni Kobe Alitusumbua sana
Man old skol for real...MJ was the dope after Magic wakaja na wengine Hakeem, Dennis Rodman, Scot, Marlone na kina Shawn Kemp nk then came Shaque, Mamba , Inverson conquered for real buried C Bulls then we have now we have Le Bron James ...

YNWA
 
Wachezaji Saba Waliowahi Kufunga Hat-trick kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya katika historia ya Liverpool hadi sasa (Champions League)

🔥Michael Owen

Hat-trick ya kwanza ya Liverpool kwenye Ligi ya Mabingwa ilifungwa na Michael Owen. Mhitimu wa akademi ya Liverpool alifunga mabao matatu katika mechi ya hatua ya makundi dhidi ya Spartak Moscow mnamo Oktoba 22, 2002.

Kikosi cha Gerard Houllier kilishinda 3-1 na kuonekana kuwa njiani kufuzu hatua ya pili ya makundi. Kwa bahati mbaya, walijikuta wakimaliza nafasi ya tatu kwenye kundi la timu nne na kuaga mashindano.

🔥Yossi Benayoun

Baada ya kupita miaka mitano tangu hat-trick ya Owen, Liverpool walipata nyingine kupitia kwa Yossi Benayoun, aliyeifumania Besiktas kwa mabao matatu katika ushindi wa 8-0 Anfield kwenye hatua ya makundi msimu wa 2007/08.

Liverpool waliendelea hadi nusu fainali chini ya Rafa Benitez kabla ya kutolewa na Chelsea.

🔥Philippe Coutinho

Ni miaka 10 kamili tangu hat-trick ya Benayoun kabla Coutinho kuandika yake. Tarehe 6 Desemba 2017, Coutinho alifunga hat-trick huku akiwa nahodha wa Liverpool katika ushindi wa 7-0 dhidi ya Spartak Moscow kwenye hatua ya makundi.

Ni ajabu kuwa wapinzani walikuwa tena Spartak Moscow. Liverpool waliendelea hadi fainali lakini walipoteza.

🔥Sadio Mane

Kama mabasi ya London, hat-trick za Liverpool kwenye Champions League zilikuja moja baada ya nyingine msimu wa 2017/18.
Sadio Mane alifunga hat-trick pekee ya hatua ya mtoano (knockout) katika historia ya Liverpool. Alifunga mara tatu dhidi ya Porto katika hatua ya 16 bora, na kuwasaidia Liverpool kushinda 5-0. Na jezi yao ya rangi ya machungwa ikakumbukwa sana.

🔥Diogo Jota

Baada ya Coutinho kuondoka, Diogo Jota alikuja kuchukua nafasi kama mshambuliaji wa nne wa Liverpool mwaka 2020. Na hakupoteza muda kuonesha thamani yake.

Ingawa mechi hiyo haikuhudhuriwa na mashabiki (kwa sababu ya COVID-19), Jota aliwastajabisha waliokuwepo kwa kufunga hat-trick dhidi ya Atalanta ugenini mnamo Novemba 3, 2020. Liverpool walishinda 5-0 kabla ya kutolewa na Real Madrid katika hatua ya robo fainali.

🔥Mohamed Salah

Ni vigumu kuamini kuwa wachezaji watatu walifunga hat-trick kabla yake tangu ajiunge na Liverpool mwaka 2017, lakini Mohamed Salah hatimaye alipata yake.

Mfungaji bora wa Liverpool kwenye Champions League alifunga hat-trick dhidi ya Rangers katika ushindi wa 7-1 kwenye hatua ya makundi msimu wa 2022/23.

Akiingia kipindi cha pili, Salah alifunga hat-trick ya haraka zaidi kwenye historia ya Liverpool – mabao matatu ndani ya dakika 6 tu.

🔥Luis Diaz

Luis Diaz alijiunga na orodha ya wachezaji wachache waliotamba kwa hat-trick alipofunga mabao matatu dhidi ya Bayer Leverkusen mnamo Novemba 5, 2024 katika hatua ya ligi (League Phase) ya Champions League.

🔥Orodha ya Hat-trick za Wachezaji wa Liverpool Kwenye UEFA Champions League

Michael Owen|Spartak Moscow| 22 Oktoba 2002| Hatua ya makundi

Yossi Benayoun| Besiktas|6 Novemba 2007| Hatua ya makundi

Philippe Coutinho|Spartak Moscow |6 Desemba 2017| Hatua ya makundi

Sadio Mane| Porto |14 Februari 2018|16 Bora (Knockout)

Diogo Jota|Atalanta |3 Novemba 2020| Hatua ya makundi

Mohamed Salah| Rangers| 12 Oktoba 2022| Hatua ya makundi

Luis Diaz| Bayer Leverkusen| 5 Novemba 2024|Hatua ya ligi

Chanzo: James Brooke

#YNWA #Liverpool
 
FB_IMG_1753595892874.jpg
 
Liverpool bila CB na DM msim ujao tuta suffer sana na dalili ndio hizo zinajionesha mapema hakuna cha friendly match
Mechi za Pre Season makocha huwa wanazitumia kujifunza/kujua timu zao, huwa ni muda wa kuweka tactic na formations mpya na kujaribu kutengeneza Bond ya players wageni na wenyeji

Usitishike kihivyo tupo pazuri japo kiukweli CB anahitajika dirisha hili kabla halijafungwa
 
Safari hii nahisi vikombe vyote vitachukuliwa na zote kubwa tofauti na msimu uliopita ila simuoni man city msimu akitamba
Kipara Pep sijui huu usajili wake kama utamwokoa aisee naona kama utawala wake unaelekea ukingoni kabisa...

Kwa usajili huu wa timu zingine bingwa atapatikana kwa taabu sana sio mteremko.

EPL itanoga sana.

YNWA
 
MJUE RIO NGUMOHA

Jina kamili: Rio Bass Ray Ngumoha Adigun

Tarehe ya kuzaliwa/Umri:Agosti 29, 2008 (miaka 16)

Mahali alikozaliwa: London, England (Newham)

Urefu: 1.70 m

Uraia:England 🇬🇧Nigeria 🇳🇬

Nafasi anayocheza: Ushambuliaji - Winga wa kushoto.

Mguu anaotumia zaidi: Mguu wa kulia.

Ameiwakilisha timu ya taifa ya Uingereza kwa level za under 15, 16 na sasa 17.

Klabu ya sasa: Liverpool FC U18

Alijiunga na klabu: Septemba 4, 2024 akitokea klabu ya vijana ya Chelsea.

Mkataba unaisha:Juni 30, 2026

Klabu ya pili:Liverpool FC UEFA U19.

Alipata nafasi ya kucheza kwa mara ya kwanza katika kikosi cha wakubwa cha Liverpool chini ya kocha Arne Slot, alipocheza dhidi ya Accrington Stanley kwenye Kombe la FA mwezi Januari 2025.

Rio Ngumoha aliandika historia katika mechi yake ya kwanza akiwa na Liverpool, baada ya kuwa mchezaji mwenye umri mdogo zaidi kuanza katika mchezo wa mashindano rasmi katika historia ya klabu hiyo.

Ngumoha alikuwa na umri wa miaka 16 na siku 135 alipopata nafasi ya kucheza na Liverpool ilipata ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Accrington Stanley kwenye Kombe la FA.

Mtindo wake wa uchezaji ulifananishwa na ule wa mshambuliaji wa Bayern Munich, Jamal Musiala, ambaye naye aliwahi kuwa mchezaji wa akademi ya Chelsea kabla ya familia yake kuhamia Ujerumani mwaka 2019.

Akizungumza na LFCTV baada ya kichapo kutoka kwa AC Milan, Harvey Elliott alimsifia kijana Rio Ngumoha kwa kiwango chake. Alisema:

Hana woga. dhidi ya AC Milan ameonyesha hilo dhidi ya AC Milan, moja ya timu kubwa barani Ulaya. Alikuwa kama mtoto aliyepo uwanjani kwa starehe – japo ni kweli yeye ni mtoto!"
"Anachotakiwa ni kuendelea tu na juhudi hizo, na sisi tutajitahidi kadri tuwezavyo kumsaidia. Nadhani kama ataendelea kucheza kama anavyofanya sasa na kuendelea kujituma, basi kijana huyu ana maisha ya mazuri ya soka yanayomngoja mbele."

Maneno ya gwiji wa Chelsea kwa klabu ya Liverpool; Liverpool wamesajili "Mchezaji wa Kiwango cha Juu" kwa kumsaini Rio Ngumoha, kijana wa zamani wa Chelsea, kwa mujibu wa gwiji wa klabu hiyo ya London, John Terry.

Rio Ghumoha alishawahi kusema kuwa Mohamed Salah ni miongoni mwa role model wake.

Chelsea walikasirishwa sana na Rio kuhamia Liverpool Kama ilivyoripotiwa na Daily Mail, klabu ya Chelsea inaelezwa kuwa "imekasirika sana" na maafisa wa Stamford Bridge "wamejaa hasira" baada ya kumpoteza "kipaji cha kipekee cha kizazi hiki" kwa wapinzani wao wa Ligi Kuu ya England.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom