I think, its time, Klopp aanze kujiangalia in the mirror.
Nimekuwa mkosoaji mkubwa sana wa FSG for the past few years, and i have been on record, nikisema kuwa Klopp anasitahili kufanya baadhi ya maamuzi at the club kutokana na kile alichofanya kwa the whole time tangu awe appointed, but power yake ya kufanya maamuzi aliyopewa na FSG, imetuongezea nini au imetupunguzia nini? tunafaidika na hii power aliyonayo sasa? muelekeo wa Club ni upi sasa? structure ya club ni ipi kwa sasa?
Klopp alivyokuwa appointed at LFC, alifanikiwa kujenga a good team na kina Edwards/Graham/Fallows/Hunter etc, wakati yeye anahusika na on-pitch activities, kina Edwards walikuwa wanahusika na off-pitch activities especially katika upande wa recruitment department, na tulifanikiwa kutengeneza a very strong team iliyofanikiwa kushinda kila aina ya kikombe, but kipindi hiki pia kilikuwa na changamoto sana, hasa katika upande wa Owners (FSG), ambao kuna vipindi walikuwa wagumu sana ku-fund transfers kutokana na kuona policy yao ya sell to buy inafanya kazi, kitu kilichofanya mara nyingi sana tuwe tunaanza msimu tukiwa short kwenye various departments.
Yes, FSG are a disgrace, but tutaendela kujificha mpaka lini kwenye kivuli chao ili kumuepushia lawama Klopp?
Mambo yalianza kwenda vibaya at LFC, baada ya mkataba mpya wa Klopp (yeah, i am so happy that he signed a new contract), but bigger picture hapa, ni kuwa mkataba mpya, ulimpa power zaidi Klopp mpaka kwenye upande wa recruitment department, ambayo at that time ilikuwa chini ya Edwards, na msigano ulianza kwenye deal ya mkataba mpya wa Henderson, ambapo Edwards aliomba Henderson asipewe mkataba mpya, but Klopp akagoma katakata, suala likawa kwa FSG wamsikilize nani? na FSG wakaamua wamsikilize Klopp, na kila owner angefanya hivyo, well kwa owners wabahili kama FSG ni lazima wamsikilize Klopp, because ndiyo their most valuable asset, so they vetoed proposal ya Edwards and gave Henderson a new contract, ambayo ilikuwa ni big mistake, Edwards lined up Bruno Guimaraes as Hendo replacement, Klopp and his coaching stuff rejected the idea.
Kuna mengine nyuma ya pazia, but hii debacle ya Henderson new contract, ilichangia sana kwa Edwards kuondoka, then akaja Julian Ward, a liverpool fan, ambaye amefanya kazi at the club kwa muda mrefu sana, but a few months as a DOF aka-put in a resignation letter, why? kwanini DOF waondoke? kuna shida gani? hawasikilizwi? hawapewi kipaumbele? then Ian Graham nae akaondoka, why?
Niliongea mimi, humu ndani few months ago, nikaonekana natunga vitu but juzi Paul Joyce ka-confirm kuwa we turned down Enzo Fernandez for £15m, kabla ya kwenda Benfica, we were offered this player through Julian Ward connections, and the coaching stuff turned it down, because they were waiting on Jude and Tchouameni, players ambao when Madrid offered them deals walitupiga chini bila hata kujiuliza mara mbili, sasa kipindi hiki ambacho Klopp alikuwa anasubiria his 2 perfect players, tumepoteza wachezaji wangapi kwa rivals? Enzo, Guimaraes, Joao Gomes, Nunes, Paqueata, etc, hawa wachezaj wote got offered to us for peanuts, tutawalaumu FSG? FSG walivyowabahili ungewapa Enzo for 15m, au Guimaraes for 35m etc wangegoma ku-sunction? tena ni kipindi ambacho walikuwa tayari ku-sunction big deals za Jude and Tchou.
Tutawalaumu FSG mpaka lini? msimu uliopita Klopp refused these alternatives, tukaanza msimu na the same MF ambayo ilikuwa imejaa injuries na fatigues, na tuliona kilichotusibu msimu mzima, msimu huu tulianza transfer window kwa kuondoa a lot of deadwoods (Keita, Ox, Milner, Henderson), then tukapata offer ambayo ilikuwa ni ngumu kui-turn down ya Fabinho (40m), kwa ujumla 5 MFs waliondoka, and practically we needed at least 4 MFs as replacements, and i am so happy we signed Mac-Allister and especially Dominik (Sikuwahi kutegemea kama tutakuja ku-sign a world class talent kama hii, na ndiyo maana nilikuwa simuweki hata kwenye my profiling data), so kudos kwa jorg (he worked on Dominik file), na pia kudos kwa Julian Ward (worked so hard on Mac-Allister file kabla ya kuhitimisha his resignation process).
Kwenye hili suala la MF rebuild, ndiyo nataka kumuongelea Klopp leo, we have signed top class 8s, theres no doubt about that, but what about a starting 6? Wataru Endo is not a starting 6, he is a squad player, tutakuwa tunajidanganya kama tukianza msimu huu na Endo as our starting 6, utakuwa ni uzembe tu kama wa last season.
Ok, lets say, we werent anticipating a fabinho bid, but ilikuja, na it took us 2 weeks ku-conclude a deal, na mpaka sasa umepita mwezi tangu Fabinho aondoke, where is his replacement? na kama kulikuwa hakuna a suitable replacement, why ukubali kumuuza? tulianza ku-negoatiate na Southampton kuhusu Lavia, kabla hata bid ya Fabinho haijaja, plan ilikuwa ni kum-phase out Fabinho slowly na kum-bed in Lavia slowly, so plan ya msimu huu ilikuwa ni Fabinho na Lavia as our starting 6s, but when bid ya Saudi Arabia ilivyokuja, we panicked, sunctioned a deal bila a realiable DM kuwa lined up, of-course we viewed Lavia kama mrithi wa Fabinho but not an instant starter, so tukaanza kuangalia good DMs kwenye market, nakumbuka mpaka leo, Club scouts na kina Fallows, walishauri tuendelee na file la Lavia, na tutafute an experienced 6 wa kumsaidia Lavia ku-bed in, but Klopp, and his friend Jorg, decided to go for Caicedo, bid 111m, (calculated bid) but chelsea ended up offering more money to his agent, Manuel Serra anafamika kwenye football world kuwa agent mpuuzi sana, kishasababishia wenzake majanga mengi sana, na ndiyo maana Chelsea wali-up tu offer kwake, they offered him pesa ya kutosha outside ya deal (nadhani jamaa wa football insider wali-publish hii), na uzuri wa Agents wahuni kama. kina Serra, wanakwambia, chelsea wameni-offer hii, nyie mnasemaje? FSG waka-withdraw bid, na sijawahi kuwalaumu, they showed ambition, kama walivyofanya kwa VVD, Alisson, Nunez etc, they backed Klopp, but again Klopp refused to listen to his scouts ambao tangu mwanzo wali-suggest Romeo Lavia, now umetumia. nguvu nyingi ku-turn a 19 year-old kid head, kumpa maneno matamu kuhusu your project, na bado akawa anakuvumilia tu unavyojaribu kum-low ball his employer (southampton), Southampton walitupa valuation ya 50m, tukaanza na 37m, then 42m, mpaka 46m, then BOOM, mchezaji na his camp wanasikia ume-move kwa Caicedo with 111m bid, na wakiuliza southampton wanaambiwa kuwa umestopisha mazungumzo, then baada ya kushindwa kwa Caicedo unarudi tena mkia nyuma, na hapo ushamuudhi owner ambaye hana structure yeyote kwenye team yake (Boely), na kuna rivaly kati yake na John kwenye ventures zao zingine USA, anaamua kuja kwa Lavia, ambaye kwake pia ilikuwa ni second choice ya Caicedo, offered more money and wages, dogo kwa umri wake anakubali, akidhani anaikomoa LFC/Klopp, Klopp akaamua kuachana na file (because tangu mwanzo alikuwa hakubaliana sana na suala la Lavia, it took a lot of convicing from our scouts kwa Klopp kuanza kulivalia njuga suala la Lavia), dogo anarudi last minutes, Klopp anakuwa ameshapata sababu ya kulitupa file kabisa, juzi nimesikia kuwa dogo anataka kufukuza his agency/washauri, but sidhani kama walikuwa wanakosa, its just football business, makosa ni ya LFC na maybe yeye kuchukulia suala la biashara kama personal, ambapo namuelewa pia, and i wish him the best at Chelsea.
Sasa, after Caicedo & Lavia debacles, reaction ilikuwa ni ipi? Endo is not a starting 6, hatuwezi kujidanganya, na kinachofanya niongee hapa ni kuwa, feeling at the club ni kuwa tunaweza kusubiri tena, yaani Endo anaweza ku-cover for now, as we feel hakuna good number 6s kwenye market, na waliopo ni too pricey, sasa najiuliza the whole world imeona uki-bid 111m for a 21 yeaf old ambaye ana games si chini ya 40 kwenye soil ya UK, unafikiri teams zingine zitakuuzia for less? tena zikiwa zimebaki. siku 9-10 mpaka TW ifungwe? gharama za kuanza msimu bila a starting 6 ni kubwa sana, msimu uliopita tulikuwa na a washed/fatigued WC 6 (Fabinho), na hakuna alichosaidia, sasa kwa. kujua hilo, how can you start a season without a young, hungry 6? wheres a plan? as a manager unakuwaje tayari ku-throw away msimu mwingine tena? anavyo-act Klopp utadhani kina Salah, VVD, Allison etc are getting any younger, we need bodies in the MF, Szobo & Macca arent enough, na kinachochekesha zaidi, unakuwaje na two world clasa 8s but unaona shida kuwatafutia a good & strong destoyer? kwanini jamaa anashindwa kujifunza? kila siku tunaanza msimu tukiwa short, FSG were ready to pay 111m for Caicedo, that means pesa/fund zipo, sasa kinachofanya Klopp aanze kuleta mambo ya perfect player ya nin?, tuna mashindano manne msimu huu, we need bodies, ok, kama Doucoure unaona ni bei, just sunction deal ya Andre now, sunction deal ya Manu Kone now, sunction deal ya Fofana now, ask Benfica kuhusu Flo Luis, Zubimendi ana RC ya 51m test the waters. Parish wa Crystal Palace hawezi kumtoa Cheick Doucoure for less than 60m kwa sasa, na huwezi. kumlaumu kabisa.
Na itabidi tuanze kujiuliza maswali kuhusu Klopp, mbona wenzake huwa wanahakikisha wanaanza msimu wakiwa wamekamilika? kwanini kila siku ni yeye tu? sasa hivi tutawalaumu FSG kwa kipi? Man City wameshinda treble na mpaka sasa wameongeza Kovacic, Josko, Doku na walikuwa tayari kutoa 85m kwa Paqueata kabla ya his betting scandal, why kila siku sisi? good values kwenye market hazipo kwasasa, na siyo kila mchezaji ana RC kwenye mkataba wake (Macca & Szo), wengi waliopo sasa you need to pay over the odds, na hakuna time ya kusubiria right player.
And, kipi kifanyike kama tuki-fail huu msimu kwa uzembe wa Klopp kwenye TW? msimu uliopita tumemvumilia, lakini kama anaona yupo above everyone at the club na anaweza kufanya anachotaka, i think FSG needs to act.