Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Sasa wakati mnasubiri kuboresha midfield na defense, na ingawa mmeleta Dominic, tupeni sisi basi hao forwards wazuri kina Luis Diaz na Darwin na sisi tuwape Nketiah na Balogun Ili muwe pia na forward ya kawaida mbalance mambo siyo mnanga'ang'ania forward Kali halafu inakuwa kazi bure kisa midfield na defense za kawaida. Amueni kuwa a proper mediocre team
Acha tupambane ya hali yetu 😀 ila kabla ya dirisha la usajili kufungwa tukifanikiwa kuleta CDM na LCB wa ukweli tunarudi kupambana na City pale juu. Balaa ni kama tutafeli kusajili hizo sehemu mbili, naona kama tutaendelea kucheza Europa na msimu ujao.
 
Diaz sio wa kumtegemea timu ikiwa inasaka ushindi. Ana mambo mengi sana uwanjani hasa akiwa kwenye box.
Mnyama ni Jota hana mambo mengi kabisa. Kwaiyo foward yetu ya kutegemea ni Jota, Salah na Gakpo.
Gakpo
Salah akishaliotea goli jamaa ni katili sana,ananyanyasa adui hadi adui anatamani kumpiga ngumi.

Diaz chenga nyingi aonekane fundi sana wa kupiga kama spider...sema ni fundi hata hivyo,mfia timu.

Jota hatabiriki kabisa
Anaotea otea tu.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha tupambane ya hali yetu 😀 ila kabla ya dirisha la usajili kufungwa tukifanikiwa kuleta CDM na LCB wa ukweli tunarudi kupambana na City pale juu. Balaa ni kama tutafeli kusajili hizo sehemu mbili, naona kama tutaendelea kucheza Europa na msimu ujao.
Nketiah mbona anawarudisha champions league fresh tu
 
Wewe kocha mwenye vyeti vya UEFA na FIFA, kocha umeshinda makombe yote

Bado unataka kumongezea mkataba Milner ,??? Bobby??? Utawaambia nini wakuelewe kiu imeshakata umri umesonga??

Kocha kama Klopp ni wa kumchezesha Jones No. 6? Ana mjadibu Jones as 6 kwamba hana mpngo na DMF? Jones hana ability wala attribute ya kucheza either 6/8. Aliyemloga Klopp amuhurumie tu kams yupo hai. Sasa naona karudi kwa Mac Allister kumchezaji 6, wapi na wapi kulazimisha mambo.

Kutoka january timu ilionesha inahitaji CB’s, RB, DMF, LCM, RCM ila mpka sasa tumesajili LCM & RCM. Kocha professional mpka sasa hajasajili mahitaji yke ma4 mpka ma5.

Kocha huyu huyu aliahidi mpka july nani akienda preseason anataka signings zake ziwe zimekamilika. Na yeye ndiye mamlaka ya usajili, bado mtu atamtetea Klopp katika hili???

Mpaka sasa hamna utofauti wowote wa kikosi cha last season na hiki zaidi naona kimepungua.

Imagine anaumia Mac Allister na Konate.

Heheh Klopp bana. Nafikiri Liverpool ndio Klabu ipo under pressure mpaka sasa.
Kwa mapungufu yote hayo uliyotaja hebu nitajie kocha gani mwengine angeweza kukibebea hiki kikosi mpaka hapo alipofikia yeye tu! Tatizo hapa ni FSG wabahili! hata hao wachezaji wazuri tulionao tuwewanunua kwa kuvizia e.g. Salah, Mane etc. wote wamekuwa wakubwa kwenye mikono ya Klopp.

Bila ya klopp kamanda na sisi tungekuwa kama Chelsea kama sio Everton.
 
Tu

Tunachompendea Nunez urefu na speed nketiah hana na hatokuja kupata, mapungufu ya nunez ni machache sana kulenga goli kuliko huyo nketiah
Kweli ila Nketiah Yuko clinical kulingana na nafasi anazopata.

Halafu Kuna lingine kuhusu Klopp.

Jamani mnamzeesha na kumsababishia presha huyo kocha. Jamaa ni bonge la kocha ila kukosa funds kunafanya amalize career yake vibaya. Mnaonaje mkitupa Klopp aje awe assistant wa Arteta wajichotee Kwa pamoja makombe yote. Sisi si umeona tulivyo vizuri kifedha? Yaani mkwanja mfuko wa shati.
 
Kweli ila Nketiah Yuko clinical kulingana na nafasi anazopata.

Halafu Kuna lingine kuhusu Klopp.

Jamani mnamzeesha na kumsababishia presha huyo kocha. Jamaa ni bonge la kocha ila kumkosa funds kunafanya amalize career yake vibaya. Mnaonaje mkitupa Klopp aje awe assistant wa Arteta wajichotee Kwa pamoja makombe yote. Sisi si umeona tulivyo vizuri kifedha? Yaani mkwanja mfuko wa shati.
Shida yake Klopp ni kwamba hicho kitendo Cha kukosa Fund naye anakifurahia ili ajitwalie umaarufu wa kutenda miujiza ya kufanya njia pasipo njia.


Unadhani mtu kama Pep angekuwa Liver,angekubali na kuchekelea upumbavu wa wajinga FSG kwamba hela hakuna?
Uandhani angetoa zile kauli alizokuwa anazitoa Klopp mwanzo wa msimu uliopita kwamba hakuna haja ya kusajili MF,tunao wa kutosha,yupo Keita,yupo Hendo ,yupo sijui nani,wengine wa nini?

Klopp naye ni mjinga bwana,msimtetee.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shida yake Klopp ni kwamba hicho kitendo Cha kukosa Fund naye anakifurahia ili ajitwalie umaarufu wa kutenda miujiza ya kufanya njia pasipo njia.


Unadhani mtu kama Pep angekuwa Liver,angekubali na kuchekelea upumbavu wa wajinga FSG kwamba hela hakuna?
Uandhani angetoa zile kauli alizokuwa anazitoa Klopp mwanzo wa msimu uliopita kwamba hakuna haja ya kusajili MF,tunao wa kutosha?

Klopp naye ni mjinga bwana,msimtetee.

Sent using Jamii Forums mobile app
Anajitahidi tu kufuata nyayo za role model wake, Arsene Wenger, mwamba mwenye sanamu lake pale Emirates. Mwamba aliyejenga uwanja mpya Kwa pesa za mauzo ya Anelka. Mwamba aliyepandisha propert prices za Ashburton Grove. Yaani Kwa kifupi Wenger ni The Boss. Sasa si mmuacheni Klopp aje kuendeleza Legacy ya Le Prof?
 
Anajitahidi tu kufuata nyayo za role model wake, Arsene Wenger, mwamba mwenye sanamu lake pale Emirates. Mwamba aliyejenga uwanja mpya Kwa pesa za mauzo ya Anelka. Mwamba aliyepandisha propert prices za Ashburton Grove. Yaani Kwa kifupi Wenger ni The Boss. Sasa si mmuacheni Klopp aje kuendeleza Legacy ya Le Prof?
Ni mpumbavu kama wapumbavu wengine asipotaka kubadilika na kujidai baba miujiza wakati msimu wa miujiza ushaisha
Mpira hautaki tena janjajanja za miujiza .
 
Tatizo la Liverpool ni Anold sema ni ngumu kufahamu hadi uangalie mechi nyingi kwa umakini, huyu dogo anapopanda tu lazima tufungwe. Tafadhari bora tuwanyang'anye Chelsea Reece James kwisha...
Dah upo sahihi kabisa! Trent anapaswa kuwa winga au awe-paired na very good CDM kama Tchuameni au Caicedo, nyuma yao kuwe na strong CBs vilele, otherwise atatufungisha siku zote eirther directly au inderictly kwa kuwapa kazi kubwa wenzake wanaomzunguka.

Kiufupi anawafanya wenzake muda wote wacheze kama tupo pungufu kwa mtu mmoja vile. Konate inabidi acheze RB na RCB. CDM inabidi acheze kama lone CDM wakati juu yake kuna two box to box (mzigo mkubwa wa kuwalinda CBs and kupatrol midfield area at the same time.

Fabinho ali-shine alipokuwa anacheza na Wijnaldum na Hendo kwa kuwa Wijnaldum alikuwa anafanya kazi ya kuharibu na kutuliza timu wakati yeye anasafisha, hendo anabakia box to box peke yake. Msimu ule defence ilifanya vizuri kwa kuwa tulikuwa na key strong person kila idara i.e. Allison, Virgil, Fabs, Winaldum.

Msimu huu tunaenda kucheza na box to box wawili i.e. Macca na Szobo, CDM mmoja ambae mpaka sasa hatujasajili specialist, huyu itabidi acheze kama lone CDM kwakuwa his partner Trent ni mzururaji hovyo. Hapa tukishindwa kuzuia kutokea mbele tu basi chance ya kufungwa kwa kila shambulizi ni close to 50% kwasababu ni rahisi CDM and defence kuwa out of position.
 
Kweli ila Nketiah Yuko clinical kulingana na nafasi anazopata.

Halafu Kuna lingine kuhusu Klopp.

Jamani mnamzeesha na kumsababishia presha huyo kocha. Jamaa ni bonge la kocha ila kukosa funds kunafanya amalize career yake vibaya. Mnaonaje mkitupa Klopp aje awe assistant wa Arteta wajichotee Kwa pamoja makombe yote. Sisi si umeona tulivyo vizuri kifedha? Yaani mkwanja mfuko wa shati.
Hakuna muongeaji sana anayepata mafanikio kwa muda mrefu,

Ni kocha mzuri ila anaendesha timu kwa mahaba na hisia mno kuliko uhalisia, tukipata roho ngumu tutawaachia
 
Shida yake Klopp ni kwamba hicho kitendo Cha kukosa Fund naye anakifurahia ili ajitwalie umaarufu wa kutenda miujiza ya kufanya njia pasipo njia.


Unadhani mtu kama Pep angekuwa Liver,angekubali na kuchekelea upumbavu wa wajinga FSG kwamba hela hakuna?
Uandhani angetoa zile kauli alizokuwa anazitoa Klopp mwanzo wa msimu uliopita kwamba hakuna haja ya kusajili MF,tunao wa kutosha,yupo Keita,yupo Hendo ,yupo sijui nani,wengine wa nini?

Klopp naye ni mjinga bwana,msimtetee.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mi nadhani he is just being proffesional, kuna makala moja nilikuwa nasoma leo inadai privately amechoshwa na lack of signings na atafikiria his options ikiwa FSG hawatompa support kwenye usajili msimu huu, inaonekana kama ana-consider post ya Germany national team .

Binafsi naamini kunaweza kuwa na ukweli coz jamaa alisema mwisho wa msimu uliopita kuwa anataka kufanya overhaoul ya midfield mapema ili apate muda wa kutosha kufanya nao kazi pre season kitu ambacho hakujatokea zaidi ya wachezaji wawili tuliosajili.
 
Ni mpumbavu kama wapumbavu wengine asipotaka kubadilika na kujidai baba miujiza wakati msimu wa miujiza ushaisha
Mpira hautaki tena janjajanja za miujiza .
Pamoja na hayo. Jamaa ukocha anaujua sana. Naweza kusema kimbinu huenda yeye ndiye kocha Bora kwenye ligi. Akifuatiwa na kina Pep na Arteta na akimuacha mbali 7hag aka Dutch David Moyes.
 
Dah upo sahihi kabisa! Trent anapaswa kuwa winga au awe-paired na very good CDM kama Tchuameni au Caicedo, nyuma yao kuwe na strong CBs vilele, otherwise atatufungisha siku zote eirther directly au inderictly kwa kuwapa kazi kubwa wenzake wanaomzunguka.

Kiufupi anawafanya wenzake muda wote wacheze kama tupo pungufu kwa mtu mmoja vile. Konate inabidi acheze RB na RCB. CDM inabidi acheze kama lone CDM wakati juu yake kuna two box to box (mzigo mkubwa wa kuwalinda CBs and kupatrol midfield area at the same time.

Fabinho ali-shine alipokuwa anacheza na Wijnaldum na Hendo kwa kuwa Wijnaldum alikuwa anafanya kazi ya kuharibu na kutuliza timu wakati yeye anasafisha, hendo anabakia box to box peke yake. Msimu ule defence ilifanya vizuri kwa kuwa tulikuwa na key strong person kila idara i.e. Allison, Virgil, Fabs, Winaldum.

Msimu huu tunaenda kucheza na box to box wawili i.e. Macca na Szobo, CDM mmoja ambae mpaka sasa hatujasajili specialist, huyu itabidi acheze kama lone CDM kwakuwa his partner Trent ni mzururaji hovyo. Hapa tukishindwa kuzuia kutokea mbele tu basi chance ya kufungwa kwa kila shambulizi ni close to 50% kwasababu ni rahisi CDM and defence kuwa out of position.
Anold ata winga hawezi, nilibaini hilo siku ya mechi na bayern na wale wajerumani wengine alichezeshwa kama kiungo akapotea na siku ya bayern ndipo kabisa maana hadi coman anamzidi mbio.

Tena siku hizi anatembea kama ameota majipu mapajani, suluhisho ni mtu wa kumnyang'anya namba tu hakuna lingine. Waingeleza wenyewe waliisha mnyang'anya namba ni mwendo wa sub kwenye timu ya taifa.
 
Hakuna muongeaji sana anayepata mafanikio kwa muda mrefu,

Ni kocha mzuri ila anaendesha timu kwa mahaba na hisia mno kuliko uhalisia, tukipata roho ngumu tutawaachia
It seems like the grass is always greener on the other side.

Sisi title contenders Arsenal pamoja na Manyumbu, Chelkenge na hata Citeh wote tunamkubali sana Klopp na ukituambia tumchukue, haswa Manyumbu, ni fasta tu.
 
Shida yake Klopp ni kwamba hicho kitendo Cha kukosa Fund naye anakifurahia ili ajitwalie umaarufu wa kutenda miujiza ya kufanya njia pasipo njia.


Unadhani mtu kama Pep angekuwa Liver,angekubali na kuchekelea upumbavu wa wajinga FSG kwamba hela hakuna?
Uandhani angetoa zile kauli alizokuwa anazitoa Klopp mwanzo wa msimu uliopita kwamba hakuna haja ya kusajili MF,tunao wa kutosha,yupo Keita,yupo Hendo ,yupo sijui nani,wengine wa nini?

Klopp naye ni mjinga bwana,msimtetee.

Sent using Jamii Forums mobile app
😄😄 Tena morinho ndiyo angewananga sana yaani sioni mchezaji yeyote ndani ya hao waliosainiwa wanazidiwa na timu ya watoto wakina koumas, Quansah na ben doak
 
Mzee baba natofautiana sana na wewe katika mtazamo wako

1. Keita - alikuwa ni box to box mzuri sana kule alipotoka, mfumo na high demand ndiyo iliyo muathiri (Liver inaongoza kwa injury crisis kwenye EPL probably kutokana na style that demands a lot from the players players)

2. Nunez - Labda amenunuliwa mapema kwakuwa bado sio finished article lakini tungechelewa asingekuwa kwenye uwezo wetu within 2 seasons. Hapo alipo sasa hivi yeye ni mmoja kati ya wachezaji wanaoongoza katika kupata nafasi za kufunga licha ya kwamba liver haikucheza vizuri msimu uliopita na yeye pia hakuchezeshwa katika his preffered role (He is a goal getter not LF also not a false 9)

3. Carvalho - He is a number 10 (attacking oriented), we did not play with a number 10 last season plus his small stature haikumsaidia kabisa kuadopt. Na pia huyu haikuwa usajili wa Klopp! alipewa tu kwasababu za kibiashara as he was one of the available promising young talents for the future.

4. Arthur - Hii ilikuwa ni panic move kwakuwa tulishindwa kusajili midfield tunaemtaka (Tchuameni) na FSG waliona wasubiri kumsajili Bellingham msimu huu kuliko kusajili tu mtu yoyote. That's why tulimchukua on loan. Ila bado tunarudi palepale, our training methods hazikumsaidia kabisa badala yake zikamuongezea injuries.

5. Luis Diaz - nakubaliana na wewe japo mtu si mbwa, ametuokoa mara kadhaa na huo umachchari wake. Kuna kitu anacho lakini yeye sio mane kama ambavyo Ronaldo sio Messi na Messi pia Ronaldo (if u understand what I mean)

6. Konate - Kamanda naomba nitajie CB mwenye kasi zaidi yake kwa statistics ndo utagundua umemuonea. Ana tatizo la concentration lakini bado experience ni ndogo, hopefull atakuwa on of the best if he stays fit.

7. Thiago - Hapa ni kama kumuomba Pirlo awe Seedorf! huyu jamaa akicheza katika timu ambayo ana uhakika nyuma yake kuna strong DM na strong CBs he is one of the best katika ku-influence tempo ya game as well as kupiga defence splitting passes, lakini saivi hatumpati katika huo ubora kwa sababu mfumo wetu kila mchezaji ana majukumu ya kuzuia kwanza halafu ndo afanye kazi yake, pia training methods zinamuongezea injuries.

Liverpool tuna attacking force nzuri only kama tutawapa uhuru wa ku-cocentrate na kazi yao. Tujenge defence yetu ili timu isitegemee wachezaji wa mbele kuzuia.
Hili swala la kutowapanga wachezaji kwenye namba zao asili namchukia zaidi sijui kwanini anasajili.
 
It seems like the grass is always greener on the other side.

Sisi title contenders Arsenal pamoja na Manyumbu, Chelkenge na hata Citeh wote tunamkubali sana Klopp na ukituambia tumchukue, haswa Manyumbu, ni fasta tu.
Shida siyo kumkubali
Shida Kuna upumbavu anaendekeza ambao unachangia tunakwama.

Klopp has the option to be better than now
but the bad thing is that he does not want to use it ,instead he's depending on miracles.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom