Captain Marvelous
JF-Expert Member
- Jul 25, 2017
- 15,313
- 32,605
Huku kumtaja Milner jamani kweli leo Klopp atampanga tu maana anavyosakwa acheze ili mtuchape safii maana kwanza kachoka kingine huyu soon atakula umeme huyu.Hiyo ni kuongeza tu confidence kwa wachezaji maana kwenye ligi kumfunga Liverpool akiwa nyumbani huwa ni ngumu sana.
Hata mimi shabiki tu mechi ya leo naiona ni ngumu japokuwa United tupo kwenye muendelezo wa matokeo mazuri na Liverpool ikisuasua ila North-West Derby pale Anfield ni mechi ya tofauti kabisa.
Tukiondoka na points 3 nitaamini kweli Liverpool imeisha.
Babu Milner weee!!! 😂
Manchester United mkishindwa kutupiga tukiwa na hali hii basi huo ubingwa naona muwachie Arsenal apambane na Manchester City maana tuweke maneno ya kishabiki pembeni Liverpool tuna hali mbaya sana kuzima au kuzuia timu imekua ni kitendawili kabisa msimu huu.
Ni kweli ni Derby ya aina yake hii ina mvuto ina presha kubwa upande mmoja yupo ETG kuanza kuweka misingi ya dynasty yake EPL n upande mwingine yupo Klopp anaepambana kuonyesha hana nuksi na eti msimu wa 7 kukosa kibarua kama ilivyo kua BVB na Mainz...
Itakua gemu murwa sana kwa kua hakuna anaetaka sare hapa zaidi ya ushindi.
YNWA


.