Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Kuisuka hii timu yetu kunahitaji ela ndefu sio pungufu ya £200m.

Haya Chugga, Klopp kajatakia mwenyewe kwanza kuwatimua wachezaji majembe lakini kingine kuwapa wachezaji wazee mikataba mirefu sana bila kusoma alama za nyakati kwamba EPL sio mahala pa kulea wazee ni wazee kiasi vijana wengi hapo unakua salama lakini kwetu wazee wengiiiiii vijana wachache sana.
Kingine Midfield waliosajiliwa toka 2018 ni wagonjwa hakuna kazi kazi tazama Kieta, Thiago na Arthur Melo hao wote ni spana mkononi muda wowote utasikia wodini.
Nitashangaa sana kama huyo Bellingham atatua Liverpool hii ya sasa.

YNWA
Hii timu ili ikae sawa ni labda Klopp aondoke,

Ama FSG waondoke

Ama waondoke wote kwa pamoja
 
Hii inaitwa dirty linen haha kila timu hua haikosi mzee.

Unajua timu ikiwa na matokeo mambaya basi kila mahala panachunguzwa eee kulikoni kutoka kushindania makombe manne msimu uliopita na kua butu na nama hii basi bhana wanafukua kila mahala wachezaji makocha wamiliki nk.
Andreas Kornmayer ni head of fitness and conditioning pale Liverpool alijiunga na Liverpool mwaka 2016 akitokea Bayern Munich alikofanya kazi zaidi ya miaka 15. Huyu bwana kwa nature ya kazi yake anafanya kazi karibu sana na idara zote pale Liverpool. Tetesi ni kwamba ni moja kati ya wafanya kazi wa karibu sana Klopp na sio tu mbali pia ni Klopp favourite fulani nadhani kutokana na hilo sasa amepata kichwa fulani kiasi baadhi ya wafanyakazi pale Liverpool wanasema jamaa ni difficult to work with.. Labda kwa kua anapendelewa na Klopp ama ndio nature yake ni ngumu kujua.

Tangu mwaka 2020 wafanyakazi wengi wameodoka wengine wakiwa ni bora sana kwenye idara zao kiasi inaonekana tunaadhirika na kuwakosa.
Kwa mfano
Mike Gordon ambae ni FSG president ameodoka nafasi yake muhimu sana kwa ndio alikua anasaka pesa na kusimamia ununuzi wa wachezaji. Ameodoka kushughulika zaidi mauzo ya Liverpool.

Michael Edwards akiondoka June 2022 akiwa bado anahitajika sana klabuni akisema anahitaji mapumziko.
Mpaka utaona the Three Musketeers ambao ni Klopp Edward Gordon wamesabaratika na sasa yupo Klopp pekee.

Ian Graham huyu ni guru kwenye kazi yake ya director of research. Anaodoka na tetesi zinasema kama alivyo Ward na huyu ni kwamba hakuna tena mazingira rafiki wao kufanya majukumu yao klabuni.

Phillip Jacobsen alikua head of performance nae aliondoka. Huyu tena hakuficha alisema medical department ya Liverpool is in real mess.

Harrison Kingston nae aliondoka Liverpool baada ya kufanya kazi Liverpool kwa miaka 8. Kazi yake lilikua post match analysts. Alikua kiungo kati ya Klopp na data science department.

Jim Moxon daktari wa Liverpool aliodoka kwa kusema kwamba kuna mgongano kati ya physiotherapy na sport science.

Julian Ward alitoa notisi November mwaka jana kwamba June 2023 ataachia ngazi. Hii taarifa iliwastua wengi akiwemo Klopp. Julian ana contact za kutosha Ureno, Uhispania, Uingereza na Amerika ya Kusini. Kuodoka kwake ni pigo kwa Klopp.

Pep Lijnders ushawishi klabuni umekua mkubwa sana kiasi tetesi zinasema huu usajili wa Cody Gakpo ni wake na hakukua na mpango wa kusajili kwa vile tayari Firmino ameonyesha nia kuongeza mkataba Liverpool. Sasa cha kujiuliza inakua aje wasajili mridhi wa Firmino kama sasa anaongeza mkataba. Huu ushawishi wa hawa wafanya kazi wawili Lijnders na Kornmayer lazima Klopp awe makini kwa sasa wao wapo hukoo wakati Klopp anakaangwa na waadishi wa habari.

YNWA
Aisee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii timu ili ikae sawa ni labda Klopp aondoke,

Ama FSG waondoke

Ama waondoke wote kwa pamoja
Saint Anne njoo huku.
Nina mashaka sana nini kinaedelea huko vyumbani maana ni kama wachezaji wanacheza ili mradi tu wapate mshahara na msimu uishe...

Kila tukipigwa Klopp na baadhi ya wachezaji wanasema mechi inayofuata tutapambana sana matokeo yake ni kipigo sasa bora wakae kimya tu.

YNWA
 
Hakuna maajabu aisee Klopp has lost this season sijui analalamika nini...

Yaaani Keita + Thiago pedestrians combination no speed.

Atulie sidano iingie. Yeye akomae na vijana wapambane tu magoli yarudi kulalamika wala hakumsaidii.

YNWA
Tujipange tu msimu ujao , keita ni project iliyo feli .
Dirisha lijalo wafanye usajiri, Liverpool imeflop ghafla sana
 
Saint Anne njoo huku.
Nina mashaka sana nini kinaedelea huko vyumbani maana ni kama wachezaji wanacheza ili mradi tu wapate mshahara na msimu uishe...

Kila tukipigwa Klopp na baadhi ya wachezaji wanasema mechi inayofuata tutapambana sana matokeo yake ni kipigo sasa bora wakae kimya tu.

YNWA
Ulinishawishi niendelee kuangalia
Disappointed

Waondoke wote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mlikuwa mnatucheka man u mmeona raha ya kuchapwa kila weekend
Screenshot_20220903-153952.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom