MR BINGO
JF-Expert Member
- Feb 12, 2016
- 1,208
- 2,591
Mtu pekee atakayeondoka Liverpool hii na itetereke ni Jurgen Nobert Klop basi siyo mane Wala Salah Wala mtu yeyote yuleMkuu mpira bhana wakati mwingine una tabirika kwa kuangalia nini kiliwakuta wenzetu au sisi kuachilia mchezaji/wachezaji tegemezi kama Mane nasema tegemezi kuanzia January 2021 mpaka ligi ndio alikua mchezaji bora pale mbele kwa magoli muhimu sana... Binadamu kua na wasiwasi na mambo kama haya ni kawaida hasa ukizingatia Mane ni kilaka alicheza Winga ya Kulia kabla hajaja Salah alivyokuja akamuachia akahamia kushoto na alivyosajiliwa Diaz ambae ni winga wa kushoto Mane akahamia false 9 bila noma wala nini na kazi kazi.. Hii sio jepesi kwani kote alikocheza Liverpool alipambana kadri awezavyo kwa ajili ya timu nadhani hii ndio inawapa wengi wasi wasi...
Wengine labda wanakumbuka haya...
Unakumbuka Makelele alivyotoka Real Madrid....
Unakumbuka Kante alivyotoka Leicester...
Unakumbuka Alonso alivyotoka Liverpool...
Unakumbuka Surez alivyotoka Liverpool....
Unakumbuka Torres alivyotoka Liverpool...
Unakumbuka Henry alivyotoka Arsenal..
Unakumbuka Viera alivyotoka Arsenal...
Unakumbuka Fergie alivyosepa zake Manchester United...
List is endless...
Usiwashangae sana wanaosikitika kuhusu Mane, tuna imani na Klopp na tuna imani na wachezaji wetu, ni wachache sana humu waliokua wanamjua Darwen Nunuez kabla ya ile mechi ya Champions League vs Benfica na hata pia Diaz ilikua hivyo hivyo na kwa sababu Klopp mara chache sana sokoni amechemk tuna imani nae anakotupeleka.
Mpaka sasa Klopp ni wachezaji wachache sana hawakufikia kiwango anachotaka hivyo tuwe na subira wataweka mambo sawa kwa kufanya mazoezi mpaka mfumo ueleweke.
YNWA
Hivi Kati ya fabinho na Mane Nani alikuwa akimiss game timu inaflop??


