View attachment 2258722
Karibu Anfield Darwin Nunez hakika umechagua mahala sahihi kabisa kukuza kipaji chako zaidi. Hapa utakumbatiwa na mahaba mazito sana na kweli unajituma kazini na wimbo watakutungia...
Hili dili imekaa utamu sana miaka 6 huyu sasa anakuka kuteka hii ligi. Ni play maker kuwaleta wengine mchezoni, anafumania nyavu kwa miguu yote miwili na vichwa yumoo.
Julian Ward mpaka sasa ameridhi mikoba ya Edwards kibishi sana yaaani hatupoi...
Tukumbashane tu Michael Edwards alijiunga na Liverpool mwaka 2011 alihudumua idara tofauti kabla ya kufikia hili la Sporting Director ina maana mpaka FSG wameamua kuajiri kwa kumpadisha Julian kutoka kua msaidizi wa Edwards na sasa kua SD ni jambo la kujivunia.
Huyu Julian Ward ni mbombezi wa soko la Spain na Ureno hivyo tupo kwenye mikono salama. Jamaa ana network nzuri sana tutulie tu afanye yake.
YNWA