Siwezi kuacha kuipenda na kushabikia Liverpool ILA Ili swala la la sadio mane kutaka KUONDOKA na tukiruhusu aondoke kisa sijui mshahara litaniuma sana na litaondoka na sehemu kidogo ya ushabiki wangu kwa hii timu yangu pendwa...tusijidanganye kuwa tunaweza pata mtu wa kuziba pengo sadio mane kwa uharaka namna hiyo hao wanaowika kwenye hizo ligi nyingine wengi tu washakuja na KUONDOKA bila lolote....Salah,sadio,firmino hawa watu pale mbele watufanyia MAKUBWA sana ingekuwa sahihi mtu akichoka anaondoka kwa heshima ila sio eti mshahara ndio liwe tatizo kwa timu kama yetu tulipofikia aisee miaka karibia mitano sijui tunajiendesha kwa faida tunashindwaje kubakisha watu wetu muhimu wakat huo tukitafuta warithi wao taratibu...DIAZ KWANGU MIMI BADO WA KAWAIDA SANA SEMA KAJA KIPINDI KIZURI AMBACHO TIMU INAPAMBANA POA ILA HUYU DIAZ NINA UHAKIKA KAMA ANGEIKUTA ILE LIVERPOOL WALIOIKUTA WAKINA MANE SALAH NA FIRMINO TUNGEKUWA TUNAMTUKANA NOW....HAWA WATU LAZIMA TUWAPE HESHIMA YA KIPEKEE WALIPOTUTOA SIO PADOGO HAO TUJARIBU KUWAONA WATAZIBA MAPENGO YAO NI NDOTO ZA MCHANA..
Mkuu upo sahihi mtihani uliopo hapa ni kwamba Mane hajakataa ofa yoyote ya Liverpool sababu Liverpool walitarajia ligi iishe na ndio waanze mazungumzo na wakala wake June 2022 na walikua positive sana kwamba haitakua kama ishu ya Salah sasa mitihani ni pale Mane kawawai mapema sana huku timu kadhaa wakisuburia rasmi Liverpool kukaribisha wanunuzi ambao wanaotajwa sana sana ni Bayern Munich na PSG kumhitaji na kutoa mshahara mnono sana wa £300k + na ma bonus za kutosha... Hivyo upo sahihi kusema kama kweli ni pesa basi zipo maana timu inatengeneza ela tangu atue Klopp wamekua wakifanya vyema na kuvutia wachezaji wazuri na makampuni bora ya biashara kuwekeza Liverpool kama Nike nk ina maana Mane kacheza kalata yake vyema sana kwenye hili katumia ule msemo ujaja kuwai hapa kawakamata pazuri sana FSG.
Upande wa pili lazima tukumbali na data zinaonyesha hazidanganyi hata kidogo kwamba Liverpool kiwango kimeshuka kwa kiasi fulani sababu umri loss of form za wachezaji wetu.. Zamani Liverpool ilikua ni moja ya klabu bora kabisa kwenye pressing especially kwenye final 3rd wanayo operate Mane Firmino Salah tulikua hatupoi lakini kwa sasa nadhani EPL tupo nafasi ya 3 au 5 kwenye pressing ya final 3rd maanake ni kwamba wachezaji wetu bora pale mbele wapo kwenye decline na sababu zipo wametumika mno kabla ya Jota na Diaz kutua Liverpool sasa hilo tu litakupa picha Liverpool ya Klopp ya zamani na sasa kuna tofauti na hili limechangiwa na umri wao definitely wear na tear ime catch up na klabu haikusubiri hali iwe mbaya chap waka sajili Jota na Diaz hawa ni damu changa lakini kama ulivyosema ni mtihani sana kuziba nafasi ya Mane lakini lazima klabu ipambane sana kuhakikisha Klopp ana maintain competitive edge ya kikosi kwa kusajili wachezaji watakaotutoa tulipofikia kwenda mbali zaidi kwa kushinda makombe zaidi... Diazi na Jota wana offer output tofauti kabisa na Mane Salah Firmino pengine Klopp sasa atabadili hata mfumo kutoka 4 3 3 attacking kwennda mfumo mwingine utakaoleta matokeo mapya kwa kua hata wachezaji anaosajili wapo tofauti na hawa wa zamani. Tuwe na subira na hii ya Klopp kusaini mkataba mpya huku akijua Mane hayupo kwenye mipango yake itakua alifanya kikao na kuhakikishiwa maboresha ya kikosi.
Hivyoo kama Mane moyo umeshahama na mpunga hapati roho safi asepe zake mapema na kingine hua nasema hakuna aliezaidi ya timu hivyo wachezaji watakuja na wataodoka na Liverpool itabaki kama Liverpool maana wao ni ma professional hawana mapenzi ya dhati ni Klabu kwamba watacheza hata bure la hasha wapo pale kikazi na maslahi kwao lazima yawe value for money mtihani sasa ukitazama Chelsea, Manchester City, Manchester United wanawalipa ma top performers wae ela za maana huku Liverpool tukilipa pea nuts na vijana wakijitoa kama wana hisa vile sababu this boys wapo humble sana ambayo ni moja ya must have ukitaka kusajiliwa Liverpool...
FSG wanaimani hivi kwamba Mane, Salah, Firmino nk hawakuja Liverpool wakiwa established names kwenye mpira ama kama walivyo sasa hapana. FSG walitumia data proven statistics ku assemble hiki kikosi from the scratch na kupata timu ilivyo sasa hivyo wao wanaamini Klopp na mawakala wa timu wana nafasi ya kumpata next Mane, next Salah, next Fabinho nk ndio maana hawapo tayari kulipa mapesa ya kutisha kuwabakiza hawa wachezaji Liverpool.
Tujikumbushe Gini dogo alichezeshwa out of position na Klopp lakini hakuwai lalamika nadhani gemu pekee alicheza kama second 10 ni ile gemu tuliwapiga Barcelona goli 4 Anfield hio gemu tu ndio Gini alicheza namba yake sahihi na aling'ara lakini alivyotaka alipwe kutokana na mchango wake klabuni akiwa ni Mr Fit all the time jamaa zako FSG wakasema hawalipi hio hela huku useless Britons wakilipwa hio ela huku wengine wakiwa wodini muda mwingi kuliko uwanjani lakini waligoma balaa kumpa dogo mshahara wa £150+ ma bonuses kwa wiki lakini chap Captain buyoo akapewa £150+huku akiwa na output ya kawaida. Kimsingi pale pale ndio taa ilitakiwa kuwaka kwa Mane, Firmino na Salah kuhusu mikataba yao kwamba FSG wapo tayari mkataba uishe lakini sio wao kutoa mi hela mchezaji abakie klabuni...
Mane anaodoka akiwa kwenye kiwango bora akiwa ame shine pale kati na huku akiwa ni mr fit na magoli muhimu sana klabuni. Dogo yupo humble hana drama off the field yeye ni kazi kazi tu.
Tayari spinning zishaanza kumtishia Mane kwamba yatamkuta ya Emre Can, Coutinho au Gini kama akihama na mpira wake ndio umefika mwisho jamani who cares especially ukiwa 30yrs na ukilipwa 300k hata kiwango kikishuka sio haba pension itakua murwa sana kwao.
Kwa bahati mbaya sana haya mambo hua ni baina ya Klabu na mchezaji na hua kuna vipengele vya kulinda siri ya mkataba hivyo ukweli wanajua wao tu na sio sisi..
Tuwe na subira inaweza ikawa design kama Ramos akiwa Real Madrid vile alikua kutishia kuodoka anapewa mpunga wa maana anatulia tuliii hivyo msije shangaa Mane huyu huyu akasaini Liverpool mkataba wa miaka miwili na mpunga safi.
Muda utasema. Ndoto yangu Mane abakie lakini usajili wa center forward uwe pale pale kwa ajili ya Klopp revolution.
YNWA