Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Sahihi kabisa Klopp hapa sasa tupite kesho salama aafu aanze profiling namna ya ku wazima hawa Real Virrareal hakuna namna ni wao ama sisi.

Manchester United gap ushindani wa huku Robo Fainali mmeachwa mbali sana. Cha msingi sasa ni kuanza upya mkakati kurejea kwenye ubora mna nafasi hio sasa kwa kuanza kupata Kocha Kiwango. Ushauri wangu nendeni mazima kwa Inzaghi anawafa zaidi kuliko kipara wa Ajax ama Pochetinho. Huyu wa Ajax wasi wasi wangu ni kuwa manage ma staa wakubwa pale Manchester United ambao siku hizi hawachezi kwa sababu ya badge yaaani unahitaji no nonsense manager.

YNWA

Wangempata Luis Enrique angewafaa sana, hana ujinga yule, aliwahi kumvimbia mpaka Messi na akamfanyia sub kwa lazima, sembuse hao kina Sanchoka na Pogba
 
Usimchukulie powa Unai huyu bwana ni masta wa Uefa.
Klopp alikutana nae akiwa Sevila fainali ya Uropa wee mbona alitupiga akiwa ametulia kama leo yaaani.
Hawa ma under dogs hua ni shinda sana aisee.
Bayern wanalia mpaka sasa.

YNWA
Master wa Europa cyo uefa........wanaweza wakawa vizuri ila cyo kwa Liverpool hii

NB:alimfunga klop ndo kwanza akiwa amepewa timu iko na kina allen, Sturidge,markovic,n.k
 
Wangempata Luis Enrique angewafaa sana, hana ujinga yule, aliwahi kumvimbia mpaka Messi na akamfanyia sub kwa lazima, sembuse hao kina Sanchoka na Pogba
Kabisa ishu jamaa amegoma kuachia timu ya Taifa ya Spain hivyo hawana namna ila pale wanahitaji a real manager ambao hayumbishwi na majina ya wachezaji.
Wakimpata meneja anaejua vyema man management kama Klopp, Thomas, Pep, Conte, Anceloti nk basi akapewa sapoti sokoni mbona wanarejea ulingoni ndani ya misimu miwili watakua top competitor.

Wanahitaji zaidi pia time flame sio kisa Sancho na Ronaldo ametua basi ndio favourite wa kushinda EPL sio rahisi ki hivyo.

Great Manchester United teams zilijengwa kwa ukuta imara na ule ukuta wao ni bogus kabisa.

YNWA
 
Saizi wanamlaum kante kule , wakati huwa wanaseme ni bonge la mido dunia nzima
Hahaha asa kwani Kante ndio mfungaji.
Watulie tulia hii ndio UCL bhana hua ina matokeo ya aina yake.

Wachonge wasichonge tuonane UCL msimu ujao kwa sasa wabaki kuwatazama wanaojua wakisonga hatua ya nusu fainali.

YNWA
 
Na ubovu wangu wa utd siwezi katu au kamwe kumcheka chelsea, kwanza nampa hongera sana amepambana, tena uwanja kama wa machinjioni wa bernabeu , kama wangelikua wanacheza na sisi tungekula goli si chini ya tano..
Cha Msingi wametolewa hakuna Cha ugeni ni wala nyumbani , kwani Bayern nyumbani walifanyiwaje?
 
Kweli mkuu , ishu ya mastaa pale ni kama ugonjwa wa covid 19...lakini kwa taarifa nilizozipata kutoka jiji la Manchester, ni kwamba bodi pamoja na uwendawazimu wao, wameamua kumpa rungu la ku ondoa unncessary wastes hao mastaa na kwamba mtu ambaye ataona haipiganii timu basi aondolewe awekwe benchi atafute timu nyingine ya kucheza kipoyoyo, na kuna watu washaanza kutafuta timu na wengine washaanza kuwaza kuondoka akina pogba na wenzake
Hii ni njia moja ya kurejea kileleni. Klopp aliwakuta pale akina Benteke nk lakini aliingia na plan na akatoa time flame mdogo mdogo akaanza utekelezaji. Akaanza na kufumua mfumo wa scouting nk na mpaka anavuna matunda kwa kupata wachezaji wazuri kwa bei chee tazama Konate, Salah, Mane, Diaz, Jota nk.. Data unit imesaidia sana Klopp kwenye kujenga kile kikosi

Moja ya kipengele cha Klopp kusaini ilikua anashirikishwa kuuza na kununua wachezaji pale Liverpool na hii imempa platform njema sana kua na ma servant wanaoedana na mfumo wake.

Kocha mpya Man U lazima apewe nafasi ya kua na say ya mwisho ya manunuzi, kuuza ama kuongeza mkataba mchezaji hii itaweka nidhamu sana kikosin.

YNWA
 
Master wa Europa cyo uefa........wanaweza wakawa vizuri ila cyo kwa Liverpool hii

NB:alimfunga klop ndo kwanza akiwa amepewa timu iko na kina allen, Sturidge,markovic,n.k
Duuh Allen Wales Xavi jamani tumetoka mbali sana na hii timu mpaka sasa ni World Beaters hakika we have seen its all.

Tupo tayari ndugu waje tu.

YNWA
 
Screenshot_20220409_085624_com.android.chrome_edit_606180054972605.jpg


Duuh jamani kufungwo inauma sana sipati picha Chugga man ana hali gani alipo.

Come on Chugga kakufunga bingwa mara 13 wa Uefa wala usihofu anaejua anajua tu.

YNWA
 
Wenzie akina lembu wanaelewa ugenini ukiwa umetanguliwa 3 sio kazi nyepesi kurudisha lakini huyu Mkaskazini muda wote yupo humu jamvini kama vile kashapita anawasubiri Kipara ama El Cholo nusu fainali.

Salute kwao leo wamecheza soka safi kabisa kasoro umaliziaji tu ndio umewaangusha.

Thomas ni mwalimu safi kabisa. Huu uwanja kuja na ile mentality si mchezo aisee.

YNWA
Wamejitahidi

Ila wasingeweza kurudisha 3 hata wangevunja viuno
 
Ni kweli usemayo mkuu , halafu eti sisi utd ndio tulikua tunalilia kuja anga hizi tunachekesha kweli
Anyway najua klopp akituliza kichwa vizuri kabisa najua ataiona loophole mahali kwa hawa maandadogi.

Mkuu huku kwa moto sana,kama haujui utapata aibu.
 
Wenzie akina lembu wanaelewa ugenini ukiwa umetanguliwa 3 sio kazi nyepesi kurudisha lakini huyu Mkaskazini muda wote yupo humu jamvini kama vile kashapita anawasubiri Kipara ama El Cholo nusu fainali.

Salute kwao leo wamecheza soka safi kabisa kasoro umaliziaji tu ndio umewaangusha.

Thomas ni mwalimu safi kabisa. Huu uwanja kuja na ile mentality si mchezo aisee.

YNWA
Sio lembu mkuu malizia kabisa ni lembua
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom