Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Screenshot_20220412_135609_com.android.chrome_edit_120818438462813.jpg


Hivi Manchester United walitoa aje £80m kwa huyu Maguire jamani.

Na ndio Kapteni duuh kweli kile kikosi kina hitaji kufumuliwa kabisaaaa.

YNWA
 
Screenshot_20220412_142305_com.android.chrome_edit_120535340861815.jpg


Aisee baada ya goli lake vs Liverpool ni kama dogo bei imepaa. Tetesi ilikuwa bei ni around £35m lakini sasa imepaa mara 2 yake.

Manchester United, Westham, Arsenal wanamtupia macho.

Liverpool washatuma ma scouts wao kumtazama ngoja tusubiri tuone itakua aje muda ukifika ila kwa sasa ningeshauri kwanza tupate CM mmoja wa uhakika waliopo hawatupi zaidi tunachotaka. Bissouma, Barrela nk ni mmoja wao anatufaa.

YNWA
 
Screenshot_20220412_141811_com.android.chrome_edit_120663630449816.jpg


Over to the next target.

Fabio wrapped and signed only now announcement na hapa ni tu wakishinda mechi moja ijayo itakua wamerejea EPL.

Karibu Liverpool dogo Fabio.
Born in Lisbon, Portugal, brought up in Uk, snatched by Liverpool now relax you are in safe hands and he can't wait for Jurgen super hug.

YNWA
 
Screenshot_20220412_140545_com.android.chrome_edit_120709775388872.jpg


😂😂😂😂😂Ni muhimu kukumbashana sie wala hatuna noma na Kipara na vijana wake zaidi ya heshima.

Ila sasa ikiwa na Liverpool vs Manchester United well i can tell you its means more kulikooooooooooo.

Tupia hapo na noisy blue neighbours ndio kabisaaa. Hivi itakua aje Origi atupie goli mechi dhidi ya Everton hahaha whats a way to say good bye.

YNWA
 
Jurgen Klopp kuhusu mechi ya Benfica:

Klopp: "Mechi iliyopita (Man City vs Liverpool) haina madhara kwenye mechi ya kesho dhidi ya Benfica. Hakuna aliyepata majeraha, lakini tunafikiria wachezaji ambao wako tayari kwa mechi hiyo."

Klopp: "Kukabiliana na Benfica kesho ni mechi muhimu sana. Msimu uliopita tulipigana kufuzu ligi ya mabingwa na sasa tunaweza kutinga nusu fainali. Hii inashangaza na ina maana kubwa kwetu."

Klopp: "Lengo muhimu zaidi ni kuwa timu ambayo hakuna anayetaka kukutana nayo. Nilipenda mechi yetu dhidi ya Benfica (Ureno).Tulicheza vizuri Sana, Benfica wanacheza mpira mgumu na kulinda vizuri na sasa tunajua vizuri jinsi ya kucheza dhidi yao."

Klopp: "Ratiba tuliyonayo ni ngumu sana, lakini nina wasiwasi na mechi ya kesho dhidi ya Benfica, kisha tutamenyana na City, United, Everton, kisha nusu fainali ya ligi ya mabingwa, kisha tukabiliane na Newcastle.."

Klopp: "Tunajaribu kujiwekea shinikizo ili kubaki washindani katika mashindano yote."

Klopp: "Ratiba tuliyonayo ni ngumu sana. Tulikabiliana na City na ilikuwa ngumu sana, lakini vipi kuhusu michuano iliyosalia? Tutakutana na Benfica na ninawafikiria tu. Tunajaribu kuchukua hatua ya mwisho na yenye maamuzi sahihi."

Klopp: "Sasa tuko mbele ya Benfica 3-1 lakini kati ya vipindi viwili. Matokeo ni ya udanganyifu kama matokeo ya 2-0 na tuliona dhidi ya Inter jinsi bao moja linaweza kubadilisha kila kitu."

Klopp: "Tunataka kuifanya Benfica kuchukia kucheza Anfield."

Klopp: "Tunataka kuonyesha hasira zetu kwa njia sahihi na natumai tuko tayari."

Klopp: "Habari mbaya kwa Benfica ni kwamba watacheza Anfield dhidi ya mashabiki wote. Tunataka kuwa timu ambayo hakuna anayetaka kukutana nayo."

Klopp: "Kikosi hiki cha Liverpool ndicho kikosi chenye nguvu zaidi ambacho nimekuwa nacho katika maisha yangu ya soka. Wote wapo tayari. Nimekuwa na vikosi vikubwa kila mara nikiwa na Liverpool, lakini hiki ndicho kikosi chenye nguvu zaidi."

Klopp: "Darwin Nunez? Kijana mzuri sana, alicheza vyema dhidi ya Konate, alikuwa mtulivu na ni mchezaji mzuri na akiendelea kuwa fiti atakuwa na mustakabali mzuri."
 
Leo Dunia nzima Ina furaha Club bingwa wa Dunia nzima anacheza Leo.

Njooni mushuhudie kandanda Safi kutoka kwa mabingwa wa Dunia nzima.

Sisi ni mabingwa watetezi na Dunia Ina furaha sana Leo

Ushindi ni lazima.
#CFC💙💙💙
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom