Jurgen Klopp kuhusu mechi ya Benfica:
Klopp: "Mechi iliyopita (Man City vs Liverpool) haina madhara kwenye mechi ya kesho dhidi ya Benfica. Hakuna aliyepata majeraha, lakini tunafikiria wachezaji ambao wako tayari kwa mechi hiyo."
Klopp: "Kukabiliana na Benfica kesho ni mechi muhimu sana. Msimu uliopita tulipigana kufuzu ligi ya mabingwa na sasa tunaweza kutinga nusu fainali. Hii inashangaza na ina maana kubwa kwetu."
Klopp: "Lengo muhimu zaidi ni kuwa timu ambayo hakuna anayetaka kukutana nayo. Nilipenda mechi yetu dhidi ya Benfica (Ureno).Tulicheza vizuri Sana, Benfica wanacheza mpira mgumu na kulinda vizuri na sasa tunajua vizuri jinsi ya kucheza dhidi yao."
Klopp: "Ratiba tuliyonayo ni ngumu sana, lakini nina wasiwasi na mechi ya kesho dhidi ya Benfica, kisha tutamenyana na City, United, Everton, kisha nusu fainali ya ligi ya mabingwa, kisha tukabiliane na Newcastle.."
Klopp: "Tunajaribu kujiwekea shinikizo ili kubaki washindani katika mashindano yote."
Klopp: "Ratiba tuliyonayo ni ngumu sana. Tulikabiliana na City na ilikuwa ngumu sana, lakini vipi kuhusu michuano iliyosalia? Tutakutana na Benfica na ninawafikiria tu. Tunajaribu kuchukua hatua ya mwisho na yenye maamuzi sahihi."
Klopp: "Sasa tuko mbele ya Benfica 3-1 lakini kati ya vipindi viwili. Matokeo ni ya udanganyifu kama matokeo ya 2-0 na tuliona dhidi ya Inter jinsi bao moja linaweza kubadilisha kila kitu."
Klopp: "Tunataka kuifanya Benfica kuchukia kucheza Anfield."
Klopp: "Tunataka kuonyesha hasira zetu kwa njia sahihi na natumai tuko tayari."
Klopp: "Habari mbaya kwa Benfica ni kwamba watacheza Anfield dhidi ya mashabiki wote. Tunataka kuwa timu ambayo hakuna anayetaka kukutana nayo."
Klopp: "Kikosi hiki cha Liverpool ndicho kikosi chenye nguvu zaidi ambacho nimekuwa nacho katika maisha yangu ya soka. Wote wapo tayari. Nimekuwa na vikosi vikubwa kila mara nikiwa na Liverpool, lakini hiki ndicho kikosi chenye nguvu zaidi."
Klopp: "Darwin Nunez? Kijana mzuri sana, alicheza vyema dhidi ya Konate, alikuwa mtulivu na ni mchezaji mzuri na akiendelea kuwa fiti atakuwa na mustakabali mzuri."