Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Mpo nafasi ya ngapi mkuu hata kama leo tukipigwa?
Binafsi ni mshabiki wa Chelsea FC na kiukweli kabisa napenda sana msimu huu Liverpool iwe bingwa kwa kumfunga Man City mechi ya leo maana Man City wakichukua ubingwa wa EPL mwaka huu wanakuwa na rekodi sawa na Chelsea FC kiubingwa mara 6.

Lakini bila uwongo kiukweli hii mechi Liverpool imezidiwa sana kipindi cha kwanza, nimeomba sana dua lakini ndiyo hivyo tena

Labda kipindi cha pili huenda kukawa na mabadiliko, lakini itoshe tu kusema Liverpool akiendelea na makosa kama ya dkk 45 za kwanza huenda akafungwa au akasuluhu.

Sent from my CPH2185 using JamiiForums mobile app
 
Ndio haina maajabu haya yako yenye maajabu ipo nafasi ya ngapi? Na hii Liverpool isiyokuwa na maajabu ipo nafasi ya ngapi?
Munapigaga kelele sana na hiki kitimu chenu cha mchongo haya leo mnapakatwa huko.
 
Hamjiamini kabisa. Leo hamchezi staili yenu viungo hawajiamini, makosa mengi
City watawafungia woga
Ngumu kuamini ndugu kama hawa ndio Liverpool lakini kama tukicheza kipindi cha pili hivi tutachezea mengi tu.

Cha msingi tucheze gemu yetu na haya mambo ya kutega off side kwa timu kama Manchester City sio kabisa lazima wachezaji waangalie vyema nani yupo nyuma kama goli la Jesus sio la kufungwo.

YNWA
 
Hahaha bhana bado dakika 45+.

Hapa atoke Mane aingie Diaz awakimbize kwanza maana mpaka hapa kipindi cha kwanza hakika Manchester City were the better side.

Kingine pale nyuma wamelegea sana sijui wamekutwa na nini leo hawa ma beki wetu yaaani makosa mengiiiiiiiii sana.

YNWA
Mkuu umewaza kama mimi
Aingie yule dogo angalau anajua kutafuta mpira aisee.

Akina Mane leo wapo kama wagonjwa humo ndani.
 
Binafsi ni mshabiki wa Chelsea FC na kiukweli kabisa napenda sana msimu huu Liverpool iwe bingwa kwa kumfunga Man City mechi ya leo maana Man City wakichukua ubingwa wa EPL mwaka huu wanakuwa na rekodi sawa na Chelsea FC kiubingwa mara 6.

Lakini bila uwongo kiukweli hii mechi Liverpool imezidiwa sana kipindi cha kwanza, nimeomba sana dua lakini ndiyo hivyo tena

Labda kipindi cha pili huenda kukawa na mabadiliko, lakini itoshe tu kusema Liverpool akiendelea na makosa kama ya dkk 45 za kwanza huenda akafungwa au akasuluhu.

Sent from my CPH2185 using JamiiForums mobile app
Wamekoswa koswa noma ila Becker ni kipa bhana huyu kipara afungwe analeta utemi kweny lig

Mi nasimama na liver pia
 
Nilishasema tangu mwanzo kabisa, huyu mtu hakustahili kuanza kwenye huu mtanange, pale kati palihitaji mtu mbunifu kama Naby sio huyu Mr. Back pass.
Kuna pasi limepiga kizembe nimetamani nimrangue makofi
 
Mkuu umewaza kama mimi
Aingie yule dogo angalau anajua kutafuta mpira aisee.

Akina Mane leo wapo kama wagonjwa humo ndani.
Hii game inahitaji baller na Diaz ni baller mzuri tu.

Klopp kwa sasa will be furious kwa wachezaji wake alichokiona kipindi cha kwanza. Yaaani kama namuona.

Manchester City wametumia makosa yetu kutuumiza.

YNWA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom