Fingers closed man. Well said.
Good to have your input on this hard-core issue ya Salah. Hata Klopp kwa kulinda maslahi ya wote hajachukua upande mmoja na kuegemea.
Ki ukweli hii ishu inatisha ukiwaza ma assist, magoli yake, mvuto wa kibiashara, mvuto kuleta wachezaji wengine Liverpool . Kila ukiwaza maisha bila Salah duuh binafsi najipa moyo Klopp atatuokoa kwenye hili ni kweli sio miracle worker lakini ndio kete pekee kutuadhirika endapo Mwarabu wetu atasepa PSG ama Juventus.
Chini ya Klopp kumekua na continuety ya mipango uwanjani na usajili labda hii linawapa jeuri kwamba watapata like for like signing. Bowen na Raphinah sio hata nusu ya Salah. Labda mmoja anunuliwe sasa aje kua understudy wake design kama Konate learning from Matip and VVD.
Worse to worse tumpate Darwin Nunez this June boy rated highly by Surez na anao uwezo to grow being a real hitman. Huyu anacheza pale mbele pote hivyo Klopp sasa atakua na utajili wa ku phase out Salah (haha as if ni that easy) lol na kuona kama kweli 4321 will be effective as our front 3 is being phased out. Itakua balaa kuwatoa Mane Firmino Salah na kuleta new line new formation bila hawa front kuwepo.
Hili la kudai crazy wage nimeangalia media nyingi hakuna mahala wakala wa Salah au Edwards/FSG wamesema wenyewe Salah anadai 500k kwa wiki ina maana ni spinning za aidha haters ama FSG kupima upepo endapo wakiamua kumuuza ama kumuacha asonge bure 2023 June. Salah anajua dhamani yake na anajua huu pengine ndio mkataba wake wa mwisho wenye maslahi mapana kwake kama ulivyosema peak yake as professional sio 4eva mpaka anatimiza 34 atakua ana drop kimtindo.
Hivi ina maana hawa FSG kweli hawatakaa wabadilike kamwe kuelewa vyema dynamics za EPL mpaka sasa miaka 12 wapo Anfield wanaelekea kufanya makosa yale yale. Maana kama Salah anadai £300k hio kwangu ni peanut ukilinganisha anacho contribute uwajani na nje ya wa uwanja. Lazima ifike mahala kama hawawezu kuedana na ukuaji wa klabu kutoka mid team na kua world beaters basi wasepe zao wauze timu sio kung'ang'ania sera za mid team maana hata hawa akina Jota, Diaz watakua kisoka na ku hit viwango vya juu sana na kwa vile wana umri mdogo sana ina maana wakija kudai kulipwa £250k wataonyeshwa mlango.
Katika vitu ambayo hua vinachosha ni FSG kupenyeza uongo kwa social media ku spin mambo ili kutimiza wanachotaka yaaani kwa Gini walifanikisha vyema sana na too bad mara chache uone hawa wachezaji wakitoka hadharani kujitetea muda mwingi wao husonga mbele na maisha.
Muda utasema ndugu kama Salah wanamuhitaji ama watamkaanga.
Salah ataodoka hakuna namna kama akiona anachopewa hakuna namna amesaidia kuturejesha kwenye ubora na sisi tumempa platform ya kua moja ya mchezaji bora kwa sasa duniani. Anaodoka akiwa mara 100 alivyokuja Liverpool. Anaodoka akiwa ni brand haswa amepikwa vyema.
Kwa sasa nishasema ana msimu mmoja na huu robo uliobakia lets enjoy while this last man.
Too bad ukweli wa anachokitaka Salah hautakaa ujulikane hivi hivi labda Rammy aamue kuweka mambo hadharani of which ngumu labda kuna vipengele vinambama kutoka hadharani. Hata Salah mwenyewe alishasema anataka tu aongezewe kiasi.
YNWA
Captain, suala la FSG kutaka ku-make profit kwa Salah halijaanza leo, lipo kwenye cards kwa muda mrefu sana, na ndiyo maana hata mazungumzo ya huu mkataba mpya walikuwa wanayachelewesha maksudi tu, but kujifanya wapo clever sana kunaenda ku-backfire now, maana Salah amebakiza mwaka mmoja tu na haoneshi nia yeyote ya kutaka kuondoka at LFC, na kama hatapata mkataba ataondoka for free, ndiyo maana FSG are busy trying to divide him na fans, leaking vile lies kuwa anataka BIG wages, sasa mchezaji ambaye anataka kubaki at the Club na kashasema wazi, ata-demand vipi hizo BIG wages ambazo zitampa disadvantages kwenye nia yake ya kubaki at LFC?
You have a top 3 best player in the world right now begging to stay, but you want to sell him for a profit because umeona PSG wanaweza kuwa desperate Mbappe akiondoka, this is not how a big club should be runned.
Salah is not slowing down anytime soon, use him, use his prime years, he still wants to offer his prime years with us, why are we refusing? reason ya FSG ni ipi? why would.you let number one attacker kwenye EPL aondoke? it doesnt make sense.
At least ningewaelewa FSG kama Salah angekuwa kishachuja AU yeye mwenyewe ana-force a move, but the thing is vyote hivyo havipo.
And, imekuwa ni ishu inayojirudia under FSG, kila star player anaondoka, anaondoka na bad image na kuonekana Villain, look at Torres, Sterling, Can, Wijanaldum, Suarez and even Coutinho, lazima wawe labelled as Villains, lazima fans wawe divided, hii yote ni njia ya FSG kujifanya hawana makosa kabisa, mfano tu kuna watu wanaamini kabisa Salah wants 500k p/w, na tayari washaanza kumuita greedy na other bad names, hawafikirii kabisa, na kwa bahati mbaya ikitokea Salah akiondoka, maneno hayo hayo ndiyo yatatoka kwa FSG through local jornos, kuwa jamaa alitaka 500k, tukashindwa kufikia na akaamua kuondoka, thats how FSG wanaplay hii game, imekuwa kama hivi for years, sasa kulikuwa na haja ya gani ya kum-label most humble player kwenye our Klopp's era (WIJNALDUM) kama greedy and ungrateful, unajua msimu wake wa mwisho Wijnaldum alikuwa anapata hate comments nyingi sana kutoka kwa fans kwenye his social media, kwasababu ya upuuzi wa FSG, mtu ana-demand haki yake, kama huwezi kuifikia mwambie huwezi then m-part ways kwa amani, siyo unaanza kumchafua ili wewe usionekane tatizo.
Now, Trent anapokea 180k p/w, mkataba wake unaisha 2025 i think, bado atakuwa very young, na mpaka sasa he is considered kama one of the best RB of his generation and bado anaendelea ku-improve kila siku, without Trent kwenye team yetu we create NOTHING, he is one of the most important players in the squad, sasa kama anapokea 180k, you think he will demand just 200k in 2025? No he will DEMAND more kulingana na kazi anayofanya LFC na his status on a global level, sasa ikifika time yake naye tutamuwekea zengwe? tutapoteza WC players wangapi kwa upuuzi wa FSG? kama Club imewa-outgrow waiuze kwa relatable investor, LFC kwasasa ni top 3 most followed/watched football club on earth, and Top 5 biggest soccer brands on earth with a lot of endorsements/deals, as a owner you need to up your pace and run with it, kuna price ya kulipa ukifikia level kama hizi, na tangu LFC ianzishwe haijawahi kufikia level kama hii brand wise.
Kila siku tutakuwa tuna-label our WC players kuwa ni greedy wakitaka they're well deserved pay-rise.
You cant get another SALAH kwenye transfer market, use him until he's done for good, build the new attacking line around him, tengeneza msingi mpya kupitia yeye, use his remaining peak years kutengeneza new attacking stars.