Klop ndo usajili wetu wa mda nguvu tulioufanya yaani jamaa anabadili wachezaji wa kawaida wawe monsters. Gini liver ndo ilimfanya akaonekana ameondoka kwa kiburi sasa yanamkuta, rejea kwa cotinho mpaka sasa anahaha kutafuta momentum aliyokuwa nayo liver bado haipati, amri can nae vivyo hivyo.
Hili ni onyo kwa salah asije akaharibu kufikiria kuondoka liver atasahaulika kwenye ramani mapema
Kwa Gini binafsi nilisema bora alisepa maana mchango wake ulikua haudhaminiki kabisa na FSG .. Haileti picha alizidiwa mshahara na almost MF wote akina Thiago, Henderson, Ox, Keita, Milner nk pale Liverpool huku muda mwingi wakiwa mezani kwa daktari huku yeye akiwa uwanjani kupambana kwa sababu ya timu na akilipwa pea nuts.. Kinachomkuta PSG ni kigeni kwake japo alisema yeye ni fighter atapambana kuisaka namba na kila akipata nafasi kucheza basi ataitendea haki..
Coutinho duuh Barcelona walitaka awe like for like kwa fundi Andres Inesta kumbe ni wachezaji wawili tofauti kabisa lakini pia mfumo ulimkataa pale Barcelona. Ngoja tumuone chini ya Steve G anaetumia 4 3 3 kama ya Klopp kama atarudisha makali...
Kwa Gini aisee any day of the week huyu mwamba alitakiwa abakie pale pale Anfield hao wengine senior MFs wangesepa tu excluding Fabinho...
Mpira bhana sometimes una matukio ya kuchanganya sana tazama Gini alinyimwa mkataba wa miaka 3 na angalau mshahara ufike £120k mpaka £150k lakini klabu hii hii wamekua wakiwapa nyongeza ya mishahara na mikataba Milner na Henderson 😀😀😀duniani zali la mentali ndio hizi...
Tetesi walimpa Gini mkataba wa miaka 2 na mshahara wa £100k kwa wiki akagoma ku saini. I support the boy kwa umri wake pengine ule ndio ulikua mkataba wake wa mwisho wenye maslahi kwake, Lakini pia alikua determined kufanya kazi na Koeman sijui ni mshahara mnono au taarifa ipi ilimvuta PSG na sio Barcelona...
In the meantime....
Ki ufupi tuna bahati sana ya kua na Klopp na pia ku collapse kwa masoko yetu kuu Real Madrid na Barcelona otherwise mpaka sasa sina uhakika kama Mane na Salah bado wangekua hapa hapa Anfield..
Nafarijika kuona Liverpool ya sasa sio tena stepping-stone ya wachezaji kutua hapa kusaka masoko kwingineko mbali sasa wanajua vyema mafanikio yanapatikana hapa hapa Liverpool...
Liverpool imekua na mvuto kwa wachezaji wengi kujiunga nasi na hii kutokana na Klopp pia ametupaisha parefu sana. Wachezaji wengi waliosajiliwa hua wanasema Klopp factor ilimsaidia kufanya maamuzi kujiunga nasi.. Hata hawa waliongeza mikataba mwaka jana Juni 2021 VVD, TAA, Allison, Fabinho, Robertson wanasema Klopp factor na uhakika wa kupambana UCL, EPL nk
Wamepita wengi Liverpool kwenda kusaka mafanikio kwingine wapi akina Coutinho, Surez, Torres, Fabio Aurellio, Sterling, Raul Mereleis nk
Kwa sasa fununu ni kwamba Firmino, Mane au wote kuna safari kuuzwa Juni 2022 hii kutokana na Klopp kupanga kufanya mapinduzi kikosini kwa ajili ya kupanga continuation ya mapambano..
Asante Klopp kwa kurudisha heshima yetu.
YNWA