Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Adjustments.jpg
 
mkuu humu ndani mushafungua dirisha jipya la usajili wa mashabiki, nimeshuhudia kuendelea kufundishwa kwa somo la ifahamu liverpool na wachezaji wake. Ombi langu kwenu naomba mumuongeze ollachuga katika list ya wanafunzi wapya, ni wiki ya tatu hii anaonekana jukwaa la wakenya kwenye battle ya nairobi.
Niseme tu Klopp is the system.

Yaani maelekezo ya Klopp na jopo lake la walimu kwa vijana yanaeleweka powa regardless nani acheze angalau juhudi zinaonekana.

Dirisha la winter Klopp hua sio muumini wa kununua January labda atokee exceptional player kama VVD ama uhitaji kutokana na majeruhi.

Ollachuga Oc msubiri utamuona wakishinda leo akituaminisha UCL wanaichukua tena.

YNWA
 
mkuu humu ndani mushafungua dirisha jipya la usajili wa mashabiki, nimeshuhudia kuendelea kufundishwa kwa somo la ifahamu liverpool na wachezaji wake. Ombi langu kwenu naomba mumuongeze ollachuga katika list ya wanafunzi wapya, ni wiki ya tatu hii anaonekana jukwaa la wakenya kwenye battle ya nairobi.
unaonaje tukimfata huko huko?
 
Wamuache tu.
Tuendelee na uchambuzi mkuu.

Ninayo mambo mengi sana kuhusu mpira natamani unifundishe.
Leo tupo na The Man of The Big Moments yaaani ni real Cult Hero wa hii Klabu.

Divock Origi.

Amezaliwa 18/4/95 nchini Ubelgiji eneo la Ostend.

Wazazi ni Wakenya. Babake ni Mike Okoth na Mamake ni Linda Adhiambo.

Origi amezaliwa akiwa mtoto wa pili kati ya watoto watatu wakiw wawili wanawake ambao ni Natasha na Dennen.

Alianza safari ya mpira timu ya Houthlen Oost.

Akiwa na miaka mitano aliniunga na KFC De Zwaluw Weismeer baadae akajiunga KRC Harelbeke na baadae KRC Genk.

Shule alikua anasoma Park Houthalen Primary School na baadae ajiunga na Sint Jan Berchmans College.

Pale KRC Genk alidumu miaka kwenye timu ya vijana.

Akiwa na miaka 15 ajiunga na Lille ya nchini Ufaransa.

Ma Scout wa Liverpool walianza kumfuatilia na baadae kuridhishwa na kiwango na potential yake wakashauri anunuliwe. Mwaka 2014 Tarehe 29 Mwezi wa 7 Liverpool wakamsajili kwa kusaini miaka 6 kwa dau la £10m kutoka Lille. na kisha kumrudisha kwa mkopo wa msimu mzima Lille.

Key Points Origi

* Alicheza mechi 44 Lille akifunga goli 9.

* Dakika ya 87 alifunga goli lake la kwanza kimataifa World Cup 2014 na kuisaidia timu yake ya Ubelgiji kusonga mbele kwa kuwafunga Urusi.

* Alicheza mechi yake ya kwanza EPL dhidi ya Manchester United 12/9/2015.

* 2/12/2015 alifunga goli lake kwanza Liverpool mechi ya League Cup dhidi ya Southampton. Mechi hii alifunga hat trick.

* Alikwenda kucheza Ujeremani kuwachezea VFL Wolfsburg kwa mkopo msimu wa 2017 2018. Alicheza mechi 31 akifunga goli 6.

* Amecheza mechi 33 Kimataifa na kufunga goli 3.

* Magoli muhimu sana Liverpool yanayomfanya kua fans favourite ni..

-Goli dhidi ya Everton dakika ya 96 baada ya makosa ya kipa wa Everton.

- Goli la kwanza Uefa alifunga dhidi ya Dortmond tukitoka sare ya moja moja.

- goli lake la kwanza EPL aliwafunga Westbromwich Albion pale Anfield.

-7/5/19 semi final ya Pili Uefa dhidi ya Barcelona pale Anfield alifunga magoli mawili muhimu sana na kusaidia Liverpool kuingia fainali ya UCL 2019 na kushinda taji hilo fainiali dhidi ya Tottenham huku pia akifunga fainali.

*Amecheza mechi 103 EPL akifunga magoli 21.

* Amecheza mechi 6 UCL akifunga magoli 4.

* anacheza nafasi zote pale mbele yaani mshambuliaji wa kati ama winga wa kushoto au kulia.

* Ana mkataba Liverpool mpaka 30/6/22 kwa kulipwa around £60,000 kwa wiki.

* anavaa jezi namba 27.

* Urefu wake ni 1.85mita.

* Magari yake anayopedelea ni Audi,Porsche Cayenne, Ford na Mini Cooper.

* maisha yake ya mahusiano hajajulikani ni jamaa asieweka hadharani mambo hayo.

YNWA
 
Leo tupo na The Man of The Big Moments yaaani ni real Cult Hero wa hii Klabu.

Divock Origi.

Amezaliwa 18/4/95 nchini Ubelgiji eneo la Ostend.

Wazazi ni Wakenya. Babake ni Mike Okoth na Mamake ni Linda Adhiambo.

Origi amezaliwa akiwa mtoto wa pili kati ya watoto watatu wakiw wawili wanawake ambao ni Natasha na Dennen.

Alianza safari ya mpira timu ya Houthlen Oost.

Akiwa na miaka mitano aliniunga na KFC De Zwaluw Weismeer baadae akajiunga KRC Harelbeke na baadae KRC Genk.

Shule alikua anasoma Park Houthalen Primary School na baadae ajiunga na Sint Jan Berchmans College.

Pale KRC Genk alidumu miaka kwenye timu ya vijana.

Akiwa na miaka 15 ajiunga na Lille ya nchini Ufaransa.

Ma Scout wa Liverpool walianza kumfuatilia na baadae kuridhishwa na kiwango na potential yake wakashauri anunuliwe. Mwaka 2014 Tarehe 29 Mwezi wa 7 Liverpool wakamsajili kwa kusaini miaka 6 kwa dau la £10m kutoka Lille. na kisha kumrudisha kwa mkopo wa msimu mzima Lille.

Key Points Origi

* Alicheza mechi 44 Lille akifunga goli 9.

* Dakika ya 87 alifunga goli lake la kwanza kimataifa World Cup 2014 na kuisaidia timu yake ya Ubelgiji kusonga mbele kwa kuwafunga Urusi.

* Alicheza mechi yake ya kwanza EPL dhidi ya Manchester United 12/9/2015.

* 2/12/2015 alifunga goli lake kwanza Liverpool mechi ya League Cup dhidi ya Southampton. Mechi hii alifunga hat trick.

* Alikwenda kucheza Ujeremani kuwachezea VFL Wolfsburg kwa mkopo msimu wa 2017 2018. Alicheza mechi 31 akifunga goli 6.

* Amecheza mechi 33 Kimataifa na kufunga goli 3.

* Magoli muhimu sana Liverpool yanayomfanya kua fans favourite ni..

-Goli dhidi ya Everton dakika ya 96 baada ya makosa ya kipa wa Everton.

- Goli la kwanza Uefa alifunga dhidi ya Dortmond tukitoka sare ya moja moja.

- goli lake la kwanza EPL aliwafunga Westbromwich Albion pale Anfield.

-7/5/19 semi final ya Pili Uefa dhidi ya Barcelona pale Anfield alifunga magoli mawili muhimu sana na kusaidia Liverpool kuingia fainali ya UCL 2019 na kushinda taji hilo fainiali dhidi ya Tottenham huku pia akifunga fainali.

*Amecheza mechi 103 EPL akifunga magoli 21.

* Amecheza mechi 6 UCL akifunga magoli 4.

* anacheza nafasi zote pale mbele yaani mshambuliaji wa kati ama winga wa kushoto au kulia.

* Ana mkataba Liverpool mpaka 30/6/22 kwa kulipwa around £60,000 kwa wiki.

* anavaa jezi namba 27.

* Urefu wake ni 1.85mita.

* Magari yake anayopedelea ni Audi,Porsche Cayenne, Ford na Mini Cooper.

* maisha yake ya mahusiano hajajulikani ni jamaa asieweka hadharani mambo hayo.

YNWA
Oh kumbe huyu ni mbelgiji!

Kumbe wa 95!!!Mdogo.

Nimefurahi kumfahamu mwamba Origi.


Natamani uendelee mkuu,
Yaani siku nzima vile nasubiri kuona comment yako.
 
Joseph Desire Job????

Mkuu tumekukumbusha mbali sana?, wengi watoto wa juzi tu hawamjui desire job.

Miaka hiyo jamaa jina lake nilikuwa nalisoma kama lilivyoandikwa nasema “desire” nilivyoliona nimeshtuka na mimi desire job ?

Alicheza Middlesbrough pale uingereza miaka ya 2000-2006, namkumbuka sana huyo mwamba.
 
Oh kumbe huyu ni mbelgiji!

Kumbe wa 95!!!Mdogo.

Nimefurahi kumfahamu mwamba Origi.


Natamani uendelee mkuu,
Yaani siku nzima vile nasubiri kuona comment yako.

Ni raia wa Ubelgiji kwa kuzaliwa na ni Mkenya kwa uraia wa wazazi wake.

Anaongea lugha 3 safi kabisa Kiswahili, Kingereza na Flemish.

Ndio Mbelgiji wa pili kufunga katika fainali ya Champions League, wa kwanza akiwa Yannick Carrasco na timu ya El Choro.

Ndio mchezaji wa Kwanza with Kenyan origin kufunga kombe la Dunia.

YNWA
 
Mkuu tumekukumbusha mbali sana?, wengi watoto wa juzi tu hawamjui desire job.

Miaka hiyo jamaa jina lake nilikuwa nalisoma kama lilivyoandikwa nasema “desire” nilivyoliona nimeshtuka na mimi desire job ?

Alicheza Middlesbrough pale uingereza miaka ya 2000-2006, namkumbuka sana huyo mwamba.

Huyo mwamba alikuwa akiupiga mwingi sana Kipindi hicho nilikuwa Fans wa Cameroon lilalia huku nikiwa Shabiki kindakindaki wa Laurent Etemi Mayer huyu ni ball controller aliyewahi kukipiga Arsenal pale miaka ya 2000 ambapo game yake ya mwanzo alitufunga sisi Liverpool kwa kuwafungia Arsenal goli la ushindi niliumia sana kwani Arsenal walikuwa wana miaka 9 hawajawahi kutufunga lakini nikajikuta najifariji kwasababu Kafunga Laurent.

Pia ilikuwa uwanjani kama sikumuona Solomon Olembe basi hiyo game siangalii!

Mwisho nikasikitishwa sana na kifo kilichotokea uwanjani cha Marc Vivian Foe.

Niliachana na kuishabikia Cameroun baada ya kizazi cha hao jamaa kuondoka na kuja kizazi cha kina Alexander Song.
 
Huyo mwamba alikuwa akiupiga mwingi sana Kipindi hicho nilikuwa Fans wa Cameroon lilalia huku nikiwa Shabiki kindakindaki wa Laurent Etemi Mayer huyu ni ball controller aliyewahi kukipiga Arsenal pale miaka ya 2000 ambapo game yake ya mwanzo alitufunga sisi Liverpool kwa kuwafungia Arsenal goli la ushindi niliumia sana kwani Arsenal walikuwa wana miaka 9 hawajawahi kutufunga lakini nikajikuta najifariji kwasababu Kafunga Laurent.

Pia ilikuwa uwanjani kama sikumuona Solomon Olembe basi hiyo game siangalii!

Mwisho nikasikitishwa sana na kifo kilichotokea uwanjani cha Marc Vivian Foe.

Niliachana na kuishabikia Cameroun baada ya kizazi cha hao jamaa kuondoka na kuja kizazi cha kina Alexander Song.
Duh Salute King Ngwaba kumbe upo long time hivyooo...

Ile Cameron ya miaka ile fire sana binafsi nilikua naishabikia aisee.

YNWA
 
Duh Salute King Ngwaba kumbe upo long time hivyooo...

Ile Cameron ya miaka ile fire sana binafsi nilikua naishabikia aisee.

YNWA
Kiukweli Nigeria na Senegal ndo team nilizokuwa nazikubali sana , Cameroon pia wakati ule kwa mbali, mnawakumbuka akina Terrible West? Babayalo, Fadiga mzee wa Cheni hahahaha, Ndief mutu mufupi,.mpaka Leo kuna best yangu mfupi sana namuita Ndief, hadi kwenye simu nimem save Ndief,

Kifo cha Marc Vivian Foe kwakweli kilinisikitisha sana pia
 
Kiukweli Nigeria na Senegal ndo team nilizokuwa nazikubali sana , Cameroon pia wakati ule kwa mbali, mnawakumbuka akina Terrible West? Babayalo, Fadiga mzee wa Cheni hahahaha, Ndief mutu mufupi,.mpaka Leo kuna best yangu mfupi sana namuita Ndief, hadi kwenye simu nimem save Ndief,

Kifo cha Marc Vivian Foe kwakweli kilinisikitisha sana pia
Jamaa walikua noma sana maana hata kimataifa walituwakilisha vyema sana Africa angalau kwenye kombe la Dunia.

Cameron walifuzu mara zote Kombe la Dunia kuanzia mwaka 1990 mpaka 2014. Kombe la Dunia mwaka 2018 hawakufuzu.

Old is gold man ilikua burudani kuwaangalia hawa wakongwe.

Senegal alitoa kali ya zote mwaka 2002 Kombe La Dunia kuwapiga Ufaransa 1 bila. Wafaransa hawakuamini kipigo kile.

YNWA
 
Duh Salute King Ngwaba kumbe upo long time hivyooo...

Ile Cameron ya miaka ile fire sana binafsi nilikua naishabikia aisee.

YNWA

Kilichonifanya niipende Cameroon nakumbuka ni kuangalia Movie tu kibanda umiza enzi hizo Nipo Zanzibar Kuna Mtaa unaitwa Chumbuni Mtaa mzima ilikuwa hakuna mwenye Video Tape player (Deki) hivyo tunaenda kwa Mzee mmoja maarufu anaitwa NDEVU kuangalia Movie za Kivita enzi za Komando Vipensi na War Bus 😂😂😂

Basi kabla ya Movie huwa tunawekewa Trailer za Mziki wa Rumba basi around mwaka 1996 au 1997 mzee NDEVU wiki nzima alikuwa akituwekea Trailer ya Pepe Kale ya Roger Miller 🎶🎶
Makanaki Makanaki 🎶🎶
Mpaka nikajikuta naipenda Cameroon.

Mshua alisoma Newscastle Upon Tyne University hivyo alikuwa Mshabiki wa NewCastle kindakindaki nikamfuata kuipenda NewCastle ya Kaven Keegan kama miaka miwili hivi si nikaja kumuona Rigobert Song yupo LIVERPOOL wakati mimi naipenda Cameroon! Nikamwambia Mshua baki na Nucasto yako mimi simo nahamia Merseyside 😂😂😂
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom