Mimi nahisi kama mnaelekeza lawama zenu kusiko.
Kevi De Bruyne anachukua tuzo ya mtoa assisst anayemfuatia ni Trent, liva kama Bayern, Madrid na timu nyingi siku hizi zinatumia attacking fullbacks. Na liva hua haitegemei kiungo kucreate chances au hata kufunga magoli.
Ndiyo maana Gini akiwa timu ya taifa hua ni scorer na assisster mzuri tofauti na akiwa liva. Mid ya liva kazi yake ni kusapot defense na kutibua mipango ya wapinzani. Chances atatengeneza Trent au Robrtson scorer atakua Mane au Salah.
Binafsi nafikiri Jota hatokua na consistentcy ya kuscore kwakua liva imetengenezwa scorer kua RWF au LWF. Na kulaumu kiungo kukosa ubunifu siyo sahihi pia kwakua hata usajili wa Thiago haukulenga aje kufanya huo ubunifu.
Akiwa bayern thiago hakua na majukumu hayo badala yake goretzika ndiye alikua ana hili jukumu na uhuru wa kuingia mpaka ndani kwenye boksi. Muda huo thiago anakua nje ya 18 no wonder hana assisst.
So klopp anajua kwake mid siyo ya kucreate chance ila fullbacks ndiyo wenye hiyo kazi. Ukisema mid haina kazi haijaonyesha ubunifu klopp anaona imefanya kazi yake vyema ya kusapot defense ndiyo maana hamjapigwa goli.