Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

gettyimages-1174616843-612x612.jpg
 
Fahamu kuwa wanaoropoka humu kuwa 'Salah anajiona Mkubwa kuliko Timu', 'Salah auzwe', na blah blah nyingi basi hawajaiona hiyo Interview wala hawajui imefanyika lini bali wanasikia tu maneno kutoka Mitandaoni.

Salah hajawahi kujiona mkubwa kuliko Liverpool hata siku moja.
Salah hajawahi kumfokea Klopp hata siku moja.
Salah kwenye Interview hajazungumza jambo baya lolote.

Lakini kuna Watu wamekurupuka From nowhere wanamshambulia kwa kitu ambacho hata hajakisema sababu tu wamekuta kiimeandikwa mitandaoni.

Mfano: Tulishuhudia Capatain Hendo kufanyiwa Sub akakereka na Kumfokea Klopp live, Mane pia alifanyiwa Sub akamfokea Klopp! Lakini kwenye hakuna aliyeibuka na kusema Wanajiona wakubwa kuliko Timu wakati uhalisia Mane na Hendo ndiyo wanavyojiona.
[/QUOTE/]
Hivi timu nyingine kama Spurs, Citizens, Man UTD huwa wanachokonolewa na media za UK kama Liverpool?
 
Huwa nawashangaa watu wanaomponda takumi

Yule dogo akitulia na mfumo watalia Sana watu pale England
Kabisa

Kila mmoja ana pace yake ya kusettle... Lakini in most games taki amecheza kuna positive results because of his pressing
 
SALAH AND THE NOTION OF HIM BEING UNHAPPY AT THE CLUB.

IS IT TRUE? please follow my article below.

Its safe to say that, we as LFC fans are enjoying the good years, hii pleasure huwa haiji mara kwa mara, especially kwa Club yetu, huwa tunapitia the good years kwa phases, ni kama tradition/mizizi iliyopo Anfield, personally, i've enjoyed 3 good phases, GH (R.I.P) phase, Benitez phase & now Klopp's phase, naweza sema kuwa nili-enjoy zaidi phase ya Benitez, because my most favourite player Stevie G was at the top of the World, it was a very good phase.

BUT, there's no doubt, Klopp ametupeleka kwenye new phase, siyo tu uwanjani, bali hata nje ya uwanja, kwenye masuala ya financial & ongezeko la fanbase world wide , hii ni most important phase in Club's history, ni phase ambayo ina top gunz wengi sana, so kwa LFC ku-raise on top kwasasa, will go down in HISTORY, it will be one of the memorable phase in our Club's history.

Again, hii phase imeshudia Club ikisajili na kukuza World Class players, mmojawapo akiwa ni MOHAMED SALAH, african born & raised, he came at the Club bila expectation kubwa kutoka kwa fans, he wasnt a star back then, so personally i was just hoping atafanya vizuri, BUT, he came in and took his career & Club at large to the whole new level, breaking records after records, then just like that, he BECAME a superstar, mpaka sasa SALAH ndiyo LFC's face world wide, he's a global superstar, LFC most marketable footballer, he won LFC a lot of TROPHIES (we cant deny it), he won LFC a lot of financial deals, especially t-shirt deals/sales etc, ame-play part KUBWA sana kwenye MAFANIKIO ya LFC ya SASA.

BUT, is he treated like a SUPER-STAR at LFC? lets be honest, kwa alichokifanya Salah (even Mane but topic yake ni siku nyingine) at LFC, kinahitaji HESHIMA kubwa sana, but personally sidhani kama anaipata hii heshima, na luckly ukiangalia my old posts utaona ni jinsi gani nimekuwa nikiongea kuhusu hili, when Salah came in at LFC na kuvunja records kibao, msimu uliofatia alitaka kuendeleza hili suala (hii ipo kwa kila player), but alianza kuwa targeted taratibu na medias za UK, kulikuwa na bad PR nyingi sana kuhusu Salah, kwa mtu ambaye hajapata nafasi (siyo bahati, because Tanzania is the most blessed country on earth) ya kuishi kwenye hizi Nchi za wenzetu, unaweza ukadharau sana suala la racism na favourtism, especially kwenye socio-culture issues, kwenye soccer la UK kumekuwa na ishu kubwa sana ya profiling, especially linapokuja suala la foreign players, Salah ni moja kati ya wachezaji ambao wanachukiwa sana na medias za UK, its like they dont want him kuendelea kuvunja hizi records, meanwhile medias huwa zinasherekea even small details za Harry Kane (he's a very good player, we cant deny it), but ingekuwaje kama Salah angekuwa ni Citizen wa England? treatment ingekuwa the same?

Now, Salah was promised by Klopp to captain game yetu dhidi ya ile team ya denmark kwa CL, but akabadilishwa in the last minute na kupewa Trent, kwasababu Club ilifikiria zaidi kuhusu Headlines za magazeti kuliko uhalisia, Club iliwaza kuhusu headlines za magazeti/social medias kuwa Scouse kid ana-captain team kwa mara ya kwanza akiwa na miaka 21, this was a very stupid idea, Salah ameifanyia hii club mambo mengi sana kuliko Trent, you can easily replace Trent, but how can you replace Salah's goals-input?, alikuwa kashajiandaa ku-captain team, then unamuondoa dakika za mwisho kwa kuhofia backlash ya UK medias? je kwa hali hii Club inasaidia kumlinda Salah dhidi ya hizi hate orianted-media houses, Club inasaidia kumpa HESHIMA yake anayositahili?

Nataka nitoe mfano kidogo, last season, wheh Fabinho got injured, Henderson aka-claim ile 6 role, na alicheza vizuri sana for 2 months, so sifa zote zikahamia kwake, British medias, LFC based medias and even the Club, ikaaminisha watu kuwa ni MOST IMPORTANT player at the Club na ndiye ame-play part kubwa ya EPL title, mimi na wewe, tunajua wazi kabisa kuwa bila SALAH, MANE, VVD, FABINHO, ALISSON, hii Club isingekuwa CHOCHOTE, but for the last 1 year imekuwa ni HENDERSON, which is not bad because medias zinafanya hivyo kwaajili ya story, kuwa a very average player ame-raise kuwa mchezaji mzuri, siyo mbaya but narrative ya kuwa ni most imporant player ni kweli? na je wenzangu wa LFC ambao mtaona kama namchukia Henderson, hiki anachokifanya Fabinho ku-cover nafasi ya Best CB in the world right now VVD bila shida wala jasho lolote lile (imekuwa rahisi sana kwake) unaona kinaongelewa wapi? Fabinho angekuwa ni UK citizen, hadithi ingekuwa tofauti sana, but ni m-brazil so haina haja ya kumpa headlines kwenye papers, hii ni profiling ambayo ipo pia kwa kina Mane, Firmino, Gini & especially Keita.

Jana, official site ya CLUB, imetumia usiku mzima kumuondoa votes Henderson kwaajili ya tuzo za BBC, which was so embarrassing, na hivi vitu huwezi ona Club ikifanya kwa kina Salah, na hatujui mengi sana yanayoendelea nyuma ya pazia, but mpaka kufikia hatua kwa Salah kuonekana kuchukizwa na suala la kuondolewa u-captain dakika za mwisho, anaona kabisa kuwa anaonewa, na yupo katika hatua za kufikia kikomo (God forbid).

Man, i always laugh juu ya new LFC fans, mtu anaweza akakwambia Salah aondoke tu, you cant replace Salah, you cant replace Mane, you cant replace Fabinho, you cant replace VVD, hapo juu nilianza na suala la Phases, maana yangu ni kuwa, kwasasa LFC fans tunahitaji sana kuwa na phase ndefu sana ya good years, good years zetu nyingi sana ziliharibika kwa kuuza key & star players, na kama tunataka kukaa on top kaa muda mwingi sana, hatutakiwi kuuza our star players, huwezi kumuuza Salah akiwa on top kwasasa, huwezi kuuza Mane akiwa on top kwasasa, tumia mpaka legs zife ndio wauze, fanya rebuild ya kikosi hawa wakiwepo, tengeneza a very young team kupitia hawa, kwasasa tupo juu sana kimpira, na kuuza wachezaji ma-star kipindi kama hiki ni kichekesho kikubwa sana.

Man, its true, Salah is unhappy at LFC kwasasa, suala la kuita AS (Spanish based NP) kwaajili ya interview ambayo lengo kubwa ilikuwa ni dig at Klopp na Club kiujumla, hii haikuwa stunt ya new contract, alikuwa anataka ku-make statement, i know the Club will try to pen him down, but hii stunt haikuwa kwaajili ya mkataba, aliona amekuwa disrespected sana, Club inaangalia zaidi its image kuliko kulinda haki za wachezaji, na huwa nashangaa sana LFC fans wanapo-side na hizi stories za kwenye medias.

Salah, ni LEGEND at LFC, ameifanyia makubwa sana hii CLUB yetu kwa kipindi alichokuwepo, anasitahili SIFA na HESHIMA kubwa sana, msimu huu, yeye, Fabinho, Robertson, Jota, Gini & Matip ndiyo wanafanya tuwe top kwenye LEAGUE, yupo kwenye GOOD FORM, na anaelekea ku-deliver tena PL title, so i urgue my fellow fans to respect this WC player, he's one of our own, he's muslim & African, thats why he's profiled sana, he's pissing their LEAGUE and they hate him for that, juzi kavunja record ya STEVIE G kwenye CL, kama ningekuwa English citizen/bitter scouser ningechukia kuona a muslim & african born & raised ana-top kila record ya the most decorated club in the UNITED KINGDOM.

And we have short memories, wote mnakumbuka jinsi medias zilivyokuwa zinamuhusisha na move ya Madrid baada ya kuvunja records nyingi msimu wa kwanza, mpaka Agent wake akaamua kuingilia kati, they wanted him to leave, because wanataka Harry Kane au Vardy ndiyo wavunje hizi records, let me ask you, tangu msimu wake wa kwanza mpaka sasa, Salah ameonekana kwenye TOTY mara ngapi? au kwenye tuzo zingine mara ngapi? Salah stats speaks for themselves, he's a World BEATER.

Rebuiding process ishaanza at LFC, Jota ndiye atakayeongoza hii process, but at 23, Jota bado anapata tabu sana ya consistency, ni aina ya players ambao wanahitaji sana muda wa kujifunza kuhusu consistency, watu wengi sana hawamjui Jota vizuri, akiwa out of form ni anakuwa zaidi ya HOVYO, his passing game siyo nzuri na ndiyo weakness yake, sasa imagine kuwa out of form na kuwa na weakness ya kupiga measured and moving passes, na kabla ya his injury alikuwa kishaanza kutoka kwenye form, BUT he's coachable.

This is it, if Salah feels like he needs to try something new then i'm not against it at all, amekuwa good servant at the Club na kuvumilia mengi sana, negative articles, profiling etc, BUT above all, ame-play part KUBWA sana kutupa hizi good years, so as an employee kama anaona mazingira aliyopo hayamfanyi kuwa na furaha, then i wont mind yeye kuondoka kabisa, he has played his part, Lakini my HEART inaombea sana aendelee kubaki na kuendeleza hii phase yetu, we need him kwenye rebuilding process, kuna watu wanafikiria FSG watanunua wachezaji aina ya Mbappe, this wont happen (though anything is possible kwenye footie), but looking at FSG model they will look at World class prospects zaidi kuliko established young stars, so kwa mtindo huu bado tutahitaji kina Salah, ili waendelee kuishikilia team huku tukiwa tuna-introduce new players (kama tunavyofanya kwa Jones).

Yes he's unhappy at the moment but we need HIM to stay, the CLUB should take responsibility for this.
Je kumhitaji huko ni kwa ghalama yoyote?
Amekosa kumshukuru Klopp kwa mafanikio alopata sasa hivi anaaza kumkosoa.
 
Huyu nae analilia vitu vya kijinga. Yeye si kapteni wa Misri bado hatosheki tu. Anataka kila kitu apewe Yeye. Kalilia mapenat mpk kapewa. Yaani milner akiwa uwanjani na Yeye anaumia roho kweli maana milner ndo atapiga kama ikipatikana. Na ndo maana mchoyo Sana uwanjani.
Anajiona messi labda
 
Huwa nawashangaa watu wanaomponda takumi

Yule dogo akitulia na mfumo watalia Sana watu pale England
Namponda sababu sasa hivi anazurula tu uwanjani juzi kfunga goli la ufundi sana lakini baada ya hapo hamna kitu.

Dakika 90 anapewa ili aimarike bado tunasubili.

Au apigwa misumali kama Shaqili?maana tulitegemea agawe dakika za wenyewe pale mbele ajabu akiingia anachachawa tu.

Jota kaja kibabe kutishia namba za wenyewe na magoli kesha lazwa tayali hawa wasio pumzika hawaumii.
 
huwa nafurahi sana timu ya Jose inavyofungwa, hawa inabidi wapigwe tena na tena, na bado akiumia son sijui itakuaje
Lazima ufurahi, hasa ukikumbuka namna alivyotumia kikosi cha pili kuwapoka ubingwa na kumpa City. Spurs siyo quality ya Liverpool kwa sasa. Hata hiyo pressure ya ubingwa tuliyoweka mpaka kabla ya game tatu zilizopita ni Mourinho master class pekee. Labda uniambie ni kocha gani angepigania ubingwa na kikosi yenye hawa akina Dele Alli, Harry Winks, Mousa Sissoko, na Lucas Moura waliochuja.

Kuhusu Son au Kane kuumia hakuna shabiki wa Spurs anataka kusikia kitu kama hicho maana kila anayeijua Spurs anajua bado imejengwa kuwazunguka hao.
 
Week nzima hii Mourinho alikuwa anapiga umbea kwa Klopp tu....Ahsante sana Leicester kwa kunitandikia hii mtu.
Alikuwa anasema ukweli. Klopp namvulia kofia kuanzi attitude mpaka mentality. Kumbuka namna alivyojifanya mjinga siku ile kwa Lampard. Ila kuhusu maneno ya Mourinho hata yeye Klopp aliyarudia kuwa anashangaa tuzo kupewa yeye na si Hans Flick. Ila ndiyo mchezo ulivyo, siyo kila kitu kitabirike kama Balon D'O.
 
Jose na Spurs tulishawalegeza ndugu hahaha....

Eti nao ni serious contenders...

Wanahitaji to borrow a leaf from Klopp and his boys...

EPL msimu huu ndugu M-mbabe imekua na matokeo yasiotarajiwa kabisa...

Ninavyoona mimi bado Manchester City is the team to beat followed by Chelsea follwed by Manchester United followed by Tottenham...

YNWA
Maoni haya yataendelea kusimama ikiwa Spurs haitafanya marekebisho dirisha dogo. Levy akifanya tena master class kama alivyofanya dirisha kubwa, raundi ya pili tuko na nyinyi. Kwa sasa hata sare Jose aifurahie tu.
 
Uwekezaji umefanyika, acha muendelee kupata mavuno. Huwa nadhani kuwa kwenye enzi ya sasa ya soka, project ya Liverpool ndiyo mfano bora zaidi wa kuigwa/kijifunzia kwa timu zinazotafuta kurujea kwenye kilele cha mafanikio kama vile Arsenal (tangu 2004), United, Barcelona, Real, na zingine. Spurs siwataji kwani najua project yao iko unique. Inabezwa kwa sasa ila huko mbele itaeleweka.
 
Je kumhitaji huko ni kwa ghalama yoyote?
Amekosa kumshukuru Klopp kwa mafanikio alopata sasa hivi anaaza kumkosoa.
The guy hajamlaumu klopp

Drama za media Tu

He was not happy kukosa armband but accepted it as a coach decision
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom