Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Muwe mnatazama mechi wazee. Au wewe umeangalia kwenye channel tofauti na sisi?
Mi nimeangalia Canal + nimeona kichwa cha Richarlson kimegonga mwamba, nimeona Adrian akistruggle kuzuia curved ball ya James, nimeona Refa akiwabeba pia
 
Hamna aliyeignore. Bali nyie ndo muliignore ability ya Liverpool kwa kudhani kwamba atakuja jichotea tu points.
Naiheshimu Liverpool hata msimu hii naipa nafasi kubwa ya kuchukua ubingwa na hata mechi leo niliamini atashinda,ila Everton msimu huu ana jambo lake hawa jamaa hawa bahatishi wanajua wanacho kifanya.
 
Mkuu ujaangalia mpira wewe everton wakawaida sana mechi ya pale anfield tunawakalisha vizuri sana,msimu ulipita pia tulitoka nao draw hapo goodson park na ubibgwa tukachukua.

Everton wakawaida sana VAR na refa vimewasaidia hawana mpira wowote wa ajabu.
Brother hayo ya mbele hamna anaye yajua au umesahau ya juzi na Aston Villa
 
Liverpool HALISI tupongeze team mentality leo,kutoka 7-2 down hadi 2-2 ktk derby sio jambo jepesi!
VAR ni sehemu ya mchezo
Tunajipanga sasa kwa mechi ijayo
 
Hamna bao lolote Adrian kasababisha leo!
Bao la kwanza ni very powerful header,beki ilitakiwa iwepo pale kuzuia
Bao la pili ni free header,beki ilitakiwa iwepo pale.
Liverpool HALISI tuwe nyuma ya team,hamna haja ya kutukana wachezaji,tuwaachie Liverpool-Pep Guardiola na Liverpool-Ancelotti wafanye hayo
 
Brother hayo ya mbele hamna anaye yajua au umesahau ya juzi na Aston Villa

Mkuu kwa mtazamo wako everton kacheza kumzidi liverpool? Au mpira ujaangalia?

Yaani everton wakawaida sana mkuu ,licha watu waliwaona kama tishio lakini wakaida sana kuhusu kuchukua ubingwa hapana mkuu Kwa mpira ule.

Liverpool tumeanza na mechi ngumu lakini tunapata matokeo gemu kubwa hivyo ndio kipimo.
 
Hawa jamaa kama leo wameshindwa kuwafunga basi sidhani kama huko mbeleni watatweza tena maana hii derby imekua ya upande mmoja muda mrefu na kipindi hiki Everton yuko vizuri sana nilitegemea washinde kabisa.

So farwamejitahidi sana Ancelloti ana jambo lake msimu huu.


Everton na Aston Villa ni sawa na Leicester City ya Msimu uliopita.
Wanaanza kwa kasi mwishoni pumzi unakata.
 
Naiheshimu Liverpool hata msimu hii naipa nafasi kubwa ya kuchukua ubingwa na hata mechi leo niliamini atashinda,ila Everton msimu ana jambo lake hawa jamaa hawa bahatishi wanajua wanacho kifanya.

Everton wakawaida sana,wangemfunga leo liverpool nyumbani kwao ningeona wako vizuri.

Sasa huko nyumbani unashindwa kumfunga anfield pale utaweza maana anfield liverpool msimu wa nne sasa ajapoteza pale anfield.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom