Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Tunaposema washabiki sio nyie wapiga kelele mitandaoni bali wenye uanachama kabisa. Sasa Man city ilikua na washabiki chini ya 10 million kufikia 2010 ila mpaka sasa wamesajili zaidi ya mashabiki million 100 duniani sasa unaweza niambia hao washabiki wapya wametokea wapi? Au walikua wanashabikia Cricket na Golf?

Pia Washabiki sio kujaza uwanja mfano chelsea kuna kipindi ilisajili mashabiki mamilion kutoka China ila wanakujaga wote stamford bridge?

Espanyol imemsajili Wu Lei kahamia hapo na washabiki mamilion wa kichina ila bado uwanja haujai sababi sio mashabiki wote wapo spain kumuangalia ila mauzo ya jezi na kadi za uanachama yameongezeka.

Sasa swali langu ni hili kama washabiki hawahami nisaidie hao wa Man city wametokea wapi na naomba unieleze wale washabiki zaidi ya million 30 wa Leeds leo hii wako wapi??

Naomba uje na data sio kelele
Kwamba unaenda kuokota data hapa unakuja simama nazo kama hoja ya kupinga jambo ?? forum ambayo ni user generated kama Jamii forum , unakuta mtu kama "Zero IQ" kashusha mambo yake unayabeba unaenda fanya reference ...


Labda nikusaidie namba ya kujua idadi ya mashabiki na ukuaji wa Brand ya club

1. Mauzo ya Jersey na mapato yatokanayo na mauzo hayo
2. idadi ya watazamaji wa mechi zinazo husu club husika
3. Social media interactions
4. Wachezaji wanao ongoza kuuza jersey zao .. top ten club inaingiza wangapi ?


ndio maana leo utashangaa Neymar anazidiwa na Nemanja matic , ni kwasababu ya fanbase ya club
Screenshot_20200330-091321.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata Van Dijk akitakiwa na timu kubwa ataondoka liverpool
Liverpool fans mna arrogance!! Trophyless EPL kwa miaka 30 then mnajikuta mna expect much?

Suarez aliwakimbia sababu hampo UCL so did Top class players waligoma kuja hapo then mnajiboast hvi mtadhani ni top class team.

Liverpool ni average british team iliokua na msimu mzuri kma Leicester 2015 ama spurs last season, na thanks to Allah kutolewa UCL hii na Atletico imewakata jeuri yote!!

Hope next season mrudi mlipotoka three seasons ago!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ni Liverpool na Manchester City ushiriki wake wa mashindano ya Ulaya last decade..

Liverpool imecheza misimu 7.. Manchester city misimu 8

Liverpool ni bingwa na kacheza final 3 mfulilizo along the way

City mafanikio yake makubwa ni nusu final moja tu , safari yake it's either round of 16 au group stage... misimu hii miwil ambayo Liverpool yote kafika final wao wameishia robo

iwe domestic au Ulaya.. city yuko miles away kutoka Liverpool alipo , na huenda asifike hapo kabisa
View attachment 1403717View attachment 1403719View attachment 1403720

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Liverpool imevuka round of 16 mara 3 pekee last decade hapo acha misimu 6 hamjashiriki UCL kabisa yaani kabisa sasa mpka hapo ushiriki wenu ni mdogo sana kuliko City.

Then last decade Man City ana makombe 10 then wewe mna mangapi mkuu?? Na usintaji club world cup na super cup ambavyo ni bonanza tu. Mtajikuta mna kombe moja pekee.

Na nimeshakueleza timu kufika UCL tu ni achievement kwa timu yeyote ile maana kuna faida nyingi sana hasa mapato na umaarufu na kuvutia top players hivyo huwezi kubeza mtu kushiriki UCL.

Na nimeweka hoja hapa Man City imekua zaidi kuliko liverpool baada ya kuongeza mashabiki zaidi ya Million 70 ndani ya miaka 5 iliopita sasa bila hizo UCL wangepata hyo coverage??

Anyway Man City wana makombe 10 naomba unitajie ya Liverpool.
 
Kwamba unaenda kuokota data hapa unakuja simama nazo kama hoja ya kupinga jambo ?? forum ambayo ni user generated kama Jamii forum , unakuta mtu kama "Zero IQ" kashusha mambo yake unayabeba unaenda fanya reference ...


Labda nikusaidie namba ya kujua idadi ya mashabiki na ukuaji wa Brand ya club

1. Mauzo ya Jersey na mapato yatokanayo na mauzo hayo
2. idadi ya watazamaji wa mechi zinazo husu club husika
3. Social media interactions
4. Wachezaji wanao ongoza kuuza jersey zao .. top ten club inaingiza wangapi ?


ndio maana leo utashangaa Neymar anazidiwa na Nemanja matic , ni kwasababu ya fanbase ya clubView attachment 1403725

Sent using Jamii Forums mobile app
Data nimetoa kwa gazeti kabisa unless nalo halipo credible kwako!!
Screenshot_2020-03-30-09-57-47.png

Mauzo ya jersey ni kipimo lakini washabiki wengi tu wa Man Utd wamenunua jersey za Ronaldo akiwa madrid. Hata washabiki wa Santos hununua jezi za Neymar akiwa PSG so lazima uwe makini kwenye kuchambua fan base kwa mauzo ya jezi.

Ndio maana kufuta controversy hizi washabiki official ni wale ambao wamesajiliwa na club husika mfano fans club za nchini kwao, season ticket holders, au subscribers wa membership sasa katika hayo makundi nimetaja ndio Man City imewazidi Liverpool kwa ukuaji.

Kwahiyo indeed washabiki huwa wanahama na kuongezeka ndio maana unaona hapo 20% ya washabiki wa Man Utd wamesepa.
 
Labda nikuulize kitu mkuu, ni kitu gani kilikufanya uhamie Atletico?

Na ulihamia mwaka gani?

Je, kama El Cholo akiondoka, unajiona ukiwa mshabiki wa team gani baadae?
Atletico nmeipenda sababu ya fighting spirit tokea kipindi cha kocha Javier Aguirre, average players ila wanajituma sana hyo tokea 2008.

Ila nimehamia miguu yote miwili hapo 2012/13 season maana kujituma kwao ni opposite kabisa na Arsenal waliokua hawajitumi vile.

El cholo akiondoka ntabaki Atletico maana nimeipenda tokea kipindi cha kina Simao,maxi Rodriguez, Aguero na Forlan. Otherwise siioni Atletico bila ya El Cholo ndio DNA ya timu na hata aina ya uchezaji ni ya El Cholo yuleyule wa 1990s.
 
Atletico nmeipenda sababu ya fighting spirit tokea kipindi cha kocha Javier Aguirre, average players ila wanajituma sana hyo tokea 2008.

Ila nimehamia miguu yote miwili hapo 2012/13 season maana kujituma kwao ni opposite kabisa na Arsenal waliokua hawajitumi vile.

El cholo akiondoka ntabaki Atletico maana nimeipenda tokea kipindi cha kina Simao,maxi Rodriguez, Aguero na Forlan. Otherwise siioni Atletico bila ya El Cholo ndio DNA ya timu na hata aina ya uchezaji ni ya El Cholo yuleyule wa 1990s.

Washabiki tuko aina tofauti tofauti mkuu, ninaweza kukuelewa.

Kuna wale ambao hatupendi presha, tunaamua kuchagua timu ambazo hazina presha pia, kwamba tufungwe ni kawaida, tukishinda ni faida (taking conservative approach). Na hii ndiyo style wewe unayoitumia.

Arsenal na Atletico wote ni wa aina ambayo kwenye Mission yao si kuwa timu bora kwenye ligi zao wala Ulaya, isipokuwa ni ushiriki madhubuti, more of a pretender not contender.

Man Utd, Liverpool, Real Madrid, Barca, Bayern na Juventus ni baadhi ya team ambazo kuwa namba mbili ni failure na watafanya kila wanachoweza kutafuta suluhu ili kurudi juu.
 
Mkuu Liverpool imevuka round of 16 mara 3 pekee last decade hapo acha misimu 6 hamjashiriki UCL kabisa yaani kabisa sasa mpka hapo ushiriki wenu ni mdogo sana kuliko City.

Then last decade Man City ana makombe 10 then wewe mna mangapi mkuu?? Na usintaji club world cup na super cup ambavyo ni bonanza tu. Mtajikuta mna kombe moja pekee.

Na nimeshakueleza timu kufika UCL tu ni achievement kwa timu yeyote ile maana kuna faida nyingi sana hasa mapato na umaarufu na kuvutia top players hivyo huwezi kubeza mtu kushiriki UCL.

Na nimeweka hoja hapa Man City imekua zaidi kuliko liverpool baada ya kuongeza mashabiki zaidi ya Million 70 ndani ya miaka 5 iliopita sasa bila hizo UCL wangepata hyo coverage??

Anyway Man City wana makombe 10 naomba unitajie ya Liverpool.
Nishasema huko juu mimi ni Shabiki wa Manchester United, niko hapa kukutoa ujinga tu na sii vinginevyo

Umeanza uefa mara unarukia ligi mara unarukia idadi sijui ya nini .. huna msimamo kwenye mada yeyote ... huna uwezo wa kujenga wala kujadili hoja yeyote, unarukaruka kama watoto wadogo



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nishasema huko juu mimi ni Shabiki wa Manchester United, niko hapa kukutoa ujinga tu na sii vinginevyo

Umeanza uefa mara unarukia ligi mara unarukia idadi sijui ya nini .. huna msimamo kwenye mada yeyote ... huna uwezo wa kujenga wala kujadili hoja yeyote, unarukaruka kama watoto wadogo



Sent using Jamii Forums mobile app
Kumbe mshabiki wa ile timu ilojifia? 🤣 🤣 🤣 ndio maana basi hata data umeshindwa kuja nazo.

Wewe umedai washabiki hawahami nimeleta data kuwa Man U mmeondokewa na 20% umeshindwa kujibu!!

Umedai Fan base ni mauzo ya jezi nmekuelewesha kuwa jezi zinanunuliwa na yeyote kulingana na upendo kwa mchezaji husika hata kama anasupport timu nyingine.....umeshindwa tetea hoja?

Umedai Liverpool is better tha city Kitakwimu nimekwambia City ina makombe major 10 huku liverpool in moja pekee na mabonanza mawili!! Umeshindwa tetea

Nimekueleza Man City imeongeza mashabiki zaidi ya Million 70 ambayo ndio kubwa kuliko timu yeyote kufikia 2018 then umeshindwa kanusha zaidi ya kujifichia kwenye quora ilihali data zipo major tabloids zote mpaka sky sports!!

Siku nyingine kama huwezi tetea hoja zako usilete ujuaji wakati hufahamu lolote, yaani ww ndio unitoe ujinga wakati hata hujui Man Utd imehamwa na mashabiki 20% umekalia ooh washabiki hawahami??

Reasoning yako inaendana na performance ya timu yako!!!
 
Mkuu Liverpool imevuka round of 16 mara 3 pekee last decade hapo acha misimu 6 hamjashiriki UCL kabisa yaani kabisa sasa mpka hapo ushiriki wenu ni mdogo sana kuliko City.

Then last decade Man City ana makombe 10 then wewe mna mangapi mkuu?? Na usintaji club world cup na super cup ambavyo ni bonanza tu. Mtajikuta mna kombe moja pekee.

Na nimeshakueleza timu kufika UCL tu ni achievement kwa timu yeyote ile maana kuna faida nyingi sana hasa mapato na umaarufu na kuvutia top players hivyo huwezi kubeza mtu kushiriki UCL.

Na nimeweka hoja hapa Man City imekua zaidi kuliko liverpool baada ya kuongeza mashabiki zaidi ya Million 70 ndani ya miaka 5 iliopita sasa bila hizo UCL wangepata hyo coverage??

Anyway Man City wana makombe 10 naomba unitajie ya Liverpool.
Hahahahahahahahah Mkuu kwa nini kila point yako unayosema imebase NDANI YA MIAKA 10 iliyopita tujadili vitu in General, Mbona kuanzia mwaka 2008 kurudi nyuma mbona hugusii kwa sababu walikua hawana Archive .
 
Mkuu Liverpool imevuka round of 16 mara 3 pekee last decade hapo acha misimu 6 hamjashiriki UCL kabisa yaani kabisa sasa mpka hapo ushiriki wenu ni mdogo sana kuliko City.

Then last decade Man City ana makombe 10 then wewe mna mangapi mkuu?? Na usintaji club world cup na super cup ambavyo ni bonanza tu. Mtajikuta mna kombe moja pekee.

Na nimeshakueleza timu kufika UCL tu ni achievement kwa timu yeyote ile maana kuna faida nyingi sana hasa mapato na umaarufu na kuvutia top players hivyo huwezi kubeza mtu kushiriki UCL.

Na nimeweka hoja hapa Man City imekua zaidi kuliko liverpool baada ya kuongeza mashabiki zaidi ya Million 70 ndani ya miaka 5 iliopita sasa bila hizo UCL wangepata hyo coverage??

Anyway Man City wana makombe 10 naomba unitajie ya Liverpool.
Mkuu Liverpool imevuka round of 16 mara 3 pekee last decade hapo acha misimu 6 hamjashiriki UCL kabisa yaani kabisa sasa mpka hapo ushiriki wenu ni mdogo sana kuliko City.

Then last decade Man City ana makombe 10 then wewe mna mangapi mkuu?? Na usintaji club world cup na super cup ambavyo ni bonanza tu. Mtajikuta mna kombe moja pekee.

Na nimeshakueleza timu kufika UCL tu ni achievement kwa timu yeyote ile maana kuna faida nyingi sana hasa mapato na umaarufu na kuvutia top players hivyo huwezi kubeza mtu kushiriki UCL.

Na nimeweka hoja hapa Man City imekua zaidi kuliko liverpool baada ya kuongeza mashabiki zaidi ya Million 70 ndani ya miaka 5 iliopita sasa bila hizo UCL wangepata hyo coverage??

Anyway Man City wana makombe 10 naomba unitajie ya Liverpool.
2001 Uefa cup
2001,2005 Uefa super cup
Fa cup 2001,2006
League cup 2001,2003
Champions league 2005 hii miaka Manchester city hakuwepo au ilikuwa haijaanzishwa Kila hoja ndani ya miaka 10 hiyo miaka mengine zaidi walikuwa wanacheza kombolela.
Since 2001 - 2006 Liverpool tulishinda trophy 8 Manchester city walishinda trophy ngapi
 
Halafu huyu kilaza hajui malengo ya wachezaji/mashabiki ni tofauti na wamiliki timu.
Wachezaji na mashabiki malengo yao ni MAFANIKIO AKA MAKOMBE
Wamiliki wa timu kwao ni PESA.
Sasa nakushangaa wewe shabiki unayeshangili eti ATM iko CL kila msimu bila ya Kombe ukafananishe na Liverpool.
Ndo maana sisi tutafukuza kocha tukiona hatupi mashabiki tunachotaka.
ATM ni masikini ndo maana wameridhika na simeona aweke basi ili tu wawe CL kila msimu. Ni kama Alivyowaaminisha mashabiki wa arsenal alipowaambia kuwa " eti kushiriki CL pia ni kombe" BUT WALIPOAMKA USINGIZINI WANAONA CHELSEA MAJIRANI WANA NDOO YA CL WAKAMFUKUZA....EMERY WAKAMFUKUZA COz wanataka KOMBE.
SUAREZ HAKWENDA BARCA KUSHIRIKI CL BALI KUCHUKUA
HENRY ALISEMA NAENDA BARCA KUCHUKUA CL SABABU ARSENAL SIWEZI KUPATA MAANA WAO CL KUASHIRIKI NDO MAFANIKIO
NA ALIPOLIPATA CHOZI LIKAMTOKA KWA FURAHA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
LONDON ,ENGLAND.
MSHAMBULIAJI wa Chelsea, Tammy Abraham amepewa jezi namba 9 ya klabu hiyo akiirithi kutoka kwa mshambuliaji wa kimataifa wa Argentina, Gonzalo Higuain.
Kwa sasa jezi hiyo inasemekana ni kama vile ina mikosi. Washambuliaji wengi wanaovaa jezi hiyo pale Chelsea katika miaka ya karibuni wamefeli. Alvaro Morata, Fernando Torres, Radamel Falcao, ni miongoni mwa mastaa ambao wamefeli katika jezi hiyo.
Kuna laana au mikosi mingi ambayo imekuwa ikihusishwa na soka.

1.AARON RAMSEY NA VIFO VYA VIGOGO.
Kiungo wa zamani wa Arsenal ambaye katika dirisha hili ametua katika Klabu ya Juventus kwa uhamisho wa bure. Ramsey alijulikana na mkosi wake wa kufunga mabao ambayo yaliambatana na vifo vya watu wengi maarufu. Mwanamuziki maarufu wa kike duniani, Whitney Houston alifariki mwaka 2012 saa chache baada ya Ramsey kuisaidia Arsenal kuichapa Southampton. Lakini pia Mwigizaji maarufu, Alan Rickman alifariki siku moja baada ya staa huyu wa Wales kuiwezesha Arsenal kuichapa Liverpool. Miongoni mwa watu wengine maarufu ambao walifariki baada ya Ramsey kufunga mabao yake ni pamoja na Steve Jobs, Osama Bin Laden, Muammar Gaddafi, Rubin Carter, Paul Walker, Robin Williams na David Bowie.

2.JEZI NAMBA 9 YA CHELSEA

Abraham aliyekulia katika kikosi cha vijana cha Chelsea ana kazi ngumu ya kuondoa mkosi katika jezi namba 9 ya Chelsea. Sio jezi nzuri kuikimbilia ukizingatia washambuliaji mahiri wanakwenda pale na sifa lukuki lakini wanashindwa kuonyesha makali yao wakivaa jezi hii. Gonzalo Higuain licha ya makali yake lakini alifunga mabao matano tu na jezi hii kuanzia Januari mwaka huu.
Kabla ya hapo mastaa wakubwa kama Alvaro Morata, Fernando Torres, Radamel Falcao na Mateja Kezman wote walivaa jezi hii lakini bila ya mafanikio yoyote. Abraham amezungumzia kuhusu mkosi huo kwa majigambo makubwa huku akisema: “Nimesikia upuuzi kuhusu jezi namba 9. Niko hapa kucheza soka langu na kujaribu.

3.MKOSI WA KUPIGA PICHA NA DRAKE.
Mamilioni ya mashabiki wa muziki duniani kote wanatamani kupiga picha na rapa maarufu wa Canada, Drake.
Hata hivyo, kwa sasa watu wameanza kujifikiria mara mbili kupiga picha na Drake. Imeibuka tabia ambapo kila unapopiga picha na rapa huyu unaelekea kushindwa katika mchezo unaoshiriki. Mastaa wengi wa soka wamejikuta wakichemsha katika hili na mmojawapo ni kiungo wa Manchester United ambaye alipiga picha na Pogba saa chache kabla ya Manchester United haijachapwa na Wolves 2-1 Kombe la FA.
Staa wa Arsenal, Pierre Emerick-Aubameyang ni mhanga mwingine ambaye alipiga picha na Drake dakika chache kabla Arsenal haijachapwa na Everton. Bondia maarufu wa Uingereza, Anthony Joshua naye alifanya kosa hilo kwa kupiga picha na Drake na kudundwa na bondia kutoka Mexico, Andy Ruiz. Wakati akipiga picha hiyo Joshua alionekana kukejeli mkosi huo lakini alijuta baadaye.

4.MIZIMU YA WARUMI BIRMINGHAM.
Inadaiwa Uwanja wa Soka wa Klabu ya Birmingham City ulijengwa katika ardhi ya mizimu ya Kirumi. Inadaiwa Klabu ya Birmingham imekuwa na mikosi mingi. Msimu wake wa kwanza katika Ligi Kuu uliiona timu hiyo ikishuka daraja. Katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia jukwaa lao kubwa liliungua moto. Winga wa zamani wa Birmingham, Barry Fry alijaribu kuukomboa uwanja huo kutoka katika mikosi kwa kutumia fomula yake binafsi. “Tulimuita mtu mmoja aje kuondoa mikosi katika uwanja huo na akatuambia kuwa njia pekee ya kuondoka mikosi katika uwanja huo ilikuwa kukojoa kila pembe ya uwanja. Mimi sio mtu ninayeamini mambo hayo lakini baada ya miezi mitatu nilikuwa tayari kujaribu kitu chochote kile kwahiyo nilikwenda na kukojoa katika kona zote za vibendera. Ilinichukua muda. Haikuwa rahisi.”

5.PAKA ALIYEUAWA KLABUNI RACING.
Klabu ya Racing ya Argentina ilikuwa moja kati ya klabu zenye mafanikio katika Bara la Amerika Kusini miaka ya 1960. Lakini baada ya kutwaa ubingwa wa Mabara wa Amerika Kusini na Kombe la Intercontinental mwaka 1967 kila kitu kilibadilika. Inadaiwa hili lilitokana na kundi la mashabiki wa timu pinzani ya Independiente kuvunja geti na kuingia Uwanja wa Racing na kufukia paka saba waliouwawa.
Kwa muongo mmoja uliofuata miaka ya 1970 klabu hiyo haikuchukua taji lolote. Mbaya zaidi Racing ikashuka daraja mwaka 1983. Kwa hiyo ili kukomesha laana au mkosi huo, Racing iliamua kufukua na kuwaondoa paka hao marehemu lakini waliweza kuondoa mizoga sita tu.
Mwaka 1998 Racing ilitangazwa kufilisika na mwaka mmoja baadaye ilimuita mchungaji kwa ajili ya kufanya maombi. Iliichukua Racing mpaka mwaka2001 kurudi katika hali ya kawaida na mwaka 2002 ilichukua ubingwa wa Argentina kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1966.

6.JEZI NAMBA 7 KLABUNI MANCHESTER UNITED.
Sio tu Chelsea ambao wanaonekana kuwa katika mkosi na jezi namba 9. Pale Manchester United jezi namba 7 imeanza kuonekana kuwa tatizo baada ya kutamba kwa muda mrefu klabuni hapo.
Wakongwe kama Bryan Robson, David Beckham, Cristiano Ronaldo na George Best waliivaaa jezi hii kwa mafanikio. Lakini tangu Cristiano Ronaldo aondoke katika dirisha kubwa la majira ya joto mwaka 2009 jezi hiyo ni kama vile imeachiwa mkosi na laana.
Mastaa wengi waliovaa jezi hiyo wameishia kutukanwa na mashabiki. Wanakuja Old Trafford wakiwa mastaa wakubwa lakini wanachemsha vibaya klabuni hapo. Baadhi yao ni Michael Owen, Alexis Sanchez, Memphis Depay na Angel Di Maria. Wakati fulani staa wa kimataifa wa Ecuador, Antonio Valencia alikacha.

7.MZIMU WA BAYER LEVERKUSEN.
Katika miaka ya 1990 na miaka ya 2000, Klabu ya Bayer Leverkusen ilijulikana kama ‘WANAUME WANAOKARIBIA’ kutokana na tabia yao ya kukaribia makombe lakini wanaambulia patupu.
Wengine waliwatania kwa jina la the Neverkusen Men. Miaka ya 1997, 1999, 2000 na 2002, Bayer Leverkusen ilimaliza katika nafasi ya pili Bundesliga. Mwaka 2000 ilihitaji pointi moja tu kutwaa ubingwa wa Ujerumani lakini ikaambulia patupu.
Miaka miwili baadaye ilipoteza uongozi wa pointi tano ambazo zilikuwa zinawapeleka katika ubingwa lakini ikapoteza mechi mbili kati ya tatu za mwisho na hivyo kuiruhusu Borussia Dortmund kutwaa ubingwa. Huo ndio mwaka ambao staa wa kimataifa wa Ufaransa, Zinedine Zidane alifunga bao la ushindi nchini Scotland katika pambano la Ligi ya Mabingwa wa Ulaya. Ukiwa Leverkusen wenyewe wanaamini kwamba hii sio bahati mbaya ya kawaida. Wanaamini kuna laana ambayo inawatafuna.
Hawaijui.

8.MZIMU WA GUTTMANN NA BENFICA.
Hii ni moja kati ya laana maarufu katika soka. Kocha maarufu wa zamani wa Hungary, Bela Guttmann aliondoka Porto mwaka 1959 na kujiunga na wapinzani wao maarufu Benfica. Mara baada ya kujiunga na klabu hiyo ilitwaa mataji mawili mfululizo. Baada ya kutamba katika soka la ndani la Ureno, Guttmann pia alikomesha utawala wa Real Madrid kwa kutwaa ubingwa wa Ulaya. Mara baada ya mafanikio hayo aliomba klabu hiyo imuongezee mshahara kutokana na pato la klabu hiyo kukua lakini katika namna ya kushangaza klabu hiyo ilimwambia HAPANA.
Hapo ndipo Guttmann alipoweka laana kubwa kwa klabu hiyo ya Ureno huku akisema:
“Sio kwa ndani ya miaka hii mia, kuanzia sasa Benfica kamwe haitatwaa ubingwa wa Ulaya.”
Ni kweli. Ni nusu karne sasa Benfica bado inasubiri ubingwa wa Ulaya. Ilipoteza fainali za Ulaya miaka ya 1963, 1965 na 1968 baada ya Guttmann kuondoka klabuni.

Chanzo:Gazeti laMwanaspoti
 
Washabiki tuko aina tofauti tofauti mkuu, ninaweza kukuelewa.

Kuna wale ambao hatupendi presha, tunaamua kuchagua timu ambazo hazina presha pia, kwamba tufungwe ni kawaida, tukishinda ni faida (taking conservative approach). Na hii ndiyo style wewe unayoitumia.

Arsenal na Atletico wote ni wa aina ambayo kwenye Mission yao si kuwa timu bora kwenye ligi zao wala Ulaya, isipokuwa ni ushiriki madhubuti, more of a pretender not contender.

Man Utd, Liverpool, Real Madrid, Barca, Bayern na Juventus ni baadhi ya team ambazo kuwa namba mbili ni failure na watafanya kila wanachoweza kutafuta suluhu ili kurudi juu.
Haaahaaa mkuu nimechekaa sana!!
Kwamba Atletico wana expect kufungwa.... Imetumia zaidi ya €300M dirisha kubwa kureplace mastar ili wawe second fiddle??

Nachoipendea Atletico ni hard work kuliko kubeba trophy (Ingawa tuna makombe mengi kuliko liver last decade) hata maisha yangu ya kawaida naitumia hii cholo mentality kufanikisha mambo mengi mno kwamba hata kama sina uzoefu mkubwa wa masuala fulani ila kujituma kutanisaidia.

By the way wenger era amekuwa na mafanikio makubwa kuliko Liverpool ya wakati wake so huwezi sema Arsenal ni timu ndogo wakati Liverpool haijawahi beba trophies nyingi kuliko Arsenal kipindi chote cha wenger ambacho ndio nlikua nasupport hii klabu.

Liverpool is an average british team sijui kwanini unaikuza sana hadi kuiweka level moja na Juventus and Bayern!! Huwezi kuwa serious.
 
Halafu huyu kilaza hajui malengo ya wachezaji/mashabiki ni tofauti na wamiliki timu.
Wachezaji na mashabiki malengo yao ni MAFANIKIO AKA MAKOMBE
Wamiliki wa timu kwao ni PESA.
Sasa nakushangaa wewe shabiki unayeshangili eti ATM iko CL kila msimu bila ya Kombe ukafananishe na Liverpool.
Ndo maana sisi tutafukuza kocha tukiona hatupi mashabiki tunachotaka.
ATM ni masikini ndo maana wameridhika na simeona aweke basi ili tu wawe CL kila msimu. Ni kama Alivyowaaminisha mashabiki wa arsenal alipowaambia kuwa " eti kushiriki CL pia ni kombe" BUT WALIPOAMKA USINGIZINI WANAONA CHELSEA MAJIRANI WANA NDOO YA CL WAKAMFUKUZA....EMERY WAKAMFUKUZA COz wanataka KOMBE.
SUAREZ HAKWENDA BARCA KUSHIRIKI CL BALI KUCHUKUA
HENRY ALISEMA NAENDA BARCA KUCHUKUA CL SABABU ARSENAL SIWEZI KUPATA MAANA WAO CL KUASHIRIKI NDO MAFANIKIO
NA ALIPOLIPATA CHOZI LIKAMTOKA KWA FURAHA.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu jifunze kwanza kuandika naona kipigo cha Atletico bado kimekuchanganya akili!!

Ni hivi Atletico sio level ya Liverpool ndio maana tuna makombe mengi kuliko nyie recently so mafanikio ya msimu mmoja kma leicester yasiwafanye muone nyie ni timu kubwa. Bado sana, yaani huna hata EPL mwaka wa 30 sasa eti Liverpool ni timu kubwa?? Mmeshiriki UCL mara 3 ndani ya miaka 10 timu kubwa??

Kwa akili hizi ndio maana katimu kenu kanapigwa ovyo cku mmejiweka kwenye class ambayo hampo. Eti unbeaten 49 mkadhani Arsenal ya enzi zile ni kama hiki kitimu cha overrated british kids Robertson,TAA na henderson??

Mnafurahisha sana, anyway naombea ligi ifutwe kabisa ili muendelee kuwa Looserfools for 30 more years!!
 
Hahahahahahahahah Mkuu kwa nini kila point yako unayosema imebase NDANI YA MIAKA 10 iliyopita tujadili vitu in General, Mbona kuanzia mwaka 2008 kurudi nyuma mbona hugusii kwa sababu walikua hawana Archive .
Kwa sababu ndio decade ambapo timu ilipaa anyway hata tukimix na kuanza 21st century bado wanawazidi makombe kwa mbali sana.

Haya liverpool tukitaka kuongelea mafanikio yenu inatupasa tujadili miaka ya 70 na 80 ambapo ndio mlikuwa timu haswaa kabla hamjaporomoka na kuwa mediocre kwa miaka 30 sasa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom