Don Clericuzio
JF-Expert Member
- Dec 8, 2017
- 16,930
- 40,586
Mkuu hujawahi sikia mchezaji anagoma kuhamia timu sababu haipo UCL?
Kushinda major trophies ni muhimu ila sio sababu pekee ya kushiriki.
Publicity, mauzo ya jezi, Tv rights, fan base, kuvutia world class players etc na ndio maana Valencia msimu uliopita waliambiwa wasijiandae na fainali ya FA Cup yao ili washinde mechi zilizobaki za ligi waibuke nafasi ya 4.
Kwahiyo unaweza ona ushiriki tu UCL ina faida sio za kikombe tu bali nyingi sana hivyo usibeze Man city kushiriki mara nyingi zaidi kuliko liverpool
Mimi naomba nieleze kidogo kitu nilichojifunza kutoka kwako.
Ulikuwa mshabiki wa Arsenal, then ukahamia Atletico; from one average team to another average team. Arsenal hajawahi kuchukua UEFA, na success yake kubwa ilikuwa ni kushiriki UEFA, same same kwa Atletico.
Hivyo style yako ya ushabiki ni ile ya kujificha kwenye timu ambazo KPI zake ni kushiriki ligi na si kuchukua ubingwa.
Pep alikuwa Bayern, kachukua domestic misimu yote, lakini ilifikia sehemu akaonekana si chochote kwa sababu hawezi kuwapa UEFA.
Juzi pia Pep kafanya interview akiwa City, ilikuwa kama joke lakini ilikuwa na maana. Alisema kama asipochukua UEFA atafukuzwa City.
Liverpool hajawahi kuwa na malengo ya kushiriki UEFA, malengo yake ni kuchukua UEFA.
Liverpool hajawahi kuwa na malengo ya kushiriki Premier League, malengo ni kuchukua. Ndiyo maana ikifika muda ikaonekana kwamba kocha hawezi kutupa ubingwa tunaachana naye.
Atletico kushiriki UEFA ni achievement kubwa, Arsenal pia. Liverpool achievement yake ni kuchukua UEFA.