Kwa mawazo yangu nadhani Sababu kuu ya Liverpool kufungwa sasa ni UCHOVU & MENTALITY ya wachazaji.
1. UCHOVU:- Wachezaji wa Liverpool wametumia nguvu kubwa sana kwa kipindi kirefu kushinda mechi. Mfano kule mbele magoli yanayofungwa ni ya kutumia nguvu sana.
Mara Salah kakokota, speed kali, kupambana na mabeki, huku kavutwa, ukija kwa mane magoli anayofunga ni zaidi ya vita anapambana nguvu nyingi mpaka na maserekasi aisee.
Achilia mbali nguvu wanayotumia mabeki kukaba na kupanda kushambulia kwa kasi na kurudi fasta kukaba.
Kwa muda uliobaki mchezaji mzuri utamuona mbaya kwa sababu ya UCHOVU, wengi hawatacheza katika kiwango bora.
2. MENTALITY:- Hili liko wazi wachezaji wanafahamu Liverpool tayari ni bingwa EPL msimu huu. Wanasubiria tuu muda ufike wabebe ndoo. Hawaoni haja saaana kuendelea kutumia energy kuuuuuubwa kumalizia mechi zilizobaki.
Ila Liverpol angekuwa anafukuzwa hapo nyuma kwa tofauti ya point chache, weee wachezaji wasingebweteka jana Watford angekula marungu ya kutosha.
Nadhani mashabiki muendelee kuwashangilia kuelekea mwisho mzuri wa kusisimua kubeba kombe. Sioni haja ya kuwasema, kuwakosoa zaidi ya kuwapongeza tuu kwa kazi waliofanya.
Aisee wanaume wametoka mbali kufukuzia huu ubingwa. Wanastahili pongezi kila siku.
Halafu wewe king Ngwaba dawa yako inachemka msimu ujao, umetusema sana kule SHUBAAAMIT zako.
Sent using Cash Money Wings