nimebahatika kuangalia mechi nane za liverpool msimu huu na mechi nne kati ya hizo ni pale walipokutana na timu zinazotoka jiji la manchester.
niwe mkweli mimi ni mshabiki wa manchester united na katika maisha yangu sijawahi kuipenda liverpool lakini napaswa niwapongeze kutokana na jitihada zao walizozionyesha msimu huu na kututoa kimaso maso timu za uingereza kama tunavyofahamu kwa miaka 5 hakuna timu ya uingereza iliofika fainal kwenye michuano ya ligi ya mabingwa.
ujio wa jurgen klopp kama mwalimu wa liverpool umeleta mageuzi makubwa sana kwa klabu hiyo hususan aina ya soka wanalocheza la kumiliki mpira na kutokumpa adui nafasi ya kukaa na mpira kwa muda mrefu lakini udhaifu mkubwa alionao jurgen klopp ni kwamba inaonekana bado anaamini uwezo wa kifedha wa liverpool ni sawa sawa na uwezo wa kifedha wa timu yake ya zamani ya dortmund kwenye soko la usajili.
alipokuwa dortmund alijenga timu nzuri sana lakini tatizo ni kwamba dortmund walikosa back up ya wachezaji wenye uwezo wa kuleta mabadiliko pindi wanapopata nafasi ya kikosi cha kwanza, ukivuta kumbukumbu mpaka msimu wa 2012/2013 ambao dortmund walifika final na hata msimu uliofuata utagundua ya kwamba kilichowarudisha nyuma dortmund ni kutokuwa na wachezaji wa kutosha ambao wana ubora ukilinganisha na wapinzani wao kama bayern munich.
kwenye wachezaji 25 borussia walitegemea zaidi miujiza ya wachezaji 11 ambao ni lewandowski, marco reus, gundogan, gotze, subotic, hummels, weidenfeller, bender, kehl, blaszczykowski, schieber na groskreutz.
inamaana wachezaji 12 waliobakia walikuwa na viwango vya kawaida sana jambo ambalo lilipelekea dortmund kukosa mipango B pindi wanapokutana na timu zenye wachezaji wa viwango vya juu.
nampenda klopp kwa tabia yake ya kutokuacha kumpa nafsi mchezaji mwenye uwezo haijalishi ana umri mdogo, nimekua nikiwaonea wivu liverpool pindi ninapowaona vijana wawili alexander arnold na robertson wanapopata nafasi kwenye kikosi cha kwanza na wakicheza soka la kiwango cha juu sana kuliko hata walinzi wa pembeni wa timu ninayoishabikia, nawashauri liverpool wawape vijana hawa maslahi mazuri ili waondokane na tamaa ya kutaka kuondoka kwenye timu hiyo na hatimae yakatokezea kama ya rahem sterling, ashley cole na kyle walker. kiukweli huyu andrew robertson amenishangaza sana aina yake ya soka analocheza na kunifanya nitafakari hivi huyu beki wetu ashley young anacheza mpira wa aina gani?
andrew robertson hakupaswa kuzaliwa kwenye visiwa vya uingereza.
nimeona andiko la
King Ngwaba akilalamika kuhusiana na liverpool kuwa na wachezaji wengi wenye viwango vya chini ukilinganisha na wapinzani wao real madrid, mimi nadhani ugonjwa wa kuwa na average player wengi kwenye kikosi si la liverpool peke yake kwa sababu hata manchester united, chelsea na arsenal pia ugonjwa huu upo na ndio maana msimu huu manchester city akabeba ubingwa kwa tofauti ya pointi 20 dhidi ya wapinzani wake.
liverpool wanahitaji wachezaji watano wenye kuendana na soka la kasi na kumiliki mpira ndipo wataweza kusimama na timu kama real madrid.
- mlinzi wa kati ambaye atasaidiana van drjik ambaye ndiye usajili bora wa mwaka huu.
- kiungo wa pembeni ambaye ataongeza ushindani dhidi ya sadio mane, jaribu kufikiria timu ya real madrid wana uwezo wa kumuanzisha bale, isco au asensio na wakapata matokeo mazuri.
- mshambuliaji mwenye uwezo wa kufunga magoli 20 kwa msimu nadhani edin dzeko bado ana uwezo wa kucheza liverpool.
- kiungo mshambuliaji ambaye hajazaliwa uingereza, nakusudia asicheze mpira wa kiingereza ambao ni wa kutokupenda kumiliki mpira.
- nafasi ya goal keeper pia iangaliwe kwa umakini.
pia klabu inapaswa ipunguze wachezaji ambao ni liability ili kuwapa nafasi young player kutoka reserves team.
ni imani yangu ya kwamba liverpool wamepoteza pambano lakini hawajapoteza vita.
kama kweli tunataka kupambana na real madrid basi makocha wa timu zetu wawe na uono wa kusajili wachezaji mahodari na kuacha kusikiliza porojo za vyombo vya habari vya uingereza za kuwasifikia average player kutoka taifa lao.
aigoooooooo nimeota manchester united tumemsajili andrew robertson
[HASHTAG]#ynwa[/HASHTAG]