View attachment 670332
Jurgen Klopp amekiri kuwa Philippe Coutinho aliweka bayana kwa kila mmoja, ikiwa ni pamoja na wachezaji wenzake kuwa anatamani kuondoka kujiunga na Barcelona, jambo ambalo isingewezekana kumbakisha Liverpool.
Uhamisho wa nyota huyo wa Kibrazili kwenda Camp Nou ulitangazwa Jumamosi, baada ya mchezaji huyo kukubali kusaini mkataba wa miaka mitano na nusu kufuatia malipo ya ada ya uhamisho ya €160 milioni na Barcelona wakiweka thamani yake kuwa €400 kwa klabu itakayomtaka.
Coutinho amekuwa shabaha ya miamba hao wa La Liga kwa muda mrefu lakini jaribio lao kumsajili liligonga mwamba mara kadhaa Julai na Agosti.
Jurgen Klopp hakufurahi kuona mchezaji huyo akiondok, ingawa hakuwa na namna ya kumzuia mchezaji huyo kwani alimweka wazi yeye na mmiliki wa klabu kadhalika na wachezaji wenzake kuwa anataka kuondoka.
Ni kwa kusita mno - sisi kama timu na klabu tunajiandaa kumuaga rafiki yetu mwema, mtu wa kipekee na mchezaji mahiri Philippe Coutinho," aliiambia tovuti rasmi ya Liverpool.
"Siyo siri kwamba Philippe alitaka kuondoka tangu Julai, mara ya kwanza nia ya Barcelona ilipofahamika.
"Philippe alinisisitizia mimi, wamiliki na hata wachezaji wenzake kuwa alitamani jambo hili litokee.
Licha ya kuwa tulifanikiwa kumbakisha mchezaji baada ya dirisha la uhamisho wa majira ya joto, tukiamini kuwa tungeweza kumshawishi kubaki na kuwa sehemu ya kile tunachotaka kufanya.
"Naweza kuwaambia mashabiki wa Liverpool kuwa, sisi kama klabu, tumefanya kila tulichoweza kumshawishi Philippe kubaki kama sehemu ya LFC, lakini yeye ndiye mwamuzi mkuu wa mustakabali wake - akaamua kwamba yeye na familia yake wanataka kwenda Barcelona.
"Ni ndoto yake na sasa nimeshawishika kuwa hakuna namna naweza kuibadili akili yake."
Coutinho alitua Merseyside mnamo 2013 na amecheza mechi 152 za Premier League, akiweka kimiani mabao 41, na Klopp amezisifia jitihada zake.
"Wachezaji watakuja na wachezaji wataondoka, huo ndio mpira, lakini kama klabu tupo thabiti na imara kuendelea na kazi yetu nzuri dimbani, hata kama tukimpoteza mchezaji muhimu.
"Hatujawahi kuwa katika nafasi nzuri kipindi cha hivi karibuni, kama klabu. Tutatumia idadi yetu na uthabiti wetu kukabiliana na hali kama hizi na bado tutasonga mbele.
"Nimekuwa hapa kwa muda mrefu kiasi cha kuifahamu vema historia ya Liverpool, wachezaji muhimu wameshaondoka - lakini klabu umesonga mbele. Huwezi kuhamisho moyo na roho ya Klabu ya Liverpool, ingawa natambua kwamba kuna klabu nyingi zinaitamani.
"Kwa hiyo tunapomuaga Philippe, tunaendelea kwenda mbele na kufanya maendeleo kwani tunapambana kutimiza lengo kuu la kuleta mataji Anfield."