Kuna vitu havina uhusiano na talent.Ubinafsi,uchoyo na superiority inayosababishwa nadhani na kaungereza.Hivi vitu haviisaidii timu hata kama mtu ana talent.Wengine tunapenda tim ipate mafanikio sio mtu mmoja tu ndo atafute 'u his highness' hata kwa kuinyima timu nafasi ya ushindi.
Unaona sturridge anapewa pasi ya mwisho na origi.Anafunga bao anashangilia bila hata credit kwa mtoa pasi.
Unaona origi yupo kwenye position ya kuscore lkn sturridge ana opt kufunga kwenye impossible angle.Timu inakuwa imekosa goli hapo!
Sasa hizi ni tabia mbaya ambazo hata mtu uwe mzuri vipi sisi hatutaki hayo mauzuri yako kama hauisaidii timu ishinde ipate points ipande kwenye msimamo.Kuna maana gani sasa we unataka kufunga wewe tu na unashangilia alafu mechi inaisha droo au mmefungwa...kwa kuwa we umefunga unajisikia fresh tu....si ujinga?Sasa ndo alivyo Sturridge huyu wa sasa.Angalia hata expression ya uso wake pale ambapo goli limefungwa namtu mwingine huku ye yupo....jamaa anatulostisha kwa sasa.
Hizi tabia hazisababishwi na ufiti wala huo uinjari pruni wake.Zipo pale hata aweje
Hakuna ST duniani ambaye siyo selfish, hakuna ST duniani ambaye atakuwa yupo katika eneo sahihi la kujaribu kufunga, then atoe pass kwa mwenzake ndani ya box labda aone hakuna uwezekano wa kufunga..
Kila mtu ana njia yake ya kushangilia goal, style ya Danny ya kushangilia imekuwa hivyo for ages, sioni tatizo HATUANGALII post-matches presser na huwa hatusomi tweets au instagram posts za wachezaji baada ya games ambapo huwa wanapeana complements za kutosha..siyo lazima amfate yule aliyempa assist, ingekuwa hivyo Kina Giroud wangekuwa wanamkimbilia Ozil kushangilia nae kwa kila goal..
Kama unataka mafanikio ya LFC, huwez ukawa unaquestion uwepo wa DS kwenye club, DS ni mmoja kati ya wachezaji walioifanya LFC icompete tena, tabia za mchezaji hazitakiwi kulinganishwa na anachojikifanya kwenye uwanja, Mtu kakumbana na majeruhi kibao lakin mnataka acheze tena kama mwanzo, kwa pace ileile na uimara ule ule, yule ni human siyo robot, Klopp anajua anachokifanya kwa Sturridge, ndo maana kampa role ya Ghost Striker kwa sasa, DS hatakiwi kukaba mipira kwa 100% na hatakiwi kucheza zaidi ya dk75..medical team na Klopp wanadeal na fitness ya DS, wanajaribu kumrudisha DS wa kabla ya injury, na haiwez kuwa ndani ya muda mfupi, kuna wachezaji kibao wamestahafu baada ya injuries za mara kwa mara, kuna wachezaji ambapo viwango vyao vilishuka sana baada ya kukumbwa na majeraha, tumeshuhudia kina Aurelio career zao zikiharibiwa na injuries, na sahiv mnataka mtu aliyekaa almost 2 seasons kwa ajili ya majeruhi ya mara kwa mara arudi uwanjani akiwa yule yule?? msimu wa 2014/15 alicheza games ngapi? na msimu kacheza games ngapi?..asa mtu kama huyo unafikiri atarudi na pace ileile?? DS ana tabia ya kujisikia, hiyo ndio tabia ya Skrtel na Emre can, hiyo tabia ndo wanayo wakina Ozil, Depay, etc..sasa sioni tabia zao zinaaffect vipi team?? DS ni mchezaji ambaye alipigania mpaka Ibe akapandishwa first team, DS ni mmoja kati ya wachezaji wa kwanza kabisa kumkaribisha Firmino LFC, DS ni mchezaji wa kwanza aliyeonesha furaha yake ya wazi kabisa kwa kina Jonathan wa Sunday Times kuhusu Ujio wa Klopp, ni DS pekee aliyeponda waziwazi uamuzi wa sterling kuondoka namna ile pale LFC, ukiachana na SG ambaye alikuja kuongea baadae kwenye media (tena hakuponda), nakumbuka kipindi kile ile game ya beskitas ambapo Balotelli alimpokonya kwa nguvu mpira captainhendo ili apige penalty, DS shouted at him palepale kwa kumkosea heshima captain wetu mpendwa..leo hii mnamgeuka jamaa kisa tu anastruggle kuhusu fitness..
Majigambo wanayo kina Ibra wa PSG, yule anamponda mpaka mwenzie cavani kwenye medias, yule anasema PSG ilizaliwa baada ya waarabu kutake over, huko ndio kujisikia, siyo kwa sturridge kutokushangilia goal na aliyempa assist, vipi kuhusu skrtel ambaye kuna siku anaweza aamke aende mazoezini na asiongee na wenzake mpaka mazoezi yanaisha?
kuna ST selfish akiwa kwenye box kama Aguero pale England??