Faana
JF-Expert Member
- Dec 12, 2011
- 31,876
- 33,308
Ipo siku huyu angemuua RPC,Jeshi la Polisi mkoani Lindi, limemfuta kazi askari No.H.2324 PC Joseph kwa kosa la kumpiga risasi askari mwenzake No J.1752 PC Onesmo Joseph wakiwa lindo katika Benki ya CRDB Tawi la Ruangwa kilichosababisha kifo chake akiwa njiani kupelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Kauli hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Lindi ACP Mtatiro Kitinkwi wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisi kwake
Askari wa jeshi la polisi aliyetambulika kwa jina la PC Joseph amemuua askari mwenzake Onesmo Joseph wakiwa kwenye kazi ya kulinda tawi la benki ya CRDB wilayani Ruangwa mkoani Lindi.
Kamanda wa polisi mkoani Lindi amesema askari hao walikuwa wakigombania pikipiki na tayari PC Joseph amefutwa kazi na atafikishwa mahakamni muda wowote kuanzia sasa.