Lazima tuwekane sawa kuhusu UKIMWI

Kama watu wanapima ukimwi na majibu wanaweka kwapani haileti maana yoyote bora wasipime na wasitangaze kama wamepima ningekuwa kiongozi ningeweka board maalumu unapima pale majibu unaona katika board na waandishi wa habari wanachukuwa kalamu zao na kuandika kisha haya majbu tuna publish katika magazeti na tovuti zetu maalumu kuweka watu hawa wazi

Sio kwamba tunawanyanyapaa bali ni kutaka kuwa wazi zaidi kuionyesha jamii ugonjwa huu ulivyosambaa na unavyoendelea kusambaa kwa kasi na nguvu mpya
 
kwani bado huyo kawawa hajafa tu maana mkewe alishakufa zamani yeye yuko sasa yeye keshapima
 
Shy na Tonga We are better than this!!!

Inashangaza pale tunapoaanza kuwaombea kufa wazee wetu ambao walijitahidi kuitumikia nchi yetu kwa nguvu zao, akili zao na maarifa yao yote.

No matter how poor or underdeveloped we are wazee wetu Kina Kawawa na Nyerere wanahitaji heshima ya kipekee.

Kutangaza matokea ya ukimwi au ugonjwa wowote ule ni hiari ya mtu binafsi na ina 'constitute' Patient and Doctor confidentiality ethics and legal requirements.

Ndio maana daktari hawezi kudisclose taarifa za mgonjwa, na specifically ktk 'ukimwi kuna ethics na 'law' ambayo ni more strict kwa hiyo ni hiari ya mtu lakini angalau wale waliopima wanajua status yao na wataweza kuwakinga wenzao, na wameonyesha mwanzo mwema...

Nenda nawe kapime kama bado na wahamasishe wengine.

Aluta Continua...
 
Shy,
Kwa taifa lengo la kupima sio cheti cha kuonyesha huna ukimwi, bali ili wale ambao wana ukimwi basi wapate ushauri na matibabu mapema na kuepusha kueneza huo ugonjwa kwa wengine.

Kwa wale waliopima na kukuta negative basi huenda ikawasaidia kuwa makini na kupunguza au kuacha unprotected sex.

Mimi nilipopima wakati naenda kusoma nje na kukuta ni negative, sikurudi kwa washikaji tena mpaka niliposafiri baada ya zaidi ya mwezi. Wakati mwingine usipojua hali yako ikoje ni rahisi ku take risks za ajabu ajabu.

Faida ya ujumla kwa taifa ni kupunguza kasi ya ukimwi.

Inabidi tumsifu mzee Kawawa kwa hili.
 
Mzee Kawawa anastahiki heshima.Tutumie maneno yenye busara kupitia huu mtandao.Hata kama tumo mtandaoni lakini ustaarabu unabaki palepale.
 
kwani bado huyo kawawa hajafa tu maana mkewe alishakufa zamani yeye yuko sasa yeye keshapima

Ndugu yangu t_tonga, kwa vile bado ni mwanachama mpya kwenye ukumbi huu, nakushauri kuwa usiwe unaandika kutumia lugha ya kashfa namna hii. Tumia sheria kuwa: "Kama unadhani kuwa mambo unayoandika ni aibu kumwambia ana kwa ana mtu unayemuandika basi usiyaandike hapa."
 
Nadhani Mzee Kawawa keshachoka, yaani hilo la kupima Ukimwi ndo ameona la muhimu? Kwanza huo ni unyanyapaa!
 
Waungwana Tujifunze kuwa na Nidhamu,Maneno mengine hayapaswi kuzungumzwa na WASTAARABU.Mzee Kawawa ni Raia huru na anapaswa kuzungumza mawazo yake!Kumkashfu hapa na kutoa maneno ya Uchafu dhidi yake ni kujishusha hadhi ktk Forum!Wale waungwana Mliotoa kshfa p/se rekebisheni lugha zenu!.Mzee ni mtu mzima mno,Tuchulie maneno yake kulingana na umri wake!!.Nimesikitishwa mno.
 
Kwa mwamko nilioupata kutokana na Uzinduzi wa KAMPENI ZA KUPIMA UKIMWI naona niweke na kusaidiwa mawazo bayana;

Nimekaa nikafikiri nipo njia ya panda tatizo langu mimi linakuja Uhakika wa kwamba Ukivaa Kondom kweli Hupati Ukimwi?

Kuntakinte,

Wengine wanasema kondomu sio kinga, na wengine wanasema ni kinga, lakini kwa mtazamo wangu, mimi naona kwamba kondomu sii kinga kwasababu sisi watumiaji hatuna msimamo nazo. Kama utatumia kondomu, basi tumia kila mara!
 
mimi ningependa kushauri wanaJF woooote walio active hapa twende tukapime ukimwi ! kwanza wangeanza JF seniors !
 
Nyie mafala nini? utamlazimishaje mtu kupima? halafu akikutwa nao sio ndio atakufa hapo hapo kwa presha!na jamii ya KTZ mtu akiwa nao basi atanyanyaswa kishenzi na wanaomnyanyasa sia ajabu nao wanao!
Unataka kusema pale JK alienda kichwa kichwa kupima? hizo siasa Tanzania ninavyowajua hapimwi mtu pale. Acheni geresha. Wote hapa mnajifanya mmepima fix tupu! lakini hiyo haimaanishi mnao!
 
Mwawado,

Nimekusoma mkuu;kwa kweli umeongea vizuri sana. Hata hivyo, bado nimesikitishwa na kauli ya Mzee wetu Kawawa kwa watu wazima tena wajumbe wa NEC ya Chama Tawala.

Kwa mawazo yangu nadhani Mzee wetu ana mengi zaidi na yamuhimu kuliko hayo ya kupima Ukimwi. Nchi hii inapelekwa-pelekwa tu na Mzee wetu amekaa kimya. Hilo ndiyo linaloniuma!
 
Ubaguzi kwa walioambukizwa ndio chanzo cha woga

WOTE tumesikia juu ya kampeni ya kitaifa ya kupima UKIMWI, ambayo, chini ya uongozi wa Jemadari Mkuu katika vita hii ya kitaifa, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ilianza rasmi mnamo Julai 15, mwaka huu.

Ndio. Kampeni inaanza rasmi siku hiyo huku kukiwa na dalili zote za kutofanikiwa kwa kampeni hiyo, kutokana na sababu nyingi ambazo tayari zimeanza kujidhihirisha. Ninafahamu dhahiri kwamba Kamati Kuu ya Utekelezaji wa Kampeni hiyo imesheheni wataalam waliobobea kwenye fani zao, wakiwa madaktari na wataalam mbali mbali. Ninafahamu dhahiri kwamba wataalam hao wameteuliwa kushika nafasi zao muhimu kwenye kamati hiyo kutokana na umahiri wao katika utekelezaji wa kazi zako, hususan katika kufanikisha kampeni hiyo. Hata hivyo, wataalam hao wataniwia radhi kwa kusema kwamba, hata kabla ya kuanza rasmi kampeni hiyo, tayari wamekwishashindwa kutekeleza wajibu wao katika kufanikisha kampeni hii.

Labda nitaonekana mwenye kibri au mwenye dharau, kwa kusema kwamba wataalam bingwa wameshindwa kufanikisha Kampeni ya Kitaifa ya Kupima Virusi vya UKIMWI, hata habla ya kuanza rasmi kwa kampeni hiyo. Je, mimi nina uwezo mkubwa zaidi yao? La hasha. Hata hivyo, ninakiri kwamba mimi si mtaalam wa afya wala sijawahi kuingia kwenye darasa linalofundisha mambo yanayohusiana na UKIMWI. Sijawahi kuchukua mafunzo yoyote juu ya ushauri nasaha kwa watu wanaotaka kupima afya zao, hususan kubaini kama wameambukizwa Virusi vya UKIMWI (VVU). Lakini, kama mtaalam wa sekta ya habari na mawasiliano, ninaweza kabisa kukuhakikishia wewe msomaji kwamba, vita dhidi ya janga hili la kitaifa tayari imekwama, kutokana na sababu zifuatazo.

Mosi: Elimu ambayo ilitakiwa kutolewa kwa wananchi, kubainisha UKIMWI ni nini, kisayansi, haijawahi kutolewa hata siku moja. Kumekuwa na mkazo wa kuupiga vita UKIMWI lakini bila ya kuwaelimisha watu kwa ufasaha wanaupiga vita kwa sababu gani. Asilimia kubwa ya ujumbe ambao umeenezwa kwa wananchi ni kwamba kiwango kikubwa cha maambukizo ya VVU hupatikana kwa njia ya kujamiiana, hivyo, watu wanapaswa kutumia kinga wakati wote wa kujamiiana. Haikuwahi kutolewa elimu kuwaeleza wananchi UKIMWI ni nini, jinsi mtu anavyoweza kuambukizwa, VVU vikoje, na kadhalika. Hakukuwahi kuwapo na mpango wa kisayansi wa kuwaelimisha wananchi kwa ufasaha, UKIMWI ni nini. Kama kungekuwapo na mpango wa kisayanzi wa kuwaelimisha wananchi kwa ufasaha UKIMWI ni nini na namna ya kuupiga vita, tusingelazimika kuendesha kampeni ya kitaifa ya kupima VVU, kwani, watu wangekuwa wakimiminika wenyewe kwenye vituo vya ushauri nasaha na kupima endapo wameambukizwa VVU kwa hiari yao wenyewe! Kama elimu hiyo ingekuwepo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania asingelazimika kuwa Mhamasishaji Mkuu wa kampeni hii. Kama... lakini elimu hiyo haikuwepo, haijakuwepo, na nina uhakika kwamba asilimia kubwa ya wajumbe waliopo kwenye kamati hiyo walikuwa na majukumu ya kutayarisha na kutekeleza mikakati ya elimu hiyo, kitaifa, jambo ambalo halikufanyika. Mpango huo, kwa uwajibikaji, ulikuwa chini ya Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI (NACP), lakini haukutekelezwa. Mpango wa Elimu ya UKIMWI kwa Umma (National Public AIDS Awareness Educational Campaign) haukuandaliwa wala kutekelezwa. NACP walikuwa wapi?

Pili: Vita ambayo imekuwa ikipiganiwa juu ya UKIMWI imekuwa kujikinga na UKIMWI, sio kuwaelimisha wananchi – ambao ndio askari muhimu katika vita hii kali – kwamba unapoambukizwa VVU sio mwisho wa maisha yako. Kumekuwa na matukio mbali mbali ya kuwabagua, kuwanyanyasa na kuwatenga watu ambao wameambukizwa VVU, kiasi kwamba hofu kubwa imetanda miongoni mwetu. Watu wameshuhudia – wanaobisha wamwulize Dk. Sebastian Ndege, anayeendesha kipindi cha redio cha “Njia Panda” kwenye kituo binafsi cha redio cha Clouds FM – jinsi ambavyo watu walioambukizwa VVU wamekuwa wakitengwa, hata na ndugu zao! Watu wameshuhudia jinsi wazazi walivyowatenga vijana wao, wake kwa waume, kwa “kosa” la kuambukizwa VVU. Watu wameshuhudia jinsi ambavyo jamii “imewatenga” na “kuwazika wakiwa hai” watu ambao wameambukizwa VVU, kiasi ambacho hofu kubwa imejengeka miongoni mwetu. Hofu hii imesababisha watu kuogopa, ama kwenda kupima VVU kwa kuhofia kupata majibu “mabaya”, au kujitangaza pale ambapo wanapobaini kuambukizwa VVU, kwa kuhofia “kutengwa” na “kuhesabiwa kuwa wamekufa”, huku, pengine, bado wangeweza kuwa na maisha mazuri, ya kawaida, kwa miaka kadhaa. Hofu hii imechangia kwa kiasi kikubwa kuongeza kiwango cha maambukizi kutokana na kwamba, watu ambao tayari wameambukizwa na hawajui kama wameambukizwa wamekuwa wakiendelea kujamiiana na watu wengine ambao hawajaambukizwa, bila kupima afya zao. Watu hawa wamekataa kupima kutokana na woga, woga wa kutengwa, kunyanyaswa na kubaguliwa na wenzao katika jamii.

Tatu: Pengine, itastaajabisha, jambo ambalo limewekewa mkazo mkubwa zaidi, yaani, matumizi ya kinga – kondomu – dhidi ya UKIMWI, nalo pia limekumbwa na utata. Tumekuwa tukipata ripoti kadhaa juu ya kukosekana kwa “silaha” hizi muhimu, kiasi kwamba kuna sehemu kadhaa ambapo watu wamekuwa “wakiwakodisha” watu wanaotaka kujamiiana “silaha” hizi ambazo tayari zimekwishatumika, na hazifai kutumika tena, ili kwenda kuzitumia katika kupambana na UKIMWI. Inaweza kuonekana kama mzaha, lakini, kuna baadhi ya vijiji ambavyo viko mbali, havifikiwi mara kwa mara na watendaji husika, jambo ambalo limewafanya wananchi wanaoishi kwenye maeneo hayo kujihisi kwamba, labda, vita hiyo haiwagusi wao, na wala wao hawahusiki na vita hiyo. Huu sio mwelekeo sahihi. Ni ajabu, lakini hata baada ya vyombo vya habari kueleza kwa kina tatizo hili la uhaba mkubwa wa “silaha” za kupambana na UKIMWI, yaani kondomu, kwenye maeneo hayo ambayo hayafikiwi kwa haraka kwa sababu ya kutokuwapo miundombinu sahihi kama vile barabara, vyombo vilivyopewa dhamana ya kupigana vita hii vimelipuuzia tatizo hili. Wananchi wanaoishi sehemu hizo wameendelea kutumia “vifanyio” kwa kukodishana, jambo ambalo ni dhahiri limechangia kasi ya maambukizi mapya ya VVU.

Jambo lingine ambalo limechangia kwa kiasi kikubwa Watanzania kupata maambukizo ya VVU kwa kiwango kikubwa ni dhana potofu juu ya UKIMWI. Leo hii, UKIMWI unaonekana kuwa ni malipo ya “dhambi” ya zinaa. Kwa kiwango kikubwa, Watanzania wanauchukulia UKIMWI kwamba ni malipo kwa watu wanaofanya zinaa, huku wakisahau kwamba, mosi, kuna vijana wadogo kabisa wanaosoma shule za msingi, sekondari na haya kwenye vyuo vya juu, ambao wameambukizwa VVU tokea wakiwa tumboni mwa mama zao. Wapo pia walioambukizwa wakati wakinyonyeshwa maziwa na mama zao. Je, na hao pia walifanya zinaa, kwa hiyo wanastahili “adhabu” hiyo? Je, na wale ambao waliambulikizwa VVU kwa kuchomwa sindano ambazo hazikuwa safi, kwenye zahanati za mitaani ambazo hazizingatii kanuni bora za afya? Je, na hao pia wana “dhambi”, ndio wastahili “adhabu” hiyo?

Mtazamo huo potofu, wa kuufanya UKIMWI kuwa ugonjwa wa “ajabu” na wa kuogopwa, na wa kumhukumu kila ambaye ameambukizwa VVU kuwa “mhalifu” ni jambo ambalo limechangia, kwa kiwango kikubwa sana, kwa watu kuendelea na hamsini zao bila kujali kwenda kupima kama wameambukizwa, na wale ambao wameambukizwa kuendelea na vitendo vya ngono bila kutumia kinga, hivyo kuendelea kuwaambukiza watu wengine bila ya wao wenyewe kujua.

Pia, kuna watu ambao wanafahamika – kwa ushahidi wa mazingira – kwamba wameambukizwa VVU, lakini kutokana na utajiri wao, haswa kwa wanaume, wamekuwa “wakibadilisha” wanawake kama wanavyobadilisha mashati yao. Watu hawa, tena kwa makusudi kabisa, wamekuwa wakitumia “visu” vyao kutembea na wasichana wadogo wadogo, na kuwaambukiza VVU, kwa kuwapa zawadi zenye thamani kubwa pamoja na kuwastarehesha. Kuna waliodiriki hata kuwachukua wasichana hao wadogo wadogo na kwenda kustarehe nao nchi za nje, kisha kuwazawadia vitu vya thamani kubwa, kama vile magari madogo aina ya “baloon”, au simu za mkononi zenye thamani kubwa. Kutokana na tamaa zao, wasichana wadogo wamekuwa wakibabaika kila wanapowaona wenzao wakipewa zawadi hizo, hivyo kujirahisisha kwa “wazito” hao, wakisababisha kukua kwa mtandao wa maambukizi mapya ya VVU.

Sasa mtaniuliza: Nini kifanyike?

Wote tunajua kwamba, unapokwenda vitani, lazima kwanza ufanye utafiti kumjua kwa undani adui yako. Lazima umjue yeye ni nani, marafiki au washirika wake ni nani, anaishi wapi, ana fikra gani, mbinu zake za kivita ni zipi, ikiwezekana, ujue kila anachofanya kwa muda wote, ili kuweza kujua ni wakati upi utakaokuwa sahihi kumvamia na kumpiga bila ya yeye kuweza kujipanga. Hizi ni mbinu za kijeshi ambazo hufanywa na wanajeshi wote duniani, kabla ya kwenda vitani. Kumchunguza adui yako uweze kufahamu udhaifu wake.

Tumeingia kwenye vita dhidi ya adui UKIMWI bila kumjua kwa undani adui yetu. Hatujamchunguza, yeye ni nani, marafiki au washirika wake ni nani, anaishi wapi, ana fikra gani, mbinu zake za kivita ni zipi, na hatujajua ni wakati gani muafaka wa kumshambulia ili asiweze kujipanga na kujibu mashambulizi yetu. Tumekwenda kumpiga vita adui UKIMWI bila ya kuwa na dira, bila ya kuwa na mpango, tumepoteza muda mwingi na fedha nyingi, huku askari wetu wengi wakiteketezwa na adui huyu. Bado tunataka kuendelea na vita hii?

Mimi ninawasifu sana watu wa Uganda, kwani, wakati UKIMWI ulipogunduliwa, vijana wengi sana – wanafunzi wa shule za msingi, sekondari na vyuo – walipukutika kama majani, kwa vifo vilivyosababishwa na UKIMWI. Vilio vilitanda kila kona ya nchi ya Uganda, sio mijini pekee bali hata vijijini.

Wananchi wa Uganda wakashtuka, wakasema: Hapana! Tutajipanga upya!

Mikakati ya kuwafundisha wananchi, kuanzia ngazi ya kijiji, kuufahamu UKIMWI, kwa undani wake, ilifanyika. Watu wakafahamu UKIMWI ni nini, wakabadilika kitabia na kifikra. Wakaacha kuwabagua, kuwanyanyasa na kuwatenga watu wengine walioambukizwa UKIMWI. UKIMWI ukaonekana kuwa ugonjwa wa kawaida tu!

Hilo ndilo jambo la msingi – kuufanya UKIMWI uonekane kuwa ugonjwa wa kawaida tu! Hapo, ubaguzi uliisha, kutengwa kukakoma, na hakukuwa na vitendo vya kuwanyanyasa watu walioambukizwa UKIMWI. Kila mtu aliendelea na shughuli zake za kawaida, lakini kwa makini zaidi. Watu walikwenda kupima UKIMWI kila mara, bila ya kuwa na hofu wala woga, wakijua kwamba, kama walikuwa wameambukizwa, wangeendelea kuishi bila matatizo yoyote. Hali ilikuwa shwari. Ukichunguza takwimu za maambukizi ya UKIMWI nchini Uganda leo, katika nchi zote za Afrika Mashariki, Uganda ina maambukizi mapya machache kuliko nchi zote za Afrika Mashariki. Uganda imefanikiwa kwa kiwango kikubwa kwenye vita dhidi ya UKIMWI.

Tujiulize. Kinachotutofautisha sisi, Watanzania, na wenzetu, majirani zetu, Waganda, ni kipi? Kwa nini wao waweze kufanikiwa kwa kiwango kikubwa huku sisi tukiwa watazamaji? Kwa nini sisi hatutaki kubadilika?

Tunaweza kubadilika, na tunaweza kufanikiwa, iwapo tutaweka mikakati thabiti, ya, kwanza, kuyajua yote ambayo tunapaswa kuyajua juu ya UKIMWI.

Tunao madaktari, ambao wanaweza kushirikiana na wataalamu wa sekta ya teknolojia ya habari na mawasiliano (TEKNOHAMA), kutayarisha makala kwenye magazeti na majarida, pamoja na vipindi maalum ambavyo vitaoneshwa kwenye luninga au kutangazwa kwenye redio. Vyombo vya habari vina nafasi kubwa na muhimu ya kutoa mchango wa elimu katika vita dhidi ya UKIMWI, kupitia majarida na magazeti, vipeperushi, mabango, luninga, redio, na pia, wasanii wa fani mbali mbali, kama vile fasihi simulizi na fasihi maandishi. Kwenye fasihi simulizi kuna tamthilia (maigizo, nyimbo, ngoma za jadi, n.k.) wakati kwenye fasihi maandishi kuna viandiko (majarida, magazeti, vitabu, mabango, vipeperushi, n.k.). Kama ikibidi, wasanii wa maigizo kwenye luninga walipwe – chini ya mpango maalum wa dharura – ili waweze kutunga michezo ya kuingiza itakayowaelimisha watu juu ya UKIMWI, namna ambavyo mtu anaweza kuambukizwa VVU, jinsi ambavyo mtu anaweza kujikinga dhidi ya maambukizo, na kadhalika. Mchango wa vyombo vya habari tayari umeonekana, kwa mfano, mpango wa kitaifa ambao umekuwa endelevu, katika kuelimisha na kuchangia vita dhidi ya saratani inayowaathiri wanawake (kwa uwingi wao) na hata wanaume (kwa uchache wao). Mchango mkubwa ambao umekuwa ukitolewa kwa Chama cha Madaktari Wanawake wa Tanzania (MEWATA) usingefanikiwa kama vyombo vya habari visingeshirikishwa kwenye kampeni hiyo. Kampeni kama hiyo inaweza pia kufanikiwa, katika vita dhidi ya UKIMWI, kama vyombo vya habari vingeshirikishwa ipasavyo. ITV na MEWATA wameonesha njia, TACAIDS na NACP wameiona?

Wengi wetu hatujui “A” wala “B” kuhusu UKIMWI. Binafsi, ukiniuliza kuna aina ngapi ya VVU sitaweza kukujibu. Nenda sehemu yoyote ya Uganda leo, waulize watoto wadogo, watakutajia aina zote za VVU. Ala? Hivi kuna zaidi ya aina moja ya VVU? Mlikuwa hamjui?

Wataalam wa teknolojia ya habari na mawasiliano wako tayari kuandaa vipindi maalum ambavyo vitawaelimisha wananchi kupitia luninga na redio, kinagaubaga, ili waweze kuujua UKIMWI. Wasanii wataweza kuandaa michoro, kutokana na maelezo ya madaktari na wataalam wa afya, ili kuweza kuonesha mifano ya maumbile ya VVU. Katika kuelezea UKIMWI, kupitia mbinu za kisayansi, tutaweza kuujua UKIMWI na tutaweza kuubomoa.

Hakuna elimu ya kutosha kwa sasa juu ya UKIMWI. Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI, katika miaka yake yote tokea ulipoanzishwa, haujaandaa kipindi hata kimoja, ambacho kingerushwa kwenye luninga au kutangazwa kwenye redio, kuwaelimisha wananchi “kisayansi”, UKIMWI ni nini. Ninakumbuka, mwanzoni kabisa, mabango yaliyokuwa “yakielimisha” wananchi juu ya UKIMWI yalikuwa na michoro ya watu waliokondeana, wakionekana dhahiri kuwa na afya mbaya. Jambo hili liliwatisha watu wengi, ikaonekana ni makosa. Lakini ile dhana kwamba ukiambukizwa UKIMWI ndio mwisho wa maisha yako, kwa kusema “UKIMWI UNAUA” ilikuwa tayari imejengeka. Bado, kuna maandishi kadhaa kwenye machapisho mbali mbali, yanayosema “UKIMWI NI HATARI. UNAUA. JIHADHARI NA UKIMWI!” Machapisho haya yanawatisha watu, yanaogopesha, yanakwamisha vita dhidi ya UKIMWI!

Kwa mtazamo wangu, lazima tukubali kwamba tulifanya makosa, na sasa bado tuna nafasi ya kujirekebisha. Sisemi kwamba “tuurembe” UKIMWI kwa kuufanya uonekane kwamba sio hatari. La hasha. Tuwe na mtazamo kwamba unapoambukizwa sio mwisho wa safari ya maisha yako. Watu wanaoishi na VVU wana nafasi kubwa katika vita hii, kwani wao ni mfano tosha kwamba unaweza kuwa umeambukizwa lakini ukaendelea kuishi maisha ya kawaida. Wao ndio walimu wetu katika vita hii, tuwape nafasi ya kutuelimisha. Hata hivyo, licha ya kukubali kwamba kuambukizwa UKIMWI sio mwisho wa maisha, hakuna maana kwamba tuache kujikinga na kuwa makini wakati wote. La hasha. Tunatakiwa tuongeze bidii katika vita hii.

Ninampongeza Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa kusimama kidete na kuwashauri wananchi kwenda kupima UKIMWI. Nimewahi kupima UKIMWI na nitapima tena siku hiyo. Nitayakubali matokeo yoyote yale. Kwani kuambukizwa UKIMWI sio mwisho wa maisha yangu.

Lakini tukumbuke: Je, tumejipanga vizuri katika vita hii kubwa kuliko zote?

Mungu Ibariki Tanzania.

Mungu Ibariki Afrika.

Naomba kutoa hoja.
 
Nakumbuka mwaka 1986-87 serikari ilijitahidi sana kuwaelewesha watu kuhusu ukimwi,sinema za mafunzo ya kujihadhari na ukimwi zilikuwa zinaonyeshwa bure tena kila sehemu za kadamnasi na nakumbuka karibu kila mtu alikuwa anajua ukimwi ni nini na jinsi onavyoambukizwa.

Miaka hiyo ni watu wachache sana walikuwa wameambukizwa (na wengi walikuwa wanaishi mipakani) na ukimwi labda 0.0001% of population.Fast forward miaka kumi mbele ukimwi umeua watanzania vibaya sana!
Je serikari ilifanya makosa gani, au ingefanya nini? Nina uhakika kama hao watu walioambukizwa kwanza wasingeeneza au wangekufa bila kufanya hivyo,Tanzania ya sasa isingekuwa na mgonjwa hata mmoja wa ukimwi!

Ni makosa gani yalifanyika?
 
Rubabi
Well nafikiri nia na madhumuni ya serikali kufanya yale yote ilikuwa ni kuwapa wananchi elimu ili nao waweze kujua ni jinsi gani wanavyoweza kujikinga au kuzuia maambukizi zaidi. Kilichofanyika ni kwamba serikali ilitumia mbinu zote kelimisha jamii ila jamii yenyewe haikuwa tayari kwa wakati ule!!! Chukulia mfano mtu aliyepima HIV na kujikuta anao miaka ile ya 86/87, tukio lililofuata kwa mtu huyo ni kukata tamaa na kuona maisha hayana maana tena > kwa hiyo alichoweza kufanya ni kuhakikisha anawaambukiza watu wengi zaidi ili tu aone anakufa kishujaa pindi UKIMWI utakapoanza kumshambulia!

Cha pili ni kwamba kama inavyoeleweka hili suala la UKIMWI ni la kisiasa & kibiashara maana kuna watu wengi sana wameajiriwa ktk sekta hii na NGO kibao zipo zinafanya kazi hizo kwa kujilipa au kulipwa mishahara minono na kutumia vibaya fedha zinazotoka kwa wahisani kwa ajili ya kutoa elimu ya kuzuia maambukizi ya UKIMWI!! Sasa ukiliangalia kisiasa unakuta kwamba hawa viongozi pia wengi wao amejaribu kutumia UKIMWI kama njia ya kuwaweka madarakani!!

Kwa hiyo Rubabi kilichofanyika ni kwamba kila mmoja alikuwa anafanya kazi ya kuelimisha juu ya UKIMWI kwa madhumuini binafsi na sio kwa lengo la kuiokoa jamii!!

Dmussa,

It is easier to be wise for others than for ourselves.
 
Back
Top Bottom